Kauli hii ya Kardinal Pengo,inatukumbusha "upande wa pili" wa Kanisa Katoliki

Kauli hii ya Kardinal Pengo,inatukumbusha "upande wa pili" wa Kanisa Katoliki

Mkuu Barafu, kuna kitu mhashamu Polycarp Pengo anakifanya nacho ni kuweka mjadala.

Moja ya sifa za mhashamu Pengo ni kwamba yeye ni mwanachama wa kitu kinaitwa kwa kiingereza "interreligious dialogue".

Yaani anaweza kuongea kitu mahali fulani kwa minajili ya kuanzisha mjadala baina ya jamii mbalimbali na yeye kubakia akifuatilia matokeo.

Hii ni sifa kuu kabisa ya matunda ya wanafunzi wa Vatican.
Hakika nimeamini hili jukwaa raia wapo vizuri ktk kuchambua mijadala inayoletwa hapa,big up[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
Acha porojo, toa mifano ya mikutano iliyohamishiwa kurasini kama una uhakika. Kuvuka malengo ya makusanyo inatokana na waumini kujitolea maana hata mimi naenda kanisani, wanaposoma kwa mfano mavuno ya mwaka 2016 wanalinganisha na 2015 ambapo unaweza hali ya baadhi ya jumuia kupanda na nyingine kushuka overall kijimbo ndiyo hayo mazidi. Usijaribia kuongea bila data.
Nenda TEC na Msimbazi miezi ya 5 6 tu 2016.

Halafu ni upumbavu kuanzia hoja kwa kumsingizia mtu na "porojo" baadae unadai ushahidi. Nimekupa ushahidi mpelekee Pengo na jpm.

Hii ni forum ya intelijensia porojo Lumumba.
 
Mkubwa hakoseagi..!

statement ya Polycarp Pengo hajaitoa kwa bahati mbaya.
 
Mkuu Barafu, kuna kitu mhashamu Polycarp Pengo anakifanya nacho ni kuweka mjadala.

Moja ya sifa za mhashamu Pengo ni kwamba yeye ni mwanachama wa kitu kinaitwa kwa kiingereza "interreligious dialogue".

Yaani anaweza kuongea kitu mahali fulani kwa minajili ya kuanzisha mjadala baina ya jamii mbalimbali na yeye kubakia akifuatilia matokeo.

Hii ni sifa kuu kabisa ya matunda ya wanafunzi wa Vatican.
Uliona ile kauli yake ilikua ni ya kuweka mjadala au ilikua"CONCLUSIVE",aisee matunda ya vatican nimeyakubali kabisaa.
 
Amesababisha mijadala kama huu tuufanyao hapa.
Sawasawa hata
* Lusekelo alisababisha Mijadala humu kwa ulevi wake.
*Gwajima alisababisha Mjadala humu kwa mahusiano yake na flora.
*Kuna Mapafri/askofu wamesababisha mijadala humu kwa scandal ya kulawiti watoto.
*Jana askofu Shoo amesababisha mijadala humu kwa kwa kusema hali huku uraini ni tete hakuna ajira.
So hakum mjadala wa maana Pengo aliouleta.
 
Nenda TEC na Msimbazi miezi ya 5 6 tu 2016.

Halafu ni upumbavu kuanzia hoja kwa kumsingizia mtu na "porojo" baadae unadai ushahidi. Nimekupa ushahidi mpelekee Pengo na jpm.

Hii ni forum ya intelijensia porojo Lumumba.

Aisee wewe ni jingalao, kwa taarifa yako pale TEC na Msimbazi ndiyo shughuli za kanisa hasa za jimbo kuu zinafanyikia na hata kanisa la tanzania kama kunahaja ya kukutana. Kwahiyo maeneo hayo kujaa siyo kwasababu ya matumizi ya serikali. Vilevile wakati wa mitihani ya bodi mfn PSPTB NA NBBA (kabla hawajajenga bunju) walikuwa wanafanyia mitihani pale hasa May na October na hii ni kwasababu pale TEC ndiyo sehemu unaweza kupata kumbi na malazi kwa wanaotoka mbali. Tatizo unaongozwa na siasa zilizojaa chuki dhidi ya Rais, Pengo na Kanisa kwa ujumla wake. HALAFU UNADHANI KILA MTU ANAYESEMA KINYUME NA WEWE NI MWANA LUMUMBA? JINGA KWELI
 
Aisee wewe ni jingalao, kwa taarifa yako pale TEC na Msimbazi ndiyo shughuli za kanisa hasa za jimbo kuu zinafanyikia na hata kanisa la tanzania kama kunahaja ya kukutana. Kwahiyo maeneo hayo kujaa siyo kwasababu ya matumizi ya serikali. Vilevile wakati wa mitihani ya bodi mfn PSPTB NA NBBA (kabla hawajajenga bunju) walikuwa wanafanyia mitihani pale hasa May na October na hii ni kwasababu pale TEC ndiyo sehemu unaweza kupata kumbi na malazi kwa wanaotoka mbali. Tatizo unaongozwa na siasa zilizojaa chuki dhidi ya Rais, Pengo na Kanisa kwa ujumla wake. HALAFU UNADHANI KILA MTU ANAYESEMA KINYUME NA WEWE NI MWANA LUMUMBA? JINGA KWELI
Matusi ni ushahidi wa kukosa hoja.

Lete orodha nzima ya mikutano ya miezi hiyo niliyokutajia kama mfano.

Siyo siri awamu hii na kanisa katoliki kupitia Pengo wamechemsha. Kama wewe huoni hivyo mimi nimekutaka ulete orodha ya mikutano ya miezi hiyo miwili kama mfano. Ukitaka na mengine utapewa ukijitia unajua sana mambo ya kanisa katoliki wengine tumo ndani. Ni kweli jpm anachukiwa sana kama hujui; ila kwa tunaomfahamu na magonjwa yake tuliwaonya tulisema na hatushangai na huu ni mwanzo tu.
 
Matusi ni ushahidi wa kukosa hoja.

Lete orodha nzima ya mikutano ya miezi hiyo niliyokutajia kama mfano.

Siyo siri awamu hii na kanisa katoliki kupitia Pengo wamechemsha. Kama wewe huoni hivyo mimi nimekutaka ulete orodha ya mikutano ya miezi hiyo miwili kama mfano. Ukitaka na mengine utapewa ukijitia unajua sana mambo ya kanisa katoliki wengine tumo ndani. Ni kweli jpm anachukiwa sana kama hujui; ila kwa tunaomfahamu na magonjwa yake tuliwaonya tulisema na hatushangai na huu ni mwanzo tu.

Hivi mwenye kuleta ushahidi ni mimi au wewe uliyesema baada ya serikali kukataza mikutano ya taasisi za serikali kufanyika kwenye mahoteli, yalihamishiwa TEC na MSIMBAZI?, Nilikuomba utaje hata vikao viwili vilivyofanyika huko ukambwela, mimi najua misururu ya matukio yanayofanyika TEC na MSIMBAZI, unajidai uko ndani ya kanisa halafu hujui lolote unabishana hata na watu usiyowajua. Mimi c tu kwamba niko ndani ya kanisa ila kila mwezi hapo TEC na msimbazi centre sikosi kufika walau mara nne au tano. TEC naijua kiundani na kazi zake pamoja na vikao na utaratibu wake, wewe utabaki kuongea siasa uchwara na chuki zako kwa Rais pamoja na Pengo.UNADAI PENGO KUSEMA HELA HAZIJAPOTEA NI KOSA, KWANI WEWE MSHAHARA WAKO UMEPUNGUZWA BAADA YA JPM KUINGIA MADARAKANI?, KAMA ULIZOEA PESA ZA RUSHWA, SEMINA UCHWARA, 10%ZA MIRADI, KUHONGWA NA WEZI WA PESA ZA UMMA, SAFARI ZA HOVYO BASI KWELI PESA IMEPOTEA KWAKO.
 
Hivi mwenye kuleta ushahidi ni mimi au wewe uliyesema baada ya serikali kukataza mikutano ya taasisi za serikali kufanyika kwenye mahoteli, yalihamishiwa TEC na MSIMBAZI?, Nilikuomba utaje hata vikao viwili vilivyofanyika huko ukambwela, mimi najua misururu ya matukio yanayofanyika TEC na MSIMBAZI, unajidai uko ndani ya kanisa halafu hujui lolote unabishana hata na watu usiyowajua. Mimi c tu kwamba niko ndani ya kanisa ila kila mwezi hapo TEC na msimbazi centre sikosi kufika walau mara nne au tano. TEC naijua kiundani na kazi zake pamoja na vikao na utaratibu wake, wewe utabaki kuongea siasa uchwara na chuki zako kwa Rais pamoja na Pengo.UNADAI PENGO KUSEMA HELA HAZIJAPOTEA NI KOSA, KWANI WEWE MSHAHARA WAKO UMEPUNGUZWA BAADA YA JPM KUINGIA MADARAKANI?, KAMA ULIZOEA PESA ZA RUSHWA, SEMINA UCHWARA, 10%ZA MIRADI, KUHONGWA NA WEZI WA PESA ZA UMMA, SAFARI ZA HOVYO BASI KWELI PESA IMEPOTEA KWAKO.
Ahsante
 
Mimi mwenyewe sijaamini kama kusema hivyo alikuwa amedhamiria,, inawezekana maneno yalimtoka bahati mbaya.. ila hata kipindi fulani maaskofu walitoa waraka juu ya katiba mpya, ila yeye akaja kupingana nao.. Mungu atusaidie sana..
Hapa kuna kitu nimejifunza!

"Mfumo"
 
Watu wametweta,wamekasirika na wengine wamefura kwa maneno mazitomazito kwa kauli ya Mwadhama P. Kardinal Pengo.Yeye Pengo kama baba wa kiroho na kiongozi wa waumini wa kanisa katoliki jimbo la Dsm hakubaliani na kauli kuwa sasa "Hela imekuwa adimu mifukoni" na sasa "maisha yamekuwa magumu tilatila".

Mbele ya mimbari ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Joseph,baba mlishi wa Yesu Kristo,fundi selemala wa Nazareth,Kardinali Pengo anapiga msumari wa moto ktk mioyo ya waumini wake.Waumini walioanza kukata tamaa na kutegemea maneno ya faraja toka kwa baba wa kiroho,wanakutana na kauli ngumungumu zinazowaumiza.

Pengine wale "waumini rasharasha" wameanza kunung'unika,wanasononeka kwa taharuki,wanajiuliza,kama huyu tuliomtegemea atusemee,mbona anatukatisha tamaa na kutokuwa upande wetu?Inastua...lkn inakatisha tamaa,pale ambapo wengi tunaongea lugha moja ya "hela imekuwa adimu",mwingine anasema "hela inazagaa",na hata akiitisha harambee,anavuka malengo ya kile alichokusudia kukusanya.

Na hii inawastua wengi,sababu siku moja kabla ya kauli hiyo,kuna watu walitembelewa nyumbani kwao.Dhumuni la ujio wa ugeni ilikuwa ni "kutoa pole ya msiba".Na hakika si tu pole,baada ya pole huwa na habari za mengineyo,hayo mengineyo hubaki kuwa siri ya mfiwa na mfariji.Waunganisha matukio wanaweza kuunganisha hizi kauli na ujio wa "kutoa pole".Na wakishaunganisha,basi wanarudi nyuma katika maandishi ya kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed"

Wakati wa utawala wa Kifashisti kule Italia,Mussolini aliona tishio la Kanisa Katoliki ktk kufikia malengo yake.Maana kwa wakati ule,kanisa lilikuwa na "kontroo "ya maisha ya kiroho na serikali ilikuwa na "kontroo" ya maisha ya kisiasa.

Alichokifanya Mussolin ni kujipendekeza kwa kanisa na kutoa "rushwa" ili yote atakayoyafanya kanisa katoliki lililokuwa na nguvu sana Italia libaki kimyaa.Alifanikiwa...

Kwanza aliamua kumbatiza mwanae wa kiume,ambaye hapo awali hakuwa amebatizwa.Hapa akaliteka kanisa kwa karata ya kwanza.

Pili alimua kufunga ndoa ya kikanisa,baada ya kuwa amekaa miaka 11 na ndoa ya "bomani" na mkewe Rachele.Hii ikawa karata ya pili ya kujisogeza na kujiweka karibu na kanisa ili kutimiza malengo yake ya ufashisti.

Karata nyingine;aliamuru kufungwa kwa maduka yote ya vileo(wine shops) na kufuta leseni za clabu zote za usiku ili kuendana na kauli ya kanisa ya kupunguza uovu mitaani kwa ulevi na anasa za usiku.Hapa kanisa katoliki likanasa mtegoni.

Alienda mbali mpaka akatangaza kuwa "Public Swearing" kama "Public Crime"...Yaani mwananchi ukiwa mtaani umnabishana,mtu akikwambia sema haki ya Mungu...Ukisema tu "Haki ya Mungu ntayafunga majizi yote,msema kweli ni mpenzi wa Mungu".Basi ujue wewe una kesi ya jinai ya kujibu.Hapa alitaka kulifurahisha kanisa kwa amri ile ya "Usitaje bure jina la bwana Mungu wako"(Kwa hiyo amri hiyo ingekuwa enzi hizi,kuna mtu angekuwa jela zamaniii(kidding))

Mussolini akaamuru kupigwa marufuku vidonge vya majira na kampeni zote za matumizi ya uzazi wa mpango kama ulivyo msimamo wa kanisa.Wakati huo wa 1920's kanisa lilitaka wanawake wabaki nyumbani ili kulea watoto na kukuza familia vyema.Mussolini akalipigia chapuo hili na kulitungia sheria ili kuwafurahisha wazee wa kanisa.

Akatunga sheria ambayo ilifutilia mbali talaka kwa ndoa hata za bomani.Hii ilikuwa ni njia ya kuungana na kanisa ktk ndoa ya mke mmoja na isiyo na talaka mpaka Mungu awatenganishe.Ndoana hii ikanasa vizuri kwa kanisa.Hawakupepesuka wala kutikisika.Mambo yote ya ndoa yakaondolewa serikalini na kubaki kuwa in "Full Control of the Catholic Church".Wale wapenda mteremko wa ndoa za bomani wakakosa pa kwenda.

Akatoa 109 acres ktk mji wa Roma ili yajengwe makao makuu ya Papa(Vatican) baada ya kuwa yalipokonywa wakati wa "Unification of Italy" ya miaka ya 1870's,na akaamuru kanisa lilipwe zaidi ya £130 milioni kwa wakati ule.Hii ilikuwa ni ndoano iliyoingia sawasawa kwa kanisa,na kanisa halikusema lolote juu ya "ufashisti" wa Mussolini hadharani;japo liliouona na kuuhisi kwake na kwa waumini wake.

Vatican ikawa nchi ndani ya mji,wakapewa mamlaka juu ya Post Office,jeshi dogo,polisi na "Rail station".Baada ya hapo,ugomvi ukawa ni nani anatakiwa "kukontrol" Elimu?Mussolini alihitaji elimu ili apandikize "ufashist" kwa watoto,na kanisa lilitaka elimu ili kupandikiza "dini" kwa watoto.

Mambo haya yote ambayo baadae,waumini wasio "rasharasha" waliona ni kama "rushwa" kwa kanisa ili liweze kusifia na kukaa kimya juu ya "serikali ya kifashisti" ya Mussolin yalifanikiwa.Si ajabu Papa John Paul II alikuja kuiomba jumuiya ya waumini na wasio waumini ktk jubilei ya miaka 2000 ya Ukristo kwa yale yote kanisa iliyoyakosea ktk kukuwa kwake.

Hakukuwa na Kardinali,askofu wala kasisi(padre) aliyeikemea serikali isiyo ya kidemokarasia ya Utawala wa Mussolini.Mengi yalitokea na kanisa lilikaa kimyaaa.Waumini waliteseka,waliumia na walipata machungu ya maisha...Lakini kanisa lilisema "hewalaaa",huu ni utawala mzuri tu,maana "umerudisha" heshima ya Papa katika nchi ya Italia.

Hatumaanishi kuwa sasa Tanzania tuna "ufashisti",lakini tunakubaliana kuwa kwa sasa Tanzania maisha ni magumu,pesa imepotea na uchumi umenyambulika na kutikisika.Hii inaweza kuwa ni matokeo ya kipindi cha mpito kuelekea uchumi wa viwanda,lakini haiwezi kuwa sababu ya kutokusema ukweli kuwa "HALI NI NGUMU"

Kama hali hii ni kwa sababu mianya yote ya wapiga dili imefunikwa basi na tusema,na sio kusema kinyume chake.Kuwa baba wa kiroho na kuongea kinyume cha yale waumini wako ambao ni sehemu ya wananchi wa Tanzania wanalalamika,ni kuwa upande wa pili badala ya ule wa waumini wako.

Ndio maana wale wanafunzi wa historia ya kale,wanaweza kustuka.Kwamba kauli hii inakuja siku kadhaa baada ya mtu kutembelewa nyumbani kwake,inaweza kuwatia watu woga.Kanisa libaki kuwa mali ya waumini wanyonge,liachane na "urafiki" wa mashaka kama ule wa "Mussolini" na "Vatican" enzi hizo za zama za giza za Ulaya.

Kama kanisa la wakati huo lilibaki kimya juu ya "ufashisti" wa Benitho Mussolini,hili la kwetu la Tanzania,lisibaki kimya juu ya "Ugumu wa maisha na hali mbaya ya Uchumi" kwa waumini wake.Kutoa kauli za aina hii hadharani,mbele ya mimbari na katika altare takatifu,inatupa mashaka na tutaamua kurudi na kupekua kurasa za kitabu cha "How The Church and Government Got The Same Bed"

Tukizifunua kurasa hizi;Tutahitimisha kwa kusema "Pengo ameongea lile alilotumwa kuongea na sio alilojituma kulitumikia"

Tutamkumbusha Pengo kuwa kuutumikia mwili ni ghalama zaidi ya kuitumikia roho.Ndio maana Lugha Mama ya Kanisa ya Kilatini ikasema "Nemo Liber Est Qui Corpori Servit"(No One is Free who is a slave of his body)

Tuitumikie Roho inayodumu milele,kuliko mwili unaooza na kuliwa na nyenyere.
Nchi ipo katika kipindi kigumu sana nani hatari sana kwa mtu credible kama yeye kuongea vitu km hivyo ila naamini hata mji wa mwizi waweza ibiwa pia vivyo hivyo hata viongozi wetu wa membalini na altare wanaweza pitiwa na shetani huko huko membalini na altareni kama waumini wengine wapitiwavyo na shetani
 
Haitoshi kumjibu ahsante badala ya kuleta mifano ya mikutano/semina za serikali zilizofanyika ktk hizo kumbi za kanisa katoliki, tuwekee na tarehe za tukio. Tuhuma nzito namna hii hazipaswi kujibiwa kwa jibu jepesi kama hilo. Lete mifano mitano tu. Vinginevyo utakuwa mtu mwongo, mropokaji na mchochezi hatari kabisa ktk taifa lenye mchanganyiko wa dini. Unachonganisha ili watu wakachome moto mali za kanisa katoliki sababu ya hasira?
 
image.jpeg

umenikumbusha kitabu nilichokisoma zamani kidogo: Priests and Politicians:The Mafias of the Soul!
Kimeandikwa na Osho!
Kitabu iki kinaongelewa "ndoa" ya Serikali na Kanisa ktk Kutawala Wananchi!
Mkuu ongezea na hivi...Jaribu kuvitafuta;au nikipata wasaa huku nilipo nitakununulia ila uwe tayari tu "kurefund"....Ukisoma hivi,si tu utajielimisha,bali pia imani yako itakuwa,na hutaiegemeza kwa mtu(binadamu/Kiongozi wa dini).

Bali imani yako itaidumisha ktk Kanisa moja,katoliki la mitume...Ambalo lenyewe litaendelea kuwepo na hawa wengine watakuja na kupita.Maana tuliambiwa...Hili ndio Kanisa alilokabidhiwa Petro,na baadae akawaachia makhalifa wake,ambao ndio hao Mapapa...
image.jpeg
 
Haitoshi kumjibu ahsante badala ya kuleta mifano ya mikutano/semina za serikali zilizofanyika ktk hizo kumbi za kanisa katoliki, tuwekee na tarehe za tukio. Tuhuma nzito namna hii hazipaswi kujibiwa kwa jibu jepesi kama hilo. Lete mifano mitano tu. Vinginevyo utakuwa mtu mwongo, mropokaji na mchochezi hatari kabisa ktk taifa lenye mchanganyiko wa dini. Unachonganisha ili watu wakachome moto mali za kanisa katoliki sababu ya hasira?
Sibishani na wajinga kama mna uhakika siyo kweli na mimi nina uhakika ni kweli hatuna namna ya kuelewana. Halafu lugha za kishari zinawafaa nyinyi tu. Hamnipati na hambadirishi ukweli. Nina imani mnajua mnachokitetea. Na mimi siyumbi kwa nilichoshudia kwa macho yangu.
 
Mleta mada hii hakujikita ktk hoja za kwamba serikali inaipendelea kanisa katoliki ila kama nimemwelewa amejikita ktk kauli ya Kadinali Pengo jinsi inavyoweza kumsababishia Mh.Raisi akawa complacent kuhusu hali halisi ya kiuchumi au mzunguko wa fedha kwa watu wengi. Pia kumpa angalizo mheshimiwa Pengo kwamba kazi yake ya msingi ni kuwatetea wanyonge na kulinda kiimani au kiroho. Hapaswi kuitetea serikali kiasi cha kuipa upofu ikajisahau wajibu wake kwa umma hasa mambo ya kiuchumi(malazi, chakula, elimu) ambayo hutegemea hali ya uchumi wa mtu husika. Ila kwa hali iliyopo changamoto ni nyingi sana.
 
Back
Top Bottom