Kenya Election 2007: Outcomes

Hii inatisha sana, raisi huyu mteule ameapa kutenda kazi zake za UHALIFU...!!!

May be am getting crazy! Kila nikiangalia huyo mzee na kipara anatamka mbele ya hadhara na kuahidi kutenda uhalifu!!! oh,, God nacheka sana hadi nahurumia mbavu zangu sasa kwani zinauma!
 
May be am getting crazy! Kila nikiangalia huyo mzee na kipara anatamka mbele ya hadhara na kuahidi kutenda uhalifu!!! oh,, God nacheka sana hadi nahurumia mbavu zangu sasa kwani zinauma!
mzee usicheke maana hili ni kubwa inabidi mzee KT alifatilia maana ni batili..ila naona haijastukiwa tu..ile ni batili ile..na nadhani waandaaji wamefanya makusudi..maana wanajua ni mhalifu kweli
 

Asante K-T,

Kuna watu wengi kwenye western media wanataka kuifanya hii issue iwe kati ya wakikuyu na wajaluo na hivyo baadhi ya wengi wasiojua (usiwalaumu sana) wana-fall for that.

Nimeona clip moja ya public TV ya US ambapo kuna analyst mmoja toka Cameroon ambaye imebidi aseme wazi kwenye TV kuwa hii sio case ya kabila moja dhidi ya jingine. Amemfahamisha mtangazaji wa hiyo TV kuwa Raila amepata kura toka makabila mengine ambazo ni zaidi ya kura toka kwa waluo.

Taratibu tu watu wengi watalewa hili na hawatajali sana simplicity inayotaka kufanywa na western media.

Asante sana kwa reporting yako.
 
Kwa hali ya sasa ya Kenya nadhani mimi namlaumu sana mwasisi wa Taifa lile, yaani Mzee Kenyatta kuliko huyu Kibaki. Inawezekana kabisa kuwa Kibaki hakuwa na haja ya kufanya yaliyotokea ila ameshinikizwa na wakikuyu walioko katika position nyingine kama Mahakama, Jeshi, Polisi na hata kwenye hiyo ECK yenyewe. Mzee kenyatta ndiye aliyejenga mazingira yanayowafanya Wakikuyu waone kama ni haki yao kuwa watawala wa Kenya. Laiti Mzee Kenyatta angejenga misngi imara ya utaifa kama alivyofanya mwenzie Nyerere, leo hii watu wasingekuwa wanashabikiana kwa ukabila bali wangekuwa wanashabikiana kwa sera kama ilivyo hapa Tanzania ingawa watu wetu hawajakomaa sana kisiasa kama wenzao wa Kenya.

Lawama pekee ninazomtupia Kibaki ni kuwa alishindwa kufahamu kuwa utawala wake umekuja katika mazingira delicate sana kuliko yale aliyokuwamo Kenyatta, na uchaguzi huu umafenyika katika mazingira ambayo siyo ya wakikuyu dhidi ya waluo kama wakati wa Kenyatta. Nilivyoona ramani ya Kenya utaona kuwa ni wakikuyu tu waliomsupport (Central, East and NorthEast) wakati Odinga kapata support ya makabila mengine yote. Angewakanya henchmen wake kuwa pamoja na kuwa aliyeshinda si mkikuyu, ni mkenya ambaye amechaguliwa kidemokrasi no matter by what margin. Afterall angekumbuka kuwa huyu huyu Odinga ndiye aliyemsaidia yeye kuingia Ikulu mwaka 2002 kwa msingi wa utaifa ambao yeye kaamua kuubomoa. Vile vile amevuruga any future prospects za kuaminiana kati ya wakikuyu na makabila mengine ambayo ilikuwa imeanza kurudi nchini Kenya tangu Kenyata amwue Tom Mboya, na Moi amwue Robert Ouko.
 
mzee usicheke maana hili ni kubwa inabidi mzee KT alifatilia maana ni batili..ila naona haijastukiwa tu..ile ni batili ile..na nadhani waandaaji wamefanya makusudi..maana wanajua ni mhalifu kweli

Happy new year y'all,

Hiyo alofanya Kibaki wakati wa kuapa inaitwa "freudian slip"...........he is guilty as sin and very, very bad news kwa kenya!!!
 

Sidhani kama Kenyatta anastahili lawama katika hili la ukikuyu. Mzee Kenyatta alitawala miaka 15, tena akiwa babu. Alifanya kazi na Jaramogi Odinga kidogo, halafu miaka mingi na Moi. Hasa ile miaka ya 1970's basically ni Moi alikuwa anaendesha hiyo nchi, mzee Kenyatta alishajichokea! Na hata baada ya hapo, Moi alipata miaka mingine 24, muda wa kutosha kabisa kurekebisha kasoro hizo. Moi alisema anafuata "nyayo", binafsi sielewi ni nyayo zipi, lakini kama alifuata hizo za siasa za ukabila, wakenya ni mashahidi, na wanaosoma hii forum wanaweza kutoa maoni yao.

Miaka ile ya 1970's, wakenya wengi waliopinga serikali ya Kenya walikuwa wakikuyu pia, japo mzee Kenyatta mkikuyu mwenzao alikuwa madarakani. Ukisoma maandishi ya akina Ngugi wa Thiong'o, Ngugi wa Mirii, Micere Mugo, n.k., na mambo yaliyowapata baada ya kuandika maandishi hayo hutahitaji ushahidi zaidi. Vitabu vya Ngugi kama "Detained" na "Devil on the Cross" vinashambulia serikali moja kwa moja. Vingine "A Grain of Wheat", "Petals of Blood", vyote wanalia kuwa uhuru bado. Mzee Odinga naye kilio chake kilikuwa hichohicho alipoandika "Not Yet Uhuru", lakini kwa sababu ya mizizi ya ukabila iliyokuwapo tangu kabla, hakuweza kuungana na hawa wakikuyu ingawa wote walikuwa wakipinga serikali hiyohiyo katika muktadha uleule. Na waandishi wa kikikuyu wakaamua kujitoa wazi na kuanza kutukuza "ukikuyu" badala ya u-Kenya. Alishaanza Ngugi wa Thiong'o ku-blend upinzani wa kisiasa na utamaduni wa kikikuyu kwenye "The River Between" na "Weep Not, Child", akitukuza hasa mila ya ukeketaji na kubeza wasiotahiriwa. Akaleta nyingine ya kikikuyu kabisa "Ngaahika Ndeenda-I will marry when I want", na siku hizi naambiwa ameamua kuandika kikikuyu tu, wala hata si kiswahili ambayo huko Kenya ni lugha ya Taifa!

Kwa hiyo kwa kutazama fasihi, ambayo kwayo kimsingi jamii hujidhihirisha kwa jamii nyingine, tunaona kuwa jamii ya Kenya haikuanza ukabila na Kenyatta wala Kibaki. Mizizi hiyo ilikuwapo tangu kabla ya uhuru, na kuna watu wangependa ibaki hivyo, na wamekuwa wakiitetea waziwazi. Viongozi wangeweza kutumia uzalendo kurekebisha hali hiyo tangu mapema. Kenyatta alikuwepo kwa miaka 15, ambayo mingi ya hiyo Moi alifanya kazi za urais (akiwa makamu) chini ya kivuli cha "babu", hadi mzee wa watu alipojifia kwa amani usingizini mwaka 1978. Moi ambaye hujulikana pia kama "profesa" wa siasa za Kenya akachukua nafasi hiyo kwa miaka 24, na kwa hakika amekuwa rais wa Kenya hadi leo hii, (inadaiwa "Mwai Kibaki" humaanisha pia "Moi Kabaki").

Kwa hiyo nani hakutimiza wajibu wake katika kupambana na jinamizi la ukabila huko Kenya? Jibu mnalo!
 
Kithuku,
Kenyatta alikuwa na nafasi nzuri sana ya kuondoa ukabila Kenya. Lakini kama alivyosema Nyerere wakati wa mazishi yake, Kenyatta aligeuka kuwa "tribal chief." Unakumbuka alienda Kisumu na kuwatukana Wajaluo kuwa hawajatahiri. Ndiye aliyeendeleza Ukikuyu serikalini na jeshini. Kuna wakati (1974) ukipiga simu Nairobi kwenye ofisi ya serikali karani ama anakujibu Kikikuyu au Kiingereza. Pia kumbuka alivyowatendea Jaramogi na Tom Mboya. He was a tribalist.
 
Hivi kuna Rais/nchi yeyote ambayo imeishatuma salaam za pongezi kwa Kibaki???
 

Umetoa references nzuri sana zitokanazo na watu waliokuwa wakiona mbali zaidi ya ukabila. Swala la ukabila katika Afrika likuwapo kabla ya mkoloni kuja kuleta mipaka hii ya sasa. Mkoloni alitumia ukabila huo kama tool ya divide and rule. Ilikuwa ni jukumu la wasisi wa Taifa kufuta misngi hiyo ya ukabila. Jaramaogi Oginga Odinga alianza kama mtoto wake, hakutaka kuwa waziri Mkuu wa Kenya wakati Kenyatta yuko ndani; alikuwa na utaifa zaidi. Kenyatta alipokuja madarakani Odinga alikuwa ni mtu mzito sana kiasi kuwa hakukuwa na namna nyingine ila kwa Kenyatta kumkubali kama vice president. Sababu zilizosababsisha Jaramogi Oginga Odinga ajitoe serikalini ndizo zinazoila Kenya leo hii, na zote zinatokana na Kenyatta.

Moi alikuwa na muda wake wa kurekebisha mambo, ana dhambi zake kwa kushindwa kufanya hivyo. Hata hivyo alizungukwa sana na watu walioachwa na Kenyatta, na kwa vile naye hakuwa na utaifa zaidi ya tamaa za kibinafsi, alikubali kuishi na status quo isipokuwa pale ambapo kulikuwa na tishio la madaraka yake kama kwa Charles Njonjo.

Tanzania tuna makabila yapata 150 na kila kabila lilikuwa na chief wake. Baada ya Uhuru, pamoja na failure nyingine za Nyerere, yeye alifanikiwa sana kupandikiza mizizi ya utaifa miongoni mwetu kiasi kuwa hadi leo hii Tanzania hakuna kabila linalojichukulia kuwa wao ndio watawala. Tumetawaliwa na makabila madogo madogo bila kinyongo chochote ingawa siku za hivi karibuni watoto wa viongozi wamejitangaza kuwa wao walizaliwa kutawala (aibu sana kwa Tanzania). Makabila makubwa hayajawahi kutawala na wala hakuna aneyalalamika kwa msingi wa ukabila bali process yenyewe.

Lililotokea Kenya na matunda ya kabila fulani kuamini kuwa wao ndio wana haki ya kutawala Kenya tu, si linginelo lolote.
 
hujasikia Marekani imetuma salaam na kuwataka Wakenya watulie na kujenga nchi yao
 
hujasikia Marekani imetuma salaam na kuwataka Wakenya watulie na kujenga nchi yao
Hapana wame-withdraw na kusema kuwa wako concerned na allegations za vote fraud. Wametamka kuwa wanashirikiana na pande zote mbili kutatua mgogoro wa kisiasa uliozuka Kenya na kusababisha vifo visivyokuwa vya lazima.
 
Hiyo aliyoharibu Kenyatta kwa miaka 15, Moi alishindwaje kutengeneza kwa miaka 24? Kama miaka 24 haikutosha kurekebisha hali hiyo ni dhahiri kwamba ama mizizi yake ni kabla hata ya uhuru na hivyo haifutiki kirahisi, au Moi was incompetent for the job ya kuondoa ukabila. Mimi naamini Moi alikuwa na nafasi nzuri ya kurekebisha hali hii kuliko Kenyatta. Na huyo huyo mkikuyu Kenyatta ndiye aliyemuwekea Moi fursa ya kumrithi, bahati mbaya Moi akaamua kurithi kila kitu ikiwa ni pamoja na kuendeleza ukabila kuliko utaifa (ingawa alijitahidi sana kuonekana kama Kenyan nationalist, lakini kwa vitendo hakudhihirisha hivyo). Moi ndiye aliyefufua ukabila huu mpya wa sasa (nitauita neo-tribalism, maana FORD na KANU zilikuwa zimeshabadilisha upepo huo) kwa kumteua Uhuru Kenyatta akidhani atapata support ya wakikuyu wenzie. Ndipo wapinzani wakajiunga katika NARC na kuteua mkikuyu pia, lakini mwenye support isiyo ya kikabila iliyojengeka kupitia upinzani. Lakini Kibaki ni wazi alipata kura za aina 2, za wapenda mabadiliko (za kitaifa), na za wakikuyu (za kikabila hizo). Uhuru alipata zaidi za wakikuyu wachache na wale Moi die-hards. Ndivyo alivyoshinda Kibaki 2002, kupitia mbegu ya kikabila iliyofufuliwa na Moi.

Kwa hiyo bado namlaumu zaidi Moi kwa kushindwa kufuta kero ya ukabila huko Kenya.
 
hujasikia Marekani imetuma salaam na kuwataka Wakenya watulie na kujenga nchi yao

Credibility & Integrity ya marekani sio kama siku za zamani kwa sasa nao wao wanaonekana manyang'au tu!!! Kwa hiyo hatuna haja ya kuona hilo ni la Muhimu,,, siku hizi tuko pamoja na EU!!!

Mangapi Marekani wameidanganya dunia? Kuna haja tena ya kuwaaamini hawa? waacheni na ubabe wao usiokuwa na maana!
 
naam leo siku ya kwanza ktk mwaka huu wa 2008.

kenya wameupokea mwaka huu ktk hali iliojaa simanzi na huzuni

mola wape amani na mapendo waja wako hawa.

jee hali inaendeleaje huko kwenye medani.

ndugu KT(au Jemedari wa ukombozi) na wengineo tuhabarisheni.

nnasikia Rais kikwete katuma ujumbe Kenya wa kuzungumza na pande zote mbili zipunguze munkari na kuangalia ni vp wataweza kuinusuru kenya
 
http://www.africanpath.com/p_blogEntry.cfm?blogEntryID=2966

http://www.nytimes.com/2007/12/31/w...l?_r=3&hp&oref=slogin&oref=slogin&oref=slogin


COMMONWEALTH YASHINIKIZWA KU SUSPEND THE KIBAKI REGIME FROM KLABU HIO

http://www.telegraph.co.uk/opinion/main.jhtml?xml=/opinion/2008/01/01/dl0101.xml


DURU ZA KUAMINIKA ZASEMA


Moi atorokea UJERUMANI na wanawe

NA LEO MAGEZITINI

Mafaktori mawili yanayomilikiwa na Moi pamoja na nyumba ya Moi huko Baringo za teketezwa moto na wananchi.Wananchi wenye gadhabu kali waliivamia makao fulani ya dikteta huyo wa awali, rafikiye Kibaki. Waliichoma hadi jivu kasri ya multi-million shilling iitwayo Kaburwo Presidential Guest House house on Mumberes farm on the Nakuru-Eldoret highway mwendo wa saa tisa za usiku Jumatatu.

Tunapanga kujiunga na raila alhamisi wapende wasipende

WE WANT OUR PRESIDENT, THE PEOPLE'S PRESIDENT

 
the true orange revolution is about to begin.. yaliyomkuta jamaa wa Ukraine na yule wa Georgia yatatokea Nairobi. Rais Kibaki atakimbia nchi na kwenda kuishi uhamishoni. Polisi wa Kenya watasita kutumia risasi zao dhidi ya ndugu zao. Tanzania iandae nyumba ya ziada kwani Kibaki na familia wako njiani.
 
Mimi naita huu ndio upumbavu wetu. Tunashindwa kung'amua matatizo makubwa yatokanayo na mambo madogo kwa ajili ya tamaa zetu za utajiri na madaraka ya haramu. Mikataba ya madini hapa Tanzania ni sehemu ya upumbavu huu huu.
 
Kila mara Rais wa Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi akiapishwa marais wengine kutoka nchi hizo huwa wanahudhuria lakini mzee Kibaki safari hii ni kama ameapishwa na wahuni. I always thought that baada ya Moi kuondoka tatizo lilikuwa limebaki Harare lakini sasa inaonekana kuwa liko Nairobi, Mugabe amepata member( he must be very happy now"
Tunashukuru sana K-T kwa kutuletea updates and we r happy that you are well and alive, we hope the same to our sister and your dad. Dalili nyingi zinaonesha kuwa Kibaki will go, sooner if not later!
 
I wonder where are Oyugi na Nicholas Biwott, hawa huenda watakuwa wa kwanza kukimbia, labda jinamizi la ouko litawajia!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…