Kazi isiyoangaliana na mlango wa Jela haiwezi kukufanya kuwa Tajiri

Kazi isiyoangaliana na mlango wa Jela haiwezi kukufanya kuwa Tajiri

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Kwema Wakuu!

Ikiwa kazi unayoifanya haijawahi kukuletea Polisi, au haijawahi kukupeleka kwenye vyombo vya kisheria ujue hiyo kazi haiwezi kukufanya kuwa Tajiri.

Utajiri na uvunjifu wa sheria ni pande mbili za sarafu moja.
Huwezi kuwa tajiri bila kuivunja sheria ya nchi, mahali popote Katika hii dunia.

Kazi yoyote yenye hatari za kukamatwa na Polisi kazi hiyo ujue inauwezo wa kukufanya uwe tajiri.

Kadiri unavyozidi kupata pesa ndivyo unavyoukaribia Mdomo wa Jela, hivyo ndio maana ni lazima ufanye Kolabo na Wakubwa ili kuyavunja Meno ya Jela ili hata siku ukiingiamo ndani yake jela haiwezi kukusaga saga.

Hiyo ni kanuni ya Kidunia.

Kanuni ya Afrika, pesa unaweza ukapata pasipo hata kutumia Uchawi au uganga Ila Inategemea na kiwango cha Pesa.

Milioni 5 sijui 10M mpaka milioni 100M hizo unaweza ukazipata Kwa nguvu zako mwenyewe hata pasipo kujiingiza kwenye Uchawi. Wala hata serikali isiwe na time na wewe.

Lakini kuna pesa ili uishike na kuilinda basi itakupasa Ujiingize kwenye Uchawi na uganga huko.
Ngumu Sana na nadra Sana mtu amiliki milioni Mia tano tuu bila ndumba hiyo ni ngumu Sana.

Najua kuna watu watanibishia, lakini huo ndio ukweli.

Kisheria na kihaki hakuna Logic ya mtu kuwa Tajiri wa mabilioni ya pesa pasipo kuvunja sheria tena Kwa makusudi kabisa, hakuna kitu Kama hicho.

Taikon leo amecheka baada ya kukutana na Bilionea mmoja huku Kahama, bilionea huyu nilimuuliza ni Kwa nini yeye ni Tajiri akanijibu; "Kwa sababu siogopi kuvunja sheria" Nikabaki namkodolea macho tu!

Nipumzike sasa!

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Kahama
 
Msuva ana bilioni moja na kaipata hapa hapa Africa. Haya hilo wasemaje?

Siku ukiingia kwenye sekta ya michezo hasa mpira wa hapa bongo utajua ni Kwa kiwango gani Watanzania ni washirikina..

Nilikuwa pale Morogoro, vitiku tuu vya mchangani, kwenye kombe la Mbuzi au kushidania milioni moja, huwezi amini timu zinaenda Kwa Waganga wa kienyeji.

Wadau wa mpira watakuja kukueleza,
 
Kwema Wakuu!

Ikiwa kazi unayoifanya haijawahi kukuletea Polisi, au haijawahi kukupeleka kwenye vyombo vya kisheria ujue hiyo kazi haiwezi kukufanya kuwa Tajiri
Wanasiasa ndio watu wanaomiliki Mali nyingi zizizo halali.

Kwa mfano Kama kwetu Kenya Kuna mwanasiasa mmoja maarufu ambaye utajiri wake unasemekana kuwa bilioni 35 za kikenya.

Aisee huyu mwamba ni mkatili Sana maana Ana skendo nyingi Sana za wizi wa Mali za serikali na kunyang'anya wanyonge mashamba yao.

Nikitaja skendo za huyo jamaa mnaweza mkashangaa Sana ila acha niishie Hapa tu Ila inauma Sana Yaani😥
 
Wanasiasa ndio watu wanaomiliki Mali nyingi zizizo halali.
Kea mfano Kama kwetu Kenya Kuna mwanasiasa mmoja maarufu ambaye utajiri wake unasemekana kuwa bilioni 35 za kikenya.Aisee huyu mwamba Ni mkatili Sana maana Ana skendo nyingi Sana za wizi wa Mali za serikali na kunyang'anya wanyonge mashamba yao.

Nikitaja skendo za huyo jamaa mnaweza mkashangaa Sana ila acha niishie Hapa tu Ila inauma Sana Yaani😥


😀😀😀

Ishia hapo hapo tuu mkuu
 
Back
Top Bottom