Snowden E
JF-Expert Member
- Apr 27, 2018
- 1,668
- 2,908
bbcCopyright: bbc
Waziri wa Afya nchini Kenya Ukur Yatani amekanusha taarifa kuwa nchi hiyo iko katika hatari ya kupoteza bandari yake kubwa kwa China ikiwa itashindwa kulipa deni lake kwa nchi hiyo, ambalo pesa zake zimetumika kwa ujenzi wa reli mpya.
Reli hiyo yenye umbali wa kilomita 472 inagharimu karibu mara tatu zaidi ya viwango vya kimataifa na mara nne ya makadirio halisi.
Magazeti ya eneo yameripoti Jumatatu kuwa China ambayo ndio iliyokopesha deni hilo, inaweza kuchukua udhibiti wa bandari ya Mombasa ikiwa Kenya itashindwa kulipa mkopo wake wa dola bilioni 3.2.
Lakini katika taarifa, waziri wa fedha amesema "Hakuna hatari ya China au nchi nyingine yoyote ile kuchukua bandari".
Alisema deni la ujenzi wa reli haliwezi "kulipwa kwa njia nyingine yoyote ile ya kuleta kipato au kupitia shirika jingine bila idhini ya bunge".
"Serikali ya Kenya haiwezi na haijawahi kuahidi mali ya serikali kama dhamana ya deni kwasababu hatua kama hiyo… inakiuka makubaliano ya sasa ya mkopo yaliyofikiwa," Bwana Yatani amesema.
Waziri wa Afya nchini Kenya Ukur Yatani amekanusha taarifa kuwa nchi hiyo iko katika hatari ya kupoteza bandari yake kubwa kwa China ikiwa itashindwa kulipa deni lake kwa nchi hiyo, ambalo pesa zake zimetumika kwa ujenzi wa reli mpya.
Reli hiyo yenye umbali wa kilomita 472 inagharimu karibu mara tatu zaidi ya viwango vya kimataifa na mara nne ya makadirio halisi.
Magazeti ya eneo yameripoti Jumatatu kuwa China ambayo ndio iliyokopesha deni hilo, inaweza kuchukua udhibiti wa bandari ya Mombasa ikiwa Kenya itashindwa kulipa mkopo wake wa dola bilioni 3.2.
Lakini katika taarifa, waziri wa fedha amesema "Hakuna hatari ya China au nchi nyingine yoyote ile kuchukua bandari".
Alisema deni la ujenzi wa reli haliwezi "kulipwa kwa njia nyingine yoyote ile ya kuleta kipato au kupitia shirika jingine bila idhini ya bunge".
"Serikali ya Kenya haiwezi na haijawahi kuahidi mali ya serikali kama dhamana ya deni kwasababu hatua kama hiyo… inakiuka makubaliano ya sasa ya mkopo yaliyofikiwa," Bwana Yatani amesema.