Katiba inasemaje kuhusu uteuzi wa Bashiru Ally?

MIGNON

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2009
Posts
4,108
Reaction score
5,110
Pamekuwa na kambi mbili katika uteuzi huu na msaada wa wadau wa katiba na sheria unaweza kutupa mwanga.

Najua kuna jukwaa la mambo ya sheria lakini uteuzi huu una athari za kisiasa ambazo inawezekana kwa sasa hazipo wazi.

Tusaidieni tujue ukweli ni upi?
 
Sijui unataka kujua nini. Kikatiba raisi anayo haki ya kumteua Katibu kiongozi.

Kama matakwa ya kikatiba yamekidhi huenda ya kisheria yamekidhi pia.

Anayaeteuliwa anatakiwa awe mwananchi. Aliyeteuliwa ni Nshomile Mtanzania halisi wala si Mganda Kyaka.

Hii ina maana naye amekidhi matakwa ya kikatiba na kwa hiyo ya kisheria. Una swali lingine?
 
Naomba unisome vizuri.JF ni sehemu ya kuelimishana nami najua kuwa atakalo rais liwe huwa linakuwa ila Kikatiba na kisheria.Ningetegemea uweke vifungu vya katiba/sheria ili tuwe na mjadala mzuri!
 
..alikuwa mtumishi wa chama.

..na ngazi ya utumishi aliyoteuliwa hairuhusu wahusika kujihusisha na siasa.

..Magufuli katoa boko.
Naomba utuwekee ibara ya katiba ya JMT inayotoa sifa za mtu anayestahili kuteuliwa kuwa CS
 
Iko mfukoni na maamuzi yapo kichwani, na hatupangiani, najiuliza mbona kama tunamtania Muumba kwa kushika vitabu vyake na kujiapiza wakati hatuyafuati tuliokula kiapo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Maumivu ya kichwa uanza pole pole........... Mwishowe Rais wa maisha
 
..hata nikikuwekea utabisha.

..kwako wewe Magufuli hakosei, na ni muhimu kuliko katiba, pamoja na nchi.
Ahaaa, acha kuwa na ubishi wa kitoto. Weka ibara gani imekiukwa ili tujadili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…