Kati ya Spika Ndugai, Balile na Gavana Luoga nani mkweli kuhusu deni la taifa?

Kati ya Spika Ndugai, Balile na Gavana Luoga nani mkweli kuhusu deni la taifa?

Bottomline is tunadaiwa tena fedha nyingi pasipo na sababu za msingi.

Kama tusingekuwa na Rasilimali ingekua sahihi ,

Tunakopa ili kufurahisha taasisi za mabeberu ambayo hayataki tuwe na uwezo wa kujitegemea.
Leo umekuwa mkosoaji(mpinzani) haaa.
 
Balile alikuwa yupo sahihi lakinj deni la nje sio trillion 78, Bali hiyo ni jumla na ya Deni la ndani.
Na pia Sasa hivi Deni ni trillion 82
Pia Magufuli aliacha Deni likiwa trillion 71
Hahahaaaa hujaulizwa magufuli aliacha deni gani bwashee huo umagufuli utawatoka lini ? Yaan mnataka kutulazimisha wote kwamba maguful alikuwa mtu safi wakati ndiye rais wajabu na shetan kuliko marais wote ambao tanzania imewahi kuwanao ndio maana wafuasi wake mna kazi ya kumsafisha huku
 
Acha kumuweka Ndugai maneno hakudema ni exactly 70T bali alisema ni karibu 70T.
Usichanganye lugha.
 
Kuna mkanganyiko mkubwa nchini katika utoaji taarifa za deni la taifa. Kuna usemi kuwa miluzi mingi huchanganya mwelekeo wa Mbwa.

Ndugai ni Spika, Balile ni Mwandishi wa Habari za Uchunguzi, Luoga ni Gavana, sasa nani ana taarifa sahihi za kutufanya tumuamini?

Ndugai amesema deni la taifa ni 70 tr, Balile (Gazeti la Jamhuri October 26, 2021) alisema ni 78 tr, Luoga anasema liko 27.9% halijafikia hata nusu ya kiwango cha kukopa.

Lipumba naye huenda akaibuka na takwimu zake, Mbatia naye anajifua kufanya uchunguzi ili aje Ki-NCCR, Tundu naye ataibuka kivyake. Baghosha!

Kwa mkanganyiko huu kama hauna sababu za kisiasa basi huenda mtu akatamani enzi ya Magufuli ya kudhibiti utoaji takwimu, kwa sababu kama nchi, tunatia aibu duniani, tunajipaka matope wenyewe, tunaonekana hatuna mifumo mizuri ya kitakwimu, utoaji taarifa nyeti, wala kumbukumbu sahihi za deni la taifa.

Hivi unawezaje kumlipa mdeni wako kama hujui kiasi sahihi anachokudai?

Magufuli alisema kazi ya urais ni ngumu, Nyerere alisema Ikulu ni mzigo, JK alisema Ikulu ni sawa na kulalia kitanda chenye kunguni wengi.

Kwa upande wa Ndugai, nadhani kauli yake imethibitisha kwamba ameamua kufanyakazi ya Msemaji Rasmi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (simjui ni nani).


Msome Balile hapa:
Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78 | JamiiForums


Msome Ndugai hapa:
Rais Samia 'ampiga' Spika Ndugai | JamiiForums


Gavana yeye alitoa ufafanuzi wake jana Jumatano Disemba 29, 2021 kwenye kipindi cha Power Breakfast kinachoendeshwa na Redio ya Clouds FM. (nimetafuta clip nimeikosa).

View attachment 2062566

View attachment 2062570

View attachment 2062577
Taswira zote kwa hisani ya google.
Luoga kaongea asilimia ya tulichokopa wakati Balile na Ndugai wametaja kiasi halisi. Ukweli ni kwamba hata kama ni asilimia 28 bado kiwangi tulichokopa ni kikubwa mno. Hicho kiwango tumepewa na wazungu ili tukope sana watukamue. Ndugai hata kama katofautiana kidogo na Balile lakini takwimu zao zinashabihiana,70 ma 78 siyo mbali sana.
 
Ccm ni genge la kihuni usimwamini kabisa yeyote... Kazi yao lubwa ni kwa pamoja kucheza na akili za watz kwa maslahi yao binafsi hakuna kingine
 
Kuna mkanganyiko mkubwa nchini katika utoaji taarifa za deni la taifa. Kuna usemi kuwa miluzi mingi huchanganya mwelekeo wa Mbwa.

Ndugai ni Spika, Balile ni Mwandishi wa Habari za Uchunguzi, Luoga ni Gavana, sasa nani ana taarifa sahihi za kutufanya tumuamini?

Ndugai amesema deni la taifa ni 70 tr, Balile (Gazeti la Jamhuri October 26, 2021) alisema ni 78 tr, Luoga anasema liko 27.9% halijafikia hata nusu ya kiwango cha kukopa.

Lipumba naye huenda akaibuka na takwimu zake, Mbatia naye anajifua kufanya uchunguzi ili aje Ki-NCCR, Tundu naye ataibuka kivyake. Baghosha!

Kwa mkanganyiko huu kama hauna sababu za kisiasa basi huenda mtu akatamani enzi ya Magufuli ya kudhibiti utoaji takwimu, kwa sababu kama nchi, tunatia aibu duniani, tunajipaka matope wenyewe, tunaonekana hatuna mifumo mizuri ya kitakwimu, utoaji taarifa nyeti, wala kumbukumbu sahihi za deni la taifa.

Hivi unawezaje kumlipa mdeni wako kama hujui kiasi sahihi anachokudai?

Magufuli alisema kazi ya urais ni ngumu, Nyerere alisema Ikulu ni mzigo, JK alisema Ikulu ni sawa na kulalia kitanda chenye kunguni wengi.

Kwa upande wa Ndugai, nadhani kauli yake imethibitisha kwamba ameamua kufanyakazi ya Msemaji Rasmi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (simjui ni nani).


Msome Balile hapa:
Balile: Magufuli katutenda, deni la nje lafikia shilingi Trillion 78 | JamiiForums


Msome Ndugai hapa:
Rais Samia 'ampiga' Spika Ndugai | JamiiForums


Gavana yeye alitoa ufafanuzi wake jana Jumatano Disemba 29, 2021 kwenye kipindi cha Power Breakfast kinachoendeshwa na Redio ya Clouds FM. (nimetafuta clip nimeikosa).

View attachment 2062566

View attachment 2062570

View attachment 2062577
Taswira zote kwa hisani ya google.
Hivi ile Sheria ya Takwimu hapa haifanyi kazi?
 
Hivi ile Sheria ya Takwimu hapa haifanyi kazi?
Si wanaharakati, wapinzani, media, watafiti na wafadhili waliungana kuichagiza serikali iipunguzie makali sheria ya takwimu waliyoiita kandamizi. Mimi ninaamini correct information is power.
 
Back
Top Bottom