Kati ya Said Michael na Masoud Kipanya, Nani mkali kwenye Katuni za uchambuzi?

Mkoloni aliiacha Tanganyika sio Tanzania, ukifuata umakini basi Masoud hapa kachemka
 
Kipanya ni legend kaanza longtime na bado anawakilisha, huyo Said nimeanza kumsikia hivi karibun. Anyway, what abt Nathan Mpangala?

Nathan namkubali na kina King kinya, Dany Mzena,Fadhili Mohamed, halafu na yule jamaa aliyekua anachora kwenye magazeti ya Kasheshe na Komesha hadi yakafungiwa,
 

Tafsiri yake ni kuwa mleta mada umepambanisha vitumbua na maandazi, vina radha tofauti na wapenzi tofauti. Matokeo yatakuwa sio sahihi
 
Kipanya anachora katuni zinazofikirisha!!! Bila kutulia huwezi kumwelewa!! Said Michael katuni zake ni za moja kwa moja...
 
Huwezi kuwalinganisha kirahisi kwa kua hawapo kwenye level ground.
Said Michael katuni zake pia nzuri ila bahati mbaya hana uwanja wa kuonyesha kazi zake kama alokua nayo Kipanya. Wengi watasema Kipanya kwa kua kila ukishika gazeti la Mwanachi unaona kazi ya Kipanya wakati Said Michael mpaka uwe mfuatiliaji wa katuni zake mitandaoni. mwanga lutila
 
Last edited by a moderator:
Masoud ni mbunifu anaumiza kichwa na anajua kuchora,said anajua sana kuchora katuna na anamzidi masoud,katuni zake ziko modern,hyo ndo tofauti yao.!!
 

Natamani mleta mada angepita hapa. Umenifanya nikose cha kuchangia. Umemaliza kabisa mkuu. Hawa ni watu wawili tofauti wenye vipaji tofauti.
 
Jamani kuna mashine inaitwa JAMES GAYO. Hiyo ni balaa kwa katuni. Namheshimu sana Kipanya lakini kwa Gayo ni mwisho wa reli. Said Michael naye anakuja juu sana.
 
Dah!.Ila Sio Siri Wengine Wanajitahidi.Ila Kipanya Anatisha.Uongo Dhambi!
 
Hapa Watu Wanakomenti Kwa Kuangalia Jina Ila Kiukweli Kuna Wachoraji Katuni Wengi Wakali Hapa Tz Ila Hawana Mambo Yakuuza Sura Ila Kazi Zao Zinatambulika Vyema Nafakiri Wasoma Magazeti Na Majarida Mnawatambua Vyema!
 
Jamani mimi natafuta katuni moja niliwahi kuiona kwenye gazeti la Majira kama sikosei ilikuwa na kichwa "USIOMBE KUPATA AJALI HALAFU WAOKOAJI WAKO WAKAWA NI WAPIGA PICHA" Sikumbuki mchoraji lakini niliipenda ilionesha jamaa kapata ajali kalaliwa na gari anaomba msaada halafu wapiga picha kibao wamefika badala ya kumuokoa wako busy na kupiga picha. Natamani kuiona tena
 
Mkuu umemaliza kabisa. Watu walikuwa wanajadili bila kuwa na elimu ya katuni. Kama ulivyosema kila mmoja ni bora katika aina ya uchoraji wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…