Katiba inakupa uhuru wa kukosoa/kutoa maoni haikupi uhuru wa kutoa lugha za kuudhi na kuchonganisha

Katiba inakupa uhuru wa kukosoa/kutoa maoni haikupi uhuru wa kutoa lugha za kuudhi na kuchonganisha

Sana tu, waambie akitoka atakuwa kanyooka.Yule muota ndoto haoti tena siku hizi
Watu kama nyinyi ndio utakuta simu unaazima ili kupost huu uharo wako na Kula yako ni kwa jirani

In God we trust
 
Mkapa alirudia tusi mbele ya JPM kwa mara ya pili akiwatukana watanzania zaidi ya mil 6 kuwa ni wapumbavu na malofa,JPM akakenua meno akichekelea!Kwako hilo sio tusi wala lugha ya kuudhi!

Point of correction. Hakutukana watanzania. Aliwatukana wale wajinga na malofa. Sikusikia popote aliposema nyie watanzania ni wajinga na malofa. Ila kwa huyo zezeta wenu Tundu Lissu alimtaja Raisi Magufuli na Raisi Mstaafu mzee wetu Mwinyi waziwazi. Sijui ni mwanasheria wa wapi anayeweza kutoa kashfa kwa kutaja watu waziwazi. Watoto wa mjini wanasema anatafuta kiki. Ataipata tu.
 
Tundu lissu kweli anawatoa jasho ccm na mtukufu magufuli yaani hamna speech ya lissu ilokosa mjadala au kumpa kesi mara analipwa na acacia mara lawyer anaegopa kushtakiwa ......all i can say its the govt vs tundu the great lissu ....
 
Rafiki wewe naona huna mpya zaidi ya kupigia makofi kila atakacho kisema Lisu.Soma uchambuzi wangu hapo ndo utagundua hoja zote alizotoa ni za uongo na uchonganishi

Nimesoma uchambuzi wako lakini naona umelalia kwenye kujipendekeza tu kwa wenye madaraka. Hivi nikuulize ni lazima uishi kwa kujipendekeza kwa wanaume wenzio ndio watoto wako wafanikiwe kutoa makinikia chooni?
 
La msingi hapa kila mmoja ahukumiwe kwa makosa yake lakini siyo kufanya references za nani kafanya nini na kufanyiwa nini! Ni vema ukijua fulani kafanya kosa, mimi, wewe au ninyi tumchukulie hatua stahiki za kisheria na siyo kunyosheana vidole au kufanya makosa yaleyale waliyoyafanya wao. Huo utakuwa ni ujinga mara dufu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakitukana kina sizonje mnakenua meno ila lisu akisema ukweli mnamkamata .yani unamkamata mtu kwa kukuambia ukweli unasema ametoa lugha za kuudhi , ndio zitakua ni za kuudhi kwasababu hampendi kuambiwa ukweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu mtoa hoja,

Nadhani ufikiri tena kidogo angalau: Ujinga si tusi, ila upumbavu ni tusi. Kila mtu ni mjinga wa jambo fulani maishani hadi anakufa!!!!! Isipokuwa Ukitaka kulikuza neno ''mjinga'' ndo litakuwa tusi.
Pili: Kama Lissu amefanya uchochezi, ni vyema ikaainishwa kwamba kamchochea nani, na wapi, na kwa namna gani. Sina maana kuwa namsapoti kwa kusema misaada izuiwe, hapana. Nakataa kauli ya misaada kuzuiwa maana ikizuiwa, hata wananchi wake pia watapata shida maana baadhi ya maendeleo yatakwama. Hivyo, nadhani hapo angetafuta lugha ya ''busara'' kuwasilisha ujumbe wake.

Tatu: Mimi ni mwana CCM damu damu. Napinga kitendo cha viongozi wa upinzani kuweka ndani kila wakati ilhali sisi tukiendelea na mikutano yetu, tena mingine inafanyika nje, na tukumbuke mikutano ya nje ilipigwa marufuku. Wao wakifanya hata wa ndani wanakamatwa!!!!! Tunakosea, na jamii inaona.

Nne: Tukubaliane kutokukubaliana ktk baadhi ya hoja, japo kusituzuie kufanya kazi maana nchi ni yetu wote. Hoja za msingi wanazosema wapinzani tuzikubali tuzifanyie kazi nchi isonge mbele. Bila hawa wapinzani, tusingejua tunaibiwa madini, na waliposema miaka mingi huko nyuma, kwa ushabiki huu huu tuliwapinga na kuwatukana ''tumbili'' leo yamekuwa kweli.

Tano: Kimsingi, hakuna mwanadamu aliye mkamilifu, waweza kubali au kukataa. Na kama ndivyo ilivyo: Basi tukubali mtu yeyote kukosolewa. Labda kama tuna ''mahaba'' na hao walioko kwenye madaraka. Na bila kukosolewa, hatuwezi kujiona madhaifu yetu.

Mwisho: Hakuna wakati mgumu ktk maisha kama wakati unapokuwa kwenye ''kilele cha mafanikio'' Sifa Zitakuwa nyingi, na hukawii kuwa na kizunguzungu cha ufahari wa mafanikio na mwisho hujikuta umeanguka!!!!! Hivyo, wanaotukosoa, tusiwabeze na kuwaona hawafai. Tufanyie kazi yale ya msingi, yasiyofaa tuachane nayo.
Barikiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeongea hoja za msingi sana.........

Ingekuwa,wanaccm wote wana mawazo kama yako, hakika nchi hii isingefika hapa tulipo ambapo nchi ipo kwenye mfumo wa vyama vingi theoretically lakini practically tupo kwenye mfumo wa chama kimoja cha CCM.
 
Nimemsikia mwanasheria wa Lisu akiongea jana baada ya kesi ya Lisu kuahirishwa na yeye(Lisu) kurudishwa rumande.Napenda tu nimkumbushe huyu mama kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inampa mtanzania yeyote uhuru wa kutoa maoni na kukosoa.Lakini katiba hii haikupi uhuru wa kutoa maneno yenye kuudhi na kuchonganisha jamii.

Nikirejea kauli ya Lisu ambayo leo imemfikisha Rumande,alisikika akisema yafuatayo:

1. Alisema anawaomba wahisani wasimsaidie Rais kwa fedha,kwanza nimkosoe kitu kimoja wahisani hawamsaidii Rais wanawasaidia watanzania maskini.Hizo pesa za donors zikija hali Rais na familia yake ni kwa ajili ya watanzania wote wakiwemo na Iramba mashariki ambako ndiko jimboni kwake.

Sasa alipitisha karatasi akachukua maoni yetu wananchi kuwa hatutaki wahisani? Rais alichaguliwa na watanzani walio wengi, kwa kauli ile ya Lisu alitumwa na watanzania wa wapi? Maana ninajua watanzania walio wengi wanamuunga mkono Rais,Wanataka barabara,wanataka huduma za maji,Elimu na hospitali.

Hii ni kauli ya kuudhi.Mimi kama mtanzania nieudhika na kauli hii na nina imani wapo wengi kama mimi ambao pia wameudhiwa na hii kauli.Kutoa lugha ya kuudhi ni kosa kisheria

2. Bwana huyu pia alisikika akisema mawazo aliyotoa Rais Mwinyi ni ujinga? Hivi hili sio tusi? Unamuitaje mtu kuwa katoa mawazo ya kijinga kisa anatofautiana na wewe? Una uhakika gani kama hakuna mtanzania mwingine ambae angependa Rais Magufuli atawale miaka zaidi ya 10?

Unadhibitishaje hili bila kupata maoni ya wananchi? And then unapata authority wapi ya kuyaita mawazo ya Binadamu mwenzio ni ya kijinga? Ok fine let me agree with you kuwa ni ya kijinga and then Yenye akili/hekima ni yapi? na una uhakika upi kuwa watanzania walio wengi wana kuunga mkono kwa hayo yako unayo dhani ndio yana hekima? ,,,,,

Hapa napo kuna kosa la kujibia, Huyu bwana aliongea lugha ya kuudhi, kaniudhi mimi na Mtanzania mwenzangu ambao tuna mawazo kama ya mzee Mwinyi kwa kutuita tuna mawazo ya kijinga ,,,hili ni tusi pia.Huwezi kuniita kuwa nina mawazo ya kijinga wakati hakuna reference point inayonipa mawazo sahihi.

Ungeweza kuniita mjinga endapo ningeshindwa kujibu 1+1=2,,Hapo sawa coz kila mtu at some point anaweza kuwa mjinga wa jambo fulani.Lakini kwa hili la kutoa maoni and then UNAYAITA YA KIJINGA NI TUSI MUBASHARA.

Kama ni katiba, katiba sio msahafu kama wananchi wakitaka katiba ibadilishwe ili Rais aendelee kutawala miaka dahari na dahari hawawi wajinga kwa kufanya hivyo bali ni hekima coz hekima ndio inawaongoza kuamua hivyo kwa kuona potential alizo nazo Rais in comparison na other presidential candidates.

3. Halafu Bwana huyu alisikika akisema kuwa Rais kafanya ukabila katika teuzi zake,,,Alitoa tuhuma ambazo sio za kweli.Alitaja viongozi wachache ambao Rais aliwataeua and by coincidence wakawa wanatokea kanda ya ziwa.Lakini kuna teuzi nyingi tu Rais kafanya ambazo hazitoki kanda ya ziwa.

Naweza mtajia Teuzi kadhaa hapa: Waziri mkuu,Mh Mwigulu,Mh Kabudi, Mh Mbarawa,Mh Ummy,Mh Kigwangala etc ,....Actually wewe pia unaweza nisaidia kumalizia hii list na mwishoni utagundua kuwa huyu Bwana (Lisu) hakuwa na lengo jingine zaidi ya kuleta chuki za kikanda na kikabila.

Hili nalo ni kosa la kujibu.

Help us spread patriotism by your like and share.
Visit us at:Dr Magufuli For Better Tanzania
ahsante kwa kutufunua uelewa
 
Nimemsikia mwanasheria wa Lisu akiongea jana baada ya kesi ya Lisu kuahirishwa na yeye(Lisu) kurudishwa rumande.Napenda tu nimkumbushe huyu mama kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inampa mtanzania yeyote uhuru wa kutoa maoni na kukosoa.Lakini katiba hii haikupi uhuru wa kutoa maneno yenye kuudhi na kuchonganisha jamii.

Nikirejea kauli ya Lisu ambayo leo imemfikisha Rumande,alisikika akisema yafuatayo:

1. Alisema anawaomba wahisani wasimsaidie Rais kwa fedha,kwanza nimkosoe kitu kimoja wahisani hawamsaidii Rais wanawasaidia watanzania maskini.Hizo pesa za donors zikija hali Rais na familia yake ni kwa ajili ya watanzania wote wakiwemo na Iramba mashariki ambako ndiko jimboni kwake.

Sasa alipitisha karatasi akachukua maoni yetu wananchi kuwa hatutaki wahisani? Rais alichaguliwa na watanzani walio wengi, kwa kauli ile ya Lisu alitumwa na watanzania wa wapi? Maana ninajua watanzania walio wengi wanamuunga mkono Rais,Wanataka barabara,wanataka huduma za maji,Elimu na hospitali.

Hii ni kauli ya kuudhi.Mimi kama mtanzania nieudhika na kauli hii na nina imani wapo wengi kama mimi ambao pia wameudhiwa na hii kauli.Kutoa lugha ya kuudhi ni kosa kisheria

2. Bwana huyu pia alisikika akisema mawazo aliyotoa Rais Mwinyi ni ujinga? Hivi hili sio tusi? Unamuitaje mtu kuwa katoa mawazo ya kijinga kisa anatofautiana na wewe? Una uhakika gani kama hakuna mtanzania mwingine ambae angependa Rais Magufuli atawale miaka zaidi ya 10?

Unadhibitishaje hili bila kupata maoni ya wananchi? And then unapata authority wapi ya kuyaita mawazo ya Binadamu mwenzio ni ya kijinga? Ok fine let me agree with you kuwa ni ya kijinga and then Yenye akili/hekima ni yapi? na una uhakika upi kuwa watanzania walio wengi wana kuunga mkono kwa hayo yako unayo dhani ndio yana hekima? ,,,,,

Hapa napo kuna kosa la kujibia, Huyu bwana aliongea lugha ya kuudhi, kaniudhi mimi na Mtanzania mwenzangu ambao tuna mawazo kama ya mzee Mwinyi kwa kutuita tuna mawazo ya kijinga ,,,hili ni tusi pia.Huwezi kuniita kuwa nina mawazo ya kijinga wakati hakuna reference point inayonipa mawazo sahihi.

Ungeweza kuniita mjinga endapo ningeshindwa kujibu 1+1=2,,Hapo sawa coz kila mtu at some point anaweza kuwa mjinga wa jambo fulani.Lakini kwa hili la kutoa maoni and then UNAYAITA YA KIJINGA NI TUSI MUBASHARA.

Kama ni katiba, katiba sio msahafu kama wananchi wakitaka katiba ibadilishwe ili Rais aendelee kutawala miaka dahari na dahari hawawi wajinga kwa kufanya hivyo bali ni hekima coz hekima ndio inawaongoza kuamua hivyo kwa kuona potential alizo nazo Rais in comparison na other presidential candidates.

3. Halafu Bwana huyu alisikika akisema kuwa Rais kafanya ukabila katika teuzi zake,,,Alitoa tuhuma ambazo sio za kweli.Alitaja viongozi wachache ambao Rais aliwataeua and by coincidence wakawa wanatokea kanda ya ziwa.Lakini kuna teuzi nyingi tu Rais kafanya ambazo hazitoki kanda ya ziwa.

Naweza mtajia Teuzi kadhaa hapa: Waziri mkuu,Mh Mwigulu,Mh Kabudi, Mh Mbarawa,Mh Ummy,Mh Kigwangala etc ,....Actually wewe pia unaweza nisaidia kumalizia hii list na mwishoni utagundua kuwa huyu Bwana (Lisu) hakuwa na lengo jingine zaidi ya kuleta chuki za kikanda na kikabila.

Hili nalo ni kosa la kujibu.

Help us spread patriotism by your like and share.
Visit us at:Dr Magufuli For Better Tanzania
ahsante kwa kutufunua uelewa
 
1. Tundu lisu alioposema wahisani wasusie, kwa mwenye akili fupi hawezi kuona usahihi wa Lisu.

Haiwezekani tuendelee kubebeshwa mizigo ya madeni ambayo tutalipa sisi walipa kodi, au kuhesabiwa tumepokea misaada ambayo matumizi yake hayafanyiki kwa mujibu wa vipaumbele na kanuni za taifa.

Nakupa mifano hii hapa chini.
a) Ninaomba useme hapa, ni lini bunge lilipitisha badgeti ya kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa chato?
b) Lini bunge lilipitisha budget ya kununua ndege zinazonunuliwa kwa cash huku watu wakifa hosptailni kwa kukosa oxygen?
c) Ni wataalamu gani walifanya maamuzi ya kuweka vipaumbele vya kiuchumi na kjamii katika hayo masuala?
d) Wewe unaona ni halali Tanzania izidi kuingia katika madeni na matumizi ya raslimali yasiyokuwa na tija lakini sisi na watoto wetu waendelee kubeba zigo la kodi kulipa hayo madeni?
Nimtu mwenye ufahamu tu ndiye anaweze kuona upeo wa Lisu.

2. Ujinga ni kukosa ufahamu, maarifa ama taarifa sahihi. No one is informed in everything. Mwinyi aliposema alionyesha kukosa ufahamu.

Mtu mjinga anaondolewa ujinga kupewa taarifa sahihi na si kwa kutokuambiwa kwamba hajui.

Huwezi kulazimisha watu wote wasikie mtu anafurunda halafu eti waseme hayo ndiyo maarifa haswa na kupiga makofi. Unaweze kupongeza ujinga ukiwa mjinga na wewe ama mnafiki. Lakini waache wenye uelewa na wasio wanafiki wamsahihishe ili aondokane na ujinga. Tatizo liko kwapi?

a) Tunaposema adui wa Tanzania ni umaskini, maradhi, rushwa na ujinga, huwa tunawatukana Watanzania? Naomba uwe serious .

b) Lisu amesema Mwniy amenena ujinga. Nani mlalamikaji katika hilo shauri la mwingi kuambiwa kanena ujinga?

Wasaidie wasiotaka kuambiwa wamenena ujinga wasinene ujinga.

Ni yupi anayetahili kukamatwa kwa uahrifu wa maneno kati ya mtu anayesema "MTU ANAYETETEA UAHRIFU NI MJINGA", na ule anayesema " WATU WANAOTETEA SHERIA, HAKI NA UHURU WA BINADAMU, DEMOKSRASIA , RASLIMALI NA MAENDELEO YA TAIFA NI MALOFA NA MPAUMBAVU"????

3. Kwa hiyo wewe unataka watu wawe na uhuru wa kukosoa kikatiba lakini hutaki raisi akosolewe?

Anapoambiwa aangalie tribalism na nepotism zinaligawa taifa anakuwa anatukanwa?

Nyerere alipoambiwa anapendelea watu wa Kazkazini aliwatukana na kuwakamata walalamikaji na kuwatia ndani?

Unapashwa kuelewa kwamba "image analysis", ni strength kwa kila kiongozi makini?

Ukituhumiwa, angalia hilo eneo na ama alitolee ufafanuzi ama arekebishe. Kuwatia watu pingu kwa kuwa wamekukosoa tena kwa nji aza amani ni dalili ya tatizo kubwa kuliko lililoko mezani kwa saas.

Kushabikia suppression za feelings za watu na kuendesha mambo kwa ubabe mkitegemea bunduki, zinaweza kuleta machafuko makubwa sana hapa nchini.

MATUMIZI YA BUNDUKI HAJAWAHI KUJENGA MTANGAMANO WA KIJAMII NA WALA HAYAJAWAHI KUWA SIASA SAFI WALA UONGOZI BORA.
Maelezo mengi but no sense in it
 
meanwhile katiba ina mruhusu JPM kuita wapinzani VILAZA.
Kilaza ni kivumishi cha sifa,,,Alimaanisha wanashindwa kuelewa kuwa katiba hairuhusu mtu kutumia lugha za kuudhi na kuchonganisha ,Ni hawa hawa pia hawajui kuwa Tanzania Ilisha kombolewa mikononi mwa wakoloni hata CIVICS/URAIA Hawajui .Mtu asiejua kitu na hataki kuelimishwa wewe ungemuitaje kwa mfano?
 
Back
Top Bottom