Katibu wa Tume ya Utumishi wa walimu adai walimu ndio wanalipwa mishahara mizuri kuliko mtumishi yeyote Serikalini

Qnet pesa ipo hukuuu njooni msikieee
 
Ulipaji wa mishahara ya serikali pia inategemea chuoni ulisoma miaka mingapi.
Haiwezekani mwalimu aliyesoma miaka mitatu alipwe sawa na mwanasheria au daktari aliyesoma miaka mitano hilo pia lazima tujue.

Tatizo la mishahara midogo sanasana liko kwa watumishi waliopo Tamisemi sababu chukulia walimu wote mmesoma kozi moja miaka mitatu lakini mwenzako akipangwa vyuo vya ualimu (ambavyo viko wizara ya elimu) anakuzidi daraja moja yeye anaanza na E wewe D.

Watu pia wanachanganya serikali kuu na mashirika ya umma ambayo yanajipangia mishahara yenyewe. Ila kwa mtumishi aliyesoma chuoni miaka mitatu siku wanaajiriwa mwalimu anakuwa na mshahara mkubwa zaidi ndicho alichomaanisha katibu. Kwa hiyo shida ni kwamba mishahara ya watumishi wote ni kidogo kwa ujumla wachache Sana Wana nafuu.
 
Hakuna mtumishi anayelipwa mshahara mkubwa serikalini
Daktari, mwalimu, mhasibu, mhandisi nk wote wanalipwa hela ya kujikimu tu
 
Wewe ni mpotoshashaji, achana na muda wa kusoma chuoni. Chukulia mfano uhasibu kozi ya miaka mitatu, na uwalimu kozi ya miaka mitatu level ya degree mishahara ni tofauti. Tatizo la mishahara kwa watumishi wa umma ni ubaguzi level moja na nyingine ingawa level ya elimu ni ileile. Kiufupi huyu katibu kadanganya
 
Fikiria kabla ya kuandika, wakipiga chini ukoo wako utaingia madarasani?? Siku walimu wataamua kugoma ndiyo mtaujua umuhimu wao!!
Mkuu wewe kumbe Mwalimu mambo ya dollar na wewe wapi na wapi

 
Kuna mwalimu (sitaki kusema kama nilimwajiri) ila tulikuwa tunaganga njaa pamoja, juzi kaja likizo ananiambia amini usiamini braza nilipokuwa kwako nilikuwa napata hela nyingi kuliko nilivyoajiriwa, sema tu kule huwa napata ya pamoja na kwako nilikuwa napata kila siku.
Nilitaka nisimwamini ila nililazimika kumwamini kwa sababu hakuwahi kunidanganya hata siku moja alipokuwa pamoja nami.
 
Watumishi wowote wawe wa umma au wa sekta binafsi kwa nchi yetu hawawezi ishi kwa mshahara tu. Kwanza kodi (PAYE) ni kubwa sana kulinganisha na nchi zingine, kwa mantiki hiyo watumishi wanategemea posho(allowances) mbalimbali kulingana na mikataba na sheria za watumishi.

Walimu scales zao za mishahara (TGTS) ni tofauti na baadhi ya scales hasa TGS. Hata hivyo mwalimu halipwi posho yoyote ingawa anafanya kazi zaidi ya masaa 8 ambayo ndiyo masaa halali ya kufanya kazi kwa siku. Posho huwa hazikatwi kodi hivyo kuwapa unafuu kada zingine. Nimeshuhudia baadhi ya walimu wakijishughulisha na kazi ya kuendesha pikipiki (bodaboda) huku akiendelea na kazi yake ya ualimu.

Yuko darasani anafundisha akipigiwa simu na mteja anaacha chaki ubaoni anatoa excuse kwa wanafunzi kuwa kuna mtu amwone mara moja kumbe aenda piga boda halafu arudi baadae. Hii yote ni ili aweze kujikimu. Ni ukweli usiopingika kuwa ualimu sio deal kihivyo, vinginevyo watu wengi wangefanya juu chini wawe walimu kama vile wanavyofanya juu chini wafanye kazi hazina au TRA.
 
Kama una akili, usimsomeshe mwanao aje awe mwalimu, utanishukuru baadae.
 
Ni uoga au unafiki unamfanya asiseme kweli iliyo moyoni mwake. Hyati mwl.J.K Nyerere alitofautisha UJINGA na UPUMBAVU.
 
Kwahiyo Rais mawaziri, wabunge, wakurugenzi, wakuu wa mikoa, wilaya nk wanalipwa chini ya Laki 7?!
 
Kwani muhasibu anayeanza ka Kwani muhasibu anayeanza kazi halmashauri anaanza na shilingi ngapi?
 
Ni kweli wanapata mishahara mikubwa ukiweka effective hours of work (masaa ya kazi) wanayofanya kwa mwaka toa siku shule zimefungwa n.k
Kuna ndugu yangu Mwalimu alinieleza hivyo hivyo
 
Na mainjini unawaweka wapi mkuu?
 
Hiyo nafasi si amepewa kama peremende na bwana yule? Unataka aongee kinyume na bosi wake kesho ajikute jalalani?
 
Moja ya vigezo vinavyotumika kupanga mishahara serikalini ni degree yako umesoma miaka mingapi(kwa kesi ya degree). Mwalimu anasoma miaka mitatu, mshahara wake utaanza chini kulinganisha na mhandisi anayesoma miaka minne. Vivyo hivyo mhandisi atakua chini kulinganisha na daktari anayesoma miaka mitano. Pamoja na hayo yote mishahara ni midogo ukizingatia kazi kubwa inayofanywa na waalimu. Kazi ya walimu ni pamoja na kuisaidia CCM kushinda kila uchaguzi.
 
Huyu ameongelea kwa watumishi wa halmashauri na wizarani tu.
1. Mwalimu wa degree TGTS D1 = 716,000/=
2. Watumishi wengine wenye degree za miaka mitatu ukiondoa kilimo na computer ni TGS D1 = 710,000/=
Tofauti ni 6,000/= Hivyo mwalimu yuko juu.
ILA SASA:
Ukienda huko kwenye taasisi, mamlaka, wakala na mashirika huko ndio mwalimu hatii pua anaweza kukimbizwa hata na mpishi au mlinzi.
Hawa mishahara yao unakula kwa urefu wa kamba yako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…