Kenya imecheza sana ujasusi wa kiuchumi dhidi ya Tanzania. Should this necessarily be "quid pro quo"?

Kenya imecheza sana ujasusi wa kiuchumi dhidi ya Tanzania. Should this necessarily be "quid pro quo"?

Kijana 254 nakuona unatetea nchi yako
Haha, mkuu, ni kweli lakini nampa vitu real huyo, ka hela hana, alafu anatarajia mambo yanyooke, urongo huo. Sahi kisomo kinaambatana na hela + connection. Bila hivyo, atabaki kulia lia tu wakati ndugu zake wanapiga kazi za kishua huku.
 
Uo ujasusi kwani Tanzania imezuiwa kuwafanyia Kenya ?

Fanyeni kazi vijana mpate pesa tuache kulia lia


Mambo ya kufanyiwa ujasusi mbona ni ya kawaida tu hata sisi kwani hatufanyi ujasusi kwa Kenya?

Na nchi zote za maziwa makuu? Acheni utoto.
 
Uo ujasusi kwani Tanzania imezuiwa kuwafanyia Kenya ?

Fanyeni kazi vijana mpate pesa tuache kulia lia


Mambo ya kufanyiwa ujasusi mbona ni ya kawaida tu hata sisi kwani hatufanyi ujasusi kwa Kenya?

Na nchi zote za maziwa makuu? Acheni utoto.
Kwanza unatakiwa kujifunza kwa aliyekutangulia kuliko kung'ang'ana na Burundi
 
Swadakta kabisa mkuu, kinachoigharimu Tz yetu ni mifumo ya hovyo na ujanja² wa kiswahili. Mtoa mada + MATAGA wanahangaika sana kulinda legacy ya Jiwe, hawataki kusema ukweli kwamba uchumi wa Tz kudorora ni matokeo ya;
  • Sheria kandamizi
  • siasa chafu
  • ulimbukeni wa viongozi
  • visasi
  • wivu wa kitoto kwa wenzetu n.k n.k
Hamna cha ujasusi wala nini.
Huu ndio ukweli.
 
Kwani baada ya kumkataa Sylivia Mulinge kuna mtanzania anayeendesha VodaCom kama CEO au shida ni Mkenya ??

Ziara ya Rais Samia ni kubwa na imechukuliwa kwa ukubwa sana na wakenya ila kwetu sisi,

Muda wote ni wanyonge kazi yetu ni kujishuku shuku muda wote, kujiona wanyonge tutapigwa, hatujiwezi. Aisee

Huu ni ulemavu hakika.

Ningekuwa Rais nchi hii, ningegawa passport kwa kila mtu akazurule huko nje labda unyoronyoro ungetoka.

Mbongo muda wote ni kulalamika na kuhisihisi kujiona anaonewa muda wote.

This is too much.
Tatizo watz maskini wa mawazo Fursa zimefunguliwa Kenya na tz utaona wenzetu watavyochangamkia Fursa sisi tutaanza kuvaa fulana za cccm nakuanza kulaumu wakenya wanachukua Fursa zetu ujinga.
 
1-umesoma?
2-umeomba kazi ukanyimwa?
3-una connection hata ya jamaa zako KE?
4-una hela ya ziada ya kujisaidia ukiwa ugenini?
5-unaweza kujituma bila kulalamika?
6-mwisho, what's your future plans wakati unataka kufanya kazi inje?

NB:Ukijijibu hayo, bila shaka hutaona wa kukubwaga maishani kwa lolote utakalotaka kufanya, pahali popote pale duniani!
Akikujibu nami niite nisome ccm imeharibu akili za matz mengi.
 
Suala la viwanda kufa Tanzania ni kutokana na mtazamo wa uchumi wa kidola tulionao pamoja na siasa.

Kuna mashirika mazuri nchi hii, lakini wakurugenzi badala ya kuwekwa wenye weledi mtu anakabidhiwa shirika kwasababu alimsaidia fulani kwenye kampeni za uchaguzi.

Au yuko karibu na mwenye madaraka au kutoka chama fulani.

Tafsiri yake mtu anapewa shirika ili atafune wakati wake, shirika likifa utamlaumu nani
Mkwamo wetu hapa ndipo ulipo

Sent from my Nokia 8.1 using JamiiForums mobile app
 
Sisi ni watu wa visingizio tu. Na tutabakia hapa hapa na umasikini wetu kama tukiendelea kudhania umasikini wetu unasababishwa na watu wengine na sio sisi wenyewe!

Yaani tunafikiri tukiwazuia Kenya kuendelea ndio sisi tutaendelea? Yaani tulikuwa tayari nafasi ya MD wa Voda apewe mmisri kuliko mkenya! Roho mbaya tu. Tumefaidikaje? Voda kampuni ya UK/SA.....Kenya haina incentive ya kuiua na kwa kweli haiwezi kuiua.....ni service industry..... ikifa Voda wateja hawahamii Safaricom.....sanasana watahamia Tigo, Airtel, TTCL nk. Stupidity at it's best!

Inanikumbusha ile stori ya jamaa aliyeambiwa na "mungu" aombe kitu kimoja kwa sharti kwamba chochote atakachoomba atapewa lakini nduguye atapewa mara mbili yake! Jamaa alivyo na roho mbaya akaomba atobolewe jicho moja.....! (Ili nduguye awe kipofu kabisa).
 
..nadhani tunakosea sana kuwakweza TISS na kukabidhi maisha yetu mikononi mwao.

..suala la viwanda kufa au kustawi linategemeana na mazingira ya kibiashara yaliyoko Tz.
Mkuu tatizo letu ni moja,sisi kazi ya usalama wa taifa ni kuwawinda wapinzani na kuwapoteza, imagine akina bashite ndio walikuwa viongozi wao wa kupanga misheni,
Wakati wenzetu wanaangalia fulsa na kuzinyakua ,
Usalama wanamlinda mtu kwa maslahi yake wanaacha nchi na uchumi unakimbiziwa nje ya nchi,
Na shida nyingine wakajigeuza wambea wa kuchunguza wananchi wenye hela na kuwanyang'anya, ili kunusuru mitaji watu wakaangalia wapi hakuna wanyang'anyi wakakimbilia huko,
Wakati huo huku tunaimbishwa wimbo wa wanyonge
 
Inanikumbusha ile stori ya jamaa aliyeambiwa na "mungu" aombe kitu kimoja kwa sharti kwamba chochote atakachoomba atapewa lakini nduguye atapewa mara mbili yake! Jamaa alivyo na roho mbaya akaomba atobolewe jicho moja.....! (Ili nduguye awe kipofu kabisa)
sema huyo alikuwa mbongo tuu hahaha
 
Mkuu tatizo letu ni moja,sisi kazi ya usalama wa taifa ni kuwawinda wapinzani na kuwapoteza, imagine akina bashite ndio walikuwa viongozi wao wa kupanga misheni,
Wakati wenzetu wanaangalia fulsa na kuzinyakua ,
Usalama wanamlinda mtu kwa maslahi yake wanaacha nchi na uchumi unakimbiziwa nje ya nchi,
Na shida nyingine wakajigeuza wambea wa kuchunguza wananchi wenye hela na kuwanyang'anya, ili kunusuru mitaji watu wakaangalia wapi hakuna wanyang'anyi wakakimbilia huko,
Wakati huo huku tunaimbishwa wimbo wa wanyonge

..Looh!!

..Wafanyabiashara ndio hao wamenyang'a nywa fedha.

..Maana yake hawana mitaji ya kushindana na Wakenya.

..Vijana nao wanaambiwa wasijifunze Kiingereza watakuwa watumwa na ni kukosa uzalendo.

..Maana yake huyu kijana akienda kwenye usaili wa kampuni ya wawekezaji wanaotoka nje atashindwa kupata kazi.

..Tunalalamika elimu yetu ni ya nadharia. Na juu ya hilo tunawalemaza vijana kwa kuwanyima communication skills.

..Tunawafanya vijana wetu wasiweze kushindana ktk soko la ajira la Afrika Mashariki. Tumesalimu amri kabla hata mchezo haujaanza.
 
Mazingira mkuu yanachangia sn
Kwani huyu mama umemuona na kasoro gani....ndo nyie muliokua mnamshabikia mwendazake kwasabb anatesa nakufunga matajiri wakati anaua uchumi....huyu mama ameanza kurekebisha mmeanza dharau zenu
 
Back
Top Bottom