Aaron
JF-Expert Member
- Nov 18, 2010
- 3,019
- 4,693
WanaJF!
Dr Slaa amepata PIGO la mwaka baada ya tume ya katiba inayoongozwa na jaji mstaafu Joseph Warioba kukataa kupokea maboksi yapatayo 17 yanayo daiwa kuwa na maoni yaliyo kusanywa na CHADEMA kutoka kwa wananchi, badala yake tume hiyo imepokea vitabu viwili tu vya randama kwa ajili ya maoni hayo.
Dr Slaa pamoja na jitihada zake zote za kufanya mikutano ya kwenye majukwaa na kupaa na "chopa" ameambulia patupu, kwa kuwa Dr Slaa pamoja na viongozi wengine wa CHADEMA walikuwa wakifanya marudio ya ile kazi ambayo tume ya jaji Warioba ya ukusanyaji wa maoni mpaka kufikia hatua ya kuandaa rasimu ya katiba mpya. Sasa iweje leo tume ipokee maboksi 17?
Aidha, Dr Slaa pamoja na viongozi wengine wa CHADEMA wanafahamu fika namna ambavyo mabaraza ya kikatiba yanavyopaswa kuendesha shughuli zake za ukusanyaji wa maoni, lakini kwa kuwa CHADEMA imezoea UKAIDI, ikaamua kufanya shughuli hiyo ya ukusanyaji maoni kwa taratibu zake yenyewe, matokeo yake ndio haya ya kukataliwa kupokelewa kwa maboksi 17 ya maoni, ingawa yalibebwa kwenye "Range Rover Sport"ambayo ndani yake alikuwamo Dr Slaa.
Dr Slaa, JIFUNZE KUFATA TARATIBU.
pigo kwa wananchi wote si kwa slaa pekee.