Kauli za Mkuu wa Mkoa wa Dar, Amos Makalla, zinakiuka Haki za msingi za Binadamu

Kauli za Mkuu wa Mkoa wa Dar, Amos Makalla, zinakiuka Haki za msingi za Binadamu

Tatizo mkuu wa nchi wa sasa haijui vizuri hii nchi. Anadhani JPM alikuwa katili ilihali alijitahidi kukomesha uhalifu na wahalifu kwa kushirikiana na kamanda Siro!
Raia wema tuliishi kwa amani.

Sasa mama yeye anadhani Tz ni kama ulaya, polisi wawabembeleze wahalifu.😲🤔 Hawajui vizuri wahalifu wa tanganyika. Ukiwachekea utaambulia mabua!

Sasa hivi mauaji kila mahali. Mara wivu wa mapenzi, wizi nk. Tofauti na awamu iliyopita. Wengi waliopotea walikuwa wahalifu. Leo hii raia wema ndio wanapotezewa uhai na wahalifu tena hadharani kwa kukatwa mapanga. Ama kwa hakika tutamkumbuka sana hayati JPM! RIP
Kipindi Cha Jiwe Hauwezi kumsikia ndani ya week Moja huyu kamuuwa mke wake ,huyu kamuuwa mpenzi wake ,huyu kambaka mtoto ,majambazi yamvamia wakala .Watu walijua Kuna mwamba anatawala ,upole usipitilize Watu wanakushika kwenye macho ,acha tujionee
 
Angeongezea au Mochwari qmmmk kuna coworker wamevamia kwake juzi night wamembaka housegirl sasa yeye hatujui maana alisema yy hawajamfanya kitu ila wameiba vitu na kuwajeruhi.
 
Ningekuwa police au Mimi ndio IGP ukikamatwa wewe panya road Unafanya uharifu unamezeshwa Uji WA cement halafu unatupwa basi.


Unaua wenzako halafu wewe ukiuawa mnaleta mambo ya haki za binadam.


Mpuuzi weww
 
Makala kwa kauli hii amezingua anasahau yeye ni wa wote wahalifu na Wema, He is Comforter in Chief at Region level kauli tata kama izo niku create tension zisizo na Msingi, Hakuna anae afika na Mambo yanayofanywa na Panyaroad ila Asingeongea ivo public na aiende security organs zake Secretly na atoe hayo maelezo makali kabisa, Ku publicly issue kama hio kuna leta maneno mengi ila pia makala sio Mahakama aache kila mtu afanye kazi yake
Wewe ni mpuuzi , kama Una mwanao panya road jiandae kuokota mzoga.
 
Hao vijana wanatoka sayari ya Mars?

Jamii ya kihalifu huzalisha jamii ya kihalifu.

Tuanze kutatua machangamoto ya malezi na shule za watoto wa Taifa hili hautakaa usikie panyaroad.

Polisi wenyewe wameajiri wahalifu kibao humo ndani ndo maana kila kukicha utasikia majanga juu ya majanga dhidi ya raia.

Kiongozi kama Makala hawanaga mikakati ya kuzuia ama kudhibiti uhalifu zaidi ya matumizi ya nguvu, ubabe na kuvunja haki za binadamu
Mama yako na familia yako ndio Wana Jukumu la kukurekebisha tusipeane majukumu.

Ukishindwa kumrekebisha mwanao jiandae kurekebishiwa na jamii. Huku atapigwa Shaba au kuchomwa Moto
 
Kauli iliyotolewa na Mkuu wa wa Dar, Amos Makala, kwa wazazi wa watoto kuwa atakayemkosa mtoto wake nyumbani, basi anapaswa aende kituo cha Polisi au hospitali kwenda angalia kama yuko huko, ni kauli ya vitisho visivyokuwa na msingi na ni kauli ambayo inakiuka Haki za Binadamu.

Najua Mkuu wa Mkoa, ametoa kauli hiyo kuhusiana na kukerwa na vitendo vya vijana wadogo, wanaofahamika kwa jina la Panyaroad, kwa vitendo vyao vya kuvunja nyumba za wakazi wa jiji la Dar, kufanya wizi wa vitu mbalimbali, kujeruhi hadi kusababisha vifo, kama ilivyotokea hapo majuzi huko Kawe.

Lakini nijaribu kumuuliza Mkuu wa Mkoa wa Dar, hivi yeye anadhani kwa kutumia vitisho hivyo, ndiyo atakuwa amepata ufumbuzi wa vitendo hivyo vya Panyaroad?

Hivi anajua "impact" ya kuyatamka maneno hayo hadharani, akiwa ndiye Mwenyekiti, wa Kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa huo wa Dar?

Nimuulize tena Mkuu wa Mkoa, hivi anajua kwa kuyatamka hayo maneno, ni kama ametoa "blessings" zake kwa Polisi wetu, waweze kujeruhi na hata kuua hao wanaoitwa Panyaroad, bila kwanza kuwahoji na kupata ushahidi wa hao wahalifu?

Hivi yeye Mkuu wa Mkoa, anatambua kuwa kwa tamko hilo anakiuka misingi ya Haki za binadamu?

Ninaposema hivyo, siyo kuwa naunga mkono vitendo hivyo vya kinyama vya hao wanaojiita Panyaroad, la hasha, nia yangu ni kulitaka Jeshi la Polisi, litende Kazi zake kwa Weledi mkubwa, kwa kufuata sheria.

Polisi wetu wanafahamu kuwa Hawama mamlaka ya kuua raia yeyote bila msingi wowote.

Tunafahamu pia kuwa Katika nchi yetu, ni mhimili wa Mahakama pekee, uliopewa mamlaka ya kumtia hatiani raia yeyote na kutoa hukumu.

Nchi hii inaendeshwa kwa kufuata misingi ya kisheria.

Hivi anaweza kutuambia kwa kuyatamka hayo maneno, ni sheria gani inayomruhusu yeye kama Mkuu wa Mkoa, aliagize Jeshi lake la Polisi, litekeleze majukumu yake, pasipo kuzingatia sheria za nchi hii?

Kwa hiyo Mkuu wa Mkoa, Amos Makala, anapaswa aombe radhi kwa wakazi wa Mkoa wa Dar, kwa matamshi aliyoyatoa, ambayo ni kinyume cha utawala bora, unaozingatia sheria.
Mkuu 'Mystery', HESHIMA MKUU, kwa sababu huwa nafurahia sana mada zako hapa jukwaani; ila sijaona umuhimu wa hii hapa, isipokuwa kama una mfupa tu wa kusaga na huyo mkuu wa mkoa.

Sitetei uvunjifu wa haki za mtu yeyote, kama nisivyopendezwa na uvunjifu wa sheria na hawa wahuni, tena watoto wadogo tu, huko mitaani.

Hawa wanatakiwa kila wakikamatwa wacharazwe viboko na kurushwa vichura hadi akkili ziwaingie kichwani.

Ni upuuzi usio na kimo kujaribu kutetea kwa njia yoyote matendo ya kishenzi yanayofanywa na hawa watoto.

Ndiyo, polisi wana mchango mkubwa sana katika kuacha hali iwe mbovu kiasi ilivyo sasa. Hivi vitendo siyo vya ghafla tu, huanza taratibu, tena kwa uoga mkubwa, wanapoona udhaifu wa jamii na polisi, wanazidi kuwa na ujasiri mkubwa kuendeleza vitendo hivui viovu na kuanza 'recruitment' ya watoto wengi zaidi.

Si lazima wauliwe, lakini mtoto yeyote anayejiingiza kwenye vitendo hivi ni lazima afahamu mbele ya safari kwamba hawezi kutoka salama. Huo ndio ujumbe muhimu unaotakiwa kusisitizwa.

Ni lazima wajuwe mbele ya safari, kwamba katika kutenda wanayotenda, inawezekana kabisa kutokuwepo na fursa ya kufikishwa mbele za sheria (mahakamani), kwa sababu matendo wanayofanya wao wenyewe hayawapi nafasi wanaowatendea nafasi ya kujitetea.

Sioni sababu ya lawama kwa mkuu wa mkoa kusema aliyoyasema; labda kama yapo ambayo siyajui.
 
Kauli iliyotolewa na Mkuu wa wa Dar, Amos Makala, kwa wazazi wa watoto kuwa atakayemkosa mtoto wake nyumbani, basi anapaswa aende kituo cha Polisi au hospitali kwenda angalia kama yuko huko, ni kauli ya vitisho visivyokuwa na msingi na ni kauli ambayo inakiuka Haki za Binadamu.

Najua Mkuu wa Mkoa, ametoa kauli hiyo kuhusiana na kukerwa na vitendo vya vijana wadogo, wanaofahamika kwa jina la Panyaroad, kwa vitendo vyao vya kuvunja nyumba za wakazi wa jiji la Dar, kufanya wizi wa vitu mbalimbali, kujeruhi hadi kusababisha vifo, kama ilivyotokea hapo majuzi huko Kawe.

Lakini nijaribu kumuuliza Mkuu wa Mkoa wa Dar, hivi yeye anadhani kwa kutumia vitisho hivyo, ndiyo atakuwa amepata ufumbuzi wa vitendo hivyo vya Panyaroad?

Hivi anajua "impact" ya kuyatamka maneno hayo hadharani, akiwa ndiye Mwenyekiti, wa Kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa huo wa Dar?

Nimuulize tena Mkuu wa Mkoa, hivi anajua kwa kuyatamka hayo maneno, ni kama ametoa "blessings" zake kwa Polisi wetu, waweze kujeruhi na hata kuua hao wanaoitwa Panyaroad, bila kwanza kuwahoji na kupata ushahidi wa hao wahalifu?

Hivi yeye Mkuu wa Mkoa, anatambua kuwa kwa tamko hilo anakiuka misingi ya Haki za binadamu?

Ninaposema hivyo, siyo kuwa naunga mkono vitendo hivyo vya kinyama vya hao wanaojiita Panyaroad, la hasha, nia yangu ni kulitaka Jeshi la Polisi, litende Kazi zake kwa Weledi mkubwa, kwa kufuata sheria.

Polisi wetu wanafahamu kuwa Hawama mamlaka ya kuua raia yeyote bila msingi wowote.

Tunafahamu pia kuwa Katika nchi yetu, ni mhimili wa Mahakama pekee, uliopewa mamlaka ya kumtia hatiani raia yeyote na kutoa hukumu.

Nchi hii inaendeshwa kwa kufuata misingi ya kisheria.

Hivi anaweza kutuambia kwa kuyatamka hayo maneno, ni sheria gani inayomruhusu yeye kama Mkuu wa Mkoa, aliagize Jeshi lake la Polisi, litekeleze majukumu yake, pasipo kuzingatia sheria za nchi hii?

Kwa hiyo Mkuu wa Mkoa, Amos Makala, anapaswa aombe radhi kwa wakazi wa Mkoa wa Dar, kwa matamshi aliyoyatoa, ambayo ni kinyume cha utawala bora, unaozingatia sheria.
Ni kweli mkuu,wewe umeona kama Mimi maana Jana alitamka kauli Kali Sana Wakati angepunguza jazba na kumezea Ili washughulike kimya kimya..

Ila kusema mtoto wako akipotea kamtafute Polisi au hospital manake ametia amri ya kupiga watu risasi,inaweza kumletea kuwa uhalifu dhidi ya ubinadamu..
 
Mama yako na familia yako ndio Wana Jukumu la kukurekebisha tusipeane majukumu.

Ukishindwa kumrekebisha mwanao jiandae kurekebishiwa na jamii. Huku atapigwa Shaba au kuchomwa Moto
Lunatic
 
Kauli iliyotolewa na Mkuu wa wa Dar, Amos Makala, kwa wazazi wa watoto kuwa atakayemkosa mtoto wake nyumbani, basi anapaswa aende kituo cha Polisi au hospitali kwenda angalia kama yuko huko, ni kauli ya vitisho visivyokuwa na msingi na ni kauli ambayo inakiuka Haki za Binadamu.

Najua Mkuu wa Mkoa, ametoa kauli hiyo kuhusiana na kukerwa na vitendo vya vijana wadogo, wanaofahamika kwa jina la Panyaroad, kwa vitendo vyao vya kuvunja nyumba za wakazi wa jiji la Dar, kufanya wizi wa vitu mbalimbali, kujeruhi hadi kusababisha vifo, kama ilivyotokea hapo majuzi huko Kawe.

Lakini nijaribu kumuuliza Mkuu wa Mkoa wa Dar, hivi yeye anadhani kwa kutumia vitisho hivyo, ndiyo atakuwa amepata ufumbuzi wa vitendo hivyo vya Panyaroad?

Hivi anajua "impact" ya kuyatamka maneno hayo hadharani, akiwa ndiye Mwenyekiti, wa Kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa huo wa Dar?

Nimuulize tena Mkuu wa Mkoa, hivi anajua kwa kuyatamka hayo maneno, ni kama ametoa "blessings" zake kwa Polisi wetu, waweze kujeruhi na hata kuua hao wanaoitwa Panyaroad, bila kwanza kuwahoji na kupata ushahidi wa hao wahalifu?

Hivi yeye Mkuu wa Mkoa, anatambua kuwa kwa tamko hilo anakiuka misingi ya Haki za binadamu?

Ninaposema hivyo, siyo kuwa naunga mkono vitendo hivyo vya kinyama vya hao wanaojiita Panyaroad, la hasha, nia yangu ni kulitaka Jeshi la Polisi, litende Kazi zake kwa Weledi mkubwa, kwa kufuata sheria.

Polisi wetu wanafahamu kuwa Hawama mamlaka ya kuua raia yeyote bila msingi wowote.

Tunafahamu pia kuwa Katika nchi yetu, ni mhimili wa Mahakama pekee, uliopewa mamlaka ya kumtia hatiani raia yeyote na kutoa hukumu.

Nchi hii inaendeshwa kwa kufuata misingi ya kisheria.

Hivi anaweza kutuambia kwa kuyatamka hayo maneno, ni sheria gani inayomruhusu yeye kama Mkuu wa Mkoa, aliagize Jeshi lake la Polisi, litekeleze majukumu yake, pasipo kuzingatia sheria za nchi hii?

Kwa hiyo Mkuu wa Mkoa, Amos Makala, anapaswa aombe radhi kwa wakazi wa Mkoa wa Dar, kwa matamshi aliyoyatoa, ambayo ni kinyume cha utawala bora, unaozingatia sheria.
Unajua magenge ya mafia ya Colombia yalianzaje? Liko wapi kosa la RC kutoa angalizo kwa wazazi? # Hebu tuiache serikali ifanye kazi zake. Inajua na kuzingatia haki za binadamu .🙏🙏🙏
 
Ila madogo acha washikishwe adabu, maana ndo tunaitwa wanaume wa Dar, yaani hatujiwezi kwa lolote mpaka tunatishwa na hivi vitoto viteja.
hofu kupitia hilo polisi wasio waaminifu waweza gonga watu wasio na hatia kauli jumuishi sio zurisana
 
Mkuu wa mkoa Hana sababu ya kuomba msamaha, Hivi unajuwa uchungu wa ndugu waliopoteza ndugu yao kwa kuuwawa na hao panya Road?? Ungepatwa na msiba ule ungekuja na kupata nguvu ya kuandika hayo uliyoandika hapa? Una maslahi gani na hao vibaka wanaotesa wananchi bila hatia? Kwanini usiandike makala ya kuwasihi wazazi juu ya kuchunga mienendo ya watoto wao? Kwanini usiandike makala ya kuwaasa hao vibaka kuacha tabia hiyo? Unajuwa maumivu ya kukatwa na mapanga wewe?

Tuondolee uanaharakati wako hapa wakati watu wanaumia. Kwani wewe ulitaka asema wazazi wakawaangalie wapi watoto wao? Ulitaka asema wakawaangalie hotelini? Au kanisani? Au ulitaka aseme wakawaangalie shuleni? Acha serikali ifanye kazi yake ya kulinda raia wake, Kama mwanao Ni mhusika mwambie aache Mara moja vinginevyo utamkuta huko ulikoelekezwa, ndio nyie mnakuwa mnatetea mambo yanayokwenda hata kinyume na utamaduni wetu kwa madai ya uanaharakati na haki za binadamu
 
Hali ya uchumi ni ngumu sana.

Hao panya road wameona uhalifu ndio suluhisho la kujipatia kipato.

Wakipora wanasaidia na familia zao.

Hili tatizo lina mizizi mirefu sana.

Halitamalizwa kwa kauli tu.
Uchumi Kama mgumu mbona wewe siyo jambazi au kibaka? Nani kakwambia Hilo ndio suluhisho, kwa hiyo uchumi ukiwa mgumu utawaambia wanao wakawe panya Road?
 
Hakuna ujinga Kama huo hao wakibainika lazima wapewe haki yao maana wametesa raia vya kutosha, Kama wewe unamwanao huko Basi utamkuta ulikoambiwa
Ndiyo maana nikasema hao Polisi wanapashwa kufanya Kazi kwa kufuata Weledi.

Kupokea maelekezo toka juu, ambayo wanajua yanakiuka sheria, itakuja kula kwao!
 
Back
Top Bottom