jimama26
JF-Expert Member
- Jul 30, 2013
- 2,839
- 2,963
Hivi Magufuli anshindwa nini kubadilisha gia angani akaja na hoja ya kujenga miundombinu ya umwagiliaji kwa wananchi, maji kwa wote, umeme kila kitongoji, masoko ya mazao na viwanda vya kusindika mazao, nyasi za bandia viwanja vyote vya michezo kila mkoa, trecta kila Kijiji? Naona Bado kakomaa na kuongeza ndege.
Ndege 5 nani azungumze? Barabara, reli, flyovers, nani amwachie? Huyu nahisi kuna kitu hakiko sawa. Ana viporo aliviwaza akiwa Mbunge wa Chato kuwa atavitekeleza maishani mwake kama Mbunge, kaukwaa Urais ndio kaanza kutekeleza(mbuga, kiwanja cha ndege).. Bado akiwa Waziri kuna vitu alitakaga kufanya hakuweza (vya kichwani mwake, sio vya katika dira ya taifa au sera za CCM). Sasa ndio kawa Rais anavifanya kwa nguvu nguvu. Waliokuwaga viongozi wake wakati ule walikuwaga wanamdhibiti kufanya fanya mambo ya kichwani mwake, ili kujikita kutekeleza yaliyoko kwenye ilani ya chama chao / dira ya taifa. Jiwe ni lazima umdhibiti, hivi hivi anakuwaga na maamuzi yasiyo na ‘busara’, ‘tija’). Kapewa rungu sasa, kasheshe tunaiona.
Hivi kweli nchi inaongozwaje hivi? Si tuna vipaumbele vyetu kama Taifa? Kwa nini analeta yake binafsi kama vipaumbele vyetu sote? Bado mwenzetu anatekeleza ahadi alizojiwekea yeye zamani kwenye mapitio yake ya maisha ya Ubunge na Uwaziri, hayuko na sisi kabisa. Huyu tumtoeni tu, aende zake Chato huko.
Hapa kura zote Watanzania wenzangu ni kwa Lissu tu. Huyu ndio mkombozi wetu. Tusipojikwamua sasa kutoka mikononi kwa mtesi wetu Jiwe, itakuwa imekula kwetu. It’s now or never. Jiwe mwenyewe haeleweki, akipita tena ndio atakuwa na mahasira na sisi balaa. Ataishia kujiongezea ukomo wa Urais, atumalize vizuri.