Sasa hivi barabara zimefunguka uelekeo wote, vijiji vyote ukiwa unatokea barabara ya njombe viko accessible, wilaya ya namtumbo pia barabara ya uelekeo wa mtwara ni lami tupu, koote huko ardhi ina rutba na mvua za kutosha, na wenyeji hawana maneno ukitua popote ulizia ofisi ya mtendaji nenda kajitambulishe eleza lengo lako utasaidiwa bila shida, ardhi ipo ya kutosha. Kwa vile unaenda vijijini basi ni vizuri kuchukua barua ya utambulisho kutoka huko utokako, na kama ulkuwa mwajiriwa ukaacha kazi beba vitambulisho vyako. Ruvuma zao kuu wanalolima ni mahindi, pia wanalima maharage, kahawa, korosho, karanga, mihogo nk, kifupi ardhi ni inakubali mazao kibao, niwewe tu. Na kwavile wewe unataka kwenda kuishi hukohuko nakushauri tafuta vijiji ambavyo haviko mbali sana na mji, Maeneo kama Mlilayoyo, Mtangimbole, Shuleyatanga, jirani na barabara kuu na pia huduma za umeme na zingine za kijamii, unaweza kujikuta unafuga samaki pia ambao wanahitajika sana Songea. Kiikubwa tafuta kijiji uhame kwanza mkuu, ukipata hata ekari 10 za jirani kijijini we lipa jenga kajumba kako zungushia uzio anza mambo.