Kauli ya CDF mstaafu kuhusu waliotaka kupindisha katiba ili Rais Samia asiapishwe inanipa picha halisi ya kwanini Bashiru na wenzake walitenguliwa

Kauli ya kwamba familia pia ilikuwa haijui inafikirisha sana, yaani mke wake Mama Janeth hakuwa karibu na mumewe kumuhudumia....... mpaka anafariki??

Hiyo yote inaonekana ni kwa amri kutoka juu, amri yake mwenyewe Magufuli.

Magufuli angetaka mkewe aende Kwa Mzena angetoa amri moja tu, hata kwa helikopta angeweza kupelekwa, mbona aliamrisha mpaka Kardinali Pengo aende?

Stories za Magufuli alivyokuwa anaiendesha familia yake zikija kutoka watu watamuangalia Magufuli tofauti.
 
Nimekuelewa..
Waendelee kutema nyongo
 
Uhaba wa taarifa unawafanya watu wakisie sana.

Sijui lawama nyingi ziende kwa nani, ila serikali kwa ujumla wake haiwezi kuzikwepa.

Hivi inajulikana kwa uhakika kwa nini mke wake hakuwepo wakati anavuta pumzi ya mwisho?

Vipi kama alikuwa kaenda tu nyumbani kupumzika kidogo na kuangalia mambo mengine na ikatokea muda ambao hakuwepo wodini ndo mume wake naye akafariki?

Yawezekana kabisa alikuwa yupo hapo kwa Mzena kwa muda mwingi tu lakini si kwa kila sekunde na dakika kwa masaa 24.

Kama umewahi kuuguza, hususan mtu mzima, huwa inatokea muda na wewe unatoka kidogo kwenda labda kuoga, kubadili nguo, na kufanya mambo mengine halafu unarudi tena kuwa na mgonjwa.

Hapa kuna uhaba mkubwa wa taarifa na tunalazimika kuhisi na kukisia baadhi ya mambo maana hata kuugua na kulazwa kwake hatukufahamishwa. Tulisikia habari kupitia njia mbadala.

Tukaja kutangaziwa kifo tu. Kuna tatizo kubwa la mawasiliano.
 
Kwa story ya Mabeyo ni kama vile familia nzima ilikuwa kept in the dark, mke wake alikuwa Ikulu tu.

Labda kwa amri ya Magufuli mwenyewe.
 
Kwa story ya Mabeyo ni kama vile familia nzima ilikuwa kept in the dark, mke wake alikuwa Ikulu tu.

Labda kwa amri ya Magufuli mwenyewe.
Mabeyo kuna mengi hakusema pia.

Lakini na waandishi waliokuwa wanamhoji nao hawakuwa wanauliza follow up questions.

Sijui kwa nini hawakuuliza kwa nini mke wake hakuwepo hapo wodini.

Kwanza sikusikia hata maswali waliyoyauliza. Ni kama vile Mabeyo alikuwa anaongea yeye tu.

Anyway, pasipo na taarifa, watu wata speculate kupita kiasi.
 
Hilo inaonekana kuwa lilikuwa sharti la Mabeyo. Kwamba ataongea tu bila maswali.

Suala lenyewe bado nyeti anaona habari nyingi hazijawa declassified bado.

Anachagua sana cha kusema.
 
Nitag uzi wa Yoga
 
Wewe itakuwa Sukuma gang siwezi kukushangaa kuongea utumbo huu. Yani hii nchi imekuwa geto lako eti Bashiru, uko serious kabisa mtu mzima unaadika huu ujinga humu. Ndio maana ulifeli form 4
 
Una point, hakusimamia vizuri majukumu yake. Alikaa muda wote akakubali wahuni waendelee na mipango miovu huku akijua kuwa wanafanya kinyume. Hata kutangaza ni kutokana na pressure alizokuwa akizipata kuwa kwa nini unashindwa kusimamia katiba.
 
Ndio maana wenye akili wanaona hata Mabeyo hakutimiza wajibu wake. Ni aibu kutamka hayo mbele ya vyombo vya habari.
 
Si mmeshaona watu walishaanza kumdelete the makamu.? Wanaanzaje kumpa atangaze. Jeshi ndio lilimpatia mandate ya kutangaza
 
Kiusalama ndio ilikua sahihi, ndio maana hakuitwa dar haraka.. mabeyo na wenzake walikua katiba inasemaje hivyo kujadili makamu akiwepo ingeonyesha mashaka zaidi wakati makamu mwenyewe anajua wajibu wake..

Hilo lianchwe kiusalama zaidi
 
Kwa maana nyingine walikuwa wanamchukulia poa makamu wa Rais.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…