Kenya imecheza sana ujasusi wa kiuchumi dhidi ya Tanzania. Should this necessarily be "quid pro quo"?

Mkuu, labda huyu mwamba My Son drink water anaweza kuwa na jibu sahihi kwako kwa maana mimi nimenukuu tu alichowahi kukisema yeye zamani mwaka 2019.
 
mkuu unajua Kuna watu uwa wanatoa maada ambazo hazina msingi au Kama story za vijiweni Yani hazina mashiko na wanashindwa kussuport wanachokianzisha
Mkuu, mimi nimezungumzia uwezekano wa yule CEO Mkenya aliyependekezwa na Vodacom kurudi tena Tanzania endapo Rais Samia atafuta documents za kazi kama alivyofanya Rais Uhuru, lakini suala la kufa kwa Vodacom limeongelewa na kaka mkubwa My Son drink water hivyo muulize yeye kuhusiana na hilo.
 
Mkuu 'Mkaruka', usidhani nakataa hayo yote uliyoandika, hasa kuhusu waTanzania kutochangamkia fursa na kuwa na visingizio. Haya ni mambo ya kawaida sana na ni mambo rahisi kabisa kuyabadili, hasa panapokuwepo na ajira finyu zinazogombaniwa na wengi. Hili haliwezi kuwa tatizo kabisa.

Ninapokataa kata kata ni juu ya hilo la "Ushindani" wa biashara.
Ni nani anayeogopa ushindani wa biashara halali?; lakini unapoleta ushindani wa "unyang'anyi" hapo ndipo penye shida.

Mama hajaweka mikakati yoyote ya kupambana na hawa wanyang'anyi. Huko kwao tu, serikali yao haina njia za kuwadhibiti - Juzi tu si umesikia KEMSA walivyoyeyusha misaada ya COVID-19 iliyotolewa kupambana na gonjwa hilo?
Ipo mifano mingi sana ya aina hiyo.

Sasa unaposema 'ushindani' utashindana vipi na watu ambao walikwishahitimu katika nyanja hizo; halafu huna njia za kuwabana, wewe unafungua tu?

Na siyo hivyo tu, si kwamba wao wanaujuzi zaidi katika mambo haya ya unyang'anyi wa mali za umma, bali tatizo linaongezeka wanapokuwa ni wakala wa makundi ya aina hiyo toka nje ya bara hili.

Tupo tayari kuwakaribisha wote hawa na tukabaki salama?
 
Na hata hilo la kuiua Vodacom sio swala la kutilia mashaka sana..., 'at least' lina mwelekeo unaoeleweka, na kutokana na mifano mingine ya aina hiyo, sio swala la kubeza.
 
Tenderpreneurs wana tofauti gani na hawa?
Mayanga
Utalii Festival
Kagoda
Meremeta
EPA
Escrow
Kiwira
Mkulima wa South
ATCL
Waharibifu wa soko la korosho kusini
CHATO airport
 
Waoga wa ushindani kwa sababu wanajijua wengi ni vihiyo.
 
Sisi tumepoteza muda mwingi tukiwa tunahangaika kuvizia wafanyabiashara na wanasiasa kwa kudukua mawasiliano na akaunti zao ili waingie kwenye kundi la 1.) Kuhujumu uchumi au,(2) kutakatisha fedha!!!!
 
Tenderpreneurs wana tofauti gani na hawa?
Mayanga
Utalii Festival
Kagoda
Meremeta
EPA
Escrow
Kiwira
Mkulima wa South
ATCL
Waharibifu wa soko la korosho kusini
CHATO airport
Ongeza kwenye orodha hiyo LUGUMI..., na wapo wengine wengi tu!

Kwa hiyo tutakuwa na nafuu tukiongeza na wajuzi zaidi ya hao waliopo hapa tayari?

Baada ya haya anayoyafanya mama; kilichobaki sasa nasubiri kusikia njia zake atakazozitumia kuhakikisha kwamba biashara huru na halali sio sawa na zile za kinyang'anyi.
Nasubiri kusikia mipango yake madhubuti aliyoiandaa kuwabana wanyang'anyi.
 
Asilimia kubwa ya watanzania sahvi ni watu wa kujishtukia...kutwa wanasema ohh tunaibiwa na malalamiko mengi yasiyokuwa na msingi

Ova
 
Usiwasahau na wanyang'anyi Task force waliokomba pesa za Mbowe na wafanyabiashara wengine kinyume cha sheria.
 
Usiwasahau na wanyang'anyi Task force waliokomba pesa za Mbowe na wafanyabiashara wengine kinyume cha sheria.
Hao siwasahau kamwe na wala siwashangilii.
Hawana tofauti yoyote na uliowaorodhesha hapo, na hawa wenye sumu kali tunaowafungulia milango huku tukiwa hatukujiandaa kwa chochote kuwadhibiti.
 
..nadhani tunakosea sana kuwakweza TISS na kukabidhi maisha yetu mikononi mwao.

..suala la viwanda kufa au kustawi linategemeana na mazingira ya kibiashara yaliyoko Tz.
TISS wanaowajibu pia wa kumonitor mazingira hayo
 
They are overrated and full of proud
Ndiyo, we’re full of pride, so kwa hivyo wataka tuwe kama nyinyi? Waoga, wanyonge kisha with low self esteem on top of that?

Tazama vile wanajf huongelea kuhusu nchi ndogo kama rwanda na burundi nyinyi mnakuwaga arrogant sana na ni wanafki wakubwa sana.

Kweli nyani haoni kundule.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…