Piga shoka,piga jembe, kata mizizi, chimba kwa hatua wapi[emoji23][emoji23] nimependa usimuliaji wako
Daah si mchezo jamaa, [emoji23][emoji23]Jamaa ni story teller mzuri sana. Explaining real life experience in form of storytelling, sio kila mtu ana huu ujuzi.
Naam kuna job unakua unapiga unaona kabisa hapa sio mahara pangu hii safari bado sana, ila kuna stage ukifika unasema hapa ndio penyewe[emoji12]
Mashamba yapo mkuu@fdizzle naweza kupata shamba kule hata ekari 1 nilime ndizi na machungwa maana kupo POA Sana kichani kibichi Cha kutosha
[emoji23][emoji23][emoji23]Maeneo yenu ya Morogoro hayana mwisho, unaweza ukasafiri kwa elfu 40 ndani ya wilaya moja
Ilitakiwa kumwaga diesel sio yataa.Kuna siku nipo maskani nishachoka zanguu,akaja jamaa akasema anaeweza kuchezea mavi twende kuna kazi huko,,
Nikamuuliza kazi gani? akasema mwenye nyumba anataka chemba ya choo tuchote mavi yote na ndooo tukamwage kwenye shamba lake ili ile chemba iongezwe urefu yani pale ilipo ifukuliwe zaidi kwenda chini..
ila huwezi kufukua zaidi bila kutoa kinyesi chote, tukamwambia si aite tu gari ya kunyonya mavi inyonye, Akasema njia ya kufika kwake gari ya mavi haifiki na hata wakifosi gharama ni kubwa mno inafika 1m na huyo mzee hiyo hela hana..
hivyo mzee katoa ofa ya watu kuchota mzgo wote na ndoo na kwenda kuumwaga huko shambani kwake, Tukauliza OFA yake sh ngapi?
Jamaa akasema kazi tunaifanya watu wa 4 tu mzee kasema atatoa 100,000 kwa kila mtu,jamaa mmoja akasema mwambie aongeze walau iwe 150,000 tukapge kazi, nazama chumvini nalamba inye live na ulimi sembuse hiyo harufu inishinde? mwambie aongeze dau...
Jamaa akavuta simu kwa mshua akamwambia vijana wa kazi wamepatikana ila wanasema 100k haitoshi waongeze 50k iwe 150k, mzee akajibu Sawa njooni.
Jamaa akasema oyaa mshua kakubali, Huyo mwingine akawambia sasa sikilizeni hapa tunaenda nunua mafuta ya Taaa kidumu cha lita 5 tunamwaga mwaga mule kwenye chemba mote Harufu inakata kazi tunapga freshi..
Kusikia hivyo tukaona jamaa katoa idea nzuri sana,kweli haooo hadi kwa mangi tukanunua mafuta ya taaa haooo safari ikaanza kwenda site.
Tumefika tukaenda kwenye chemba, ilikua tayari ishabomolewa lile zege la juu hivyo limebaki shimo pana tu unaona inye live live,mafinyo finyo live live, Jamaa akamwaga mafuta ya taaa pwaaaaaa koteee..
Tukaletewa ndooo kila mtu na ndoo yake,gloves kazi ikaanza nikadumbukiza nikachota ndoo ya kwanza nikatoa,jamani jamani jamani nilienda kumwaga shambani nikapitiliza huko huko sikurudi nyuma tena.
Asee inye isikieni tu,ile 150,000 nikaona wala isinipe presha mimi,na niikose tu siwezzi chezea gwede gwede kama vile ni rost... nimeondoka nimefika maskani nasimulia waliobaki,nusu saa haijaisha namuona mwenzangu mwingine huyu hapa karudi, aaah weee kuna kazi za kufanya bwana sio kazi ya kuchezea tope la binadamu..
Nahizi shuhuda ni kama church tu, sema hapa zinakuja kwa njia ya vichekesho flani hv na burudani. Mungu aendelee kitupigania hakuna kuta tamaa.Haijalishi unapitia changamoto gani katika maisha
Haijalishi unapitia magumu gani katika maisha yako
yawezekana umechoka,unahisi kama unateseka peke ako
si kweli', ukipitia huu uzi utagundua wote wanayoyasimulia haya
sifa yao kuu ni 1 "uvumilivu" na "kutokukata tamaa",usikatishwe tamaa
na mapito unayoyapitia kwa wakati huu,wenzako walishayapitia na sasa
imebaki kama simulizi za kuchekesha,lakini nakwambia hivi sio vichekesho
wakati watu wakiyapitia haya walikua wakilia machozi,wakivuja jasho,mioyo yao
ilikufa ikasinyaa,nk lakini leo hii zimegeuka kama "SHUHUDA" tunacheka tunafurahia
Chochote unachopitia sasa,Hali ngumu yoyote unayoiona mbele yako sasa amini
nakwambia ni "linapita" hutoteseka milele,hutoonewa milele,hutolia milele,hutohuzunika
milele,kesho yako itakua kicheko na simulizi na shuhuda kwa wengine,Kwa sasa
piga moyo Konde songa zako mbele Mkombozi wa kesho yako ni wewe mwenyewe,Usichoke kupambana,Mungu yupo anakuona.
And lets all say Amen!
Ameeen.......
We ni kijana wa mzee Mrina? hahaaaa eti shallow...wako.Nimeosha vyombo ila hapa hapa bongo na haikunishinda,ni 1 ya kazi ambazo kupitia hiyo kazi mafanikio yangu mzizi wake ni hiyo kazi.
Ni kazi yangu ya kwanza iliyonifundisha mengi sana maana hapo kazini kulikua na jiko hivyo nimejua vitu vingi sana kupitia hapo,ila nilikaribishwa kama "muosha vyombo" tena wakati napewa kazi boss aliniuliza "unaweza sugua masufuria yale makubwa" akanipointia yale masufuria ya sherehe,yakang'aaa kama mapya?
nikamwambia shaka ondoa naomba kazi boss,akasema pita karoni Anza kazi nikuone,Nilisugua sufuria aliporudi akauliza,nani kanisaidia kuzisugua,wafanyakazi wakamwambia "huyo sharo wako hapo" kasugua,Nikaajiriwa rasmi kama muosha vyombo.
Kazi niliiipenda nilijivunia mnooo,japo wakati naianza niliianza kwa ugumu na shida sana,si rahisi kama ninavyoandika na kusmulia hapa.
Ki ufupi upambanaji ule wenyewe wenyewe niliuanza kwenye kibarua hicho,Godoro langu la kwanza,kodi yangu ya cghumba cha kwanza DAR nilipata hela kupitia kazi hiyo.
MOSHI HOTEL/MANZESE-TIP TOP
Daaaah mkuu mwaga stori mwaga stori jinsi maboya yanavyopigikaUganga ndio kazi pekee ambayo unaweza kulipwa bila mteja kuona matokeo,
mtaji wake ni maneno mengi na lugha zisizoelewa, ilizi zakufumafuma tu na ndani unaweka chochote kile hata mavi ya kuku, kaniki nyeusi na nyekundu, sanda kadhaa, vibuyu kadhaa kamba na kibuyu kimoja unakipa jina almaarufu kibuna.
mkwara siku ya kwanza target mmeshampimia akija mganga hafanyi kazi leo amepandisha majini makali hata kuona mtu kabisa, hapo unajifanya unakunywa damu ya paka na maiti ya paka mweusi iko pembeni, umazungusha kama wiki hivi, siku akija anakukuta mtulivu mpole unasikiliza shida zake zoote, halafu unashitaki kwa mzimu kibuna hapo bob chura kashafanya spying ya kutosha tushatumia na hela kadhaa dah mwamba kibuna anatema cheche balaa, target hapo anapigwa hela ys mahitaji afanyiwe kazi yake ikiwepo kucha za maiti wa siku 7 kidole cha mwisho, kipande cha mkia wa fisi, nk hapo mnakula kama 500K next move sasa alizima achojoke kadhaa at the end anakuwa chuma ulete.......hahahaha
mitaaa yetu ya kujidai watoto wa kwa sheikh Pazi na mfuga mbwa....kitambo sana.Pamoja mkuu.Mrina alikua jirani tu mkuu
sweet manka nimefurahi ila wakati nasoma nimekubali wewe ni mpambanaji uko na hustles za maana...abeba trip zote ile ya mwisho akajikuta kaingia period ghafla.Kilichomfanya abebe aongezee hela akalipe kibati.
Tena akiwa hai bila kufa kwanzaMzee umenichekesha kweli,ulikua unahisi kama unawafata malaika huko huko walipo sio
Kama mimi vile, kila mtu ananiona kama akili zinataka kunirukaNacheka hapa naonekana kichaa [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Nilirudi nyumban bega na mkono umechubuka achaga tu hii kazi sio rahisi afu nlikua na homa pindi naenda ila kurudi homa yenyewe ikapotelea kusikojulikanaKubeba zege
Jamaaa we ni fala aisee ko mwana dege dege ukamtafuta alipo alooo nimecheka sana aiseee mwamba umepitia mengi lakin inaonesha hupendi shida aisee mana kila ikifikia pagumu unapotea aiseeeMimi nishawahi kutwa na msala wa gerezani wa kazi flani Ngumu sana kuifanya,nikaona huu ushenzi
hiii kazi nisipoangalia ntaja fia hapa hapa,nikaangalia huku na kule kisha nikajidondosha chini puuuu
nikaanza kurusha miguuu kama nina dege dege,huku natoa mapovu( hapo nishakusanya mate kibaooo)
nikawa nayatema kwa pembeni kidogo kidogo,nikaskia wana wanasema Oyaa huyu atakua ana dege dege
askari akaitwa akaja akasema mbebeni muwekeni pale kivulini,nilipopelekwa kivulini nikasema hapa nikitulia
tuu ntalishwa rungu kwa sana watanishtukia, basi nikazidisha drama nikajirusha kama jongooo nakwambia
askari akaona huu msala atatufia huyu,nikabebwa ikaitwa TAX dakwa speed hadi gerezani,kufika gerezani nikajifanya
napumua haaaaaa huku nakoromaa,ndio ikawa pona yangu ila bila ile tekniki Ningefia pale walahi vile...