Dan Zwangendaba
JF-Expert Member
- Apr 25, 2014
- 5,814
- 8,118
Magufuli aliamini sana jeshi, sana kupita kiasi. Aliamini jeshi hakuna kitu linashindwa. Ndivyo madikteta wanakuwa hivyo lakini.Kwanini magufuli alimtumia mabeyo??? Angali viongozi wake wa juu wapo??? Magu alimuamini Sana mabeyo, alijiona yupo salama akiwa Naye kuliko kiongozi yoyote.
Pitia top profile iliyopururwa kwa mizengwe ya kimtindo labda utapa majibu mkuu.Je, kulikuwa na 'mzozo' wa kutaka aapishwe mtu mwingine badala ya Makamu wa Rais? Je, huo 'mzozo' kama ulikuwepo na pengine kupelekea kuchelewesha kuapa, ulianzishwa na nani? Je, nani aliyekuwa anakusudiwa kuapa badala ya Makamu wa Rais?
Kwani kwa mujibu wa Katiba, ni CDF ndiye mwenye wajibu wa kufanya hivi? Je kuugua kwa JPM kuliwekwa bayana? Kama hakukuwekwa bayana, ni mazingira gani yangewezesha kumtangaza Samia kama Kaimu Rais?..kosa la Mabeyo ni kutokumpa taarifa Makamu wa Rais.
..Rais anapokuwa hawezi kutimiza majukumu yake iwe kwa ugonjwa au sababu nyingine Makamu anatakiwa kuziba pengo lililojitokeza.
..hiyo " mijadala " isingekuwepo kama Mabeyo angefuata na kuheshimu katiba tangu awali.
Tema mate chini. Wasingeshindwa kumchukua yeyote kutoka popote ndani ya Jamhuri na kumpa sifa ya uzanzibari mkuu.Nitajie mwanamke mwenye ushawishi zanzibar unayemjua kwenye siasa 2015/2020.
Shida ipi?Kwa shida inayoendelea hapa nchini!
Hao watu walikuwa sahihi sana
Samia she's misfit to the position.Dhaifu mno,hatoshi.Habari zenu wanaJF wenzangu, ama baada ya salam ningependa kuendelea na mada yangu hapa jukwaani.
Ndugu zangu kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Wakati raisi Samia alipoingia madarakani, haikupita hata miezi sita akaanza pangua pangua ya viongozi wakubwa pale ikulu akiwemo aliekuwa katibu mkuu kiongozi mhe Dr Bashiru ambae alikuwa amechukua nafasi hiyo muda mfupi tu baada ya aliekuwepo kufariki.
Wengi walianza kulalamika na kumlaumu Rais kwa hatua yake hiyo ya pangua pangua pale state house, mpaka wengine wakafikia hatua ya kusema kuwa raisi ana ugomvi sijui na sukuma gang, team Magufuli nk. Ila nyuma ya pazia hawakuwa wanajua ni kwanini raisi aliamua kufanya vile na kwa sababu gani.
Cheo cha katibu mkuu kiongozi ni cheo kikubwa sana kimamlaka, hivyo sio rahisi kuondolewa tu hivi hivi kienyeji bila kuwa na sababu ya msingi. Hivyo raisi kumuondoa mhe Bashiru katika nafasi ile ghafla bin vuu kulikuwa na sababu maalumu ambayo wengi hawakuijua.
Leo hii ukisikiliza kwa makini ile interview ya CDF mstaafu mhe Mabeyo, na kile kilichotokea baada ya mama kuingia (pangua pangua) utaona kabisa ni kina nani ambao walikuwa na mpango wa kupindisha katiba. Nakumbuka CDF Mabeyo wakati wa hotuba yake pale msibani alimwambia mhe raisi kuwa ana ujumbe wake ambao atamwambia pindi watapokuwa falagha kati yake na raisi.
Miezi kadhaa mbele baada ya msiba kuisha Rais Samia akaanza pangua pangua ambayo ilipelekea mhe Bashiru kuwa miongoni mwa waliotenguliwa, huku waziri mkuu na mawaziri wengine wakiendelea kubaki na vyeo vyao hadi leo.
So Rais anapotengua au kutea mtu huwa anafanya hivyo baada ya kupata taarifa za kutosha za anaeteuliwa au tenguliwa.
Leo niishie hapa.
😂😂😂 Jibu kanipa, sema lisilonyooka vizuri.Hapo lazima akwepe kukupa jibu linaloeleweka. Hakuna mtu ambae anaweza kuzifungua hizi kodi moja kwa moja.
Umewaza na kumjibu vile vile kama nilivyomjibu mimi huko juu. Hawa vijana wengi hawakuwepo hiyo 1995, wala 2000.Kwamba mara zote Magufuli alilazimishwa Samia awe makamu wake au? Yaani Magufuli huyu wa 2020 alikuwa akiogopa watu kiasi apangiwe makamu? Samia was the perfect person kwa umakamu na so far ni best president ever kuwa naye.
By the way, tangu 1995, kuna makamu gani aliyeheshimiwa na kupewa hadhi ya umakamu hasa? Ulikuwa wapi wakati Dr. Omar, Shein, Bilal wanatembea na mikasi tu?
Maswali ni mengi na mazito, lakini yanahitaji ujuzi, ueledi na ufahamu mzuri kuyajibu. Let's wait wenye sifa za ujuzi, ueledi na ufahamu mzuri waje wayajibu. Hata kama sio leo basi kesho, keshokutwa na kuendelea...Je, MABEYO AMESEMA YOTE JUU YA NI NINI KILIMSIBU RAIS MAGUFULI KABLA HAJAFA?
'Kisha, baada ya miaka mitatu, nilipanda kwenda Yerusalemu, ili nionane na Kefa, nikakaa kwake siku kumi na tano' - Mtume Paulo (Wagalatia 1:18).
Katika kitabu chake kiitwacho 'Paul and Peter Meeting in Jerusalem', Askofu Prof. Kenneth Cragg wa Church of England alifafanua mstari huo katika kurasa 96. Katika kitabu hicho, Prof. Cragg alijaribu kujibu swali hili: Je, katika siku hizo 15, Kefa (Mtume Petro) na Mtume Paulo waliongea nini? Lakini hoja kwa nini maudhui ya maongezi hayapo katika kitabu cho chote cha Paulo haijajibiwa na Prof. Cragg. Hii ndio sehemu ya utafiti ambao Askofu Mwamakula amekuwa akifikiria kuufanya baadaye.
Wakati Askofu akiwaza hayo, Mkuu wa Majeshi mstaafu wa Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo aliibuka na kuongea na vyombo vya habari kuhusu kifo cha Rais Magufuli tarehe 17 Machi 2021. Jenerali Mabeyo alitumia muda mfupi (pengine saa 1) kuongea na wanahabari juu ya nini kilitokea kwa Rais Magufuli ndani ya kipindi cha masaa 24 kuanzia kati ya tarehe 16 na 17 Machi 2021.
Jenerali Mabeyo ameacha maswali mengi kwa watu ambayo pengine pia yatahitaji kujibiwa na waandishi wa habari za uchunguzi, watafiti na hata wana usalama katika miaka mingi ijayo. Baadhi ya maswali ni: Je, kwa nini katika saa za mwisho za maisha yake hapa duniani, Rais Magufuli hakuruhusiwa kuwa na familia yake - mke au watoto? Je, ni kitu gani kilichelewesha kuapishwa kwa Makamu wa Rais kuwa Rais hadi baada ya siku mbili badala ya masaa 24?
Je, kwa nini taarifa za msiba asipewe kwanza Makamu wa Rais, badala yake wakapata Waziri Mkuu na Katibu Mkuu Kiongozi? Je, kule Tanga alikokuwa Makamu wa Rais na kule Dodoma walikokuwa hao wengine wapi ndio karibu? Je, kulikuwa na 'mzozo' wa kutaka aapishwe mtu mwingine badala ya Makamu wa Rais? Je, huo 'mzozo' kama ulikuwepo na pengine kupelekea kuchelewesha kuapa, ulianzishwa na nani? Je, nani aliyekuwa anakusudiwa kuapa badala ya Makamu wa Rais?
Je, kuna mtu yeyote mwenye mamlaka ya juu miongoni mwa aliowasema Mabeyo ambaye angeweza kusahau katiba inasema nini juu ya lililotokea wakati alikuwa ameapa kuilinda? Je, maelezo ya msemaji wa familia wakati ule wa msiba na maelezo ya Jenerali Mabeyo kuhusu sala ya mwisho kwa namna gani yanalingana na kwa namna gani yanatofautiana? Kama ipo tofauti, ni makusudi au nahati mbaya? Je, kama kuna tofauti, umma ufuate maelezo ya nani? Je, zile siku kadhaa kabla ya kifo chake (kipindi cha ikimya), Rais alikuwa wapi? Je, alitoa wosia au maelekezo gani? Kama aliweza kutoa amri kutaka arejeshwe nyumbani wakati amezidiwa, alishindwaje kutoa amri ya kutaka familia yake?
Ili kuyajibu maswali yote hayo itahitajika utafiti utakaotoa maelezo ya kutosha kuandika kitabu chenye kurasa 2000. Kuishi na watu wa aina ya Askofu Mwamakula inahitaji uvumilivu mwingi. Ukuikosa uvumilivu unaweza kumtumbukiza katika pipa la tindikali ili kumbukumbu ya mwili wake isiwepo, asipelekwe Itunge katika Isyeto (makaburi) la Chifu Mwamakula. Maswali yake hufanya watu waanze kufikiria kinachofanyika katika 'Sayari ya Mirithi'!
Kama Jenerali Mabeyo, angenyamaza kimya, Mwamakula angekuja na maswali yake haya ya 'kipumbavu'? Je, ni kwa nini watu husema chini chini wakijiuliza maswali kama hayo? Je, watu wanaogopa nini kuyajadili wakati Jenerali pia Mabeyo ameamua kufunua pipa jalalani? Hivi mtu akilifunua pipa jalalani, utawezaje kulaumu na kuwaadhibu kuku wanaochakura wadudu?
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Dar es Salaam, 18 Machi 2024; saa 12:25 jioniView attachment 2938629
tuendelee na Mtori....Bado hamjasena
Mabeyo hana lawama hapa..Mabeyo anastahili lawama.
..Kwanini MAKAMU WA RAIS hakuwa mtu wa kwanza kupewa taarifa kuwa Rais amefariki?
..Nimemsikia Mabeyo akisema eti kulikuwa na mjadala wa nani atangaze kifo cha Rais.
..Hivi Mabeyo na usomi wake, kutumikia jeshini kwa miongo kadhaa, na kutembelea nchi mbalimbali, hajui nani ana mamlaka ya kutangaza kifo cha Raisi? Kwamba walihitaji majadiliano?
Nani tena anaemlaumu mzee wetu Mabeyo kwa kosa lisilo lake?Mabeyo hana lawama hapa
Baada tu ya Magufuli kufariki, mambo hayakuwa rahisi kama unvyofikiri...Mabeyo anastahili lawama.
..Kwanini MAKAMU WA RAIS hakuwa mtu wa kwanza kupewa taarifa kuwa Rais amefariki?
..Nimemsikia Mabeyo akisema eti kulikuwa na mjadala wa nani atangaze kifo cha Rais.
..Hivi Mabeyo na usomi wake, kutumikia jeshini kwa miongo kadhaa, na kutembelea nchi mbalimbali, hajui nani ana mamlaka ya kutangaza kifo cha Raisi? Kwamba walihitaji majadiliano?
Watumishi wengi wa uma hawajui na wala hawatendi kwa mujibu wa katiba na sheria (kuanzia chini hadi Rais). Husikiliza matakwa ya Rais au upepo wa siasa za ndani na nje...Mabeyo anastahili lawama.
..Kwanini MAKAMU WA RAIS hakuwa mtu wa kwanza kupewa taarifa kuwa Rais amefariki?
..Nimemsikia Mabeyo akisema eti kulikuwa na mjadala wa nani atangaze kifo cha Rais.
..Hivi Mabeyo na usomi wake, kutumikia jeshini kwa miongo kadhaa, na kutembelea nchi mbalimbali, hajui nani ana mamlaka ya kutangaza kifo cha Raisi? Kwamba walihitaji majadiliano?
Nafikiri wewe haukufuatilia kwa makini yale mahojiano ya cdf.Kwann jpm alimuita cdf badala ya makamu? Mjue mam alikuwa na shida
Kwani wakati wa JPM vyombo vya kijeshi si ndio aliviweka mbele zaidi ilikuwa sawa kwa wakati huoHahahah
Katika tafakuri nawaza labda mtoa hoja angeweka maswali yenye kuibua fikra tunduizi kwenye kufahamu kwa nini CDF, IGP na DGIS walikuwa ndiyo wamekizunguka kitanda alicholazwa Rais badala ya watu walioainishwa kwenye Katiba kuwa ndiyo waratibu wa kila hatua?
Je, nchi inaendeshwa kwa mujibu wa mwongozo wa Kijeshi? Maana tunaunga nukta kuhusu ushiriki wa Mfumo na Polisi kwenye mchakato wa uchaguzi na kupiga kura.....