Kazi ya kwanza ya Wizara mpya ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari iwe ni kuruhusu Watanzania kupokea malipo kupitia Paypal

Kazi ya kwanza ya Wizara mpya ya Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari iwe ni kuruhusu Watanzania kupokea malipo kupitia Paypal

YEHODAYA

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
36,902
Reaction score
52,001
Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ambayo ni mpya tunatarrajia ifanye mambo makubwa ya kuongeza ajira kwa vijana mitandaoni.

Tanzania kumekuwa na tatizo kubwa la ajira. Njia moja ya kuondoa hilo tatizo ni kwa watu kutafuta kazi za kufanya online, yaani mitandaoni. Kazi zipo nyingi. Mfano, waweza pata kazi ya kutafsiri website ya kampuni au mtu kwa Kiswahili au kutafsiri kitabu. Unafanya online malipo yanakuwa kwa njia ya PayPal hela inaingia hata kwenye simu yako ya mkononi, hata mwajiri au mnunuzi awe Ulaya au Marekani au popote duniani.

Waandishi wa vitabu waweza andika vitabu na kuviuza online na watunmzi wa nyimbo bk waweza kulipwa online kwa njia ya paypal chap chap mtu aki click tu na kudownload kitabu au wimbo nk malipo muda huo huo yanaingia.

Pia, mtu waweza chora hata katuni, ramani za nyumba n.k ukauza online. Au, ukajitungia wimbo wako wa kienyeji binafsi nyumbani kwako bila hata kwenda studio, ukauweka kwa mfumo wa video au audio ukauuza online kwenye maduka kibao ya online.

Tatizo kwa Tanzania haijaruhusu matumizi ya kupokea pesa kwa njia ya PayPal ambapo mtu aki-click tu kununua bidhaa yako, pesa yako inaingia chapchap kwenye PayPal account yako.

Kenya walisharuhusu; vijana wengi hushinda mitandaoni wakitengeneza pesa wakiuza bidhaa zao, viwe vichekesho, michezo ya kuigiza n.k ambavyo huviuza online. Wanaweka clip zao kwenye maduka ya online mtu ananunua anamlipa online kupitia Paypal.

Kuna shughuli nyingi za ujasiliamali online. Kikwazo kwa nchi yetu ni upataji wa pesa wa kazi yako au mauzo yako online. Bado tuko enzi za mawe tukiamini minjia ya kizamani ya kupokea hela. Na hivyo kuifanya nchi yetu kuwa ni ya kulipa zaidi pesa za kigeni na si ya kupokea pesa za kigeni.

Serikali ikiruhusu upokeaji pesa kupitia PayPal itafanya vijana wengi waingie mitandaoni kutafuta pesa.

Biashara za online zaweza kufungua Watanzania wengi kupata pesa toka nje, sababu ni juhudi ya mtu binafs na ubunifu wake i tu auze nini. Waweza kujirekodi unarukaruka kama ngedere ukiimba hovyohovyo tu bila hata vyombo halafu ukaita wimbo Crazy Monkey Song ukauweka online na ukauza. Wapo watu wana pesa wanapenda vituko wananunua.

Taasisi za elimu nazo ziweke kwenye mitaala ujasiliamali wa online wasibakie tu kufundisha ujasiriamali wa kuzurura tu juani wa kimachinga.
 
Hiyo wizara ni bosheni tu kama mpaka sasa wameshindwa kurudisha kasi ya internet kama zamani na bila vpn hauingii baadhi ya mitandao ya kijamii kazi wizi wa kura tu ndio fisiemu wanaweza ila sio kukimbizana na kasi ya Dunia kiteknolojia
 

YEHODAYA

Hongera Sana umetoa ushauri mzuri wenye uzito wa hali ya juu,Kazi mtandaoni ziko nyingi sana na malipo haya kutumia paypal ni makubwa sana kwa takwimu za kimataifa Paypal kwenye robo tatu ya mwaka huu imefanyika miamala bilioni 3.74 yenye Thamani ya dola za marekani bilioni 246.Na mwaka jana 2019 imefanyika miamala yenye Thamani ya dola za marekani bilioni 712 DUNIANI.Sasa kama sasa Serikali inaruhusu malipo hayo itakuwa jambo jema sana.Vijana wengi waliomaliza vyuoo vikuu wataweza kufanya kazi nyingi.Kenya vijana wanalipwa mpaka dola 350 kila mwezi wengi sana kupitia Paypal.
Nadhani serikali italingalia hilo.Na pia hilo tunalizungumzia kwenye miamala ya simu kwa paypal ila Kwenye mabenk nadhani hilo lipo sasa.

LUMUMBA
 
Paypal ni nzuri sana na ita boost sana our economy. Lakini hicho ndo kitakuwa kifo cha mpesa,tigopesa etc. Paypal gharama ya kutoa pesa ni kama bure...wakati mpesa ukitoa 10000 wanakata 1300...zaidi ya 13%.
Serikali ndo chanzo cha makato ya miamala kuwa kubwa.
Serikali haiwezi kukubali kupoteza hii pesa.
 
Paypal ni nzuri sana na ita boost sana our economy. Lakini hicho ndo kitakuwa kifo cha mpesa,tigopesa etc. Paypal gharama ya kutoa pesa ni kama bure...wakati mpesa ukitoa 10000 wanakata 1300...zaidi ya 13%.
Serikali ndo chanzo cha makato ya miamala kuwa kubwa.
Serikali haiwezi kukubali kupoteza hii pesa.
Pesa zitatua kwenye namba za simu za Tigopesa,Mpesa nk kutoa wataendelea kuchaji kama kawaida tu Hakuna watakachopoteza wenye kampuni za Mpesa,Tigo pesa nk sana sana idadi ya miamala itaongezeka na faida kwao itaongezeka na TRA wataongeza mapato sababu kila ukitoa pesa TRA nao chao hupata kwenye huo muamala
 
Kimsingi ICT bado kuna fursa nyingi ambavyo hazijavunwa
Ni kweli fursa ziko nyingi mno mfano waweza tengeneza hata tangazo la biashara la kampuni yeyote duniani au nembo au chochote bila kuombwa ukawarushia online wakilipenda wakalichukua ukalipwa chako

angalia mfano huyu dada Anayesikika kwenye simu anayesema mteja unayempigia hapatikani kwa sasa

 
Miezi ya hapo nyuma nilifanya kazi fulan nikiwa na imani hela itaingia moja kwa moja, nilifikisha kias cha $123 sasa kwenye kuichukua c wakadai vya PayPal nami nilijua inafanya kaz hapa bongo(uelewa mdogo) kumbe wapi, mpk saiz hiyo hela naiangalia tu kwenye akaunt niliyojiungaga🙄🙄🙄. Ila umetoa ushauri mzur sanaaa, serikali ikiufanyia kazi nina uhakika lile wimbi la cc kulalamika kuhusu ajira litapungua😇
Naomba waufanyie kazi huu ushauri huenda nami nikaja kuitoa ile $123😂😂😂
 
Naomba kuuliza swali la ufahamu....je huduma pekee ya kupokea pesa toka nje ni paypal?!...hakuna huduma zingine kama moneygram, huduma za visa na mastercard?!
 
Kuna haja ya kubadilika,ulimwengu ulishabadilika siku nyingi sana...
fursa nyingi za kibiashara zipo na zinafanyika kwenye cyber space.....
TRA wajiongeze tu wanawezaje kupata kodi yao huko......
manake unaweza ukapiga mahela mengi huko...
siku unayaingiza Tz ukaambiwa Money Laundering.....kwa kuwa tu hizo biashara hawazitambui na hukulipa kodi
 
Naomba kuuliza swali la ufahamu....je huduma pekee ya kupokea pesa toka nje ni paypal?!...hakuna huduma zingine kama moneygram, huduma za visa na mastercard?!
Visa na mastercard ni za kulipia tu sio kupokelea hela na moneytram sio njia ya kufanya malipo au kupokelea malipo online.Moneygram ni njia tu ya kupokea pesa kama ilivyo western union tu

Watanzania wengi sana wana Visa na Mastercard lakini hizo kazi zake kulipia tu huduma au bidhaa online hazipokei pesa!!!

Paypal ni njia ya kufanya malipo na kupokea malipo online
 
Kuna haja ya kubadilika,ulimwengu ulishabadilika siku nyingi sana...
fursa nyingi za kibiashara zipo na zinafanyika kwenye cyber space.....
TRA wajiongeze tu wanawezaje kupata kodi yao huko......
manake unaweza ukapiga mahela mengi huko...
siku unayaingiza Tz ukaambiwa Money Laundering.....kwa kuwa tu hizo biashara hawazitambui na hukulipa kodi
TRA hawana cha kupoteza sababu kutoa miamala kawaida kila ukitoa muamala uwe benki au kwenye simu yako TRA wanapata chao
 
Hiyo wizara ni bosheni tu kama mpaka sasa wameshindwa kurudisha kasi ya internet kama zamani na bila vpn hauingii baadhi ya mitandao ya kijamii kazi wizi wa kura tu ndio fisiemu wanaweza ila sio kukimbizana na kasi ya Dunia kiteknolojia
Tumechoka na habari za kuibiwa kura kilichotokea ni kwamba mlidhibitiwa na upuuzi wote wa kutaka kuharibu uchaguzi,, poleni sana,,, hivi kama mliibiwa mbona hamuendi huko ICC na kwa baba zenu mabeberu kama mnao ushahidi?? Jeshi na polisi walikuwa kwa ukaribu ili kuhakikisha hao wavuta bangi wa kusubiri au kulinda kura mita 200 wasijaribu,,, ulisikia wapi duniani ati kulinda kura sii bangi hizo LETENI VIDHIBITI msiwe kama Trump,,,
 
Tumechoka na habari za kuibiwa kura kilichotokea ni kwamba mlidhibitiwa na upuuzi wote wa kutaka kuharibu uchaguzi,, poleni sana,,, hivi kama mliibiwa mbona hamuendi huko ICC na kwa baba zenu mabeberu kama mnao ushahidi?? Jeshi na polisi walikuwa kwa ukaribu ili kuhakikisha hao wavuta bangi wa kusubiri au kulinda kura mita 200 wasijaribu,,, ulisikia wapi duniani ati kulinda kura sii bangi hizo LETENI VIDHIBITI msiwe kama Trump,,,
Screenshot_20201207-151011.png
 
Back
Top Bottom