Kauli hii ya Pastor Tony Kapola inachochea ukatili dhidi ya wanawake walioko kwenye ndoa! Wanawake msifuate ushauri huu

Kauli hii ya Pastor Tony Kapola inachochea ukatili dhidi ya wanawake walioko kwenye ndoa! Wanawake msifuate ushauri huu

Mchungaji yupo sahihi.

Ndoa nyingi zinavunjika kwa sababu mnaingia huko mkiwa mmejiandaa kuachana.

Na jamii inachangia sana ndoa kuvunjika kwa mtazamo kama wa mleta mada.
 
Hata mimi ningekuwa na mamlaka ninge wafutilia mbali nyinyi midume mlio jaa mawazo ya kifenist ndani ya nchi hii maana ndo chanzo cha ndoa nyingi kuvunjika.

Ww feminist una ujinga mwingi eti wana ume mzima unajiita mama samia upuuzi tu.
Sasa Mama Samia nae kaingiaje hapa,ebu naomba kuuliza!!??
 
Mchungaji yupo sahihi.

Ndoa nyingi zinavunjika kwa sababu mnaingia huko mkiwa mmejiandaa kuachana.

Na jamii inachangia sana ndoa kuvunjika kwa mtazamo kama wa mleta mada.
Hayupo sahihi kwenye mifano yake na ndio ilipo hoja ya mleta uzi, uvumilivu sio wa kupigana, kuvumiliana kwenye mengine sawa, lakini domestic violence inapaswa kukemewa pakubwa sana, anasema binti anashtaki kapigwa na mumewe, mama ake nae anamjibu mbona baba ako ananipiga ila navumilia wth!

Mimi binafsi wazazi wangu wana karibu miaka 60 pamoja lakini sikuwahi wala kuwahi kuona wakipigana wala kufokeana na hao wamezeeka pamoja lakini najua wamevumiliana kwa mengi na wanaheshimiana pia,

Also hakuna kitu kibaya mzazi kumwambia mwanae ukishindwa rudi nyumbani, kwenye malezi ya mtoto mzazi anatakiwa amfanye mtoto wake ajisikie huru kua kwao na sio kuishi kama mkimbizi kwa kigezo cha ndoa
 
Hayupo sahihi kwenye mifano yake na ndio ilipo hoja ya mleta uzi, uvumilivu sio wa kupigana, kuvumiliana kwenye mengine sawa, lakini domestic violence inapaswa kukemewa pakubwa sana, anasema binti anashtaki kapigwa na mumewe, mama ake nae anamjibu mbona baba ako ananipiga ila navumilia wth!

Mimi binafsi wazazi wangu wana karibu miaka 60 pamoja lakini sikuwahi wala kuwahi kuona wakipigana wala kufokeana na hao wamezeeka pamoja lakini najua wamevumiliana kwa mengi na wanaheshimiana pia,

Also hakuna kitu kibaya mzazi kumwambia mwanae ukishindwa rudi nyumbani, kwenye malezi ya mtoto mzazi anatakiwa amfanye mtoto wake ajisikie huru kua kwao na sio kuishi kama mkimbizi kwa kigezo cha ndoa
Watu wamekuwa wapumbavu mno kiasi cha kutetea ukatili ili kulinda ndoa. Mimi nimekulia familia ambayo mama kupigwa mbele ya watoto ilikuwa kitu cha kawaida. Imesababisha hadi huku ukubwani niwe na maelewano madogo mno na baba yangu. Nadhani bado sijamsamehe kwa kumbukumbu mbaya alizonitengenezea kwenye ubongo wangu. Kimsingi ni ngumu mtoto wa kiume kuvumilia kuona mama yake analia baada ya kipigo. Baba yangu nitamuiga mambo mengi ila sio ukatili kwa mke wangu. Hata kama alikuwa ana makosa bado haihalalishi kumshushia kipigo mbele ya sisi watoto wake. Huwa ninafurahi sana kulalamikiwa kuwa nampendelea mama.
 
Inasikitisha sana huu uchochezi kufanywa na huyu mtumishi wa Mungu.

Sikutegemea kabisa kuona maneno kama haya yakitolewa na mtu kama huyu

Ningekuwa na mamlaka makanisa kama haya ningeyafutilia mbali.

Hiki ndicho alichokisema:

"Mama zetu walivumilia kwa sababu baba zao hawakuwa tayari kuwaona wanarudi nyumbani. Wakienda kusemelea kwa mama yake, mama mimi John ananifanyia hivi na hivi. Ananitesa, ananinyanyasa, ananipiga. Mama yake anamwambia hivi Mbona mimi baba ako ananipiga, ni kawaida, vumiia tu mwanangu"

"Siku hizi mama ako mwenyewe, kaachika. Anakwambia hivi "akikunyanyulia mkono chumba chako bado kipo. Kwa hiyo binti anaingia kwenye ndoa anajua kabisa chumba chake bado kipo. Kijana jichanganye"


Ni kauli kama hizi zinazofanya wanawake wabaki kwenye ndoa ambazo zimejaa manyanyaso na ukatili uliokithiri.

Ripoti ya World Bank iliyotoka mwaka 2022 ilisema kabisa kuwa asilimia 40 ya wanawake wenye umri kuanzia miaka 19 hadi 40 wameshawahi kupigwa au kufanyiwa vitendo vya ukatili.

Kwa takwimu kama hizi, mtu mashuhuri kama huyu anajitokezaje kwenye halaiki ya watu na kutetea ukatili kwa wanawake.

Kwanini Pastor asingetumia muda huu wa kutetea ukatili kwa wanawake, kuwasema wanaume wanaopiga wanawake zao?

Inasikitisha sana!
Huyu siyo pastor au mchungaji bali mchunaji tena garbage. Utakuta kumbaff kama hili linanyanyaswa na mkewe lakini likitoka nje linajishebedua nyambaff kubwa.
 
Kua na familia imara ni bahati, hata uwe mjanja vipi au uwe makini vipi kwenye kuchagua kama bahati haipo upande wako talaka zitakuhusu.
Hujui usemacho. Sema tukufundishe siyo kujumuisha na kuonyesha uzwazwa mwanangu.
 
Huyu jamaa ni ndina sana kwa kujifanya mtetezi wa wanawake humu jf.
Angejua wanawake wanavyo tuchukulia wala hasingepoteza muda kujifanya mtetezi wao.
Kiufupi ningekuwa na mamlaka hivi vijitaasisi vinavyo eneza itikadi za kifeminist kwa mgongo wa kutetea haki za wanawake ninge vifyekelea mbali maana vimejaa ushetani mtupu.
Wewe nenda kwa topics za wale wanaochukia wanawake akina Natafuta Ajira , ndio mada zinazokuna mtima wako wa kuwa wounded from your mother, ukiona mada zinazosupport wanawake pita kushoto usiwe hurt your big ego.
 
Inasikitisha sana huu uchochezi kufanywa na huyu mtumishi wa Mungu.

Sikutegemea kabisa kuona maneno kama haya yakitolewa na mtu kama huyu

Ningekuwa na mamlaka makanisa kama haya ningeyafutilia mbali.

Hiki ndicho alichokisema:

"Mama zetu walivumilia kwa sababu baba zao hawakuwa tayari kuwaona wanarudi nyumbani. Wakienda kusemelea kwa mama yake, mama mimi John ananifanyia hivi na hivi. Ananitesa, ananinyanyasa, ananipiga. Mama yake anamwambia hivi Mbona mimi baba ako ananipiga, ni kawaida, vumiia tu mwanangu"

"Siku hizi mama ako mwenyewe, kaachika. Anakwambia hivi "akikunyanyulia mkono chumba chako bado kipo. Kwa hiyo binti anaingia kwenye ndoa anajua kabisa chumba chake bado kipo. Kijana jichanganye"


Ni kauli kama hizi zinazofanya wanawake wabaki kwenye ndoa ambazo zimejaa manyanyaso na ukatili uliokithiri.

Ripoti ya World Bank iliyotoka mwaka 2022 ilisema kabisa kuwa asilimia 40 ya wanawake wenye umri kuanzia miaka 19 hadi 40 wameshawahi kupigwa au kufanyiwa vitendo vya ukatili.

Kwa takwimu kama hizi, mtu mashuhuri kama huyu anajitokezaje kwenye halaiki ya watu na kutetea ukatili kwa wanawake.

Kwanini Pastor asingetumia muda huu wa kutetea ukatili kwa wanawake, kuwasema wanaume wanaopiga wanawake zao?

Inasikitisha sana!
Picha linaanza mwanamke anakula tunda na kumsababishia mwanamme matatizo.

Dini yenyewe imekaa kumuangushia mwanamke jumba huelewi wapi?
 
Picha linaanza mwanamke anakula tunda na kumsababishia mwanamme matatizo.

Dini yenyewe imekaa kumuangushia mwanamke jumba huelewi wapi?
Tukiachana na hadithi za kwenye bible tujikite kwenye hii kauli ya huyu baradhuli Tony.
 
Uchungaji ni wito na sio upigaji kelele! Sijui wanasomeaga wapi uchungaji! Kwanza kuna wachungaji ukiwapelekea kesi eti nimepigwa na mme wananishangaa mwanaume unampigaje mwanamke! Hivi Kama Mchungaji Mgogo anaweza kusema hayo kweli ?
 
Uchungaji ni wito na sio upigaji kelele! Sijui wanasomeaga wapi uchungaji! Kwanza kuna wachungaji ukiwapelekea kesi eti nimepigwa na mme wananishangaa mwanaume unampigaje mwanamke! Hivi Kama Mchungaji Mgogo anaweza kusema hayo kweli ?
Mgogo naye mropokaji. Alishawahi kusema elimu kwa mtoto wa kike sio muhimu.
 
Aloo! Kupigana kupo.. kunaweza kusiwe kwa vitendo ila kupo, mwanamke akija physically atakutana na kitu fiziko ila kwa ajili ya self defense. Then nita retaliate as a Gentleman maana siwezi ruhusu upuuzi wake unipeleke Sentro.
Ila Kama akinikosea na bado akawa mkaidi naenda kutafta mtoto mbichi zaidi yake naanza upya ye namuacha na life lake..
Mnawaza Sana kuhusu clean shit ya “Kutokuvunjika kwa Ndoa” mnasahau mustakabali mzima wa Wanandoa..
in reality Ndoa ni fungamano tu la kidhahania ila halina practical evidence yoyote zaidi ya Cheti na Maandiko ya kiimani.
Zinatakiwa zivunjike hiviii mpaka itafika steji watakao kua wanaoana ni watu waliomaanisha haswa… sio saizi watu wanaoa kwa sababu za desturi za kimapokeo ambazo ukiangalia chimbuko lake ilikua ni mikataba ya kiutawala, biashara na njia kujirasimishia viburudisho enzi za Zama za mawe za kale…
Finally nimepata mtu anayeongea lugha sawa na mimi. Kuwepo prenups, kuwepo urahisi wa talaka ili kusudi wanaokimbilia ndoa wajue kuwa wana wajibu wakuzijenga na kuziishi. Which watakuwa wachache na zitakuwa bora.


Hapo pa mustakabali wa wanandoa hapo… Jamii inatia pressure watu kuoana ila haisemi kitu kuhusu wanandoa kujitahidi kuishi misingi na kutendeana kwa wema… It’s like watu wanatiana pressure ya kwenda kuteseka 😀 Nadhani focus ilitakiwa kupelekwa katika “existing ones” ambapo zikiwa nzuri za mfano automatically kila mtu atatamani.

Sheria za ndoa zimejengwa katika misingi ya ukandamizaji, Zote za kidini, kiserikali na kitamaduni.

Wamebaki wachache sana waliocustumize ndoa zao kwa mahitaji yao ndio wanaishi vizuri, kwingine kote kasheshe.
 
Back
Top Bottom