Katiba Mpya ya nini kama hii tuliyonayo hatuiheshimu?

Katiba Mpya ya nini kama hii tuliyonayo hatuiheshimu?

Mimi nimekuwa muumini wa katiba mpya tangu enzi na enzi. Kabla hata JF haijazaliwa.

Niliamini hivyo kwa sababu unapobadili mfumo wa kisiasa, basi ni lazima pia ubadili sheria na taratibu zitazotumika kuuongoza huo mfumo mpya.

Hivyo basi, ilipaswa tokea mwanzo, yaani 1992, tuliporudi tena kwenye mfumo wa vyama vingi, kubadili kabisa katiba ili iendane na hayo mazingira mapya.

Hilo halikufanyika. Kilichofanyika ni kubadili badili tu vitu vidogo vya hapa na pale kwenye katiba iliyokuwepo wakati huo, basi.

Tokea 1995, tumeona ni jinsi gani watawala wa CCM wanavyoweza kuikiuka hii katiba tuliyo nayo.

Mifano ipo mingi. Nitaitaja miwili ya hivi karibuni ambayo wengi mtakuwa mnaikumbuka.

Baada ya kuingia madarakani, Rais Magufuli alipiga marufuku watu kufanya shughuli za kisiasa kwa kisingizio kwamba ‘siasa sasa zimeshaisha na ni wakati wa kufanya kazi’. Hiyo ni licha ya kwamba shughuli hizo ni haki za kikatiba kwa Mtanzania yeyote yule.

Baada ya Rais Magufuli kufariki, baadhi ya wajuzi na wajuvi wa mambo ya katiba walituambia kwamba Rais Samia alipaswa kulivunja baraza la mawaziri na kuunda serikali mpya.

Hilo halikufanyika. Hivyo maana yake ni kwamba naye aliikiuka katiba.

Sasa nimewaza: kama hii katiba iliyopo inakiukwa wazi wazi namna hii na hamna lolote la maana linalofanyika kupinga ukiukwaji huo, hiyo katiba mpya inahitajika ili iweje?

Mara karibu zote ambapo katiba imeonekana kukiukwa, hakuna cha maana ambacho wananchi tumefanya zaidi ya kujimwambafy humu kwenye mitandao.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani na kupinga. Hakuna aliyefungua kesi mahakamani. Tumelia lia tu humu mitandaoni.

Sasa hiyo katiba mpya tukiipata, ikikiukwa ndo itatuwezesha kupata ujasiri wa kupinga kukiukwa kwake?

Nimeanza kudhani pengine tatizo letu si katiba mpya pekee. Tatizo letu kubwa ni sisi wenyewe. Tunaachia tu mambo yaende hata kama yapo kinyume na katiba.

A new constitution will not be worth the paper it’s written on if we allow and let the one we have to be breached with impunity!
Upo sahihi 💯
 
Umeona jinsi unavyoruka ruka kama maharagwe, yaani WATANZANIA kitu tunachokiweza ni kulaumu laumu n kukosoa wengine.
Sasa ukapinge kitu hujui nini kimeandikwa ndani? Hizo nchi nyingine kuweka mahakama kuu kulinda katiba ya nchi wajinga hao? kazi ya mwanasheria mkuu ni nini? wewe kwa akili yako unadhani kila mtu anaweza kusoma katiba na akailewa kama unasoma gazeti. ndio mikataba inapitiwa na wana sheria sio unakurupuka tuu ku sign kuna lugha inatumika humo na vipengele ni watu waliobobea tu ndio wanaweza kutafsiri sio kila.

Mikataba midogo tu inaandikwa na mwanasheria sembuse katiba. hiyo katiba inauzwa madukani ununue usome, kila kitu kinafichwa tu sehemu pekee naiona inashikwa siku anaapishwa mtu na wala hasomi yeye kaibeba tu naapa kuilinda katiba ukimuuliza unaapa unajuwa kilichopo ndani hawajui. nenda nchi zote zilizoendelea katiba inalindwa na mahakama na bunge.
 
Endelea kusubiri Mahakama iwe inasimamia haki ambazo hata wewe mwananchi unatakiwa kuzilinda.
Mimi sikuelewi unataka nilinde kitu sijawahi kukisoma wala sijui kilichoandikwa ndani? wawakilishi wa wananchi bungeni ndio wanawakilisha watu na wanaapa kulinda maana wako kwa kazi hiyo hawajui kilichomo unataka mimi naye amka asubuhi kutafuta rizki mpaka usiku nikakae nasoma kitabu watoto wale nini? kila jukumu limepangiwa watu wake. wale tunawachagua kutuwakilisha, kutunga sheria na kulinda katiba ya nchi wao wanaweza kupiga hata kura ya kutokuwa na imani na rais ikiwa anavunja sheria sio mimi. Mimi ukiisha uchaguzi imeisha hiyo.
 
Upatikanaji wa Katiba Mpya una ugumu ule ule au zaidi ya kuiondoa CCM madarakani, suala la kuvunjwa Katiba iliyopo na CCM hao wanaoiongoza nchi ni kwasababu wameshajizoea, wanajiona wao ndio alfa na omega hakuna wakuwatisha, wametapakaa kuanzia vyombo vya ulinzi na usalama mpaka bungeni.

Binafsi ningeona ulichokiandika kina uzito zaidi kama huo uvunjwaji wa Katiba iliyopo unafanywa na makundi mengine kwenye jamii, kama vyama vya upinzani, au asasi za kiraia, lakini kama uvunjwaji huo unafanywa na CCM, hiyo kwangu inazidi kuwa sababu ya kuitafuta Katiba Mpya ili ituweke wote kwenye mazingira sawa, kisiasa, kijamii, n.k.
Mkuu umemuelewa toa mada? Yeye anauliza hii katiba mbovu tulionayo kuna baadhi ya mambo Rais/na baadhi ya viongozi wanafanya kwa kukiuka katiba na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa

Sasa swali la msingi hiyo katiba mpya ikiwepo na CCM ikaendelea kuvunja katiba ni hatua gani zitafuata au tutaendelea kulalamika JF kwa kuficha majina yetu?
 
Mifano mitatu tu wakati JPM kukataza mikutano ya kisiasa au kuandamana ni haki ya wananchi lakini mahakama kimyaa. Hawa wabunge 19 kila mtu anajuwa katiba imevunjwa mahakama kimyaa. kuna mtu kaachiwa usiku kenda kuapishwa mbunge mahakama kimyaa. DPP anaweza ku bargain kabla ya kufungua mashtaka lakini leo kesi iko mahakamani DPP akawa yeye kama judge anaenda ana bargain mtu anaachiwa kwa makosa ya wizi makubwa tu. kuna watu wamefungwa makosa ya kawaida tu labda mtu aliiba TV mwambia rudisha TV toka, kaiba mbuzi lipa mbuzi toka.
Yote hayo unayosema Mahakama kimyaaa kuna Wananchi/Mwananchi yoyote alikwenda kulalamika na Mahakama ikakataa kumsikilza?

Na kama sote Wananchi tunakubali kuwa matendo hayo ni uvunjifu wa amani ni hatua gani tumechukua kuhakikisha kuwa katiba yetu tunailinda? Au sisi ni watu wa bora liende na kupiga mbinja mitandaoni?
 
Yote hayo unayosema Mahakama kimyaaa kuna Wananchi/Mwananchi yoyote alikwenda kulalamika na Mahakama ikakataa kumsikilza?

Na kama sote Wananchi tunakubali kuwa matendo hayo ni uvunjifu wa amani ni hatua gani tumechukua kuhakikisha kuwa katiba yetu tunailinda? Au sisi ni watu wa bora liende na kupiga mbinja mitandaoni?
Kutochukua hatua ndiyo upuuzi wenyewe wa kitanzania
 
Kutochukua hatua ndiyo upuuzi wenyewe wa kitanzania
Na Watanzania kwa jinsi tulivyo hata akija kiongozi wa aina gani atatubuluza tu tunamaneno meeengiiiii tukikaa kwenye vijiwe vya kahawa au JF lakini vitendo 0
 
Mimi nimekuwa muumini wa katiba mpya tangu enzi na enzi. Kabla hata JF haijazaliwa.

Niliamini hivyo kwa sababu unapobadili mfumo wa kisiasa, basi ni lazima pia ubadili sheria na taratibu zitazotumika kuuongoza huo mfumo mpya.

Hivyo basi, ilipaswa tokea mwanzo, yaani 1992, tuliporudi tena kwenye mfumo wa vyama vingi, kubadili kabisa katiba ili iendane na hayo mazingira mapya.

Hilo halikufanyika. Kilichofanyika ni kubadili badili tu vitu vidogo vya hapa na pale kwenye katiba iliyokuwepo wakati huo, basi.

Tokea 1995, tumeona ni jinsi gani watawala wa CCM wanavyoweza kuikiuka hii katiba tuliyo nayo.

Mifano ipo mingi. Nitaitaja miwili ya hivi karibuni ambayo wengi mtakuwa mnaikumbuka.

Baada ya kuingia madarakani, Rais Magufuli alipiga marufuku watu kufanya shughuli za kisiasa kwa kisingizio kwamba ‘siasa sasa zimeshaisha na ni wakati wa kufanya kazi’. Hiyo ni licha ya kwamba shughuli hizo ni haki za kikatiba kwa Mtanzania yeyote yule.

Baada ya Rais Magufuli kufariki, baadhi ya wajuzi na wajuvi wa mambo ya katiba walituambia kwamba Rais Samia alipaswa kulivunja baraza la mawaziri na kuunda serikali mpya.

Hilo halikufanyika. Hivyo maana yake ni kwamba naye aliikiuka katiba.

Sasa nimewaza: kama hii katiba iliyopo inakiukwa wazi wazi namna hii na hamna lolote la maana linalofanyika kupinga ukiukwaji huo, hiyo katiba mpya inahitajika ili iweje?

Mara karibu zote ambapo katiba imeonekana kukiukwa, hakuna cha maana ambacho wananchi tumefanya zaidi ya kujimwambafy humu kwenye mitandao.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani na kupinga. Hakuna aliyefungua kesi mahakamani. Tumelia lia tu humu mitandaoni.

Sasa hiyo katiba mpya tukiipata, ikikiukwa ndo itatuwezesha kupata ujasiri wa kupinga kukiukwa kwake?

Nimeanza kudhani pengine tatizo letu si katiba mpya pekee. Tatizo letu kubwa ni sisi wenyewe. Tunaachia tu mambo yaende hata kama yapo kinyume na katiba.

A new constitution will not be worth the paper it’s written on if we allow and let the one we have to be breached with impunity!
Mifano uliyotoa ndio sababu ya kudai Katiba Mpya. Hao uliosema wamevunja Katiba ni marais wa nchi yetu na kwa Katiba iliyopo hawawezi kushtakiwa popote kwa lolote watakalotenda wakati wa urais wao. Kwa sababu hiyo kufungua mashtaka dhidi yao ni kupoteza wakati. Ni kama ilivyo sasa hivi kwa Spika ambae nae amepewa immunity na hivyo kumruhusu kufanya lolote atakalo bila kuogopa atawajibika. Katiba mpya hopefully itarekebisha yote haya na kuwarudishia wananchi nguvu za kuwawajibisha viongozi wao pale ambapo wataenda kinyume na matakwa ya Katiba.

Amandla...
 
Nyani Ngabu Mkuu let's be open minded, why we need newer constitution, I say newer because ours is still new, not even 50 years old. Katiba sio msahafu unaweza badilishwa time yoyote ili mradi uwe kwa manufaa ya waTanzania wote.
 
Yaani sasa unasema kitu ambacho kulingana na umuhimu wake na 'exposure' yako eti ni 'kelele', kaaazi kwelikweli....
Hata kuandika ukaeleweka huwezi!

Kusoma na kuelewa ulichokisoma utaweza kweli???
 
Mifano uliyotoa ndio sababu ya kudai Katiba Mpya. Hao uliosema wamevunja Katiba ni marais wa nchi yetu na kwa Katiba iliyopo hawawezi kushtakiwa popote kwa lolote watakalotenda wakati wa urais wao. Kwa sababu hiyo kufungua mashtaka dhidi yao ni kupoteza wakati. Ni kama ilivyo sasa hivi kwa Spika ambae nae amepewa immunity na hivyo kumruhusu kufanya lolote atakalo bila kuogopa atawajibika. Katiba mpya hopefully itarekebisha yote haya na kuwarudishia wananchi nguvu za kuwawajibisha viongozi wao pale ambapo wataenda kinyume na matakwa ya Katiba.

Amandla...
Fundi umenielewa kweli?

Sawa, hata kama katiba yetu ya sasa hairuhusu viongozi wetu hao wa juu kushitakiwa kibinafsi, hiyo haina maana ndo wawe wanavunja katiba.

Wanapovunja katiba sasa hivi, kwenda mahakamani dhidi yao si kwa kuwashitaki wao binafsi na wakipatikana na makosa wafungwe jela.

La hasha! Bali lengo ni kutaka kubatilisha hicho walichokifanya ambacho ndo kimekiuka katiba.

Magufuli alikataza watu kufanya shughuli za kisiasa nchi nzima. Jambo ambalo ni kinyume kabisa na katiba.

Nani alienda mahakamani, hata kwa kujaribu tu, kuipinga amri hiyo?

Jambo linaruhusiwa kikatiba. Yeye akalikataza. Kwa nini mahakamani yetu haikutoa tafsiri juu ya uhalali wa katazo hilo?

Kama mtu angeenda mahakamani na kufungua shauri la kupinga katazo hilo, hiyo haina maana kuwa mtu huyo alienda mahakamani kumshitaki Rais Magufuli kama mtu binafsi.

Au labda mimi tu ndo sijui na labda wapo walioenda mahakamani na kupinga katazo hilo na mahakamani ikalitolea uamuzi?

Kwa hiyo, hivyo ndivyo ninavyomaanisha ninaposema kwamba hata hii katiba ya sasa inapokiukwa, hatufanyi chochote kile. Tunaachia tu ikiukwe halafu tunajipa moyo na kujifariji kuwa hatuwezi kufanya chochote kwa sababu Rais hawezi kushitakiwa!

Sasa tukipata katiba mpya na bado ikaendelea kukiukwa, tutafanya nini endapo hii ya sasa huwa inakiukwa na hatufanyi chochote kile?
 
Fundi umenielewa kweli?

Sawa, hata kama katiba yetu ya sasa hairuhusu viongozi wetu hao wa juu kushitakiwa kibinafsi, hiyo haina maana ndo wawe wanavunja katiba.

Wanapovunja katiba sasa hivi, kwenda mahakamani dhidi yao si kwa kuwashitaki wao binafsi na wakipatikana na makosa wafungwe jela.

La hasha! Bali lengo ni kutaka kubatilisha hicho walichokifanya ambacho ndo kimekiuka katiba.

Magufuli alikataza watu kufanya shughuli za kisiasa nchi nzima. Jambo ambalo ni kinyume kabisa na katiba.

Nani alienda mahakamani, hata kwa kujaribu tu, kuipinga amri hiyo?

Jambo linaruhusiwa kikatiba. Yeye akalikataza. Kwa nini mahakamani yetu haikutoa tafsiri juu ya uhalali wa katazo hilo?

Kama mtu angeenda mahakamani na kufungua shauri la kupinga katazo hilo, hiyo haina maana kuwa mtu huyo alienda mahakamani kumshitaki Rais Magufuli kama mtu binafsi.

Au labda mimi tu ndo sijui na labda wapo walioenda mahakamani na kupinga katazo hilo na mahakamani ikalitolea uamuzi?

Kwa hiyo, hivyo ndivyo ninavyomaanisha ninaposema kwamba hata hii katiba ya sasa inapokiukwa, hatufanyi chochote kile. Tunaachia tu ikiukwe halafu tunajipa moyo na kujifariji kuwa hatuwezi kufanya chochote kwa sababu Rais hawezi kushitakiwa!

Sasa tukipata katiba mpya na bado ikaendelea kukiukwa, tutafanya nini endapo hii ya sasa huwa inakiukwa na hatufanyi chochote kile?
Ado Shaibu akiwakilishwa na Fatma Karume alimshitaki Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kuvunja Katiba katika uteuzi wake wa Feleshi kuwa Attorney General kwa sababu Feleshi hakuwa na sifa zilizoainishwa kwenye Katiba. Mahakama ika rule kuwa mashtaka hayana mashiko kwa sababu ya immunity ya urais aliokuwa nao mshtakiwa. Baada ya hapo Fatma akashughulikiwa na kunyang'anywa leseni yake ya uwakili.

Amandla...
 
Ado Shaibu akiwakilishwa na Fatma Karume alimshitaki Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa kuvunja Katiba katika uteuzi wake wa Feleshi kuwa Attorney General kwa sababu Feleshi hakuwa na sifa zilizoainishwa kwenye Katiba. Mahakama ika rule kuwa mashtaka hayana mashiko kwa sababu ya immunity ya urais aliokuwa nao mshtakiwa. Baada ya hapo Fatma akashughulikiwa na kunyang'anywa leseni yake ya uwakili.

Amandla...
Ok!

Vipi kuhusu kutokufanya siasa kwa vyama vya upinzani?
 
Mimi nimekuwa muumini wa katiba mpya tangu enzi na enzi. Kabla hata JF haijazaliwa.

Niliamini hivyo kwa sababu unapobadili mfumo wa kisiasa, basi ni lazima pia ubadili sheria na taratibu zitazotumika kuuongoza huo mfumo mpya.

Hivyo basi, ilipaswa tokea mwanzo, yaani 1992, tuliporudi tena kwenye mfumo wa vyama vingi, kubadili kabisa katiba ili iendane na hayo mazingira mapya.

Hilo halikufanyika. Kilichofanyika ni kubadili badili tu vitu vidogo vya hapa na pale kwenye katiba iliyokuwepo wakati huo, basi.

Tokea 1995, tumeona ni jinsi gani watawala wa CCM wanavyoweza kuikiuka hii katiba tuliyo nayo.

Mifano ipo mingi. Nitaitaja miwili ya hivi karibuni ambayo wengi mtakuwa mnaikumbuka.

Baada ya kuingia madarakani, Rais Magufuli alipiga marufuku watu kufanya shughuli za kisiasa kwa kisingizio kwamba ‘siasa sasa zimeshaisha na ni wakati wa kufanya kazi’. Hiyo ni licha ya kwamba shughuli hizo ni haki za kikatiba kwa Mtanzania yeyote yule.

Baada ya Rais Magufuli kufariki, baadhi ya wajuzi na wajuvi wa mambo ya katiba walituambia kwamba Rais Samia alipaswa kulivunja baraza la mawaziri na kuunda serikali mpya.

Hilo halikufanyika. Hivyo maana yake ni kwamba naye aliikiuka katiba.

Sasa nimewaza: kama hii katiba iliyopo inakiukwa wazi wazi namna hii na hamna lolote la maana linalofanyika kupinga ukiukwaji huo, hiyo katiba mpya inahitajika ili iweje?

Mara karibu zote ambapo katiba imeonekana kukiukwa, hakuna cha maana ambacho wananchi tumefanya zaidi ya kujimwambafy humu kwenye mitandao.

Hakuna aliyethubutu kuingia barabarani na kupinga. Hakuna aliyefungua kesi mahakamani. Tumelia lia tu humu mitandaoni.

Sasa hiyo katiba mpya tukiipata, ikikiukwa ndo itatuwezesha kupata ujasiri wa kupinga kukiukwa kwake?

Nimeanza kudhani pengine tatizo letu si katiba mpya pekee. Tatizo letu kubwa ni sisi wenyewe. Tunaachia tu mambo yaende hata kama yapo kinyume na katiba.

A new constitution will not be worth the paper it’s written on if we allow and let the one we have to be breached with impunity!
Bado sijaelewa logic ya hoja yako!

Kwamba kama ulikuwa unalala nyumba inayovuja hutakiwi kukarabati kwa sababu nayo itakuja kuvuja!
 
Bado sijaelewa logic ya hoja yako!

Kwamba kama ulikuwa unalala nyumba inayovuja hutakiwi kukarabati kwa sababu nayo itakuja kuvuja!
Katiba siyo nyumba!

Si ajabu ndo maana hujaelewa!!!!
 
Ok!

Vipi kuhusu kutokufanya siasa kwa vyama vya upinzani?
Mwaka jana Mahakama ya Afrika ilitoa ruling kuwa kuzuia watu kupinga matokeo ya kura za urais ni kuvunja Katiba na hivyo watu waruhusiwe. Kilichofuata ni kutangaziwa kuwa hakuna ruksa kwenda kwenye Mahakama ya Afrika na kuwa Tanzania ina nia ya kujitoa kwenye hiyo Mahakama!

Amandla...
 
Mwaka jana Mahakama ya Afrika ilitoa ruling kuwa kuzuia watu kupinga matokeo ya kura za urais ni kuvunja Katiba na hivyo watu waruhusiwe. Kilichofuata ni kutangaziwa kuwa hakuna ruksa kwenda kwenye Mahakama ya Afrika na kuwa Tanzania ina nia ya kujitoa kwenye hiyo Mahakama!

Amandla...
Ulichojibu sicho nilichokuuliza!
 
Back
Top Bottom