Kebehi dhidi ya Nyerere na Magufuli, ni ishara Watanzania wana uelewa mdogo. Viongozi hawa wajengewe kumbukizi

Kebehi dhidi ya Nyerere na Magufuli, ni ishara Watanzania wana uelewa mdogo. Viongozi hawa wajengewe kumbukizi

Mleta mada Naona umepata unachostahili!Kwa comment za juu ni wazi watu wamekataa usichanganye pumba na mchele
Alichofanya wala siyo kuchanganya pumba na mchele kwani vyote viwili vinaweza kuwa chakula cha kuku. Amejaribu kuchanganya vitu visivyoweza kuchanganyika kabisa; mfano sukari na mchanga!
 
Wa Tanzania tuache unafiki. pamoja na Udikteta wake Yapo mambo makubwa aliyofanya Magufuli. Au mnataka kumuondoa katika fikra za WaTz ili wengine waonekane leo kuwa wanafaa? Mtoa mada anatukumbusha haya.
Nyie mnaomkosoa Magufuli Yote maslahi tuu!
Kutokana na udhaifu wake mkubwa kiuongozi na kielimu alitafuta njia ya kufunika tatizo hilo kubwa. Aliamua na kufanikiwa kuwateka mawazo watu wenye uelewa mdogo na wanaosumbuliwa na umaskini kwa kuwajengea fikra kuwa dhiki yao inasababishwa na sheria na taratibu za nchi kuhusu biashara, watumishi wa serikali, matajiri na wazungu! Aliwawaburudisha na kuwafurahisha kwa kuwadhalilisha hadharani na kuwaumiza watumishi wa umma, wanasiasa wa upinzani na hata wasaidizi wake wakuu!
 
Nyerere alikuwa dikteta na Magufuli alikuwa dikteta wote wanafanana tu. Nyerere alizuia TV, redio binafsi na tulisikiliza RTD tu na ilikuwa ni misifa juu ya misifa. Sema tunamuheshimu kwa sababu alikuwa raisi wa kwanza. But alikuwa dikteta tena afadhali hata ya Magufuli.
Ulishuhudia uongozi wa Nyerere ukiwa na akili au umesikia tu. Nyerere hakuhitaji kusifiwa hovyo hovyo. Sana sana kulikuwa na nyimbo za kuelimisha kuhusu siasa za nchi na sera zake; siyo kiongozi!
 
Nyerere muoga kwa mabeberu? Hii umeitoa wapi ndugu? Alikuwa na mapungufu yake tena mengine yanatuathiri hadi leo lakini sijui hilo.
Labda kama tabia na ushahidi wa kiongozi kutowaogopa mabeberu ni kujifungia ndani ya nchi yake na kutoshirikia mikutano yoyote ya ya nje ya nchi yake. Nyerere angewaogopa mabeberu asingekuwa anakwenda kwenye majukwaa ya kimataifa kukutana nao na kujibizana nao kwa nguvu ya hoja.
 
Kutokana na udhaifu wake mkubwa kiuongozi na kielimu alitafuta njia ya kufunika tatizo hilo kubwa. Aliamua na kufanikiwa kuwateka mawazo watu wenye uelewa mdogo na wanaosumbuliwa na umaskini kwa kuwajengea fikra kuwa dhiki yao inasababishwa na sheria na taratibu za nchi kuhusu biashara, watumishi wa serikali, matajiri na wazungu! Aliwawaburudisha na kuwafurahisha kwa kuwadhalilisha hadharani na kuwaumiza watumishi wa umma, wanasiasa wa upinzani na hata wasaidizi wake wakuu!
Nakubaliana nawe kwenye hili la kuwadhalilisha watendaji hadharani, jambo ambalo sio la kistaarabu kabisa. Lakini je, hakutusoma WaTz na kutuelewa udhaifu wetu? Maana sikumbuki kusikia ama kuona mtu ama watu wakimjibu kwa yale ambayo hayakuwa ya kiungwana. Ajabu hata Spika wa Bunge alikuwa kama kitoroli chake, na ndio mfano mzuri wa Watz. Alijaribu kutumia mfumo wa "Dikteta Mwema" kuwavutia masikini kwa vile alijua hakuna wa kumpinga. Ila, je hakuibadilisha nchi hii? Tuseme, katika kupima mema na maovu yake, mizania itaegemea upande upi zaidi kwa uzito?
 
A
Aliiba nini ndg yang...??? Alimuua nan...??? Huwez kuongelea wizi kipind cha JPM huko n kulogwa na pesa unazokula za kumchafua CHUMA.

Aliiba kitu gan au ufisadi gan yan... Ivi ukila pesa za kumchafua JPM ndio inabid kuwa na roho ya upofu kwa kias hicho... Waambie wakuongez mshahar kwa maan hiyo kaz n ngum sn.

Uvccm wezi sn wanatajana, kifaa cha milion 20 wananunua kwa 170 milions, ngorongoro imeuzwa kwa UAE na masai wanaondolewa, tozo kila kitu, mifumuko ya bei, maisha magumu, uongoz wa ovyo, safar zisizo na tija, usaliti uliokithiri, kesi za mchongo kwa viongozi wa upinzan, kuharibu vyama pinzan mfn NCCR

Huo kwako ndio uongozi, mikopo mpk nchi imewekwa mstari wa hatari na hakuna lolote la maana linafanyika... Shenzi kbsa

JPM hastahili hata kutamkwa na wajinga na mahaini kama nyie
Ile 1.5 tr unajua ilo wapi? Au bei ya ndege alizonunua unajua bei yake? Ben Saanane unajua yuko wapi?
 
Usimweke Hayati Baba wa Taifa Mwl. J.K. Nyerere kwenye kundi moja na huyo kituko. Ni kashfa kubwa na dharau kwa baba yetu mpendwa wa taifa.

Nyerere alikua a state man, a visionary leader, a man of unquestionable integrity and very intelligent man. Mungu aendelee kumpa punziko jema la milele.

Huyo mwingine ni aibu ya taifa, hakuwa na akili, hakuwa na emotional intelligence, mkabila, mwongo, mbadhirifu,na ata kiingereza hakuwa anajua kuongea. Ni abu kwa taifa
Nikikumbuka hapo kwenye aibu kwa Taifa huwa nafikiria sana
 
Mama katambua mchango specifically Nyerere na JPM katika Mradi wa Nyerere
 
Achana na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, hakuhusu.
Huyu RNA ndiyo wale Samia anawaita born 1990s. Wanadhani Tanzania imeanza kipindi Jakaya Kikwette ni Rais.

Kumhusisha Nyerere kwenye mjadala wenye Magufuli ni umaskini wa mawazo na uelewa
 
Huyu RNA ndiyo wale Samia anawaita born 1990s. Wanadhani Tanzania imeanza kipindi Jakaya Kikwette ni Rais.

Kumhusisha Nyerere kwenye mjadala wenye Magufuli ni umaskini wa mawazo na uelewa
mna muonea sana JPM
 
Wewe mtoa mada mwondoe Nyerere kwenye hilo andiko lako tafadhali. Kumuweka pamoja na Magufuli muuaji, mwizi, mwongo, mnyang'anyi ni KUMTUKANISHA baba wa Taifa.

Nyerere huwa anaongelewa na calibre za akina Nelson Mandela, Nkrumah, Mahatma Gandhi nk.

Magufuli mjadili kwenye mada za akina Iddi Amin Dada, Mobutu Seseseko, Nguema na Bokassa
Ujinga ni mzigo mzito sana,wakati mwingine muwe mnakaa kimya,kwani kila kitu ni lazima uchangie?
 
Habari,

Nimekuwa nikipitia mitandao mingi ya Kijamii wachangiaji wakitoa maneno ya kashfa na kuudhi dhidi ya hawa viongozi wetu, ingawa ukipita mitaani hali ni tofauti na kwenye hii mitandao.

Swali ni kwamba kuna vijana huwa wana ajiriwa kwa shughuli hii chafu?

Mwalimu Nyerere na Magufuli ni Marais PEKEE waliopambana na kuhubiri kupinga Ufisadi wazi wazi bila kuogopa, kifupi hizi kebehi na kwamba watu wengi hawafuatilii mambo ila wanafuata mkumbo kama wangeelewa tusingeona haya mambo.

Je, kwa namna walivyojipambanua kupambana na Ufisadi na kuwa Wazalendo kuna haja ya kuweka Sanamu zao pale Dodoma kama Ishara ya Uzalendo? Vijana tukipita tupate hamasa!

View attachment 2237718
View attachment 2237721
Uwezi kuwa mwerevu mmoja mbele ya wajinga 100, itaonekana wewe ndio hujui,huwezi kuwa mpenda haki mmoja mbele ya wapenda haki 100,hivyohivyo Kwa magufuli yeye kama mwanadamu ana mapungufu yake Ila alikuwa na maadui wengi Kwa kuwa alichokuwa anakitaka kiwe Kwa watanzania wengi,wapo wachache hawakukubaliana nacho na ndio wenye mamlalka na nguvu za kiuchumi, hivyo ilikuwa lazima iwe vile watanzania hawapendi kujipatia Kwa juhudi Ila ni watu wa njia za mkato.
 
Uwezi kuwa mwerevu mmoja mbele ya wajinga 100, itaonekana wewe ndio hujui,huwezi kuwa mpenda haki mmoja mbele ya wapenda haki 100,hivyohivyo Kwa magufuli yeye kama mwanadamu ana mapungufu yake Ila alikuwa na maadui wengi Kwa kuwa alichokuwa anakitaka kiwe Kwa watanzania wengi,wapo wachache hawakukubaliana nacho na ndio wenye mamlalka na nguvu za kiuchumi, hivyo ilikuwa lazima iwe vile watanzania hawapendi kujipatia Kwa juhudi Ila ni watu wa njia za mkato.
Magufuri alileta:-
1.Uchama
2.Ubaguzi
3.Ukabila
4.Wizi
5.Ubinafsi
6.Kiburi
7.Dharau
8.Mmomonyoko wa maadili ya Mtanzania
9.Mfarakano
10.Ujinga
11.Upumbavu
12.Uchawa
13.Kutowajibika
14.Uvivu
15.Ukupe.
 
Back
Top Bottom