Kati ya Mwingereza na Mmarekani Ni yupi huwa unamuelewa kwa urahisi akiwa anaongea kingereza?.

Kati ya Mwingereza na Mmarekani Ni yupi huwa unamuelewa kwa urahisi akiwa anaongea kingereza?.

Huwa napata ugumu kidogo nikiwa namsikiliza Mmarekani ila namuelewa kwa urahisi zaidi mwingereza.

Wataalam wa kingereza karibuni.
Naelewa wote ila kuna baadhi ya British accents/dialects huwa zinanipa tabu muda mwengine kuelewa mfano cockney huwa wana silent "T" sasa jua kwamba maneno yoote yenye "T " wao wanameza mfano Maji kwa kiingereza "Water" inatamkwa "Wota" wao wanatamka "wo a" hapo bado zile intonations kuna pia scottish accent .

Kwa marekani english yao ni very simple ila kuna "Black american venacular " au "ebonics " na hii inategemeana na maeneo sasa ukute yule aliyekulia kwenye ghetto's hizi kumuelewa ni ngumu maana wana misamiati yao ambayo kwenye standard american english haipo .

Kingine ukiacha ya kuwa american english ni rhotic language ( yaani wanaweka emphasis kwenye mid na Last "R" ) hakipo tofauti saaana na british english labda kwenye matamshi na kuna vitu vina majina tofauti.

Kwa mimi nadhani ni ishu ya accent & dialect sana sana ila viingereza vyoote vinaeleweka haijalishi maeneo.
 
ngeli ya mwingereza haijawahi kunipa tabu kuielewa
nilifanya field na waingereza tukawa tunaelewana bila shida yoyote
ila shida hua inakuja nikiwa nawasikiliza wamarekani
Huwa inachukua muda kidogo kuelewa walichokiongea haijalishi ni face 2 face conversion au kinyume
Umeshakutana na wale wa kutoka Scotland au Ireland? Nilikutana na mmoja nilichoka. Neno moja lenye herufi 4 au zaidi herufi unaweza kuzisikia zikitamkwa zinaweza kuwa 2 tu
 
Sikiliza interview za sky sport za wachezaji wa kiingereza wa EPL ndio utajua haujui.

Halafu msikilize Mzee Biden pamoja na Trump tower utapata jibu kama kiingereza cha wasomi wa Tz ni rahisi kukielewa sababu wasomi wanazungumza kwa kutumia kigugumizi ili wasidhalilike.
😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂

Nimecheka sana
 
Hilo ni kweli, lakini si ukweli wote.

Hata weusi kwa weusi [Foundational Black Americans] wana lafudhi tofauti tofauti kulingana na eneo watokalo.

Kwa mfano, weusi [Foundational Black Americans] wa Texas wana lafudhi tofauti kabisa na weusi wa Georgia.

Weusi wa Maryland wana lafudhi tofauti kabisa na weusi wa Mississippi.

Weusi wa Virginia wana lafudhi tofauti kabisa na weusi wa Alabama.

Malcolm X na Martin Luther King walikuwa na lafudhi tofauti.

Malcom X alizaliwa Omaha, Nebraska na akakulia Milwaukee, Wisconsin, Lansing, Michigan, na Boston, Massachusetts.

Martin Luther King Jr., alizaliwa na kukulia Atlanta, Georgia.

Hawa wawili ukizisikiliza hotuba zao utagundua walikuwa na lafudhi tofauti.

Pia, hata wazungu kwa wazungu nao wana lafudhi tofauti.

Wazungu wa Arkansas na Kentucky wana lafudhi tofauti na wazungu wa South na North Dakota.

Wazungu wa Kansas wana lafudhi tofauti na wazungu wa Alaska.

Sababu hasa ya tofauti hizo siijui au sizijui. Ila ninachojua elimu nayo huwa na mchango mkubwa sana.

Mambo mengine ambayo huchangia utofauti huo ni maeneo ya kijiografia na labda exposure na contact na watu wa sehemu zingine.

Kwa mtu ambaye hujaishi na Wamarekani kwa muda mrefu, baadhi ya tofauti hizo za kilafudhi ni ngumu kuzibaini.

Ni kama vile ambavyo wao wakija huku kwetu, itawawia vigumu kuzibaini lafudhi za wazungumzaji wa Kiswahili ambao ni Wasukuma, Wachaga, au Wahehe.

Ila mimi na wewe haitotuwia vigumu kumbaini Ngosha ni yupi na Mangi ni yupi.

Na hata kwa Wasukuma, sisi kwa sisi kupitia lafudhi huwa tunagunduana kirahisi yupi ni Mnyantuzu, yupi ni wa Shinyanga, na yupi ni wa Mwanza.

Ila Mnyakyusa ambaye hajaishi na Wasukuma, kwake atasikia lafudhi tu ya Kisukuma.
Asante kwa elimu
 
Jaribu kuzungumza na waingereza toka LIVERPOOL, unaweza kuhisi ni kichaga, si kichaga, si kipare, ni hatari.
 
Scotland aka Scottish, Australians

Kiingereza ni lugha ya kuungaunga sana.
Lugha gani ambayo watu kutoka maeneo tofauti wanaongea tofauti na unaweza usielewe.

Sasa kuna wahindi, wanijeria, wajamaica nao wamekuja na kiingereza chao basi kazi kwelikweli.

Ngoja nasisi wa mtoni mtongani tuanze kuongea English yetu mixer kimakonde, kimakua, kizaramo, unaweka na kisukuma inakuwa getegete kabisa.
Wa Scottish ndiyo hawaeleweki kabisaa!

Mimi huwa hata sijui kama wanazungumza kiingereza.
 
We mtoa mada hujui ngeli ya mwingereza akiongea huwezi sikia neno hata moja British accent sio mchezo kiujumla American English ni maarufu na imesambaa sana kupitia miziki films zote hizo ni American English
Kiengera ni cha waengereza BBC unaelewa zaid kuliko CNN au fox anaebisha hajui hata kiengereza ni nn
 
Movies na music vimefanya iwe rahisi kuwaelewa Wamarekani kuliko Waingereza. Ila Wanaigeria watolewe kwenye nchi zinazozungumza kiingereza.
 
Movies na music vimefanya iwe rahisi kuwaelewa Wamarekani kuliko Waingereza. Ila Wanaigeria watolewe kwenye nchi zinazozungumza kiingereza.
😂 wanatamka maneno kama yalivyo, hawataki shida. Na wanatumia nguvu kubwa kama ugomvi vile
 
Back
Top Bottom