We zombie......Akirudi ana kuta barua mezani ya uhamisho kwenda swekeni kama sio tukuyu Au huko nkasi basi mabamba mpakani na burundi [emoji23][emoji23][emoji23]
Huyo inatakiwa wasiishie hapo, awe mfano kwa wengine wenye tabia kama zake.Huyu Sio kama hajui, ameamua kujifukuzisha kazi analijua hilo, na hata hao viongozi wanajua,
Issues ni kwamba Jee wataishia hapo?
Ni mengi ajabuCWT kuna maokoto acheni utani 🤠🤠
Wameamua kumkomalia kisa kukataa teuzi,sio kila mtu ni mtumwa wa teuzi,waache ushamba.
Hili ni tatizo kubwa na athari zake zinakwenda mbali sana. Maisha ya aina hii hayatoi genuine competition au ku-reward watu kulingana na uchapakazi wao badala yake wanafiki, walaghai na waongo ndiyo wanapendwa na watawala na kuwa rewarded handsomely.Unaweza ukafanya ujinga mdogo kwenye maisha na ukakukomoa!
Maisha ya Bongo ni unafki ili uendelee
Ni mpuuzi, anadhani kama alikua na ubabe wake kwa waliokua chini yake ndio utafanya kazi kila sehemu??Huyo inatakiwa wasiishie hapo, awe mfano kwa wengine wenye tabia kama zake.
😂😂We zombie......
Tukuyu ni town sana aje tu tutampokea na stick za kugomea mamlaka
Maganga. Kagangamala ngosha ze doni hataki ujingaHalmashauri ya Manispaa ya Temeke imeanza mchakato wa kufungua shauri la nidhamu dhidi ya Katibu Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Japhet Maganga baada ya kutorejea katika kituo chake cha kazi tangu alipotakiwa kufanya hivyo Oktoba Mosi mwaka huu.
Maganga ambaye cheo chake ni Mwalimu Mwandamizi katika Manispaa ya Temeke, aliomba kibali cha kuazimwa kuitumikia CWT Agosti 2017 hadi Septemba 30, 2020, akaomba tena Juni 1, 2020 na kumalizika Septemba 30, 2023, na baadaye aliomba kibali hicho kwa mara ya tatu lakini Katibu Mkuu UTUMISHI hakuridhia maombi hayo na kumtaka kurejea kwenye kituo chake cha kazi cha awali.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke, Elihuruma Mabelya amesema Maganga ni mtumishi wa Temeke na alitakiwa kuripoti kazini kama alivyotakiwa katika tangazo la wito, lakini hadi sasa hajaripoti, hivyo kinachofanyika ni kuchukua hatua za kinidhamu dhidi yake.
"Yule ni mtumishi wa Serikali hapaswi kuigomea Serikali, sisi tunachojua yeye ni mtumishi wetu, kule aliko kibali kimeisha sio tena sehemu yake ya kazi, amesema.
Maganga alichaguliwa Desemba 2022 na Mkutano Mkuu wa CWT kuwa Katibu Mkuu akichukua nafasi ya Deus Seif
ambapo awali alikwa akitumikia nafasi ya Naibu Katibu Mkuu.
Mnamo Januari 25, mwaka huu, Maganga, Makamu wa Rais wa CWT, Dinna Mathaman na Rais wa CWT, Leah Ulaya waliteuliwa na Rais Samia Suluhu kuwa Wakuu wa Wilaya lakini Maganga na Mathaman hawakufika kuapa.
Swahili Times.
Pia soma:
Waalimu bhanaa wanamlipa katibu wao mil 7 wao wanakula vihela mbuziiii...!! Jamaa kashajipanga hata kama akifukuzwa kazi sawa tu shida kama wataenda kwenye biashara zake na mali zake binafsi.Ni mpuuzi, anadhani kama alikua na ubabe wake kwa waliokua chini yake ndio utafanya kazi kila sehemu??
Kwa namna yoyote hii game haitaisha vizuri upande wake...
Kuiba kaiba, haina ubishi, anachotafta ni kufukuliwa makaburi..
Lakini hata wakiamua wamkomeshe kibabe pia hawashindi.
Walimkomaliaje?Nazani spika Perosi kama sijakosea jina lake alimkomalia trump na yeye wakaja kumkomalia...!
Ndio mambo yanavyo kuwa
Hivi alikua anakula M7? Huyu kwa ufupi amejitosheleza,Waalimu bhanaa wanamlipa katibu wao mil 7 wao wanakula vihela mbuziiii...!! Jamaa kashajipanga hata kama akifukuzwa kazi sawa tu shida kama wataenda kwenye biashara zake na mali zake binafsi.
Mbona huyo Dinna waliyegoma naye kwenda kuapishwa yeye haadhibiwi? Hii ni double standard. Nchi ya kipuuzi sana hii inayopenda kulipiza kisasi ndio maana imelaaniwa kwa sababu za kishetani kama hizi.Mnamo Januari 25, mwaka huu, Maganga, Makamu wa Rais wa CWT, Dinna Mathaman na Rais wa CWT, Leah Ulaya waliteuliwa na Rais Samia Suluhu kuwa Wakuu wa Wilaya lakini Maganga na Mathaman hawakufika kuapa.
Mimi nashangaa. Ni hatua gani za kinidhamu wanataka kumchukulia? Mbona sheria ikpo wazi mtu asiporipoti kazini kwa siku 3 mfululizo anakuwa amejiachisha kazi yeye mwenyewe? Wanataka kumfunga jela au wanamtafutia sababu ya uhujumu uchumi wa CWT wamfunge jela za wahujumu uchumi?Hivi alikua anakula M7? Huyu kwa ufupi amejitosheleza,
Yeye Angefuata taratibu tuu za kuomba hata kustaafu, atemane nao..
Kosa alilofanya kihalisia adhabu yake ni kuachishwa kazi tuu, ila kwakua juu wanajua huyu kazi sio tena kipaombele chake, na hua wanapenda kuhakikisha maamuzi yao yanakuumiza, hapa ndio watamfuta nje ya hapo sasa.
Sheria ziko wazi. Mtumishi asipoenda kazini kwa siku 3 mfululizo bila ruhusa anakuwa amejifuta kazi. Huyu hajaenda kazini tangu oktoba mosi halafu anahesabika kuwa ni mtumishi wewe huoni kwamba hapo kuna tatizo? Kuna mahali naye anamtega mwajiri amle kichwa. Tutasikia mengi.Huyo achunguzwe, hawezi kuwa na kiburi cha kiwango hicho kama hajapiga pesa nyingi za CWT.
Maswahili akipata...
Sasa akama amekataa uteuzi kwa sababu hiyo na amegoma kwenda kazini adhabu yake auawe au afukuzwe kazi? Hebu tuambie sheria za kazi zinasemaje? Kutorudi kazini kwa mujibu wa sheria kuna uhusiano gani na ung'ombe wake na maokoto ya CWT?Ungechunguza kujua sababu ya kugomea uteuzi ungegundua kumbe naye ni Ng'ombe tu sio kichwa kama unavyodhani.
Sababu ni hiyo nafasi aliyokuwepo kwa muda anaingiza okoto la uhakika zaidi kuliko kwenye UDC alikotakiwa kwenda,uliza mwalimu yeyote.