Kazi nilizowahi zifanya na zikanishinda kwenye utafutaji

Daah hii ishu ya degedege kuna mwana ilimkuta wakati tunasubiri mchina atufikirie kiwandani kwake maeneo ya sokota kiwanda cha rangi, Jamaa mzima mzima akadondoka miguuni mwangu mara anavibrate uku anatoa mapovu mdomoni wee nilitaka kimbia sema kuna mshkaji wangu akanidaka nisikimbie then akamuwahi mwana kwenye mdomo Sijui Ili asijing'ate akawaambia na wengine wamshike miguu hali ya jamaa ilivyokaa sawa sikutaka kubaki apo kama kazi yenyew nkasema basi...
 
Hicho kifafa
 

[emoji23][emoji23]
 
Niliuza machungwa mitaa ya Tanga mjini, siku wife kanikuta mtaani Hadi ananionea huruma, nimepauka hatarii, mimi mweusi ila nimekuwa kama chungu kwa jua, yaani wie acha TU, hadi machozi yalimtoka

Ulikuwa unauzaje hadi unachafuka hivyo
Anakupenda mkeo jamani natumain mpo nae hadi sasa
 

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] hambebi oksijen?
 
Kwenye ulinzi,sikia tuu niwepeleka mtumiwa kituoni nikageuziwa kesi nambiwa kabizi vitu hapa ingia ndani na wewe itakuwa mmeshindana masirahi na mtuhumiwa,ikabidi mwizi anitete lakini wapi,utulivu akajaimaliza mkuu wa kituo,jambo limeaza saa Tisa usiku nimekuja kuachiwa kumepambazuka Tena nambiwa kaoge uje tukutane mahakamani maana ni ulikuwa mradi wa serikali,nikazima na simu nikabeba na begi langu ikawa chanzo Cha kuhama mkoa,sijui ilikuwaje nyuma huku Kama walimuachia au walimfunga,ilaa tusikakate tamaa kiukweli.

Sent from my TECNO KB8 using JamiiForums mobile app
 
Polisi wa Tanzania ni vituko vitupu. Wanakuuzia kesi mchana kweupe!
 
Mi nikikugundua lazima ni kurefi...
Babakeee
 
kuna miti unachimba kisiki,inafika muda unaacha kuchimba unabonyeza ule mti ni Mti au Jiwe

maana kila unavyoonyesha juhudi kisiki kimekaa tu kinakuangalia yani kama unakitekenya hiviii
Hii imenikumbusha jamaa alipewa tenda ya kung'oa mbuyu, naye vilevile alipouliza bei akaambiwa unataka upewe ngapi akasema nipeni elfu 80 tena aliamua aanzie bei ya juu ili wakishusha waangukie kwenye damu lake la elfu 60.. Bahati yake nzuri wakamwambia watampa hiyo 80 ila ndani ya siku 3 mbuyu uwe chini maana kuna ujenzi unataka kuanza. Jamaa anakuambia alichimba, alichoma moto huo mbuyu lakini mpaka siku ya 5 hata robo ya kazi badoo [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
 
Mmmh 2023 hii,kuna kazi nimeiangalia tu kwa macho na kuuliza mawili matatu,nmewaambia ngoja nikachukue sururu hapa nipo mbezi natmbea kwa miguu kurudi kibaha.Kuna kazi na adhabu,hii ni zaidi ya adhabu,ukimaliza salama hela yote inaenda kuishia kwa daktrari wa masikio, Kinywa na koo.
 
[emoji28][emoji28][emoji28] kwa hyo umekimbia kazii??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…