Katika msitu mnene, ulikuwa ukikusanya miti kwa ajili ya kujenga makazi yako. Jua lilikuwa linachoma kwa nguvu, na baada ya siku ndefu ya kazi, mwili wako ulianza kuchoka. Ukajikunyata chini ya mti mkubwa na kusingizia kidogo kabla ya kuzama kwenye usingizi mzito.
View attachment 3253472
Ulipoamka, ulijikuta upo peke yako, huku jua likionekana kuanza kuzama. Ulipotazama pembeni yako, macho yako yalikutana na maajabu – kulikuwa na chui mmoja aliyejilaza karibu nawe, akiwa amelala pia.
Je utajinasua vipi kutoka kwenye hii changamoto, utaendelea kuuchapa usingizi, ama utaamka na kukimbia?