Kenya ‘haiwezi kukabidhi bandari’ kwa China kama njia ya kulipa deni la SGR

Kenya ‘haiwezi kukabidhi bandari’ kwa China kama njia ya kulipa deni la SGR

Snowden E

JF-Expert Member
Joined
Apr 27, 2018
Posts
1,668
Reaction score
2,908
bbcCopyright: bbc

Waziri wa Afya nchini Kenya Ukur Yatani amekanusha taarifa kuwa nchi hiyo iko katika hatari ya kupoteza bandari yake kubwa kwa China ikiwa itashindwa kulipa deni lake kwa nchi hiyo, ambalo pesa zake zimetumika kwa ujenzi wa reli mpya.

Reli hiyo yenye umbali wa kilomita 472 inagharimu karibu mara tatu zaidi ya viwango vya kimataifa na mara nne ya makadirio halisi.

Magazeti ya eneo yameripoti Jumatatu kuwa China ambayo ndio iliyokopesha deni hilo, inaweza kuchukua udhibiti wa bandari ya Mombasa ikiwa Kenya itashindwa kulipa mkopo wake wa dola bilioni 3.2.

Lakini katika taarifa, waziri wa fedha amesema "Hakuna hatari ya China au nchi nyingine yoyote ile kuchukua bandari".

Alisema deni la ujenzi wa reli haliwezi "kulipwa kwa njia nyingine yoyote ile ya kuleta kipato au kupitia shirika jingine bila idhini ya bunge".

"Serikali ya Kenya haiwezi na haijawahi kuahidi mali ya serikali kama dhamana ya deni kwasababu hatua kama hiyo… inakiuka makubaliano ya sasa ya mkopo yaliyofikiwa," Bwana Yatani amesema.
 
Hawa marafiki zetu Ni mabeberu wabaya kuliko wale wa magharibi
1615905797117.png


1615905834566.png


1615905891702.png
 
Wachina wanaweza kuja kuwa wakoloni waina mpya, naona kule Zambia wanadhibiti hata jeshi lao la police,

Hapa kwetu walitaka kujimilikisha bandari ya bagamoyo kwa kushirikiana na Oman,

Lakini na wakenya wamezidi mno corruption, mnawezaje kujenga mradi Mara tatu ya gharama halisi za ujenzi?!

Ufisadi unaiharibu sana Africa.
 
Hamna cha bure hapa duniani...ni kuminyana tuu
Tanzania sisi ni wema sana hatuna tuyem'minya, hata Kenya wanatuminya, Malawi wanatuminya wanasema ziwa Nyasa lote ni lao, sisi wetu mchanga tu wa pwani. Zambia wanatuminya, haturuhusiwi kutoa mkurugenzi mkuu Tazara, yaani ni full kuminywa.

Msumbiji waliua na kutimua raia wetu waliokuwa wakifanya BIASHARA huko.

Je, sisi tutaminywa hadi lini?

Kenya hawataki hata mahindi yetu yaingie kwao, so wanayaona yana kunguni?
 
Acha Rutto aendelee kuwanunua, Tanzania iko kipindi hapo nyuma kati pale Musoma walinunuliwa hadi kupiga deki barabarani.

Kenya mkuje Tanzania mpate darsa ya kushughulika na Ruto.
 
Tanzania sisi ni wema sana hatuna tuyem'minya, hata Kenya wanatuminya, Malawi wanatuminya wanasema ziwa Nyasa lote ni lao, sisi wetu mchanga tu wa pwani. Zambia wanatuminya, haturuhusiwi kutoa mkurugenzi mkuu Tazara, yaani ni full kuminywa.
Msumbiji waliua na kutimua raia wetu waliokuwa wakifanya BIASHARA huko.
Je sisi tutaminywa hadi lini.
Kenya hawataki hata mahindi yetu yaingie kwao, so wanayaona yana kunguni?
mkuu,kwenye ziwa hapo rekebisha.inshu ya ziwa ,ilishawekwa sawa,mpaka upo katkat ya ziwa.ndio maana mpaka Sasa Doria zinapigwa na jeshi letu la maji.kuna kipindi Malawi walikua na tabia ya kuzamisha boti za wavuvi wetu,nasisi tulipo toa demo ya kuzamisha viboti vyao,jamaa wakaacha hiyo tabia.
 
Mbona wameshachukua management ya hiyo reli kutoka kwa wachina. Hivi kuna deni lisilolipika....?!
 
mkuu,kwenye ziwa hapo rekebisha.inshu ya ziwa ,ilishawekwa sawa,mpaka upo katkat ya ziwa.ndio maana mpaka Sasa Doria zinapigwa na jeshi letu la maji.kuna kipindi Malawi walikua na tabia ya kuzamisha boti za wavuvi wetu,nasisi tulipo toa demo ya kuzamisha viboti vyao,jamaa wakaacha hiyo tabia.
Sawa, Sasa sisi tunamminya Nani?
 
Yaan hapo wa kenywa wana danganywa
Iv ulale na deni la mtu then umpangine namna ya kumlipa in case ukashindwa kulipa bac lazima uwe na kakitu kukaweka rehani kenye thaman na lile deni ...... Majiran zetu ilo deni ni kubwa sana ...iv mtaanza lini ku generate profit ?
 
Back
Top Bottom