Kauli za kuwaita mawaziri wapumbavu ama nonsense zitafutwa na Katiba Mpya

Kauli za kuwaita mawaziri wapumbavu ama nonsense zitafutwa na Katiba Mpya

Mama yupo sawa! Hoja ya kuzuia sukari ya nje haina mashiko! Maana viwanda vyetu bado havitutoshelezi.
Jee aliyeweka msimamo huo ni Waziri au Serikali nzima? Mama angeweza ku overrule kauli ya Waziri wake bila kui crush tena kwa lugha isiyo na staha.
 
Sasa unazuiaje sukari nje?, Kwani matokeo yake hujayaona? Viwanda vichache, bei ikapanda hadi sukari ikawa adimu kupatikana, acha mataifa mengine yajaze sukari nchini ushindani uwe mkubwa bei iwe chee!

Mama yupo sahihi kwenye hili. [emoji3581]
Wewe ni wale mnaotakiwa kuitwa n..........e

Tafuta ufumbuzi wa kutatua upungufu wa sukari ndani ya nchi yako. Ikiwa ni pamoja na kuongeza uzalishaji kwa viwanda vilivyopo na kuanzisha viwanda vipya.

Kuagiza sukari toka nje ya nchi na ikawa nchi hiyo ghalama za uzalishaji ziko chini sana kamwe viwanda vilivyoko nchini kwako havitaendelea. Na hiyo inakuwa ni kaburi la ajili nchini kwako. Fikilia kwa mapana zaidi mkuu acha ushabiki.
 
Daah! Mkuu ulinzi wa bidha za ndani unafanywa hata na mataifa makubwa. Sembuse hii dona kantre?
Vijana wana ubongo lakini hawautumii ubongo wao kwa mambo ya maendeleo bali kwa ushabiki.
 
Katiba yetu inampa Rais mamlaka makubwa sana nchi hii. Rais ni kama Mungu kwa mujibu wa katiba yetu.

Mawaziri wanatwezwa lkn hawana cha kufanya. Wakijuzulu "mungu" anaweza kutafsiri hatua hii kama dharau na kuamua kuwashughulikia. Wanalazimika kuipokea kauli ya "mungu mtu" kwa mikono miwili.
Na kazi iendelee.
 
Daah! Prof Mkenda kadhalilishwa mpk namhurumia
Hahahaha si ilisemekana itatumika kalamu, badala ya kufoka.Naona Kalam haiwezi kutoa wino sawasawa, inakwaruza🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Wewe ni wale mnaotakiwa kuitwa n..........e

Tafuta ufumbuzi wa kutatua upungufu wa sukari ndani ya nchi yako. Ikiwa ni pamoja na kuongeza uzalishaji kwa viwanda vilivyopo na kuanzisha viwanda vipya.

Kuagiza sukari toka nje ya nchi na ikawa nchi hiyo ghalama za uzalishaji ziko chini sana kamwe viwanda vilivyoko nchini kwako havitaendelea. Na hiyo inakuwa ni kaburi la ajili nchini kwako. Fikilia kwa mapana zaidi mkuu acha ushabiki.
Ni muda mwingi sasa umepita, viwanda vya ndani vimeshindwa kukizi hitaji la ndani. Toka sukari ipande kuwa 3000 kwa kilo imeshindikana kushuka. Hoja yako naiunga mkono kwa bidhaa ambazo si za lazima Sana kwa mahitaji ya kila siku.
 
Katiba yetu inampa Rais mamlaka makubwa sana nchi hii. Rais ni kama Mungu kwa mujibu wa katiba yetu.

Mawaziri wanatwezwa lkn hawana cha kufanya. Wakijuzulu "mungu" anaweza kutafsiri hatua hii kama dharau na kuamua kuwashughulikia. Wanalazimika kuipokea kauli ya "mungu mtu" kwa mikono miwili.

Rais Magufuli aliwaita mawaziri Dr. Philip Mpango na Prof. Kabudi WAPUMBAVU mbele ya hadhara. Wakapokea kauli hii kwa mikono miwili. Sote tukabakia tumeduwaa. Ni kwasababu hawakuwa na la kufanya mawaziri hawa. Walimwogopa "mungu" na malaika wake

Rais Samia ametamka hadharani kwamba uamuzi wa Prof. Mkenda kuzuia sukari toka nje ni NONSENSE. Sote tumebaki tumepigwa na butwaa. Hana la kufanya Prof. huyu akirogwa kujiuzulu "Mungu" ama malaika wake watamshughulikia.

Tuiangalie upya Katiba yetu inayomjenga mtu kuwa "Mungu".
Hapa NONSENSE inamaanisha UPUUZU na siyo UPUMBAVU
 
Waziri ni kiongozi na mtu mzima. Hapaswi kutwezwa utu wake. Fikra kama zako hazitakiwi ktk jamii maana zimejaa udikteta.
Hizi heshima za kupewa ndio wanatufanyia mambo ya kikhanithi, mwingine anaenda kukodi software kwa bilioni 60+, huyu huku anataka kufanya sukari iwe shida.

Kama wanafanya upumbavu waambiwe, kikubwa tu anaewaambia wapumbavu nae akifanya upumbavu akubali kuambiwa.
 
Wakati wa mazunguzo ya Marais Samia na Museveni wa Uganda mbele ya vyombo vya habari, Rais Museveni alilalamikia 'pin' iliyopigwa na Prof. wa uchumi kwenye maeneo ya 'macroeconomics' ya kutokuagiza sukari kutoka nje ya nchi. Ifahamike kuwa mke wa Prof. huyo ni Daktari wa falsafa! Rais Samia aliiondoa 'pin' hiyo na kusema alichokifanya Prof. huyo ni 'nonsense'! Rais Samia anamnukuu Prof. "hatutanunua, hatutakubali" na kusema hiyo ni 'nonsense'! (Angalia video clip hapo chini).

Nonsense maana yake ni 1. maneno yaliyoandikwa au kutamkwa ambayo hayana maana au hayaleti maana. Pia inaweza kuwa na maana ya kutokukubaliana; 2. maana nyingine ni 'upumbafu' au 'tabia isiyokubalika.' Pia yaweza kuwa ni 'upuuzi'. Kwa Prof. kufanya jambo linalofananishwa na 'nonsense', basi picha ya huyo Prof. ni hiyo kwenye maana hizo hapo juu!

Maswali:
  1. Je, Rais Samia hakusikia au kuongea na waziri huyo juu ya jambo hilo kabla ya Rais Museveni kulalamika siku hiyo ya ugeni wake hapa Bongo?
  2. Je, utafiti aliofanya Prof. huyo na kuzingatia masuala ya muda mrefu mfano kukuza viwanda vya ndani ili kutoa ajira na kumuinua mkulima ulikuwa haufai kwa mujibu wa Rais Samia kwa msaada wa washauri wake wa uchumi? (Angalia video hapo chini)
  3. Hivi Rais Samia alifahamu sababu na ushahidi wa Prof. kusema 'hatutanunua, hatukubali'?
  4. Rais akiwa kama diplomat number 1, si angesema ombi la Rais Museveni watalifanyia kazi?
  5. Kwa mujibu wa Prof. huyo, waagiza sukari walifikia hatua ya kutaka kumpa rushwa ili atoe vibali, je jambo kama hilo haliwezi kufanyika kwa Rais?
  6. Halafu kama Prof. alitaka kupewa rushwa, je alitoa taarifa hiyo TAKUKURU?



 
Katiba yetu inampa Rais mamlaka makubwa sana nchi hii. Rais ni kama Mungu kwa mujibu wa katiba yetu.

Mawaziri wanatwezwa lkn hawana cha kufanya. Wakijuzulu "mungu" anaweza kutafsiri hatua hii kama dharau na kuamua kuwashughulikia. Wanalazimika kuipokea kauli ya "mungu mtu" kwa mikono miwili.

Rais Magufuli aliwaita mawaziri Dr. Philip Mpango na Prof. Kabudi WAPUMBAVU mbele ya hadhara. Wakapokea kauli hii kwa mikono miwili. Sote tukabakia tumeduwaa. Ni kwasababu hawakuwa na la kufanya mawaziri hawa. Walimwogopa "mungu" na malaika wake

Rais Samia ametamka hadharani kwamba uamuzi wa Prof. Mkenda kuzuia sukari toka nje ni NONSENSE. Sote tumebaki tumepigwa na butwaa. Hana la kufanya Prof. huyu akirogwa kujiuzulu "Mungu" ama malaika wake watamshughulikia.

Tuiangalie upya Katiba yetu inayomjenga mtu kuwa "Mungu".
Uamuzi wa waziri kweli ni NONSENSE. Nitaeleza
  1. JPM akiwa Uganda alitoa ombi kwa serikali ya Uganda iruhusu sukari ya Uganda kuuzwa Tanzania na ombi hilo likakubaliwa; lengo ilikiwa ni kukabili upungufu wa sukari;
  2. Katika jitihata za kupambana na upungufu wa sukari huku tukilinda viwanda vyetu yapo maelekezo kuwa ni wenye viwanda vya sukari tu ndio wanaoruhusiwa kuingiza sukari kutoka nje ya nchi ili kujazilizia kiasi wanachopungukiwa. Balozi Ami Mpungwe kathibitisha hilo kuwa Tanzania bado inaagiza sukari kutoka Uganda igawa alisema bei yake siyo rafiki;
  3. Tanzania kama sehemu ya jumuia ya Afrika Mashariki inapaswa kuruhusu kusambazwa kwa bidha kutoka kwa wenza wake bila vikwazo- hili linahusu sukari pia. Toka waziri atoe hilo tamko hupiti hata na kilo moja ya sukari kutoka Uganda kuingia Tanznaia
  4. sasa tunakuwa je na waziri asiye jua hayo na kuyazingatia kabla ya kutoa tamko? Halafu akiambia NONSENSE mlete uprofessa kama chanjo ya kumkinga- Hapana. Hawa mawaziri lazima wajue kuwa wao ni wasaidizi na ukishakubali kuwa msaidizi ujue ndo mwisho wa kutumia akili yako- unasubiri ya yule aliyekupa usaidizi.
 
Katiba yetu inampa Rais mamlaka makubwa sana nchi hii. Rais ni kama Mungu kwa mujibu wa katiba yetu.

Mawaziri wanatwezwa lkn hawana cha kufanya. Wakijuzulu "mungu" anaweza kutafsiri hatua hii kama dharau na kuamua kuwashughulikia. Wanalazimika kuipokea kauli ya "mungu mtu" kwa mikono miwili.

Rais Magufuli aliwaita mawaziri Dr. Philip Mpango na Prof. Kabudi WAPUMBAVU mbele ya hadhara. Wakapokea kauli hii kwa mikono miwili. Sote tukabakia tumeduwaa. Ni kwasababu hawakuwa na la kufanya mawaziri hawa. Walimwogopa "mungu" na malaika wake

Rais Samia ametamka hadharani kwamba uamuzi wa Prof. Mkenda kuzuia sukari toka nje ni NONSENSE. Sote tumebaki tumepigwa na butwaa. Hana la kufanya Prof. huyu akirogwa kujiuzulu "Mungu" ama malaika wake watamshughulikia.

Tuiangalie upya Katiba yetu inayomjenga mtu kuwa "Mungu".
Katiba ya sasa imetoa nguvu kwa baraza la Mawaziri kumfukuza kazi rais anayefanya mambo kama hayo, ila hawajui kutumia nguvu hizo.
 
Naweza kusema ni serikali ya pipuuzi kwa kweli, how on Earth mtu kama Bashite, Sabaya et all wanakua viongozi wa umma tena kwenye ofisi nyeti, and then bado unajiita uko serious na unaupiga mwingi, tulipoacha kufuata maadili weledi na unyeyenyekevu pamoja na uzalendo wa kweli ndipo tuliharibu hii nchi, kuna watu mpaka sasa wamo lakini believe me hawakustahili hata kuwa wenyeviti wa vijiji Trust me
 
Katiba ya sasa imetoa nguvu kwa baraza la Mawaziri kumfukuza kazi rais anayefanya mambo kama hayo, ila hawajui kutumia nguvu hizo.
Hiyo nguvu imepokwa na haipo. Waziri kateuliwa na rais huyo huyo. Anaweza kumtumbua kabla hakujapambazuka.

Rais pia ndiye mmiliki wa spika. Ili mjadala ufanyike bungeni lazima spika aridhie. Huyu spika ni mwanachama wa chama ambacho rais ndiye mwenyekiti wake.

Atampa maagizo/shinikizo spika asiukubali mjadala. Spika akizingua asubuhi tu atavuliwa uanwchama na kupoteza uspika.
 
Kama kuna mtanzania anadhani hilo li nonsense ni kwa ajili ya waziri basi amepotea.

Hilo tusi ni la jumla jumla kwa baraza zima na watendaji woote na wananchi
Muwage mnacomment kwa kuchuja habari kwanza.

Chukua hotuba ya waziri Mkenda inayozungumzia masuala ya mashamba ya miwa, viwanda vya sukari, uhaba wa sukari na utaratibu wa uagizwaji na uingizwaji wa sukari.

Ukitoka kuisikiliza hiyo, chukua hotuba ya rais Samia aliyoitoa Chato wakati wa ziara ya rais M7, utaelewa dhahiri mtoa mada alichomaanisha.

Tukichukulia sura ya rais na baraza lake la mawaziri ni mfano wa familia moja ya ndoa, mtu na mke wake kiutendaji.

Hatutegemei mke wa mtu azungumze jambo, halafu baadaye atoke mumewe hadharani kuliponda ama kulikanusha jambo hilo!

Majirani tutashangaa na kuona dosari iliyo wazi katika familia hiyo!

Haiwezekani jambo moja linalopikwa katika chumba kimoja likatoka na maelezo tofauti ya msigano!

Kwa mantiki ya mfano nilioutoa ni kwamba waziri hawezi kukurupuka kutoa msimamo wa serikali bila baraka za rais, never on earth!

Ikitokea msigano wa wazi hivyo, yampasa waziri kujitathimini na kubwaga manyanga ili kulinda hadhi yake!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naweza kusema ni serikali ya pipuuzi kwa kweli, how on Earth mtu kama Bashite, Sabaya et all wanakua viongozi wa umma tena kwenye ofisi nyeti, and then bado unajiita uko serious na unaupiga mwingi, tulipoacha kufuata maadili weledi na unyeyenyekevu pamoja na uzalendo wa kweli ndipo tuliharibu hii nchi, kuna watu mpaka sasa wamo lakini believe me hawakustahili hata kuwa wenyeviti wa vijiji Trust me
Kimsingi nchi yetu kwa sasa imejaa chuki za aina mbili

1. Za kisisa. Kwasabb waliopo madarakani hawakuchaguliwa na wananchi. Na sisa zinendeshwa kwa figisu
2. Za kiuchumi. Kwasabb mifumo ya masoko na ajira inavurugwa na wakubwa. Wao wanajipendelea na hawajali wengine
 
Hata katiba mpya ikiwepo mawaziri wataburuzwa na kutukanwa tu. Ni masuala ya kibinadamu zaidi.

Katiba mpya sio muarobaini wa kila tatizo tunalolifahamu.
 
Back
Top Bottom