DOKEZO KCMC sitorudi nikiwa na akili timamu

DOKEZO KCMC sitorudi nikiwa na akili timamu

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Kesi yako inanikumbusha mama Anna Nghwira ambaye alikuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, ambaye alifariki dunia mwaka jana.

Huyo mama alikuwa ana bifu kubwa na zito (binafsi?)na hospitali ya KCMC, mara zote alikuwa akiwasema vibaya tu, lakini tunaambiwa kuwa huyo mama alikuwa akiumwa ghafla, wasaidizi wake watamuwahisha hapo hapo KCMC kutibiwa na anapona, lakini shukrani hatoi zaidi ya kuropoka shombo na kuwakejeli.

Sasa mziki ukatokea baada ya kutumbuliwa ukuu wa mkoa wa Kilimanjaro, halafu mwezi huo huo kuna mama fulani ambaye ni rafiki/ndugu yake alifikishwa hapo KCMC mbio mbio ikisemekana akiwa ameshafariki dunia lakini ndugu wakidai alikuwa bado yupo hai ila KCMC ikazembea. Sasa ghafla hiyo issue ikamuibua te mama Nghwira na kuja kulalamika kuwa ndugu/rafiki yake amepoteza maisha kwa sababu ya uzembe wa KCMC!

Haukupita muda mrefu sana mama Nghwira akaugua akiwa Arusha na kulazwa Mount Meru Hospital, watu wa karibu wanasema hali yake ilipaswa kulazwa KCMC lakini kwa sababu ya mtazamo wako kuhusu KCMC mama akaachwa hapo hapo Mount Meru Hospital mpaka akafariki dunia.

Funzo ni nini?
Matatizo ya hospitali za umma za Tanzania tunayafahamu, mengi yanafanana, sio busara sana kujiapiza kuwa hutataka kutibiwa huko wakati hatuna option bora zaidi.
Acha watu waongee ukweli, utumbo wao inabidi usemwe tuu na next time please hakikisheni mna document mpaka majina yao, vyeo , utumbo uliofanyika, muda etc hii itatusaidia sisi wamiliki kuchukua hatua zinazostahili kuweka mambo sawa, tunawalipa hawa hawafanyi kazi bure na nyie mnalipia huduma mnatakiwa kuzipata bila usumbufu au kona kona za wapuuzi wachache tuliowaajiri, msikae kimya na uliyeleta huu uzi asante sana
 
Pole sana. Mm pia nashangaa kwa nini waninyime majibu ya vipimo vyangu? Nilienda kupiga x-ray hospital ya Dar Group. Jambo la ajabu walikataa kunipa picha yangu ya x-ray ingawa nililipa huduma hiyo
Walikupiga boss na hawakukufanyia x-ray, wahuni watupu wamejaa kwenye afya, hakuna sehemu yenye afadhari kila kona ni upigaji tuu
 
Hapo KCMC nilienda kumwona mgonjwa saa za kuona wagonjwa,nipofika ward husika nikaulizwa umekuja kumwona mgonjwa gani?nikasema mgonjwa X,nikaambiwa huyu kuna mtu ameshakuja kumwona,huwa tuna ruhusu mtu mmoja tu kumwona mgonjwa aisee niliduwaa sana pale na mimi nilifunga safari toka wilaya nyingine!kifupi nilikwazika sana na siitamani hiyo hospital.
 
KCMC imebaki jina tu, hospitali hii pendwa kwa miongo kadhaa sasa nakiri mbele ya umma, labda nipelekwe sijitambui ila kwa huduma nilizopata na kushuhudia kwa wateja wengne, hakika huu ndio mwisho wangu kutia miguu hospitali hii.

1. Customer care mbovu, hawajali wagonjwa /wateja.
Madaktari wengne wanafoka bila sababu za msingi, wewe daktari uliyenifokea kisa nimekaa kwenye kiti tofsuti na ulichotaka pasipo kufaham nimekusamehe bure.

2. Kujuana kwingi, mtu amekuja saa 1 asubuhi anapewa namba 70 mwingne anakuja saa 6 anapewa namba 40, yaani wewe unapita mizunguko ya kutosha ila wengne wanakuja na kupata huduma ukishangaa kwenye bench.

3. Wahudumu/ madaktari wengi nlowaona ni vijana wadogo wadogo tu, hawako serious wanapiga stori za kubeti na kombe la dunia tu[emoji848]

4. Vipimo vya mchongo, baada ya kumwona daktari anakushauri kuchukua kipimo kingne kwa daktari mwingne anakutajia na pesa umpe, la ajabu zile pesa zinachukuliwa kwa siri na risiti hakuna.

5. No privacy, inakuaje hospitali kubwa kama hii wagonjwa mnasikilizwa kwa pamoja km mko darasani?

6. Mgonjwa anaumwa macho anaambiwa aende arudi siku nyingne muda umekwisha akati ameshinda hospitali tangu asubuhi, eti akameze paracetamol km ana maumivu.
Wewe dada uliyekuwa chumba cha miwani tareh 25-11-2022 saa 11 jioni Mungu akusamehe hukustahili kuwa muhudumu wa afya kabisa.

7. Huduma moja nimetajiwa bei mbili tofauti na wahudumu wawili tofauti tena chumba hicho hicho, tofautivya elfu 30, is it possible?

8. Hospitali ya rufaa haina lens ya miwani kweli hadi waagize tena nisubiri miezi miwili[emoji848]

9. Mgonjwa unatibiwa hupewi maelezo ya tatizo lako kwa ufasaha na hupewi document yoyote kuhusu majibu ya vipimo, taarifa zinabaki kwenye computer zao, huu ni uungwana?

10. Mapokezi naulizwa dini yangu ili nini? Kwamba huduma za afya zinachagua dini???

NB. Nimeandika kwa ufupi tu ila hayo ni baadhi ya mambo yaliyonisibu KCMC na kunifanya niamue rasmi kuipa kisogo hii hospitali.

Sina ubaya na mtu yeyote anayehusika na hospitali hii na wala simfahamu yeyote ila nawasihi watumishi tuheshimu mahali pa kazi.
Nenda CCBRT wakayamalizie macho yako, mwaka 2016 nilikwenda CCBRT nikapima macho na nikalipa shs.50,000/= nikaambiwa nirudi siku ya pili, niliporudi siku ya pili nikaambiwa siku yangu ilikuwa jana siyo leo hivyo natakiwa nilipe tena ili nitibiwe! Nilipochachamaa wakanipa vijidawa na kuniagiza watanitibu bure! siku inayofuata, nikaachana nao nikafunga safari toka Dar nikaenda KCMC nilifika jioni nikalala kwenye gesti iliyo nje ya hospitali. Asubuhi nikaingia hospitali kwenye saa saba nikapimwa nikapewa kitanda japo sikulala asubuhi nikaingia, mchana nikafanyiwa upasuaji nikalala wodini, siku iliyofuata asubuhi wakaiondoa plasta na kuniruhusu, jicho lilikuwa jipya zaidi ya la kijana na siku iliyofuata nikarudi Dar, kwa kifupi CCBRT siitaki kwani kuna malalamiko ya wengi kuharibikiwa macho kabisa. Mwaka jana 2021 nilikwenda tena KCMC kwa ajili ya jicho jingine na nilikaa kwa siku zilezile nne kama mwanzo, sikuona wala kusikia malalamiko kama yako, japo kuna watu wanataka wapimwe na kufanyiwa upasuaji siku hiyohiyo! Huenda nawe ni mmoja wapo, pole kwa mkasa.
 
Halafu inaendeshwa na shirika la dini, hizi imani za Kizungu zilizokuja kwa meli.
 
Hii hiko Hosp nyingi kwa sasa
AICC unapajua,, hata pale ipo..

Ukienda na bima ndio utabaki na ile karatasi 1
Ukiwa wa cash, utapata tu risiti za bills
Ila ukiomba printout unapewa
 
No offence, Taasisi zilizo chini ya KKKT zina changamoto nyingi sana kwenye kutoa huduma.
Kcmc Hopsital, Kcmc University, Tumaini University kuna ufisadi sana.
hydom pia wako hoi,wachungaji na maaskofu wanajaza mifuko
 
Sasa mkuu alikuwa anaumwa kweli huyo wife au alikuwa anakuzuga? Wakati mwingine msiwe mnaendeshwa na wake zenu.

Mtu kaugua ghafla tena tatizo linaloonekana kuwa ni kubwa saa nane usiku. Then akaishia kunywa mchai chai na halijarudia tena. Na bado unataka kulaum Hospitali haikukupa huduma uliyoyarajiwa?
ndo maana walichukua vipimo daktari anaju njia bora ya kutuliza tatizo,au mtu atundikiwe drip ndo uridhike?
 
Pale Bugando nilipewa huduma nzuri sana ya upasuaji 2020 . Nikamwambia jamaa yangu kumbe watu wa Mwanza mpo motivated sana na hii hospitali.

Jamaa akaniambia ,aliyebadili mfumo wa hii Hosp ni JPM . Hapa kulikuwa na harufu za kujuana na rushwa.

Daah! Nashukuru MUNGU sikupitia kipindi kigumu
mpaka sasa kwangu ni the best wanajitahidi hata kama kuna changamoto lakini wanajitahidi
 
KCMC imebaki jina tu, hospitali hii pendwa kwa miongo kadhaa sasa nakiri mbele ya umma, labda nipelekwe sijitambui ila kwa huduma nilizopata na kushuhudia kwa wateja wengne, hakika huu ndio mwisho wangu kutia miguu hospitali hii.

1. Customer care mbovu, hawajali wagonjwa /wateja.
Madaktari wengne wanafoka bila sababu za msingi, wewe daktari uliyenifokea kisa nimekaa kwenye kiti tofsuti na ulichotaka pasipo kufaham nimekusamehe bure.

2. Kujuana kwingi, mtu amekuja saa 1 asubuhi anapewa namba 70 mwingne anakuja saa 6 anapewa namba 40, yaani wewe unapita mizunguko ya kutosha ila wengne wanakuja na kupata huduma ukishangaa kwenye bench.

3. Wahudumu/ madaktari wengi nlowaona ni vijana wadogo wadogo tu, hawako serious wanapiga stori za kubeti na kombe la dunia tu[emoji848]

4. Vipimo vya mchongo, baada ya kumwona daktari anakushauri kuchukua kipimo kingne kwa daktari mwingne anakutajia na pesa umpe, la ajabu zile pesa zinachukuliwa kwa siri na risiti hakuna.

5. No privacy, inakuaje hospitali kubwa kama hii wagonjwa mnasikilizwa kwa pamoja km mko darasani?

6. Mgonjwa anaumwa macho anaambiwa aende arudi siku nyingne muda umekwisha akati ameshinda hospitali tangu asubuhi, eti akameze paracetamol km ana maumivu.
Wewe dada uliyekuwa chumba cha miwani tareh 25-11-2022 saa 11 jioni Mungu akusamehe hukustahili kuwa muhudumu wa afya kabisa.

7. Huduma moja nimetajiwa bei mbili tofauti na wahudumu wawili tofauti tena chumba hicho hicho, tofautivya elfu 30, is it possible?

8. Hospitali ya rufaa haina lens ya miwani kweli hadi waagize tena nisubiri miezi miwili[emoji848]

9. Mgonjwa unatibiwa hupewi maelezo ya tatizo lako kwa ufasaha na hupewi document yoyote kuhusu majibu ya vipimo, taarifa zinabaki kwenye computer zao, huu ni uungwana?

10. Mapokezi naulizwa dini yangu ili nini? Kwamba huduma za afya zinachagua dini???

NB. Nimeandika kwa ufupi tu ila hayo ni baadhi ya mambo yaliyonisibu KCMC na kunifanya niamue rasmi kuipa kisogo hii hospitali.

Sina ubaya na mtu yeyote anayehusika na hospitali hii na wala simfahamu yeyote ila nawasihi watumishi tuheshimu mahali pa kazi.

IMG_1139.jpg

Umefanya la maana I hope wahusika wafikishiwe habari!
 
Back
Top Bottom