Katiba mpya,wananchi na wadau tuangalie maeneo haya kwa kina - Tanzania kwanza

Katiba mpya,wananchi na wadau tuangalie maeneo haya kwa kina - Tanzania kwanza

Binafsi naona dhahiri mapendekezo ya katiba mpya ya muungano imedhamiria kuvunja muungano wenyewe! Serikali moja INATOSHA!
 
CCM = ASP + TANU ==> Serikali Mbili.
Ndani ya Serikali 3, Hakuna CCM, Ndani ya Serikali Moja CCM ipo, ila hapa CCM - Bara wanajua Kabisa kuwa Zanzibar (Mtaji wao) Hawatakubali huo Muundo.
Ndo Maana CCM wanahaha kushawishi watu Muungano wa Serikali 2, watafanya kila Hila kushinikza hili, ni Kama Kuku anayekata Roho akijaribu Kupigania Uhai wake wakati Tayari keshalekezwa Kibra na Kisu kikali kishapita Shingoni Mwake.

Sema Noooooooo to Serikali Mbili, Sema Ndio to Serikali Tatu, na ikishindikana Serikali tatu Sema Ndio to Serikali Moja.
Otherwise, Let Zanzibar and CCM go
Full stop
 
serikali iwe moja , rais mmoja, nchi moja, sarafu moja kama mliweza kuunganisha vyama kwann isiwe serikali? km wazenji hawataki basi wasepe zao sisi hatutaki walalamishi na tumechoka na ngonjera zao.
Hizo hoja nyingine mf. majeshi, sera za sarafu naunga mkono hoja.
Mwisho ndio umebadili tabia yako ya matumizi mabaya ya madaraka na kufanya siasa chafu ama bado?
 
Kwa mara ya kwanza umeonge "POINT" na nimekupa "LIKE", kumbe sometimes akili yako inafanya kazi....
 
Other things Remain Constant,
Vijana na watoto wetu ndio tunategemewa kuitumia zaidi katiba mpya. Mabaraza yanaanza, kama wadau nawaomba TUISOME RASIMU, TUTAFAKARI, TUJADILI, TUTOE MAONI KWA KUITANGULIZA TANZANIA MIOYONI MWETU. SIO KULENGA KULIKOMOA KUNDI FULANI AU UPANDE FULANI WA NCHI.
Nawashauri tuyaangalie maeneo kwa kina. Kwa kuanzia tuangalie:

A) Ibara ya 223(1) inasema kutakuwa na Jeshi la wananchi wa Tanzania litakalokuwa na mamlaka ya kusimamia ulinzi na usalama.... Ibara ya 232(1) inasema bila kuathiri mashariti ya katiba hii, nchi washarika wa muungano wanaweza kuanzisha vikosi vya ulinzi na usalama .... ktk maeneo yao.

Pili ibara ya 227(1) kutakuwa na Jeshi la Polisi la jamuhuri ya muungano litakuwa na jukumu la ulinzi wa wa watu wao, Ibara ya 232 inaongelea vikosi vya washirika kuhusika na ulinzi wa watu wao Pia 233 (1) kutakuwa na idara ya usalama wa Taifa wa jamuhuri ya muungano ... Ibara 235 inasema bila kuathiri masharti ya katiba hii, nchi washirika wanaweza kuanzisha idara za usalama.

Analysis, swala la usalama ni nyeti muundo huu utategemea tu mazingira na busara ya viongozi. Vinginevyo nirahisi vikosi vya muungano kupigana na vya nchi washirika kufuatia maelekezo ya viongozi wao siku wakitokea sio wataifa.

B) ibara ya 217(1) kutakuwa na benki kuu ya jamhuri ya muungano na majukumu yameainishwa...... ibara ya 218 serikali washirika zitakuwa na BENKI ZAO zakusimamia sera za kifedha na kibenki
Analysis; hakuna namna unaweza kuwa na monetary policy tatu ktk nchi moja ukafikia malengo. Ni kama gari kuwa na sukani tatu na madreva wa tatu at per, the will miss the right direction.

C) ibara ya 1(1), 1(2) na 57(1) zinazungumzia shirikisho, nionavyo mimi ni makosa. Jamhuri ya muungano ni nchi sio shirikisho. Kupata shirikisho ni sharti kwanza nchi washirika tupige kura kama tunataka kujiunga na shirikisho au laa kama tulivyokataa la afrika mashariki.

Hata muundo wa serikali tatu vijana nawaomba mliangalie kwa utulivu bila jazba ya kelele za ndugu zetu wa upande mwingine kusema wananyonywa pia bila kuangalia mungano wa serikali mbili kuwa ni msimamo wa CCM. TANZANIA BARA ITAKUWA NA SERIKALI MBILI YAANI YA BARA NA YA MUUNGANO ambayo haitahusika na maisha ya watanzania bara kupitia mambo yenye mguso wa moja kwa moja. NITAWALETEA SIKU NYINGINE IMPLICATION ZAKE KIUCHUMI KWA TAKWIMU NA JINSI KODI ITAKAVYOPANDA KUKIDHI NYONGEZA YA SERIKALI. BE BLESSED

Kama serikali tatu ni gharama, kwanini serikaliya CCM imeongeza majimbo, wilaya na mikoa? Katika serikali tatu, Zanzibar na Tanganyika zitakuwa na magovernor , Rais na makamu wake ni wa Jamhuri tuu no PM. Delete vyeo vya ukuu wa Mkoa/wilaya.
 
Hata muundo wa serikali tatu vijana nawaomba mliangalie kwa utulivu bila jazba ya kelele za ndugu zetu wa upande mwingine kusema wananyonywa pia ..........................

Well said ila jifunze kutumia Lugha isiyomkwaza mtu.
 
Hii analysis yako iko verry poor, ukizingatia lengo na madhumuni yako.

Kwanza Mchakato wa kuanzisha Katiba mpya mlikuwa hamuutaki kwa sababu itapunguza ulaji na mapango yenu yote ya kufanya uhalifu pamoja na ufisadi...

Ninauhakika nyinyi mnahofu kubwa sana ya kuwa na katiba mpya yenye vyombo vya sheria, ulinzi, Usalama na Uchaguzi huru kwani kufanya hivyo ninauhakika mtashindwa kupendelewa na hatimaye kufikishwa mahakamani na pengine kufungwa kwa sababu ya uovu mnaoufanya.

Wanganyika wanachotaka ni Tanganyika yao na Zanzibar wanachotaka no Zanzibar yao yenye mamlaka kamili nyinyi manataka serikali mbili ambayo imekuwepo tangu 1964 mpaka leo na mnataka kuendelea nayo kivipi???

Nyinyi hamna nia njema na Katiba mpya kwa sababu hamna uchungu na waTZ mko tu kwa ajili maslahi yenu tu na watanzania hawako tayari kudanganyika safari hii.


Hata mimi nakubaliana na wewe.

Analysis yake iko very poor kwa mtu mwenye madaraka makubwa sana nchini kupitia chama twawala. Alichofanya hapa ni kuweka vipengere ambavyo anadai vinaweza kuwa na utata ............... kitu ambacho nakubaliana naye kwa kiasi fulani. Lakini kwa cheo chake na elimu yake tunayoambiwa ya First class in Economics hakutakiwa kuishia hapo kama akina Nape wenye elimu za kuungaunga. He could have gone deeper!!

Nasubiri analysis yake ya gharama za serikali tatu!!
 
Haya ndiyo mambo ambayo kwa sasa Watanzania tunatakiwa tuyape uzito katika maongezi yetu ya kila siku.

Tatizo lililopo kwenye hii rasimu ni kunataka kujenga nyumba ya gorofa kwenye msingi wa nyumba za tembe.

Hata tume ya Jaji Warioba haikuwa na choice kutokana na kufungwa mikono na hadidu za rejea na matokeo yake ndiyo haya.

Kwa nini wananchi wasiulizwe kwanza kama wanataka kuendelea na hili 'dudu' Muungano, na kama wengi watakubali basi waseme ni muungano gani wanapenda uwepo ili tume ipate political legitimacy.

Hata waingereza pamoja na kuwa na nguvu kiuchumi na pia katika banking sector, waliona haiwezekani kuwa na muundo wa benki kama huu wa Jaji Warioba.

Kwenye eneo la majeshi halina complement. Huwezi ukawa na majeshi ya aina zaidi ya moja ukategemea hakutakuwa na mitikisiko katika nchi ya demokrasia changa kama Tanzania.

Huu muungano uliopo na unaopendekezwa katika misingi hii ni kaput.
 
Halafu sura yako inatisha! Kweli muuaji ni lazima ufanane na kazi yako. Damu za watu zimetapakaa mikononi mwako.
 
Mimi ni TANGANYIKA KWANZA mengine baadae.

Lakini kwa jinsi inmavyoonekana Tanzania inaweza kuwa na majeshi ya ulinzi matatu, hapo ndio matatizo yatakapoanzia kwa sababu kila mtu ataiona ana comand upande wake.

Mimi nadhani ni vyema kila nchi ijetegemee kivyake na tubaki marafiki kama kenya na sie . ... Mbona EAST AFRICA ilivunjika?
Mbona Sudan imegawanyika?

Hizi ndoa zenye manung'uniko kila kukicha ndio matokeo yake siku moja unakuta mzazi mmoja kwatilia sumu familia nzima ili wote wakose.

TANGANYIKA KWANZA!

Japo sikupendi kwa jinsi unavyoichukia CDM, kwa hili nakupa hongera. Mara watuite wanyonyaji, nk. Tanganyika kwanza.
 
Kama unavyosema ni kweli hatuwezi kuwa na monetary policy tatu... Hapa mpango mzima ni Serikali moja tu kama wale wa Zenji hawawezi tunasema let Zanzibar go, sitaki serikali tatu, Gari itakuwa vipi na misikanio mitatu!? Mpango mzima ni Tanzania moja...
.. Mkuu umenena SERIKALI MOJA TU, ndiyo inayotufaha kwa sasa.
 
Halafu sura yako inatisha! Kweli muuaji ni lazima ufanane na kazi yako. Damu za watu zimetapakaa mikononi mwako.
Jadiri hoja siyo sura za watu kama huwezi unaweza ukawa mjumbe msomaji wa mabandiko.
 
Hivi ndugu yangu Mwigulu unaona unatenda haki kutetea serikali mbili? Sina imani na mtu yeyote anayesema tubaki hivi hivi Mhe. Kwa upande wa Uchumi ni serikali moja ila mbawaogopa wazenji kwa kukubaliana nao ati serikali mbili!!! Fake Tanganyikans will accept two gvts. Aidha iwe moja au ziwe tatu mbili hapanaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
kama Tanganyika na Zanzibar ziliungana mwaka 1964 Tukapata Tanzania. baada ya miaka50 ya majaribio tulitegemea huu muungano ukomae na kuwa serikali moja, ili tutamke kwa jeuri kuwa kuna nchi moja, Taifa moja, serikali moja, bunge moja, na dola moja. kwa hiyo ifikapo 26/4/2013 tungeizika zanzibar rasmi kama tulivyoizika tanganyika miaka hamsini iliyopita. Kama tutarudi kwenye serikali tatu au kuendelea na serikali mbili, mimi naona hakuna haja ya muungano, hapo ndoa imeshindikana hapo kila mmoja arejee kwa wazazi wake.

...mkuu uko juu, tunahitaji Tanzania MOJA yenye serikali moja, nchi moja, Taifa moja, bunge moja, na dola moja:
- Rais moja
- Makamu wa rais mmoja
- Waziri Mkuu mmoja
- Baraza la mawaziri moja
- Katiba Moja
- Uwakilishi wa UTAIFA mmoja
- Kila kitu mfumo mzima uwe kwenye kofia moja,KWA SASA NDIYO DAWA pekee.
 
Japo sikupendi kwa jinsi unavyoichukia CDM, kwa hili nakupa hongera. Mara watuite wanyonyaji, nk. Tanganyika kwanza.
Mkuu tuweke vyama pembeni tuangalie maslahi yetu ya muda mrefu kwa faida ya vizazi vijavyo

Kama mmoja anaruhusiwa kudai haki yake kwa nini na sisi tusidai Tanganyika yetu?
 
  • Thanks
Reactions: SG8
Mimi ni TANGANYIKA KWANZA mengine baadae.

Lakini kwa jinsi inmavyoonekana Tanzania inaweza kuwa na majeshi ya ulinzi matatu, hapo ndio matatizo yatakapoanzia kwa sababu kila mtu ataiona ana comand upande wake.

Mimi nadhani ni vyema kila nchi ijetegemee kivyake na tubaki marafiki kama kenya na sie . ... Mbona EAST AFRICA ilivunjika?
Mbona Sudan imegawanyika?

Hizi ndoa zenye manung'uniko kila kukicha ndio matokeo yake siku moja unakuta mzazi mmoja kwatilia sumu familia nzima ili wote wakose.

TANGANYIKA KWANZA!
Leo umeongea point. Nakuunga mkono 100% Tanganyika kwanza...
 
Katika siku ambazo nimeona pumba zimeandikwa leo ndio nimeona!! Nyie vikina ccm sio kama mnauchungu sana na hii nchi!! Nyie lengo lenu ni kulinda kura zenu za kule zenji sasa mtake msitake kama si serikali moja basi hapa ni kwenda kwenye serikali tatu!! Kiukweli kifo cha ccm nakiona kabisa!!!! Inamaana hao mlio wachagua wala swala hilo hawakuliona mpaka mlione wenyewe kama vipi nyie wenyewe ndio mjilahumu!!!! Hatudanganyiki kabisa
 
GOOD OBSERVATION, si wakati muafaka kuwa na majeshi matatu, benk tatu za serikali na serikali tatu
 
mwigulu kaleta mada nzuri acha watu waoneshe maoni yao na muelekeo wao.
 
Back
Top Bottom