Mwande na Mndewa
JF-Expert Member
- Feb 26, 2021
- 1,117
- 3,153
KATIBA MPYA NI KETE KWENYE ILANI YA CHADEMA 2025.
Leo 09:15hrs 07/07/2021
Je CCM itakuja na agenda hii kwenye ilani ya kutafutia kura? Je tumeutafakari uzuri na ubaya wa katibs tuliyonayo!? Je tumeshatafakari uzuri na ubaya wa katiba Mpya tunayoitaka!?
Katiba tuliyonayo haikutuvusha wakati wa msiba bali hekima za Watanzania,Busara za Watanzania,na Uvumilivu wa Watanzania,tusiwekeze kwenye hekima,Busara na Uvumilivu tuwekeze kwenye katiba Mpya itayotoa ridhaa ya Watanzania wote baada msiba maana kesho na kesho kutwa watakuja watu wasio na hekima, Busara wala Uvumilivu.
Katiba ya sasa haifikii ukuu wa taasisi ya Urais,Ukuu wa katiba unaishia pale Rais anaposhika madaraka,Sasa hili ni tatizo kubwa kwa maana itahitaji utashi wa Rais kuendesha nchi,tuwekeze kwenye katiba Mpya kwenye madhara ya uvunjaji wa katiba, Rais aweze kuwaji bishwa na taasisi nyingine.
Je ipitishwe katiba pendekezwa ya Warioba au tuanzie alipoishia Jaji Warioba au tuanzie kwenye sheria inayoruhusu kuandika katiba mpya,ni kweli katiba Mpya haipo kwenye ilani ya CCM lakini utashi wa Mh Rais unaweza kuileta katiba Mpya,mambo muhimu yote yatafanywa tukiwa na katiba inayotia mkazo maendeleo ya nchi,
Nimalizie kwa kusema Ilani ni nyenzo ya kutafutia kura Uchaguzi ujao.
Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
Leo 09:15hrs 07/07/2021
Je CCM itakuja na agenda hii kwenye ilani ya kutafutia kura? Je tumeutafakari uzuri na ubaya wa katibs tuliyonayo!? Je tumeshatafakari uzuri na ubaya wa katiba Mpya tunayoitaka!?
Katiba tuliyonayo haikutuvusha wakati wa msiba bali hekima za Watanzania,Busara za Watanzania,na Uvumilivu wa Watanzania,tusiwekeze kwenye hekima,Busara na Uvumilivu tuwekeze kwenye katiba Mpya itayotoa ridhaa ya Watanzania wote baada msiba maana kesho na kesho kutwa watakuja watu wasio na hekima, Busara wala Uvumilivu.
Katiba ya sasa haifikii ukuu wa taasisi ya Urais,Ukuu wa katiba unaishia pale Rais anaposhika madaraka,Sasa hili ni tatizo kubwa kwa maana itahitaji utashi wa Rais kuendesha nchi,tuwekeze kwenye katiba Mpya kwenye madhara ya uvunjaji wa katiba, Rais aweze kuwaji bishwa na taasisi nyingine.
Je ipitishwe katiba pendekezwa ya Warioba au tuanzie alipoishia Jaji Warioba au tuanzie kwenye sheria inayoruhusu kuandika katiba mpya,ni kweli katiba Mpya haipo kwenye ilani ya CCM lakini utashi wa Mh Rais unaweza kuileta katiba Mpya,mambo muhimu yote yatafanywa tukiwa na katiba inayotia mkazo maendeleo ya nchi,
Nimalizie kwa kusema Ilani ni nyenzo ya kutafutia kura Uchaguzi ujao.
Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.