Kauli ya Waziri Mkuu kutilia shaka barakoa za kisasa na kutaka watu wajishonee matambara na kuyavaa usoni haiwezi kuachwa bila kujadiliwa

Kauli ya Waziri Mkuu kutilia shaka barakoa za kisasa na kutaka watu wajishonee matambara na kuyavaa usoni haiwezi kuachwa bila kujadiliwa

Leo Mheshikiwa Rais naye anasema tuwe makini na hizo barakoa, najiuliza TMDA wanafanya kazi gani ?


Ina maana wananchi ndio tumepewa jukumu la kukagua quality ya vifaa vya kutumia?
20210221_133420.jpeg
 
Kinachonishangaza kwa huyu mzee Magufuli ni kwa nini yeye hapatwi na haya maradhi licha ya kuwa mkaidi toka ugonjwa huu upige hodi hapa nchini

Hebu fikiria Maalim kaugua korona muda mfupi baada ya kukutana na huyu bwana,msaidizi wake naye kapata maradhi haya akiwa ofc moja,waziri Mipango na viongozi wengi tu wanaokuwa katika direct contact na Magufuli wamepata ama kufa kwa korona wakati yeye hana hata Mafia

Hebu jiulize Magufuli kila siku yuko kwenye mikusanyiko bila kuvaa barakoa wala kuosha OSHA mikono lakini hatujamuona akipata haya maradhi

Nihitimishe kwa kusema hivi "Kuna taarifa za SIRI anazozijua huyu mzee kuhusu haya maradhi" na kama sio hivyo niseme tena " usimuige kichaa kula jalalani,kwani vichaa wanalindwa na kile kilichowatia ukichaa"
 
Ni propaganda za kipuuzi tu za viongozi wa hovyohovyo wa awamu ya tano.

Ukienda pale TBS ubungo au pale TMDA river side, utakuta wafanyakazi wamevaa barakoa hizo za kutoka nje.

Hata hao viongozi wa hovyohovyo kwenye maofisi yao wafanyakazi wanavaa hizo za kutoka nje.

Lakini wakiwa majukwaani ni kama kuna pepo la mauaji limewaingia.
IMG_20210211_163253.jpg
 
Hapa nakumbuka kisa cha bokasa cha kuwauwa wanafunzi waliogoma kununua sare zilizoshonwa kwenye kiwanda cha mke wake.Hii ni harufu ya biashara, watawala wa kiafrica wanafanana.
 
Kinachonishangaza kwa huyu mzee Magufuli ni kwa nini yeye hapatwi na haya maradhi licha ya kuwa mkaidi toka ugonjwa huu upige hodi hapa nchini..
Alidungwa chanjo toka China kwenye msafara wa china Chato.we endelea kutembea kifua mbele tza hakuna corona
 
Serikali ya awamu hii mambo yake ni too unprofessional....
 
Wanataka kupotosha kuwa barakoa toka nje ndio zimeleta corona hii second wave. Nadhani hawakukumbuka kuwa kwenye huo upotoshaji wao wanaotaka kuufanya, TBS wana wajibu huo. Haya ndio mambo yanayozidi kuchochea upatikanaji wa katiba mpya, kwani inaonekana kabisa mtu mmoja anapokuwa na maamuzi yote ya nchi nini kinaweza kutokea.
Kwani uongo?
 
Sasa wafanyabiashara waloingiza hizo barakoa watakuwa wageni wa nani maana nani atazinunua wakati wao wameshalipia ushuru wa forodha n.k

Au barakoa hazinaga kodi ya ushuru wa forodha kwa kuwa ni medical tools?
 
Sasa wafanyabiashara waloingiza hizo barakoa watakuwa wageni wa nani maana nani atazinunua wakati wao wameshalipia ushuru wa forodha n.k

Au barakoa hazinaga kodi ya ushuru wa forodha kwa kuwa ni medical tools?

Lakini pia kuna gharama za manunuzi itakuwaje labda?
 
Ina maana barakoa haziangaliwi ubora na TMDA/TBS..


Tufute hayo mashirika kama hayawezi kutambua barakoa fake au zenye madhara.
IMG_20210221_143854.jpeg
 
Huu ni mwendelezo WA Serikali ya Tanzania isivyojali wananchi wake katika ugonjwa WA corona,Barakoa sio kitambaa chochote kile kuweka usoni, kuna vingine vinaruhusu virus na nyingine haziruhusu ,Wataalamu engine wanashauri uwe una double barakoa kwa uhakika zaidi WA kujilinda
 
Back
Top Bottom