Sakasaka Mao
JF-Expert Member
- Sep 29, 2016
- 12,826
- 17,371
Niliona kama kauma na kupuliza, sisi wananchi hatuhusiki hapo.Mbona umemponda unayemjibu lkn ktk maelezo yako unaungana naye?
Hoja yangu ni kwamba umungu mtu wa rais ukipunguzwa waziri atakuwa huru kutumia utashi wake wa kujiuzulu ama kubakia ktk nafasi yake endapo patatokea misigano kati yake na rais.Hata katiba mpya ikiwepo mawaziri wataburuzwa na kutukanwa tu. Ni masuala ya kibinadamu zaidi.
Ahaa! SawaNiliona kama kauma na kupuliza, sisi wananchi hatuhusiki hapo.
Ni dharau ya wazi ya rais kwa wateule wake.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ndiyo hajabwaga manyanga sasa unafanyaje?Muwage mnacomment kwa kuchuja habari kwanza.
Chukua hotuba ya waziri Mkenda inayozungumzia masuala ya mashamba ya miwa, viwanda vya sukari, uhaba wa sukari na utaratibu wa uagizwaji na uingizwaji wa sukari.
Ukitoka kuisikiliza hiyo, chukua hotuba ya rais Samia aliyoitoa Chato wakati wa ziara ya rais M7, utaelewa dhahiri mtoa mada alichomaanisha.
Tukichukulia sura ya rais na baraza lake la mawaziri ni mfano wa familia moja ya ndoa, mtu na mke wake kiutendaji.
Hatutegemei mke wa mtu azungumze jambo, halafu baadaye atoke mumewe hadharani kuliponda ama kulikanusha jambo hilo!
Majirani tutashangaa na kuona dosari iliyo wazi katika familia hiyo!
Haiwezekani jambo moja linalopikwa katika chumba kimoja likatoka na maelezo tofauti ya msigano!
Kwa mantiki ya mfano nilioutoa ni kwamba waziri hawezi kukurupuka kutoa msimamo wa serikali bila baraka za rais, never on earth!
Ikitokea msigano wa wazi hivyo, yampasa waziri kujitathimini na kubwaga manyanga ili kulinda hadhi yake!
Sent using Jamii Forums mobile app
Point kubwa sana umeongeaKimsingi nchi yetu kwa sasa imejaa chuki za aina mbili
1. Za kisisa. Kwasabb waliopo madarakani hawakuchaguliwa na wananchi. Na sisa zinendeshwa kwa figisu
2. Za kiuchumi. Kwasabb mifumo ya masoko na ajira inavurugwa na wakubwa. Wao wanajipendelea na hawajali wengine
Ndiyo kizazi cha sheitwaani haoMbona umemponda unayemjibu lkn ktk maelezo yako unaungana naye?
Mtoa mada kalisemea hilo.Ndiyo hajabwaga manyanga sasa unafanyaje?
Ninachojua kuanzia awamu ya 5, tumeshuhudia unyumbu kwenye uongozi serikalini, 'herding behaviour', Herding behaviour is an occurrence of thoughtful people suspending their individual reasoning because of fear, in this case fearing their leadersKatiba yetu inampa Rais mamlaka makubwa sana nchi hii. Rais ni kama Mungu kwa mujibu wa katiba yetu.
Mawaziri wanatwezwa lkn hawana cha kufanya. Wakijuzulu "mungu" anaweza kutafsiri hatua hii kama dharau na kuamua kuwashughulikia. Wanalazimika kuipokea kauli ya "mungu mtu" kwa mikono miwili.
Rais Magufuli aliwaita mawaziri Dr. Philip Mpango na Prof. Kabudi WAPUMBAVU mbele ya hadhara. Wakapokea kauli hii kwa mikono miwili. Sote tukabakia tumeduwaa. Ni kwasababu hawakuwa na la kufanya mawaziri hawa. Walimwogopa "mungu" na malaika wake
Rais Samia ametamka hadharani kwamba uamuzi wa Prof. Mkenda kuzuia sukari toka nje ni NONSENSE. Sote tumebaki tumepigwa na butwaa. Hana la kufanya Prof. huyu akirogwa kujiuzulu "Mungu" ama malaika wake watamshughulikia.
Tuiangalie upya Katiba yetu inayomjenga mtu kuwa "Mungu".