Katiba imeshampa Ushindi Mgombea wa CCM kabla ya Uchaguzi, Vyama vingi Kiini macho

Katiba imeshampa Ushindi Mgombea wa CCM kabla ya Uchaguzi, Vyama vingi Kiini macho

Prof Koboko

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2020
Posts
350
Reaction score
2,550
Kuna sababu zaidi ya 99% kua mgombea wa CCM amepewa ushindi na katiba ya JMT kwa sababu za msingi zifuatazo, labda wananchi waamue wenyewe kutokujali katiba hii.

SABABU ZENYEWE
1. Mwenyekiti wa CCM na mngombea wa Urais ndiye anayewateua mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi na makamishna wake. Yaani kocha wa Yanga ateue waamuzi mchezo kati ya Yanga na Simba?

2. Matokeo ya Uchaguzi hayahojiwi Mahakamani. CCM wanajua kabisa kwamba hata wasiposhinda Mwenyekiti wa NEC akiamua kumtangaza mshindi ndio ingeshatoka hiyo na atakayehoji anaweza kudhibitiwa kisheria. Kwahiyo hapa Mwenyekiti anaweza kutangaza tu hata asiposhinda.

3. Katiba inamtambua Rais mpaka pale atakapoapishwa mpya.Kwahiyo haijalishi kua anagombea Urais bado yeye ni Rais na anaweza kufanya maamuzi yeyote ya nchi akiwa katika wadhifa huo. Yaani yeye ni Rais na hapo hapo ni mgombea na anatumia rasilimali zote za umma.
 
Inashagaza kuwa tangu upinzani uanze 1992 mpaka leo wapinzani wanashiriki uchaguzi bila kufanya marekebisho ya mambo kama hayo.
 
Inashagaza kuwa tangu upinzani uanze 1992 mpaka leo wapinzani wanashiriki uchaguzi bila kufanya marekebisho ya mambo kama hayo
Wapinzani wanafanyaje marekebisho wao kama wao.
 
Umeamua kukata tamaa siyo?

Awali, Andiko kama hili hatukuliona zaidi ya nyimbo nyingi kuhusu Msomi na nguli wa Sheria asiyemwachia Mungu maswala yake, ila hujipambania mwenyewe Mungu awe Pembeni kwanza.
 
Tume ipo huru na atakae teuliwa raisi hawezi kumfanya kitu na ili kuachishwa kazi kuna vigezo na masharti

Matokeo yanahojiwa mahamani acha kupotosha watu hapa!!

Kwan mkuu we ultaka uraisi ukome lini? af nani awe raisi kwa wakati huo?
 
Inashagaza kuwa tangu upinzani uanze 1992 mpaka leo wapinzani wanashiriki uchaguzi bila kufanya marekebisho ya mambo kama hayo
Tume huru imepigwa chini,katiba mpya imepigwa chini!
Upinzani watumie njia gani?Maana naona njia zote za kihalali bado CCM wanaweka bambi!

Imebaki njia moja tu ambayo haijatumika,"violence"!Hii kwakweli ni mbaya na sipendi itokee kabisaa ila njia hiyo huwa inazaa matunda!
 
Tume ipo huru na atakae teuliwa raisi hawezi kumfanya kitu na ili kuachishwa kazi kuna vigezo na masharti

Matokeo yanahojiwa mahamani acha kupotosha watu hapa!....
Hujui kama matokeo ya urais hayahojiwi mahakamani ?Unaishi nchi gani?Yaani akishatangazwa na tume ndio hivyo imepita hiyoo!
Umesahau yaliyotokea Zanzibar? Baada ya kuona Maalim Seif ameshashinda,wakaamua kufuta uchaguzi!

Eti wakasema uchaguzi umevurugika Zanzibar na wakatu huo huo kura zilipigwa za aina mbili,za ZEC na NEC na kituo ni kimoja na muda ni mmoja!Ila kura za ZEC zikafutwa na zile za NEC zikafanywa kuwa halali!Huu ni mfano tu kukuonesha wateuliwa wa tume wanamtumikia nani!
 
Not exactly,

Nakubaliana na wewe CCM imehodhi dola na katiba ( kwa sabab wao ndio waliokuwa itunga). Issue kwamba wanapata ushindi wa moja kwa moja kam unavosema si kwel.

They have something f to prove,

Opposition ya aina ya Tundu Lissu, critical with brain ni rahis sana kubadili system kwa ku mobilize mass demand. CCM wa jiandae na mabadiliko tu na wayakubali kwa mustakabali mwema wa Taifa letu
 
Huu mchezo wa siasa za Tanzania hauhitaji gwiji wa siasa. Bila mapendekezo ya katiba yaliyomo kwenye tume ya Warioba ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.

Ajabu bado kuna wapinzani kila uchaguzi wanashiriki huku wakijua wamefungwa miguu,mikono na midomo. Kama haitoshi awamu hii ni miezi 2 tu kati ya miezi 60 vyama vya siasa pinzani vinaporuhusiwa kufanya siasa.

Ukishazuiwa kufanya siasa utawafikiaje wananchi?
 
Ni ukwel mchungu, ukiachilia mbali hayo... Njia nzuri ya kupambana na adui cha Kwanza kubali uwezo wake alaf utafte udhaifu wake upitie hapo, CCM inatambua uwezo wa Chadema na inatambua udhaifu wao , na ndo mana Kwa miaka mitano wamepambana na Chadema kufa na kupona, miez hii miwili ya kampeni wanasuuuza tuu , mitambo yote imetegeshwa kuleta ushindi,....

Chadema haijui uwezo wa CCM na inatumia nguvu nyingi kutotaka kujua , yes they know some how udhaifu wa Kijani, but still they work hard to remain blindness , silaha kubwa Za CCM ni Katiba ya nchi, wananchi wa kijijini na wanawake , wazee na watu wa makamo, inashangaza kuona JPM anapita road to road akikutana na wananchi anasimama anaongea dk tano anatatua kero onspot, anajipatia shangwe anasepa.

Mashabiki wa Chadema Wengi ni watumishi wa uma hasa walimu, wasomi wasio na ajira, wakereketwa wa nje ya nchi and some how na vijana wa kitaa...Yeees.

Kundi hili ni la watu wenye exposure na ushawishi hasa kwenye social &digital platforms lakn ni very poor na ineffective kwenye kumpitisha mgombea.

Hawapigagi kura ni wachache sana watakaopanga foleni kuanzia asubh mpak sa kumi wakipigwa jua ili kusubir kupiga kura,
Kampeni zao za kuruka ruka na kutegemea vyombo vya habar viwafikishie ujumbe wananchi .

Wakat Wenzao wanafanya kila mbinu kuhakikisha wanashinda...wao kutwa ni kutukana na kushangilia helpless nyomi linalotokea kwenye mikutano yao huku wakibeza uwezo wa adui yao.
 
Hujui kama matokeo ya urais hayahojiwi mahakamani ?Unaishi nchi gani?Yaani akishatangazwa na tume ndio hivyo imepita hiyoo!
Umesahau yaliyotokea Zanzibar?Baada ya kuona Maalim Seif ameshashinda,wakaamua kufuta uchaguzi!Eti wakasema uchaguzi umevurugika Zanzibar na wakatu huo huo kura zilipigwa za aina mbili,za ZEC na NEC na kituo ni kimoja na muda ni mmoja!Ila kura za ZEC zikafutwa na zile za NEC zikafanywa kuwa halali!Huu ni mfano tu kukuonesha wateuliwa wa tume wanamtumikia nani!
kama hujui hata kama matokeo yanaojiwa mahakamani then wewe na uzi woko wote ni nyumbu

check your facts before writing utopolo hapa
 
kama hujui hata kama matokeo yanaojiwa mahakamani then wewe na uzi woko wote ni nyumbu

check your facts before writing utopolo hapa
Wewe mwenyewe jisahihishe,matokeo ya urais hayahojiwi mahakamani,tume ikishatangaza ndio imeisha hiyo!
 
Back
Top Bottom