Katiba Mpya: Kwanini CCM hawataridhia kirahisi

Katiba Mpya: Kwanini CCM hawataridhia kirahisi

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Pamoja na kuwa Mama Samia anaweza kuwa anayo nia njema na ya dhati kuhusiana na haki, uhuru na usawa wa watu, kizingiti kitaendelea kuwa wale wahafidhina wanaomzunguka.

CCM hao watakuwa ndiyo walio waasisi wa ile salamu yetu pendwa ya "Kazi Iendelee" na hata kile kidokezo chetu cha "JPM = Samia" kwa maana halisi.

Pamoja na jitihada zake binafsi alizokwisha onyesha yawezekana bado atakuwa kwenye mashinikizo makubwa kuuishi u mwendazake.

Lengo na madhumuni ya wahafidhina hao yumkini ni kuendeleza misimamo ya bwana JPM bila JPM kuwepo. Kikubwa zaidi kikiwa ni kuyalinda maslahi yao binafsi.

Mengine tunayoyaona yatakuwa ni janja ya nyani tu.

Yatambulike mambo ya msingi yaliyokuwa katika rasimu ya katiba ya Warioba:

IMG_20210704_223949_912.jpg

Hii ni kama ambavyo mjumbe huyu ndugu mjumbe Domhome (heshima kwako sana mkuu) alivyoyaweka kwa ufasaha kabisa.

Kwa hali kama hiyo, ni CCM gani katika waliojimilikisha hii nchi na vyote vilivyomo watakaoridhia mchakato wenye rasimu yenye maudhui kama hayo kirahisi bila ya kuwapo na mpambano wa haja kweli kweli au wenye resistance ya kutosha?

Pana haja ya kupanua wigo wa washirika katika vita vitakatifu hivi vyenye vionjo vyote vya kuturejeshea yote tuliyokuwa tumepokwa na kujikuta tumekuwa:

Wabambikiziwa kesi, wahanga wa dhuluma, kubebeshwa mizigo ya kodi zisizotuhusu, Ku, kubagazwa nk.

Hayupo asiye pendwa usawa wala uwepo wa utawala ambapo mihimili yote itakuwa na uhuru kamili.

Asasi za dini, kiraia, wana harakati na hata vyama vingine vya siasa vitakavyokuwa tayari.

Uelekeo ni wazi, kulishiriki vuguvugu hili ni thwawabu.

Ninawasilisha!
 
Nakazia:

 
Pamoja na kuwa Mama Samia anaweza kuwa anayo nia njema na ya dhati kuhusiana na haki, uhuru na usawa wa watu, kizingiti kitaendelea kuwa wale wahafidhina wanaomzunguka.

CCM hao watakuwa ndiyo walio waasisi wa ile salamu yetu pendwa ya "Kazi Iendelee" na hata kile kidokezo chetu cha "JPM = Samia" kwa maana halisi.

Pamoja na jitihada zake binafsi alizokwisha onyesha yawezekana bado atakuwa kwenye mashinikizo makubwa kuuishi u mwendazake.

Lengo na madhumuni la wahafidhina hao ilikuwa ni kuendeleza misimamo ya bwana JPM bila JPM kuwepo. Kikubwa zaidi kikiwa ni kuyalinda maslahi yao binafsi.

Mengine tunayoyaona yatakuwa ni janja ya nyani tu.

Yatambulike mambo ya msingi yaliyokuwa katika rasimu ya katiba ya Warioba:


Hii ni kama ambavyo mjumbe huyu bwana Domhome (heshima kwako sana mkuu) alivyoyaweka kwa ufasaha kabisa.

Kwa hali kama hiyo, ni CCM gani katika waliojimilikisha hii nchi na vyote vilivyomo watakaoridhia mchakato wenye rasimu yenye maudhui kama hayo kirahisi bila ya kuwapo na mpambano wa haja kweli kweli wa kutosha resist?

Pana haja ya kupanua wigo wa washirika katika vita vitakatifu hivi vyenye vionjo vyote vya kuturejeshea yote tuliyokuwa tumepokwa na kujikuta tumekuwa:

Wabambikiziwa kesi, wahanga wa dhuluma, kubebeshwa mizigo ya kodi zisizotuhusu, Ku, kubagazwa nk.

Hayupo asiye pendwa usawa wala uwepo wa utawala ambapo mihimili yote itakuwa na uhuru kamili.

Asasi za dini, kiraia, wana harakati na hata vyama vingine vya siasa vitakavyokuwa tayari.

Uelekeo ni wazi, kulishiriki vuguvugu hili ni thwawabu.

Ninawasilisha!

Cc: BAK
Hata mtoto wakati wa kuachishwa ziwa la mama yake huwa ni ngumu sana lakini mwisho anazoea. Watazoea tu
 
CCM hawawezi kubali sababu , viwanja ni vyao , masoko yote Tz yao,
 
Mchakato wa katiba kama kuanza labda 2025 kwa sasa wanaharakati wawe wapole tu.

Inafahamika kuwa ni hila za CCM kutaka kurefusha suala la katiba mpya bila ukomo kwa sababu wao ni wanufaika wa katiba iliyopo.

Kwamba CCM wanadhani kuwa:

1. Wanaotaka katiba mpya ni wastaarabu na kwamba kwa kukomaliwa watakuwa wapole tu.
2. Wanaotaka katiba mpya watasusia chaguzi za 2024/25.

Kwamba kwa mawili hayo yatawaacha CCM madarakani pia hata baada ya 2025.

Kumbuka ni inafahamika kuwa katiba mpya haiwezi kupendwa na walioko madarakani. Ila ni vizuri wakafahamu zama hizi ni nyingine:

#1. Safari hii kama watawala wanachagua kiumane, kitaumana. Haturudi nyuma.

#2. Safari hii kususia chaguzi maana yake ni kuwa "chaguzi hazifanyiki."


Tunajua lugha mbili hizi mtazielewa tu.
 
Inafahamika kuwa ni hila za CCM kutaka kurefusha suala la katiba mpya bila ukomo kwa sababu wao ni wanufaika wa katiba iliyopo.

Kwamba CCM wanadhani kuwa:

1. Wanaotaka katiba mpya ni wastaarabu na kwamba kwa kukomaliwa watakuwa wapole tu.
2. Wanaotaka katiba mpya watasusia chaguzi za 2024/25.

Kwamba kwa mawili hayo yatawaacha CCM madarakani pia hata baada ya 2025.

Kumbuka ni inafahamika kuwa katiba mpya haiwezi kupendwa na walioko madarakani. Ila ni vizuri wakafahamu zama hizi ni nyingine:

#1. Safari hii kama watawala wanachagua kiumane, kitaumana. Haturudi nyuma.

#2. Safari hii kususia chaguzi maana yake ni kuwa "chaguzi hazifanyiki."


Tunajua lugha mbili hizi mtazielewa tu.
Corona imeleta matatizo makubwa ya uchumi wa dunia na sisi hatuwezi kukwepa huo mdororo. Katiba inaweza kusubiri mpaka 2025.

Wengi wanaoongelea katiba kwa sasa ni wanasiasa na wapambe wao, mwananchi wa kawaida kabisa kule Chunya anataka afikishiwe maji na umeme.

Mwananchi wa kawaida kule Ngara Rulenge anataka afaidike na Kabanga Nickel kuliko kufuatilia mijadala ya vifungu vya katiba kwa muda huu.

Mwananchi wa kawaida kabisa kule Ruangwa Lindi anataka aanze kufaidika na uwepo wa graphite iliyo chini ya ardhi anayoikanyaga kila siku.

Katiba inapigiwa kelele humu jukwaani walipo wanasiasa na mashabiki wao.
 
Corona imeleta matatizo makubwa ya uchumi wa dunia na sisi hatuwezi kukwepa huo mdororo. Katiba inaweza kusubiri mpaka 2025.

Wengi wanaoongelea katiba kwa sasa ni wanasiasa na wapambe wao, mwananchi wa kawaida kabisa kule Chunya anataka afikishiwe maji na umeme.

Mwananchi wa kawaida kule Ngara Rulenge anataka afaidike na Kabanga Nickel kuliko kufuatilia mijadala ya vifungu vya katiba kwa muda huu.

Mwananchi wa kawaida kabisa kule Ruangwa Lindi anataka aanze kufaidika na uwepo wa graphite iliyo chini ya ardhi anayoikanyaga kila siku.

Katiba inapigiwa kelele humu jukwaani walipo wanasiasa na mashabiki wao.
Kwani katiba inazuia nini mkuu.
 
Kwani katiba inazuia nini mkuu.
Inapoteza muda wa kufanya masuala yenye umuhimu zaidi kwa sasa. Unapopewa rasilimali za madini, mito na maziwa na bahari yenye kilomita 1400 halafu ukapoteza muda kwenye siasa hata huyo Mungu anabakia kukushangaa.
 
Corona imeleta matatizo makubwa ya uchumi wa dunia na sisi hatuwezi kukwepa huo mdororo. Katiba inaweza kusubiri mpaka 2025.

Wengi wanaoongelea katiba kwa sasa ni wanasiasa na wapambe wao, mwananchi wa kawaida kabisa kule Chunya anataka afikishiwe maji na umeme.

Mwananchi wa kawaida kule Ngara Rulenge anataka afaidike na Kabanga Nickel kuliko kufuatilia mijadala ya vifungu vya katiba kwa muda huu.

Mwananchi wa kawaida kabisa kule Ruangwa Lindi anataka aanze kufaidika na uwepo wa graphite iliyo chini ya ardhi anayoikanyaga kila siku.

Katiba inapigiwa kelele humu jukwaani walipo wanasiasa na mashabiki wao.

Corona? Si kuwa CCM hawawezi kukosa sababu hata zisizokuwapo?

Msikilize Mwanazuoni huyu:



Tume ya katiba ilikwenda nchi nzima hadi kuliko wavuvi, wakulima, wapagazi, serikalini, wafugaji, yaani kada zote.

Wananchi wanataka katiba mpya.

Takwimu zenu mnapata wapi?

"Katiba ni yetu sisi wananchi. Hatutaki kuendelea kubambikiziwa kesi, hatutaki dhuluma, hatutaki kubebeshwa mizigo ya kodi ya wengine, tunataka mihimili ya utawala iliyo na huru kamili, tunataka usawa, tunataka uwajibikaji, tunataka mawazo yetu kusikilizwa nk."

Ni wazi kama anavyosema Mwanazuoni huyo kuwa wasiotaka katiba mpya wana maslahi binafsi na iliyopo.

Habari ndiyo hiyo.
 
Inapoteza muda wa kufanya masuala yenye umuhimu zaidi kwa sasa. Unapopewa rasilimali za madini, mito na maziwa na bahari yenye kilomita 1400 halafu ukapoteza muda kwenye siasa hata huyo Mungu anabakia kukushangaa.

Mwananchi wa kawaida anayejielewa, hatutaki kuendelea kubambikiziwa kesi, hataki kudhulumiwa, hataki kubebeshwa mizigo ya kodi ya wengine, anataka mihimili ya utawala iliyo na uhuru kamili, anataka usawa, anataka uwajibikaji, anataka mawazo yake kusikilizwa nk.

Asiyetaka hayo ni uelewa mdogo au kuwa na maslahi binafsi.

Katiba iliyopo ni kikwazo kwa hayo yote. Wananchi wote wanaojitambua wanahitaji katiba mpya tena kwa hali ya dharura sana.
 
Mwananchi wa kawaida anayejielewa, hatutaki kuendelea kubambikiziwa kesi, hataki kudhulumiwa, hataki kubebeshwa mizigo ya kodi ya wengine, anataka mihimili ya utawala iliyo na uhuru kamili, anataka usawa, anataka uwajibikaji, anataka mawazo yake kusikilizwa nk.

Asiyetaka hayo ni uelewa mdogo au kuwa na maslahi binafsi.

Katiba iliyopo ni kikwazo kwa hayo yote. Wananchi wote wanaojitambua wanahitaji katiba mpya tena kwa hali ya dharura sana.
Poleni sana.
 
Corona? Si kuwa CCM hawawezi kukosa sababu hata zisizokuwapo?

Msikilize Mwanazuoni huyu:

View attachment 1842109

Tume ya katiba ilikwenda nchi nzima hadi kuliko wavuvi, wakulima, wapagazi, serikalini, wafugaji, yaani kada zote.

Wananchi wanataka katiba mpya.

Takwimu zenu mnapata wapi?

"Katiba ni yetu sisi wananchi. Hatutaki kuendelea kubambikiziwa kesi, hatutaki dhuluma, hatutaki kubebeshwa mizigo ya kodi ya wengine, tunataka mihimili ya utawala iliyo na huru kamili, tunataka usawa, tunataka uwajibikaji, tunataka mawazo yetu kusikilizwa nk."

Ni wazi kama anavyosema Mwanazuoni huyo kuwa wasiotaka katiba mpya wana maslahi binafsi na iliyopo.

Habari ndiyo hiyo.
Huu ni muda wa kuzalisha mali na tuutumie vyema kuliko kuupoteza kwenye mijadala mirefu ya siasa.
 
Pamoja na kuwa Mama Samia anaweza kuwa anayo nia njema na ya dhati kuhusiana na haki, uhuru na usawa wa watu, kizingiti kitaendelea kuwa wale wahafidhina wanaomzunguka.

CCM hao watakuwa ndiyo walio waasisi wa ile salamu yetu pendwa ya "Kazi Iendelee" na hata kile kidokezo chetu cha "JPM = Samia" kwa maana halisi.

Pamoja na jitihada zake binafsi alizokwisha onyesha yawezekana bado atakuwa kwenye mashinikizo makubwa kuuishi u mwendazake.

Lengo na madhumuni la wahafidhina hao ilikuwa ni kuendeleza misimamo ya bwana JPM bila JPM kuwepo. Kikubwa zaidi kikiwa ni kuyalinda maslahi yao binafsi.

Mengine tunayoyaona yatakuwa ni janja ya nyani tu.

Yatambulike mambo ya msingi yaliyokuwa katika rasimu ya katiba ya Warioba:


Hii ni kama ambavyo mjumbe huyu bwana Domhome (heshima kwako sana mkuu) alivyoyaweka kwa ufasaha kabisa.

Kwa hali kama hiyo, ni CCM gani katika waliojimilikisha hii nchi na vyote vilivyomo watakaoridhia mchakato wenye rasimu yenye maudhui kama hayo kirahisi bila ya kuwapo na mpambano wa haja kweli kweli wa kutosha resist?

Pana haja ya kupanua wigo wa washirika katika vita vitakatifu hivi vyenye vionjo vyote vya kuturejeshea yote tuliyokuwa tumepokwa na kujikuta tumekuwa:

Wabambikiziwa kesi, wahanga wa dhuluma, kubebeshwa mizigo ya kodi zisizotuhusu, Ku, kubagazwa nk.

Hayupo asiye pendwa usawa wala uwepo wa utawala ambapo mihimili yote itakuwa na uhuru kamili.

Asasi za dini, kiraia, wana harakati na hata vyama vingine vya siasa vitakavyokuwa tayari.

Uelekeo ni wazi, kulishiriki vuguvugu hili ni thwawabu.

Ninawasilisha!

Cc: BAK
HATUTAKI KIONGIZI YOYOTE WA CHAMA CHA KISIASA KUJADILI KATIBA YA WANANCHI.
 
Back
Top Bottom