Katiba Mpya: Dk. Slaa awasilisha maboksi 17 - Yanahusu maoni ya Katiba, Warioba agoma

Katiba Mpya: Dk. Slaa awasilisha maboksi 17 - Yanahusu maoni ya Katiba, Warioba agoma

WanaJF!

Dr Slaa amepata PIGO la mwaka baada ya tume ya katiba inayoongozwa na jaji mstaafu Joseph Warioba kukataa kupokea maboksi yapatayo 17 yanayo daiwa kuwa na maoni yaliyo kusanywa na CHADEMA kutoka kwa wananchi, badala yake tume hiyo imepokea vitabu viwili tu vya randama kwa ajili ya maoni hayo.

Dr Slaa pamoja na jitihada zake zote za kufanya mikutano ya kwenye majukwaa na kupaa na "chopa" ameambulia patupu, kwa kuwa Dr Slaa pamoja na viongozi wengine wa CHADEMA walikuwa wakifanya marudio ya ile kazi ambayo tume ya jaji Warioba ya ukusanyaji wa maoni mpaka kufikia hatua ya kuandaa rasimu ya katiba mpya. Sasa iweje leo tume ipokee maboksi 17?

Aidha, Dr Slaa pamoja na viongozi wengine wa CHADEMA wanafahamu fika namna ambavyo mabaraza ya kikatiba yanavyopaswa kuendesha shughuli zake za ukusanyaji wa maoni, lakini kwa kuwa CHADEMA imezoea UKAIDI, ikaamua kufanya shughuli hiyo ya ukusanyaji maoni kwa taratibu zake yenyewe, matokeo yake ndio haya ya kukataliwa kupokelewa kwa maboksi 17 ya maoni, ingawa yalibebwa kwenye "Range Rover Sport"ambayo ndani yake alikuwamo Dr Slaa.

Dr Slaa, JIFUNZE KUFATA TARATIBU.

pigo kwa wananchi wote si kwa slaa pekee.
 
mbona gambaz mnaweweseka sn na mda bado! kwani hizo randama 2 si maoni ya cdm? hayo mabox ni ushahidi tu wa hzo randama
 
hivi dr slaa bado yuko hai,maana kafulia kisiasa na akili.

Wahi kapange foleni Lumumba. Kesho wamesema watoa buku saba7 watakuwa na watu wengi. Hivyo kesha mlangoni maana unatumikia kitu usichokielewa
 
Zanzibar mlifika lakini?sipendi ushabiki
#Ex Tanzania Simper aliquid novi#
 
Mimi nilivyoelewa ni kwamba maoni hayo yalichukuliwa na kuandikwa kwenye vitabu viwili ambavyo Dr. aliviwakilisha na hayo mabox ni kama ushahidi pindi tume ikipenda kujilidhisha na sio kama wengine wanavyotaka kuaminisha wengine kwamba maoni yamekataliwa
 
siasa bwana mhe. Alikua kwenye ''range rover''. Alipowasilisha hayo maoni.

Zito alisema tusiwaamini wanasiasa.

'' Mr. politician practice what you preach'
 

Kuhusu Kingunge
Akizungumzia kauli ya Kingunge Ngombale- Mwiru, aliyoitoa juzi kuhusu umuhimu wa serikali mbili, Dk. Slaa alisema Watanzania wanapaswa kumsamehe mzee Kingunge kwa kuwa sasa amechoka.

Yaani Slaa anamwambi age-mate wake kuwa amechoka!!!

Naona Slaa anajitahidi kupoliticize zoezi zima la Katiba Mpya. Katiba mpya isitumiwe kama political capital...
 
Katiba mpya mtaisikia kwenye bomba tu, hii ndo ccm bwana..!
 
Katiba mpya mtaisikia kwenye bomba tu, hii ndo ccm bwana..!

Tunaelewa hivo Sio mpaka tuambiwe! Ila hili swala ni la kitaifa zaidi ingawa Ccm mnataka kulimiliki Hilo! Ila Labda wewe uwe kwenye system ya hao mtakaofaidika lakini Kama katiba ikija mbovu yani hii itakua hasara ata kwako pia na jamii yako!
 
Yani hayo maboksi ni bora Tume ingayapokea lakini kuyakataa na kuyaacha yabaki kwa Cdm ni kosa kubwa sana! Yani huo ni ushahidi wa kutosha!
 
Tunaelewa hivo Sio mpaka tuambiwe! Ila hili swala ni la kitaifa zaidi ingawa Ccm mnataka kulimiliki Hilo! Ila Labda wewe uwe kwenye system ya hao mtakaofaidika lakini Kama katiba ikija mbovu yani hii itakua hasara ata kwako pia na jamii yako!
Nani wa kujikaanga na mafuta yake mwenyewe? Hata kama wewe ndo ungekuwa JK bado usingekubali kuwa na katiba safi kwa maana ni kitanzi kwako..! Hapa ni kilichopo ni kuongeza kasi ya M4C ili tutwae nchi in 2015 baada ya hapo ndo tutengeneze katiba iliyoenda shule..! Expect the least from MAGAMBA GROUP OF COMPANIES
 
siasa bwana mhe. Alikua kwenye ''range rover''. Alipowasilisha hayo maoni.

Zito alisema tusiwaamini wanasiasa.

'' Mr. politician practice what you preach'
Mkuu umeona eehhh wote hawa ni waizi wanatutumia kama daraja tu......
 
Hawa watu kusema ukweli kwao dhambi.

Na mbaya zaidi Gazeti la Tanzania Daima maeneo mengi halipatikana wamekwisha linunua ili watu wengi wasisome habari hii;

Naishauri tanzania Daima kurudia habari hii iliweze kusomeka kwa wengi na kuaanza kutambua Unafiki wa Warioba na Tume yake ili siku ya siku mambo yakiendea kombo tuje pakuanzia.



Kuhusu idadi ya watu waliotoa maoni yaliyowasilishwa jana, Dk. Slaa alisema hadi juzi walipokuwa wakifunga randama, kulikuwa na watu zaidi ya milioni 3.4 waliotoa maoni kwa njia mbalimbali.

CDM wanatakiwa na wao kuanza kusambaza kilichomo kwenye Randama waliyoikabidhi Wairoba na tume yake ili wakifanya uchakachuaji watu 3.4milioni waweze kupaza sauti kufikisha wang'wi wa hapana mpaka pale magogoni - 2015.




Aidha, Dk. Slaa alisikitishwa na utaratibu wa tume hiyo kushindwa kuwa na mpango maalumu wa kupokea maoni na kuweka kumbukumbu ya upokeaji huo.

“Sijui kama hawa watu walijipanga juu ya upokeaji wa maoni, angalia sisi kama tusingelazimisha watugongee muhuri kwa ajili ya uthibitisho wa upokeaji tungeondoka hivi hivi, sasa hali hii wamefanyiwa watu wangapi ambao hawana kitabu cha kusaini?” alihoji Dk. Slaa.


Usiri wa Tume kwa waandishi
Dk. Slaa pia alisema licha ya tume kuweka suala la uwazi kuwa ni moja ya tunu za taifa, bado imeshindwa kudhihirisha uwazi huo kwa kuwazuia waandishi wa habari kuingia na kushuhudia makabidhiano yanayofanywa katika ofisi za tume.
 
Nimesikitishwa na kushangazwa na kichwa cha habari cha gazeti la Majira la leo jumapili tarehe 01/09/2013 kinachosomeka "Chadema yakwama".Hii habari inahusu uamuzi wa tume ya kukusanya maoni ya katba kukataa mapendekezo ya CHADEMA ambayo kimsingi ni maoni ya wananchi na si maoni ya CHADEMA kama chama cha siasa.

Mimi naomba kumuuliza mhariri atuambie katika uamuzi huo wa tume ni CHADEMA au ni Demokrasia ndio imekwama?Katika hali akili ya kawaida tu(commonsense) ukweli hapa waliokwamishwa ni wananchi waliotoa maoni yao na si CHADEMA.Kwa maneno mengine wananchi waliotoa maoni yao "wamepuuzwa" na si CHADEMA.Pia ikumbukwe kuwa idadi ya wananchi waliotoa maoni hayo yaliyokuwa kwenye maboksi 17 ni takribani watu milioni 3.5.K

Kwa kuzingatia ukweli huu, ndio napohoji uwezo na uzalendo wa huyu mhariri.Lakini pia inawezekana ndio ule mwendelezo wa waandishi wa habari kutumika kisiasa kwa malengo ya wanasiasa na vyama vyao.Haiingii akilini kwa mwandishi mzalendo kuandika habari ile "kishabiki" kiasi kile!

Waandishi wa habari mtende haki na mjue mna mchango mkubwa katika maendeleo na ustawi wa hii nchi katika kila nyanja iwe siasa,uchumi,elimu,jamii n.k.
 
Tatizo ni pale njaa inapohama toka tumboni na kukimbilia kichwani. Usiombe hali hiyo ikukute, unaweza kula mpaka wanao!
 
Tatizo ni pale njaa inapohama toka tumboni na kukimbilia kichwani. Usiombe hali hiyo ikukute, unaweza kula mpaka wanao!
kuu ni kweli aisee....dah INASIKITISHA mno.sasa katiba itakuwa kwa maslahi ua magamba. ..
Kweli magamba wametawala nchi.ukizingatia policcm nao wana wapa support kubwa.. . ..basi jiyo katiba mpya haitakuwa na mplapya..mambo yatakuwa ni yale yale.
 
Mhariri wa Majira si mzalendo, mtizamo wa CDM?? :tape::tape::tape::tape::tape::tape:
 
Hawa ndiyo wahariri na waandishi wa habari wanaotakiwa na ccm, Akitokea shujaa na msemakweli kama Jerry Muro ccm humshughulikia haraka na kubaki na mapanki kama huyu wa Majira na wengine wenye akili za kiccm.
 
Back
Top Bottom