Siku ya ya jana tarehe 13 Machi 2025 ITV walikuwa wakirusha matangazo mbashara kipindi cha malumbano ya hoja mada ikiwa
'kutofanyika kwa dabi ya Simba na Yanga nini kifanyike?'.
Wakati kipindi kinaendelea akakaribishwa
mchangiaji mmoja akijulikana kwa jina la Ramadhan Kampira, Mwenyekiti wa wachezaji wa zamani wa Yanga ambaye kabla hajaanza kuzungumza
akawaomba watangazaji na wachangiaji wengine wasimame kwa dakika 1 kumuombea Rais Samia.
Niliona
watangazaji wakabaki kwenye Dilema na baadae wakaamua kusimama, katikati ya maombi
mtangzaji mmoja akashindwa kujizuia akatoa kicheko.
Kujipendekeza, uchawa vimetamalaki kila kona mpaka vinakua sugu.
Pia soma:
Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
View attachment 3270118