Katiba Mpya ya nini kama hii tuliyonayo hatuiheshimu?

Katiba Mpya ya nini kama hii tuliyonayo hatuiheshimu?

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
Mimi nimekuwa muumini wa katiba mpya tangu enzi na enzi. Kabla hata JF haijazaliwa.

Niliamini hivyo kwa sababu unapobadili mfumo wa kisiasa, basi ni lazima pia ubadili sheria na taratibu zitazotumika kuuongoza huo mfumo mpya.

Hivyo basi, ilipaswa tokea mwanzo, yaani 1992, tuliporudi tena kwenye mfumo wa vyama vingi, kubadili kabisa katiba ili iendane na hayo mazingira mapya.

Hilo halikufanyika. Kilichofanyika ni kubadili badili tu vitu vidogo vya hapa na pale kwenye katiba iliyokuwepo wakati huo, basi.

Tokea 1995, tumeona ni jinsi gani watawala wa CCM wanavyoweza kuikiuka hii katiba tuliyo nayo.

Mifano ipo mingi. Nitaitaja miwili ya hivi karibuni ambayo wengi mtakuwa mnaikumbuka.

Baada ya kuingia madarakani, Rais Magufuli alipiga marufuku watu kufanya shughuli za kisiasa kwa kisingizio kwamba ‘siasa sasa zimeshaisha na ni wakati wa kufanya kazi’. Hiyo ni licha ya kwamba shughuli hizo ni haki za kikatiba kwa Mtanzania yeyote yule.

Baada ya Rais Magufuli kufariki, baadhi ya wajuzi na wajuvi wa mambo ya katiba walituambia kwamba Rais Samia alipaswa kulivunja baraza la mawaziri na kuunda serikali mpya.

Hilo halikufanyika. Hivyo maana yake ni kwamba naye aliikiuka katiba.

Sasa nimewaza: kama hii katiba iliyopo inakiukwa wazi wazi namna hii na hamna lolote la maana linalofanyika kupinga ukiukwaji huo, hiyo katiba mpya inahitajika ili iweje?

Mara karibu zote ambapo katiba imeonekana kukiukwa, hakuna cha maana ambacho wananchi tumefanya zaidi ya kujimwambafy humu kwenye mitandao.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani na kupinga. Hakuna aliyefungua kesi mahakamani. Tumelia lia tu humu mitandaoni.

Sasa hiyo katiba mpya tukiipata, ikikiukwa ndo itatuwezesha kupata ujasiri wa kupinga kukiukwa kwake?

Nimeanza kudhani pengine tatizo letu si katiba mpya pekee. Tatizo letu kubwa ni sisi wenyewe. Tunaachia tu mambo yaende hata kama yapo kinyume na katiba.

A new constitution will not be worth the paper it’s written on if we allow and let the one we have to be breached with impunity!
 
Upatikanaji wa Katiba Mpya una ugumu ule ule au zaidi ya kuiondoa CCM madarakani, suala la kuvunjwa Katiba iliyopo na CCM hao wanaoiongoza nchi ni kwasababu wameshajizoea, wanajiona wao ndio alfa na omega hakuna wakuwatisha, wametapakaa kuanzia vyombo vya ulinzi na usalama mpaka bungeni.

Binafsi ningeona ulichokiandika kina uzito zaidi kama huo uvunjwaji wa Katiba iliyopo unafanywa na makundi mengine kwenye jamii, kama vyama vya upinzani, au asasi za kiraia, lakini kama uvunjwaji huo unafanywa na CCM, hiyo kwangu inazidi kuwa sababu ya kuitafuta Katiba Mpya ili ituweke wote kwenye mazingira sawa, kisiasa, kijamii, n.k.
 
Siyo Chadema tu, hats CUF siku watakapochukua hatamu na wananchi kuwaunga mkono kwa kura zote ndipo sisi CCM tutaelewa
 
Upatikanaji wa Katiba Mpya una ugumu ule ule au zaidi ya kuiondoa CCM madarakani, suala la kuvunjwa Katiba iliyopo na CCM hao wanaoiongoza nchi ni kwasababu wameshajizoea, wanajiona wao ndio alfa na omega hakuna wakuwatisha, wametapakaa kuanzia vyombo vya ulinzi na usakama mpaka bungeni...
Umemwelewesha vema
 
Upatikanaji wa Katiba Mpya una ugumu ule ule au zaidi ya kuiondoa CCM madarakani, suala la kuvunjwa Katiba iliyopo na CCM hao wanaoiongoza nchi ni kwasababu wameshajizoea, wanajiona wao ndio alfa na omega hakuna wakuwatisha, wametapakaa kuanzia vyombo vya ulinzi na usakama mpaka bungeni...
Sawa. CCM ndo wanavunja katiba.

What have you done about it?
 
Tunataka katiba mpya ili tuweke kipengele cha kuiheshimu

Katiba inavunjwa kwa sababu ni mbaya katiba ikiwa bora inajilinda yenyewe

Mfano kuteuliwa kwa Nasari watu wangeenda makamani na angetemeshwa ukuu wa wilaya haraka sana maana tungezuia kuapishwa kwake
 
Sawa. CCM ndo wanavunja katiba.

What have you done about it?
We have nothing to do since katiba hii tunayotumia ni ya mkoloni haijaweka room ya kufanya chochote na ndiyo maana tunataka katiba mpya.

Mkiwa mnabeba box msiwe mnaweka utosini maana mnazidi kupoteza akili za kufikiri mambo madogo kama haya.
 
Sawa. CCM ndo wanavunja katiba.

What have you done about it?
Not only me, it's you & me, coz nawe umejinasibisha kuidai Katiba Mpya toka enzi, mimi napiga kelele huku jf kama wewe, kama ikitokea movement nyingine I will join.
 
Not only me, it's you & me, coz nawe umejinasibisha kuidai Katiba Mpya toka enzi, mimi napiga kelele huku jf kama wewe, kama ikitokea movement nyingine I will join.
Kwa hiyo kelele zako unazopiga huku JF ukiwa umejificha zimesaidia nini?
 
Mimi nimekuwa muumini wa katiba mpya tangu enzi na enzi. Kabla hata JF haijazaliwa.

Niliamini hivyo kwa sababu unapobadili mfumo wa kisiasa, basi ni lazima pia ubadili sheria na taratibu zitazotumika kuuongoza huo mfumo mpya...

Kutokufuatwa kwa katiba iliyopo ni kutokana na madhaifu yaliyoko kwenye katiba yenyewe yanayotoa nafasi kwa baadhi ya watu kutokuiheshimu na bado wasiwajibike. Katiba mpya itaziba mianya hiyo.

Mifano ni mingi lakini ya msingi kabisa ni hii ya watendaji wakuu (Rais, Spika, na wenzao) kutokuwajibika kwa makosa YOYOTE wawepo ofisini.

Tume ya uchaguzi, Vyombo vya dola, bunge na mahakama nk kuwajibika kwa serikali ambayoeti ni mhimili uliojichimbia zaidi.

Tunataka katiba yenye kurejesha uwajibikaji wa serikali nzima kwa wananchi. Katiba ambayo mihimili yote ya utawala itakuwa huru.

Ya bwana Nyani Ngabu ni kelele nyingine za watu wale wale, za kujaribu kutuondoa kwenye reli kwa mara nyingine.

Hatudanganyiki!

Habari ndiyo hiyo.
 
Katiba mpya ya nini kama hii tuliyonayo hatuiheshimu na kuifuata?
Nyani Ngabu una hoja nzuri sana. Kusema kweli katiba ya nchi ni kitabu kama vitabu vingine tu kama viongozi hawana utashi wa kuifuta na wananchi hawana utashi wa kuitetea. Lakini hebu tuweke hivi:

Tuwe na katiba ambayo itamzuia kwa kiasi kikubwa iwezekanavyo mtawala ambaye ataamua kutoifuata. Yaani jambo la muhimu kabisa la kuzingatia wakati wa kuandika katiba mpya ni kuweka system ambayo hata akipatikana kiongozi msigina katiba iwe vigumu kuweza kufanya hilo jambo.

Ndiyo maana mimi hata ile katiba ya Warioba bado naiona kama imepitwa na wakati. Katiba nzuri ni ile itakayorudisha madaraka kwa wananchi, ma possibly tugawe madaraka ya urais, tuwe na waziri mkuu mtendaji na kusiwe na teuzi zinazompa nguvu mtu mmoja. Hili linawezekana kabisa japo halitaondoa kabisa tatizo, lakini litapunguza.
 
Back
Top Bottom