Kati ya DED na DAS nani bosi wa mwingine?

Kati ya DED na DAS nani bosi wa mwingine?

DED na DAS wanapoteuliwa na kuanza kazi kwa pamoja nani anakuwa juu kimshahara kumzidi mwenzake.?
Kweli nimeamini kwamba ujinga ni Sawa na zigo la mavi, na uaipo lishusha kwa uzito wake basi utalituwa kwa harufu yake.......
 
DED na DAS wanapoteuliwa na kuanza kazi kwa pamoja nani anakuwa juu kimshahara kumzidi mwenzake.?
Kijana, huku kuchamba kwingi kutakufanya ushike hajakubwa.... tehteehhh
 
Ded anaweza asiguse mshahara wake mpk ana acha u-ded.

Maposho na visafari za hapa na pale ni vingi.

Mafungu anayokusanya, ni mengi sana.

DC, DAS, RAS, wanaweza mzidi ded mshahara lkn DED ana chanzo cha pesa kikubwa kuliko hao wote
 
DED na DAS wanapoteuliwa na kuanza kazi kwa pamoja nani anakuwa juu kimshahara kumzidi mwenzake.?
Hata mwaka haujaisha mmeingia kwenye mgogoro. Umetoka kuuliza nani ni boss kati ya DAS na DED... ghafla umehamia kwenye mshahara[emoji23] [emoji23] [emoji23]

Hawa yuuu dedi masifa [emoji137]
 
PS permanent secretary, mshahara wa RC ni 3.6
RC anakula 6.8-7M
Lkn pia inategemea,

Kama mtu alikuwa ktk nafasi kubwa serikalini mfn. Mkuu wa taasisi i.e tanesco, tbs na anapokea mshahara mkubwa zaidi ya 10M, basi akiteuliwa RAC, PS au RC mshahara una panda zaidi.
 
DAS anawajibika kwa RAS, hali kadhalika DED. Hivyo hakuna line ya uwajibikaji wa moja kwa moja wa DED kwa DAS. Hata hivyo kiitifaki DAS yupo juu zaidi ya DED.

Niongeze kwamba DAS anauwezo wa kumuita DED ofisini kwake na akamuagiza cha kufanya. Lakini DED hawezi kufanya hivyo kwa DAS.
Sijui kama upo sahihi sana, ninavyojua ni kwamba DAS ni human resource administrator ktk level ya wilaya, kwenye mashirika umma tunawaita HR. Juu yao kuna watendaji yaani Mkurugenzi. Wilayani kuna Mkurugenzi wa halmashauri yaani DED, kweli mashirika ya umma kuna Mkurugenzi mkuu.
 
Ndiyo, mbona zipo wilaya kibao tu zina halmashauri zaidi ya moja! DC mmoja, DAS mmoja, wakurugenzi wa Halmashauri wawili na pengine watatu.

Mfano ni hiyo wilaya ya kahama ina wakurugenzi wa halmashauri watatu
Asante mkuu, nimekueleawa
 
DED = District Executive Director, DAS = District Administrative Secretary & DC = District Commissioner. Wote hao ni kuteuliwa na kutumbuliwa wakati wowote. Nani mkubwa hapo
DC, maana yeye ndiye raisi wa wilaya.
 
Wadungu naomba nami nichangie mada hii ambayo wengi wanaona kama uhusiano wa DED na DAS ki-protokali unachanganya. Mchango wangu utazingatia sheria, kanuni na taratibu za nchi.
1. Mkuu wa Wilaya (DC)
Mkuu wa Wilaya anateuliwa na Raisi kwa mujibu wa kifungu cha 13 (2) cha sheria ya Tawala za Mikoa (The Regional Adminstration Act, 1997). Majukumu yake ni pamoja na kuwa mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya. Kwa mantiki hiyo anakuwa muwakilishi wa Raisi katika kusimamia ulinzi, usalama na shughuli za maendeleo kwa ujumla. Akishateuliwa mkuu wa Wilaya anaapishwa na kusimamiwa kiutendaji na mkuu wa Mkoa (kifungu 13 kifungu kidogo cha 3).

2. Katibu Tawala wa Wilaya (DAS)
Kifungu cha 16 (2) cha sheria ya Tawala za Mikoa kinamtambua DAS kama principal adviser (yaani mshauri mkuu) wa DC. Kifungu hiki pia kinasema DAS anateuliwa kwamujibu wa sheria ya Utumishi wa Umma. Bahati mbaya sina hiyo sheria hapa na nimetafuta mtandaoni sijaweza kuipakua. Ila natoa hoja yangu hapa kwa kuzingatia uteuzi wa Ma-DAS uliofanywa tarehe 5.8.2018 na Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma. Katika tangazo lake kifungu cha 1.2 Waziri alisema, "Leo nimewaita kuzungumza nanyi kuhusu Uteuzi na Uhamisho wa baadhi ya Makatibu Tawala wa Wilaya. Kwa mamlaka niliyokasimiwa kwa mujibu wa Sheria nimefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa Wilaya ili kujaza nafasi wazi kumi nane (18) zilizopo katika wilaya za Kinondoni, Mpwapwa, Dodoma, Iringa, Bukoba, Kigoma, Siha, Mtwara, Newala, Misungwi, Njombe, Kondoa, Manyoni, Kilindi, Chunya, Pangani, Bagamoyo na Handeni".
Hivyo, kwamujibu wa tangazo la Waziri mwenye dhamana ya Utumishi wa Umma ambalo nimenukuu hapa, uteuzi wa DAS upo chini yake kisheria.

3. Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya (DED)
Kwa mujibu wa kifungu cha 22 (2) cha Sheria ya Utumishi wa Serikali za Mitaa ( The Local Government Service Act, 1982), DED anateuliwa na Raisi. Majukumu kiutendaji DED anakuwa Chief Executive wa Halmashauri na anaripoti kwa Katibu Tawala wa Mkoa (RAS).

Hitimisho
Kwangu mimi sioni mkanganyiko wowote wa kisheria kati ya DED na DAS, maana DED anateuliwa na Raisi na DAS anateuliwa na Waziri wa Utumishi wa Umma. Sema DAS anaweza kuonekana katika mazingira flani kuwa boss wa DED pale ambapo anatekeleza kazi anazotumwa na DC. Pia, nimewahi kuona mahala DAS anaudhuria vikao vya Council Management (CMT) ambavyo DED ndio mwenyekiti. DC ni mkuu kiitifiki kwa DED ingawa wote wanateuliwa na Rais, utofauti wao unatokana na majukumu. DC anapolinda amani, usalama na maendeleo ni pamoja na kazi anazofanya DED na wakuu wengine wa vyombo vya Ulinzi na Usalama kwenye ngazi ya Wilaya.
Huu ni uelewa wangu kwa kadri nilivyoelewa sheria husika, kama kuna mahala nimekosea niko tayari kukosoloewa maana mimi si mwanasheria kitaaluma. Asanteni
Asante sana Mkuu. Pia DC ni political figure wakati DED ni Mtendaji na anamiliki rasilimali. DAS ni arm ya DC na uteuzi wake ni Waziri wa Utumishi hivyo huwezi kuwa juu ya DED mteule wa Rais. Kiukweli DAS wako redundant kidogo wala hawaonekani sana kwa kuwa wamegunikwa na DC na DED. Hivyo basi DAS huwezi kufuatwa na DED kiprotokali kabisa. DED anaweza kumfuata DC tu na pia siyo lazima. Tena bora miaka hii DC wanasikika. Huko nyuma DC walikuwa ni shida na wakati mwingine utawakuta wamekaa kwa DED kwa kuwa huko ndiko mapeni yapo. Na UTARATIBU wa kimuundo ni DED kwa RAS na DAS kwa DC.
Pia office ya DAS iko kwa DC. DED OFFICE yake imeajiri wataalam ambao ni non political japo kimoyomoyo kila mmoja ana uhuru wa itikadi ya siasa anayoitumikia. Kiujumla DC hana manpower kubwa yuko na political figures wa wilaya husika ambao wana office zao zinazojitegemea in a way mfano madiwani, maofisa Tarafa n.k
 
Rc, RAS zipo chini ya wizara gani? Sio tamisemi? (Tawala za mikoa na serikali za mitaa?)
Niliona Jafo akiagiza Ma RC.

Pia mbona nilishaona RC akimsimamisha ded kwa uchunguzi?
Mkuu wa Mkoa ni sawa na Waziri, na ana wafanyakazi wake ambao ni RAS, DAS, DC na Assistant RASs na watumishi wengine.
Kwa hiyo Waziri hawezi kumfukuza kazi au kum-critcize mkuu wa mkoa and viceversa.
Lakini anaweza kufanya hivyo kwa DED.

Mkuu wa mkoa na RAS uteuzi wao upo kikatiba na REGIONAL ADMIN. ACT '97.
DED ni LOCAL GOVERNMENT ACT '82
 
Mkuu wa Mkoa ni sawa na Waziri, na ana wafanyakazi wake ambao ni RAS, DAS, DC na Assistant RASs na watumishi wengine.
Kwa hiyo Waziri hawezi kumfukuza kazi au kum-critcize mkuu wa mkoa and viceversa.
Lakini anaweza kufanya hivyo kwa DED.
Ikitokea umeteuliwa RAS, na uiatumbuliwa, je utaendelea kupokea mshahara? Au utapangiwa kazi nyingine? Usipopangiwa kazi nyingine utakuwa unakaa nyumbani tu?

Je Mtu kama Mafuru aliekuwa Mkuu wa hazina, alivyotumbuliwa na huku hatujasikia akipata uteuzi mwingine anaebdelea kulipwa mshahara? Anashinda nyumbani tu?
 
Ikitokea umeteuliwa RAS, na uiatumbuliwa, je utaendelea kupokea mshahara? Au utapangiwa kazi nyingine? Usipopangiwa kazi nyingine utakuwa unakaa nyumbani tu?

Je Mtu kama Mafuru aliekuwa Mkuu wa hazina, alivyotumbuliwa na huku hatujasikia akipata uteuzi mwingine anaebdelea kulipwa mshahara? Anashinda nyumbani tu?
Unakuwa huna kazi wala mshahara.
 
Back
Top Bottom