Lipumba na Seif lazima tuwaogope kama tunavyoogopa CCM. Wapo tayari kwa lolote, ili wao na familia zao waishi maisha mazuri.
anajishaua tu lipumba. ccm ilisimama kwa miguu yake wala haikuhitaji mbeleko za mtu yeyote. zile ni siasa za maji taka ili waislam wamwonee huruma. kwanza hata elimu ya dini ya kiislam haijui
Vipi hebu tudondoshee kaushahidi ka video mwanangu akikiri naye alimbeba Kikwete na CCM baada ya jahazi kuelekea kuzama kama tulivyomuona Lipumba akikiri na kama tulivyoona ndoa ya mkeka kule visiwani.
Hivi Lipumba aliposema jahazi lilikuwa linaelekea kuzama na CCM na Kikwete wangeshindwa si alikuwa anamaanisha kushindwa na Dkt. Slaa na CHADEMA!
Sasa mbona unapingana na profesa majalala anayetumika na CCM bhana, acha hizo bhana, usiende kinyume na mafunzo ya profesa, kutumika na CCM.
Vipi hebu tudondoshee kaushahidi ka video mwanangu akikiri naye alimbeba Kikwete na CCM baada ya jahazi kuelekea kuzama kama tulivyomuona Lipumba akikiri na kama tulivyoona ndoa ya mkeka kule visiwani.
Hivi Lipumba aliposema jahazi lilikuwa linaelekea kuzama na CCM na Kikwete wangeshindwa si alikuwa anamaanisha kushindwa na Dkt. Slaa na CHADEMA!
Sasa mbona unapingana na profesa majalala anayetumika na CCM bhana, acha hizo bhana, usiende kinyume na mafunzo ya profesa, kutumika na CCM.
Hapa usitegee arudi kukujibu.
Salute Chief!
Mimi kwangu ni maajabu kusikia kuwa Haruna Lipumba ni profesa hasa wa kusoma shuleni na baadaye chuoni. Kipindi cha mwanzo nilidhani ni class moja na Prof. Maji Marefu
Wenzangu wanabodi, hususan wale waliberali, turudini kwenye ile hoja nyingine, maana mntaka kutumia 'kombora' la uliberali kama exit ya zile tuhuma nyeti zinazowakabili CUF na hasa mwenyekiti wenu na mgombea urais wa maisha, Profesa Ibrahim Haruna Lipumba, kuwa;
1. Ni washirika wakubwa wa CCM kiasi mlijitoa mhanga, mkaligawanya taifa kwa misingi ya udini, ili CCM inusurike kuondoka madarakani iendelee kutawala.
2. Profesa Lipumba ni kati ya viongozi wa siasa wanaopaswa kuogopwa kama ukoma hapa nchini kutokana na kuwa na malengo ya kuwagawa Watanzania (wanaopendana kama ndugu) katika misingi ya imani za dini, hasa uislamu na ukristo. Inaonekana hata hatambui haki za watu wenye imani za dini zingine tofauti na hizo mbili na wapagani.
Ni mtu hatari sana huyu!
Lakini katika hali inayoonesha au kudhihirisha kumkoma nyani gidari...Tume ya Katiba Mpya, kupitia rasimu yake ya juzi, imepigilia msumari, hasa katika ibara ya 75(h)...
Ibara hiyo inayozungumzia sifa za mtu kuwa rais inasema;
Mtu atakuwa na sifa ya kuchaguliwa kushika nafasi ya kushika madaraka ya Rais wa Jamhuri ya Muungano, ikiwa;
(h) Sera ZAKE au sera za CHAMA CHAKE, si za mrengo wa kuligawa taifa kwa misingi ya ukabila, udini, rangi au jinsia.
Wandugu wangu, hapo kwenye herufi kubwa msisitizo ni wa kwangu. Lakini hapa CUF ambao siku za hivi karibuni wameskikika wakililia 'utamu' wa kuwa mojawapo ya vyama vya upinzani, wakati keki yao walishaila baada ya kuamua kuungana na CCM kisirisiri kwenye uchaguzi mkuu kama alivyotoboa Profesa Lipumba kwenye ule mkanda wake wa udini na wakaungana na CCM kwanza sirini, kisha hadharani huko Zanzibar, hawachomoki.
Hadi tunavyozungumza hapa, si CUF wala Profesa Lipumba waliotoa hoja za maana juu ya ule mkanda wa video unaomuonesha Prof mzima akifanya kazi ambayo hata mtoto wa chekechea, akisimuliwa atasema 'hakuna maana ya kwenda shule, kama elimu haijamsaidia hata huyu profesa...kuwagawa watu...kwa udini'.
Atashindwa nini kutugawa kwa ushia, sunni, ukabila, kisha maeneo!
Tunashukuru watu wa tume, katika eneo hili, hakuna Mtanzania mpenda nchi yake, atapingana nanyi hapo. Ingawa kunasikika minong'oni kuwa Profesa na watu wake watakataa, maana ndiyo uchochoro wanaotaka tena kuutumia kuibakisha CCM madarakani, maana wao kama wao, hawawezi kushinda. Wanajua.
Watanzania wote, bila kujali tofauti zetu zingine tuiunge mkono hii ibara hasa hicho kipengele.
Wote wataanguka anguko moja, maana wako pamoja.
Vp familia yake imempa baraka ya kugombea tena?
una kizunguzungu wewe, mbona hapo kwenye red chadema imekufa??? au ndio zile zile za kuchukua tuhuma zenu kuwageuzia wenzenu
mke wake aliporwa na slaa
(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa
Katiba hii na sheria za nchi;
(b) ni mwenye akili timamu;
(c) angalau mmoja kati ya wazazi wake ni raia wa kuzaliwa wa
Jamhuri ya Muungano;
(d) wakati wa kugombea, ana umri usiopungua miaka arobaini;
(e) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri
ya Muungano kwa mujibu wa Katiba hii;
(f) anayo angalau shahada ya kwanza ya chuo kikuu
kinachotambuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi;
(g) ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha
siasa au mgombea huru;
(h) sera zake au sera za chama chake si za mrengo wa kuligawa
Taifa kwa misingi ya ukabila, udini, rangi au jinsia;
(i) ni mwadilifu na anafuata maadili ya Taifa;
(j) mwenendo wake binafsi hautiliwi shaka na jamii;
(k) hajatiwa hatiani kwa kosa lolote la jinailinalohusu kukosa
uaminifu; na
(l) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi
Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa
kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.
IBARA HIYO YA 75 KUHUSU SIFA ZA MGOMBEA URAIS NDIZO ZINAZOMMALIZA KABISA DR SLAA KWANI SI MWADILIFU, MAISHA YAKE BINAFSI YANATIA SHAKA KUTOKANA NA KUPORA WAKE ZA WATU NA CHAMA CHAKE CHA CHADEMA KINA SERA ZA MAJIMBO AMBAYO IMEPAMBANULIWA ZAIDI NA WARIOBA KUWA ZINA MWELEKEO WA KULIGAWA TAIFA KWA MISINGI YA UDINI, UKABILA NA UKANDA SAMBAMBA NA KUGAWA RASLIMALI ZA TAIFA
subutu? eti tanga ipo kanda ya kaskazini. tanga haipo huko. chadema wamegawa kanda zao kwa misingi ya udini zaidi