Kayumba Nyamwasa: Rwanda imekuwa ikiiba madini ya Congo kwa muda mrefu sana

Kayumba Nyamwasa: Rwanda imekuwa ikiiba madini ya Congo kwa muda mrefu sana

Marie Antoinette

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2019
Posts
426
Reaction score
412
SEHEMU ya I




"Inshu ya Banyamulenge, ni kisingizio tu! Ni kitu ambacho hakipo. Iliisha mwaka 2002". Anasema Nyamwasa.

Baada ya vifo vya wanajeshi wa Afrika kusini kufia vitani nchini DRC, mpaka sasa inaripotiwa wanajeshi 14 ndo waliopoteza maisha.

Hili jambo lilizuwa maswali mengi, wengine wakiituhumu serikali ya Afrika kusini, kuwataka wanajeshi hao wapigane na M23, huku wakiwa hawana mafunzo ya kutosha na vifaa vya kukabiliana na waasi wa M23.

News Room Afrika, chombo cha habari cha nchini Afrika kusini, kilimualika Kayumba Nyamwasa kuweza kuwajuza wasikilizaji mengi yanayohusiana na mgogoro huo.

Kayumba Nyamwasa, aliyekuwa mkuu wa majeshi nchini Rwanda, badae akawa Balozi wa Rwanda nchini India, ambaye kwa sasa anaishi nchini Afrika kusini,Kayumba pia aliwahi kuwa mkuu wa kitengo cha upelelezi chini Rwanda, kabla hajatofautiana na raisi Paul Kagame. Cheo chake ni Lutenanti General.

Akiulizwa na mwanahabari,kuhusu hali ya wakimbizi wa mwaka 1959 nchini Rwanda, iliyomsababishia(Kayumba) kuzaliwa nje ya nchi yake, aliulizwa, ni kipi anaona kinaweza kusaidia kuleta amani katika ukanda wa DRC,RWanda na Burundi.

Kayumba: Nadhani, njia sahihi na ya kipekee kufikia muafaka wa jambo hili la mashariki mwa DRC, ni mazungumzo tu. Lakini, si kwa Congo tu, pia kwa ukanda wote. Ukiangalia tatizo la Congo, ambapo Rwanda imekuwa ikishiriki huo mgogoro kwa zaidi ya miaka 30. Kuanzia mwaka 1996, Rwanda ilikuwa vitani nchini Congo.

Kwenye utawala wa Mobutu, utawala wa Desire Kabila, utawala wa Joseph Kabila, na sasa kwenye utawala wa Tshisekedi.

Tuliwahi pia kuwa na mahusiano mabaya sana na nchi ya Uganda: kuna vita baina ya Rwanda na Uganda huko Kisangani(Nchini DRC. Vinaweza kuongelewa hapo badae kama hiyo threat itakuwa na umhimu), kufungwa kwa mipaka, na mambo mengine kama hayo. Mahusiano yetu na Tanzania, pia kuna kipindi hayakuwa mazuri.

Mwaka 2013, Rais Kikwete na Rais Kagame walipotofautiana. Upande wa Burundi, kuanzia 2015, Rwanda na burundi hawaangaliani kwa jicho la amani. Kwa sasa hivi tunaongelea vita nchini Congo. Lakini pia,kuna uwezekano kukatokea jambo lolote pia huko Burundi. Hata jana, raisi wa Burundi, alitangaza kwamba amejiandaa vita na Rwanda.

Ngoja tuongelee watusti huko Congo kuhatalishiwa maisha. Hilo jambo ni kweli.

Watu huongelea mauaji ya kimbali nchini Rwanda, dhidi ya watutsi. Ni kweli yalitokea.

Lakini, kama unataka kutatua tatizo la ukanda, huwezi kukomboa watusti, kwa kuanzisha vita kwa watu wengine, kutafuta suruhu la watutsi, haimaanishi unatafuta suruhu la kuzuia genocide.

Tukiangalia DRC, tunaongelea watutsi zaidi ya laki 5, waliokimbilia Rwanda.

Je, ni mamilioni mangapi ya makabila mengine(Balega, Bahunde, Bahutu in Congo,Banande, hawa wote wamekuwa wakikimbia miaka yote hiyo 30.

Leo hii ukisema unaenda kuanzisha vita dhidi ya FDLR, hivi vita vinaenda kuwaondoa watu katika makazi yao. Kwangu, hilo siyo suruhisho.

Suruhisho ni kwamba, kwa serikali ya Congo, inatakiwa ikae meza ya mazungumzo na M23. Rwanda pia, inatakiwa iongee na wapinzani wake. Kwa sababu Rwanda inao wengi. Huu ukanda tu,iwe Afrika kusini, iwe Malawi, Zimbabwe,Mozambique wakimbizi karibia wote ni wanyarwanda. Lakini,serikali ya Rwanda, inalichukulia kama hakuna lolote lililotokea. Ongezea na wengine wote waliokimbia nchi, na kwenda ugaibuni. Ni kwamba wanahofia usalama wao. Sasa, kama hao ndo wanaoifadhili FDLR, kwa nini waifadhili?

Leo hii, hata ukiondoa tatizo la M23, wakimbizi wa Rwanda wataendelea kuwepo. Watakuwa kila kona.


Inaendelea................................................................
 
Kagame katika mahojiano na CNN kasema kuna Migodi ya Coltan Nchini Rwanda na kama mwandishi wa CNN yuko tayari waende akamuonyeshe sasa huyu Kayumba labda ana chuki binafsi na Kagame.

Kweni Coltan iko Congo pekee au Zahabu ziko Kongo pekee...?
 
-Hakuna mwandishi wa habari wa kwenda kuomba raisi ampeleke machimboni.

-Alitofautiana na Boss wake, akakimbia. Unategemea atasemaje? Japo kwa anaeelewa, yapo ya kweli anayoyaongea, yapo yasiyo ya kweli. Ila asilimia kubwa ni ukweli. Kwa cheo alichokuwepo nacho, kubali anajua mengi sana. Hapo issue iwe tu kumuumbua boss wake, japo na lenyewe halina madhala kihivyo.
 
Kagame katika mahojiano na CNN kasema kuna Migodi ya Coltan Nchini Rwanda na kama mwandishi wa CNN yuko tayari waende akamuonyeshe sasa huyu Kayumba labda ana chuki binafsi na Kagame.

Kweni Coltan iko Congo pekee au Zahabu ziko Kongo pekee...?
Hapo sasa
 
Sehemu ya II


Anaongea Kayumba : Huwezi ukasema kwamba, kwa sababu nimemaliza tatizo la M23, baaaasi. Kazi imeisha. La hasha. Tatizo bado litakuwa FDLR. Je, suruhisho ni lipi? Liquidate, eliminate. Maana yake ni nini!!! Ni kuwaua tu.
Unawezaje kuuwa raia wa taifa? Tukirudi kwenye swala la jenoside, nilikuwepo. Na mimi nilisaidia kuhakikisha mauaji hayo yanakomeshwa. Na mimi, ni mtutsi; hii ishu naiongelea kama mtu ninaeielewa. Toka kipindi hicho mpaka leo, Rwanda haijawahi kukaa na kuzungumza na hao watu walioshindwa.

Mwanahabari: tukiwa bado hapo kwenye swala la FDLR. KAtika mapigano ya Sake,waziri wetu wa ulinzi na mkuu wa majeshi, walisema kulikuwa na majibizano ya makombola kati ya DRC na Rwanda,ambapo DRC ilirusha makombola nchini Rwanda, na Rwanda ikajibu mapigo. Je, na wewe maoni yako, ni kwamba FDLR, ipo nchini Congo, na inaungwa mkono na raisi Tshisekedi?

KAYUMBA: Siwezi kusema kwamba Rwanda haitakiwi kujishughulisha na FDLR. Taifa lolote lenye makundi ya waasi wanaotumia silaha za moto, nchi hiyo lazina iwajibike. Lakini, unamaliza mzozo vipi? Ni kukaa na watu hao na kutafuta suruhisho. Labda niongezee kitu: Tulikuwa na uchaguzi Rwanda. Raisi, akajipatia kula asilimia 99.9; na umekuwa madarakani kwa muda wa miaka 30. Hata Mandela, nadhani kama angekuwa hai, sidhani kama hizo asilimia angepata kwa kuchaguliwa. Hii, inakupa picha halisi kwa nini watu hawa wanakuwa wapinzani wa serikali ya Rwanda.
Nikisema tatizo la wakimbizi, usifikilie tu watu wa FDLR waliopo nchini Congo. Kuna haya mataifa mengine niliyokutajia, ikiwemo Malawi, Mozambique, Zimbabwe, Zambia, Ulaya, kila kona. Halafu pia, kuna hawa manusura wa mauaji ya 1994 dhidi ya watutsi. Wapo kama mimi, niliepigania uwepo wa serikali iliyopo madarakani leo hii. Sasa basi, haya yote usipoyaangalia, ukasema tu unaenda kuongelea swala la M23, ni sawa na hujafanya chochote, unatatua tatizo nusu tu.
Shida nyingine, ni kwamba unatatuaje tatizo la ukanda! Kati ya Rwanda na mataifa mengine!!! Kama Burundi inasema yaliyopo kwa sasa, kama unafunga mipaka na Uganda. Kinachotokea ni nini! Labda, vita vinaenda kuhama kutoka DRC kuelekea Burundi. Na hapa tunapoongea, M23 karibia inaingia na Bukavu. Ikishafika Bukavu, ina maana tupo Kivu kusini, na mwambao wa Rusizi. Ukishakuwa katika mwambao huo, ndipo M23 itaungana na RED-TABARA. Kinachotokea, kilichopo Kivu kasikazini, ndo kitakachokuwa Kivu kusini.
Hapa ni wazi kwamba tatizo ni uongozi. Tunapoongelea nia ya kisiasa, tusimuangalie tu Tshisekedi. Kwa nini tusione na nia ya kisiasa ya raisi Kagame! Vyote ni sawa tu. Usihisi kwamba matatizo yaliyopo Congo, yanatofautiana na yaliyopo Rwanda. Ukija kuangalia, utagundua kwamba idadi ya wakimbizi wa DRC,haitofautiani na idadi ya wakimbizi wa Rwanda. Au pengine wa Rwanda wakawazidi idadi wa DRC.

Mwanahabari: Ni wiki sasa, jeshi la South Africa, limepoteza wanajeshi 14 huko Sake, katika vita na M23. Kwa mtazamo wako, ni nini kimeipa nguvu M23, kuweza kuwa na silaha za kisasa, na kuhimili kwa mta mrefu vita, na kupigana kwa wakati mmoja zaidi ya eneo moja?

KAYUMBA: Hili jambo lipe uhalisia wake: Mwaka 2020 na 2023, raisi Tshisekedi, aliingia makubaliano na raisi Museveni wa Uganda, wa kupeleka jeshi lake nchini Congo, na ujenzi wa barabara kutoka Uganda kwenda DRC ukafanyika.
Alikubaliana pia na Burundi,kupeleka jeshi lake Kivu kaskazini. Rwanda, haikupewa chance hiyo. Rwanda, ilikasirika. Na Raisi Kagame akasema, sijaalikwa nchini DRC, mi ntakwenda bila kualikwa. na aliposema tutaenda huko bila kualikwa, ndipo M23 ilipoanza mambo yake.
Hii kauli kwamba DRC haijawa na uungwana, ni uongo mtupu. Nakupa mfano: Kwenye uongozi wa Kabila, Rwanda iliruhusiwa kuingia nchini DRC kuitafuta FDLR.
Kuna kipindi ilifanyika oparesheni ijulikanayo kama umoja wetu. Watu wengi sana waliuliwa, wengine wakaimbia makazi yao. Mashirika ya kitaifa yalilalamika sana.
Mwaka 2019, raisi Tshisekedi, aliruhusu uongozi wa Rwanda kwenda DRC na kuuwa viongozi wa FDLR. Na waliwaua.
Hivi kweli, Rwanda inahitaji iruhusiwe mara ngapi kwenda Congo!

Zingatia: kuna kipindi, mkuu wa jeshi la Congo alikuwa mnyarwanda. Miaka! Walifanya nini? Leo hii eti wanataka kuingia Congo! Ngoja nikwambie kitu. FDLR ni kweli ipo. Na madai yake, yana mashiko. Kuwatakia uhuru kabila la watutsi, ni halali. Lakini, inakuwaje utafute amani ya kabila moja, makabila mengine uyaangamize?

Mwanahabari: Kwa haya yanayoendelea, unadhani ni nani anastahili kuwajibishwa matatizo haya yamayoleta mpaka vifo? Pia, umoja wa mataifa, umekuwa ukidai kwamba M23 inaungwa mkonono na serikali ya Rwanda. Je, kuna chochote unachoelewa kuhu hili?

KAYUMBA: Ahhhh, najua sana. Siyo kundi la kwanza tulilounga mkono. Ni kitu kilicho wazi. Hata sielewi kwa nini watu wanafichaficha. Unaona, Rwanda ndo iliweka kikomo kwenye utawala wa Mobutu. Mwaka 1996, tulipofuata wakimbizi na kuwarudisha kwao. Na hilo ndo lilikuwa lengo kubwa. Lakini, baada ya kukamilisha, tulitakiwa tubadili namna ya kuongoza nchi. Rwanda ilitakiwa kuongea na DRC kuhusu namna ya kuishi kwa amani na utulivu. Jambo la pili, ni upotoshaji. Kwamba M23 ni wanyamlenge. Issue ya Banyamulenge ilishaisha kitambo sana. Miaka ya 2002. Tena naweza kusema mwaka 1998, General James Kabarebe alipoondoka Kinshasa (Ndo alikuwa mkuu wa jeshi la DRC).
Kipindi cha utawala wa Kabila, Azarias Ruberwa, alikuwa makamu wa raisi. Ni mnyamulenge. Nyarugabo, alikuwa naibu spika, General Marick, arikuwa naibu kamanda wa jeshi, Bisengimana, ndo alikuwa mkuu wa Polisi. Ni wengi. Mpaka leo, kuna wanyamulenge wengi wenye vyeo kwenye ngazi za usalama. Na Generali Masunzu, hivi karibuni aliepewa kuwa mkuu wa jeshi wa kanda, ni mnyamulenge. HAta mawaziri, wapo wanyamurenge. Waziri wa miundombinu, ni mnyamulenge. Kwa hiyo, huku South Afrika, wakiongelea wanyamulenge, ni upotoshaji tu. Si kweli.
Issue ya wanyamulenge na M23, ni vitu viwili tofauti. Sema tu watu hawaelewi.


Itaendelea...................................................................................
 
Siasa za ukanda wa maziwa makuu,toka niko mdgo naskia wanapgana tu had nimezeeka bado wanapgna tu!! Hakika ni siasa za ajabu sana.
 
Kagame katika mahojiano na CNN kasema kuna Migodi ya Coltan Nchini Rwanda na kama mwandishi wa CNN yuko tayari waende akamuonyeshe sasa huyu Kayumba labda ana chuki binafsi na Kagame.

Kweni Coltan iko Congo pekee au Zahabu ziko Kongo pekee...?
cheki hili nalo😂😂😂Maroboti ya kagame yako mengi??

sasa kati ya ww mtanzania mtusi mkimbizi
na general wa kagame nani anaujua ukweli??


YAAN HILI KICHANI NI ROBOTI VIDOLE ROBOTI!
Linasubiri kusetiwa! Hata likiambiwa PaKa n malaika litakubali
 
Sasa ndo napata picha, huu mgogoro nilikuwa sijauelewa vizuri lakini angalau nimepata mwanga, weka muendelezo wa mahijiano mkuu
 
Sehemu ya II


Anaongea Kayumba : Huwezi ukasema kwamba, kwa sababu nimemaliza tatizo la M23, baaaasi. Kazi imeisha. La hasha. Tatizo bado litakuwa FDLR. Je, suruhisho ni lipi? Liquidate, eliminate. Maana yake ni nini!!! Ni kuwaua tu.
Unawezaje kuuwa raia wa taifa? Tukirudi kwenye swala la jenoside, nilikuwepo. Na mimi nilisaidia kuhakikisha mauaji hayo yanakomeshwa. Na mimi, ni mtutsi; hii ishu naiongelea kama mtu ninaeielewa. Toka kipindi hicho mpaka leo, Rwanda haijawahi kukaa na kuzungumza na hao watu walioshindwa.

Mwanahabari: tukiwa bado hapo kwenye swala la FDLR. KAtika mapigano ya Sake,waziri wetu wa ulinzi na mkuu wa majeshi, walisema kulikuwa na majibizano ya makombola kati ya DRC na Rwanda,ambapo DRC ilirusha makombola nchini Rwanda, na Rwanda ikajibu mapigo. Je, na wewe maoni yako, ni kwamba FDLR, ipo nchini Congo, na inaungwa mkono na raisi Tshisekedi?

KAYUMBA: Siwezi kusema kwamba Rwanda haitakiwi kujishughulisha na FDLR. Taifa lolote lenye makundi ya waasi wanaotumia silaha za moto, nchi hiyo lazina iwajibike. Lakini, unamaliza mzozo vipi? Ni kukaa na watu hao na kutafuta suruhisho. Labda niongezee kitu: Tulikuwa na uchaguzi Rwanda. Raisi, akajipatia kula asilimia 99.9; na umekuwa madarakani kwa muda wa miaka 30. Hata Mandela, nadhani kama angekuwa hai, sidhani kama hizo asilimia angepata kwa kuchaguliwa. Hii, inakupa picha halisi kwa nini watu hawa wanakuwa wapinzani wa serikali ya Rwanda.
Nikisema tatizo la wakimbizi, usifikilie tu watu wa FDLR waliopo nchini Congo. Kuna haya mataifa mengine niliyokutajia, ikiwemo Malawi, Mozambique, Zimbabwe, Zambia, Ulaya, kila kona. Halafu pia, kuna hawa manusura wa mauaji ya 1994 dhidi ya watutsi. Wapo kama mimi, niliepigania uwepo wa serikali iliyopo madarakani leo hii. Sasa basi, haya yote usipoyaangalia, ukasema tu unaenda kuongelea swala la M23, ni sawa na hujafanya chochote, unatatua tatizo nusu tu.
Shida nyingine, ni kwamba unatatuaje tatizo la ukanda! Kati ya Rwanda na mataifa mengine!!! Kama Burundi inasema yaliyopo kwa sasa, kama unafunga mipaka na Uganda. Kinachotokea ni nini! Labda, vita vinaenda kuhama kutoka DRC kuelekea Burundi. Na hapa tunapoongea, M23 karibia inaingia na Bukavu. Ikishafika Bukavu, ina maana tupo Kivu kusini, na mwambao wa Rusizi. Ukishakuwa katika mwambao huo, ndipo M23 itaungana na RED-TABARA. Kinachotokea, kilichopo Kivu kasikazini, ndo kitakachokuwa Kivu kusini.
Hapa ni wazi kwamba tatizo ni uongozi. Tunapoongelea nia ya kisiasa, tusimuangalie tu Tshisekedi. Kwa nini tusione na nia ya kisiasa ya raisi Kagame! Vyote ni sawa tu. Usihisi kwamba matatizo yaliyopo Congo, yanatofautiana na yaliyopo Rwanda. Ukija kuangalia, utagundua kwamba idadi ya wakimbizi wa DRC,haitofautiani na idadi ya wakimbizi wa Rwanda. Au pengine wa Rwanda wakawazidi idadi wa DRC.

Mwanahabari: Ni wiki sasa, jeshi la South Africa, limepoteza wanajeshi 14 huko Sake, katika vita na M23. Kwa mtazamo wako, ni nini kimeipa nguvu M23, kuweza kuwa na silaha za kisasa, na kuhimili kwa mta mrefu vita, na kupigana kwa wakati mmoja zaidi ya eneo moja?

KAYUMBA: Hili jambo lipe uhalisia wake: Mwaka 2020 na 2023, raisi Tshisekedi, aliingia makubaliano na raisi Museveni wa Uganda, wa kupeleka jeshi lake nchini Congo, na ujenzi wa barabara kutoka Uganda kwenda DRC ukafanyika.
Alikubaliana pia na Burundi,kupeleka jeshi lake Kivu kaskazini. Rwanda, haikupewa chance hiyo. Rwanda, ilikasirika. Na Raisi Kagame akasema, sijaalikwa nchini DRC, mi ntakwenda bila kualikwa. na aliposema tutaenda huko bila kualikwa, ndipo M23 ilipoanza mambo yake.
Hii kauli kwamba DRC haijawa na uungwana, ni uongo mtupu. Nakupa mfano: Kwenye uongozi wa Kabila, Rwanda iliruhusiwa kuingia nchini DRC kuitafuta FDLR.
Kuna kipindi ilifanyika oparesheni ijulikanayo kama umoja wetu. Watu wengi sana waliuliwa, wengine wakaimbia makazi yao. Mashirika ya kitaifa yalilalamika sana.
Mwaka 2019, raisi Tshisekedi, aliruhusu uongozi wa Rwanda kwenda DRC na kuuwa viongozi wa FDLR. Na waliwaua.
Hivi kweli, Rwanda inahitaji iruhusiwe mara ngapi kwenda Congo!

Zingatia: kuna kipindi, mkuu wa jeshi la Congo alikuwa mnyarwanda. Miaka! Walifanya nini? Leo hii eti wanataka kuingia Congo! Ngoja nikwambie kitu. FDLR ni kweli ipo. Na madai yake, yana mashiko. Kuwatakia uhuru kabila la watutsi, ni halali. Lakini, inakuwaje utafute amani ya kabila moja, makabila mengine uyaangamize?

Mwanahabari: Kwa haya yanayoendelea, unadhani ni nani anastahili kuwajibishwa matatizo haya yamayoleta mpaka vifo? Pia, umoja wa mataifa, umekuwa ukidai kwamba M23 inaungwa mkonono na serikali ya Rwanda. Je, kuna chochote unachoelewa kuhu hili?

KAYUMBA: Ahhhh, najua sana. Siyo kundi la kwanza tulilounga mkono. Ni kitu kilicho wazi. Hata sielewi kwa nini watu wanafichaficha. Unaona, Rwanda ndo iliweka kikomo kwenye utawala wa Mobutu. Mwaka 1996, tulipofuata wakimbizi na kuwarudisha kwao. Na hilo ndo lilikuwa lengo kubwa. Lakini, baada ya kukamilisha, tulitakiwa tubadili namna ya kuongoza nchi. Rwanda ilitakiwa kuongea na DRC kuhusu namna ya kuishi kwa amani na utulivu. Jambo la pili, ni upotoshaji. Kwamba M23 ni wanyamlenge. Issue ya Banyamulenge ilishaisha kitambo sana. Miaka ya 2002. Tena naweza kusema mwaka 1998, General James Kabarebe alipoondoka Kinshasa (Ndo alikuwa mkuu wa jeshi la DRC).
Kipindi cha utawala wa Kabila, Azarias Ruberwa, alikuwa makamu wa raisi. Ni mnyamulenge. Nyarugabo, alikuwa naibu spika, General Marick, arikuwa naibu kamanda wa jeshi, Bisengimana, ndo alikuwa mkuu wa Polisi. Ni wengi. Mpaka leo, kuna wanyamulenge wengi wenye vyeo kwenye ngazi za usalama. Na Generali Masunzu, hivi karibuni aliepewa kuwa mkuu wa jeshi wa kanda, ni mnyamulenge. HAta mawaziri, wapo wanyamurenge. Waziri wa miundombinu, ni mnyamulenge. Kwa hiyo, huku South Afrika, wakiongelea wanyamulenge, ni upotoshaji tu. Si kweli.
Issue ya wanyamulenge na M23, ni vitu viwili tofauti. Sema tu watu hawaelewi.


Itaendelea...................................................................................
weka source mkuu
 
Kayumba Nyamwasa anaweza kuwa na bifu na Kagame mimi nimemnukuu Kagame katika mahojiano na CNN sasa kunituhumu mimi kama mimi unakuwa hunitendei Haki.
👇

View: https://youtu.be/qW36WN7q7cc?si=4QXBEHwCz4ucThAT

sasa unanukuu nn mtu anasema hajui vikos vyake havipo??
Yaan anajua vyoote kasoro Vikosi vya jeshi lake?

Anajua mambo ya kongo
Anajua kuhusu watusi wanaonyanyaswa kongo
Anajua kuhusu waasi wa kongo
anajua kuhusu migogoro ya kongo

LAKINI HAJUI KAMA JESHI LAKE LIPO KULE😂😂😂we kama huelewi n chizi
 
Rasilimali za Congo DRC zinaibwa na mataifa mengi Rwanda akiwepo
SEHEMU ya I




"Inshu ya Banyamulenge, ni kisingizio tu! Ni kitu ambacho hakipo. Iliisha mwaka 2002". Anasema Nyamwasa.

Baada ya vifo vya wanajeshi wa Afrika kusini kufia vitani nchini DRC, mpaka sasa inaripotiwa wanajeshi 14 ndo waliopoteza maisha.

Hili jambo lilizuwa maswali mengi, wengine wakiituhumu serikali ya Afrika kusini, kuwataka wanajeshi hao wapigane na M23, huku wakiwa hawana mafunzo ya kutosha na vifaa vya kukabiliana na waasi wa M23.

News Room Afrika, chombo cha habari cha nchini Afrika kusini, kilimualika Kayumba Nyamwasa kuweza kuwajuza wasikilizaji mengi yanayohusiana na mgogoro huo.

Kayumba Nyamwasa, aliyekuwa mkuu wa majeshi nchini Rwanda, badae akawa Balozi wa Rwanda nchini India, ambaye kwa sasa anaishi nchini Afrika kusini,Kayumba pia aliwahi kuwa mkuu wa kitengo cha upelelezi chini Rwanda, kabla hajatofautiana na raisi Paul Kagame. Cheo chake ni Lutenanti General.

Akiulizwa na mwanahabari,kuhusu hali ya wakimbizi wa mwaka 1959 nchini Rwanda, iliyomsababishia(Kayumba) kuzaliwa nje ya nchi yake, aliulizwa, ni kipi anaona kinaweza kusaidia kuleta amani katika ukanda wa DRC,RWanda na Burundi.

Kayumba: Nadhani, njia sahihi na ya kipekee kufikia muafaka wa jambo hili la mashariki mwa DRC, ni mazungumzo tu. Lakini, si kwa Congo tu, pia kwa ukanda wote. Ukiangalia tatizo la Congo, ambapo Rwanda imekuwa ikishiriki huo mgogoro kwa zaidi ya miaka 30. Kuanzia mwaka 1996, Rwanda ilikuwa vitani nchini Congo.

Kwenye utawala wa Mobutu, utawala wa Desire Kabila, utawala wa Joseph Kabila, na sasa kwenye utawala wa Tshisekedi.

Tuliwahi pia kuwa na mahusiano mabaya sana na nchi ya Uganda: kuna vita baina ya Rwanda na Uganda huko Kisangani(Nchini DRC. Vinaweza kuongelewa hapo badae kama hiyo threat itakuwa na umhimu), kufungwa kwa mipaka, na mambo mengine kama hayo. Mahusiano yetu na Tanzania, pia kuna kipindi hayakuwa mazuri.

Mwaka 2013, Rais Kikwete na Rais Kagame walipotofautiana. Upande wa Burundi, kuanzia 2015, Rwanda na burundi hawaangaliani kwa jicho la amani. Kwa sasa hivi tunaongelea vita nchini Congo. Lakini pia,kuna uwezekano kukatokea jambo lolote pia huko Burundi. Hata jana, raisi wa Burundi, alitangaza kwamba amejiandaa vita na Rwanda.

Ngoja tuongelee watusti huko Congo kuhatalishiwa maisha. Hilo jambo ni kweli.

Watu huongelea mauaji ya kimbali nchini Rwanda, dhidi ya watutsi. Ni kweli yalitokea.

Lakini, kama unataka kutatua tatizo la ukanda, huwezi kukomboa watusti, kwa kuanzisha vita kwa watu wengine, kutafuta suruhu la watutsi, haimaanishi unatafuta suruhu la kuzuia genocide.

Tukiangalia DRC, tunaongelea watutsi zaidi ya laki 5, waliokimbilia Rwanda.

Je, ni mamilioni mangapi ya makabila mengine(Balega, Bahunde, Bahutu in Congo,Banande, hawa wote wamekuwa wakikimbia miaka yote hiyo 30.

Leo hii ukisema unaenda kuanzisha vita dhidi ya FDLR, hivi vita vinaenda kuwaondoa watu katika makazi yao. Kwangu, hilo siyo suruhisho.

Suruhisho ni kwamba, kwa serikali ya Congo, inatakiwa ikae meza ya mazungumzo na M23. Rwanda pia, inatakiwa iongee na wapinzani wake. Kwa sababu Rwanda inao wengi. Huu ukanda tu,iwe Afrika kusini, iwe Malawi, Zimbabwe,Mozambique wakimbizi karibia wote ni wanyarwanda. Lakini,serikali ya Rwanda, inalichukulia kama hakuna lolote lililotokea. Ongezea na wengine wote waliokimbia nchi, na kwenda ugaibuni. Ni kwamba wanahofia usalama wao. Sasa, kama hao ndo wanaoifadhili FDLR, kwa nini waifadhili?

Leo hii, hata ukiondoa tatizo la M23, wakimbizi wa Rwanda wataendelea kuwepo. Watakuwa kila kona.


Inaendelea................................................................
 
sasa unanukuu nn mtu anasema hajui vikos vyake havipo??
Yaan anajua vyoote kasoro Vikosi vya jeshi lake?

Anajua mambo ya kongo
Anajua kuhusu watusi wanaonyanyaswa kongo
Anajua kuhusu waasi wa kongo
anajua kuhusu migogoro ya kongo

LAKINI HAJUI KAMA JESHI LAKE LIPO KULE😂😂😂we kama huelewi n chizi
Akikujibu ni tag.
 
Back
Top Bottom