Kenya imeiacha Tanzania parefu sana kimaendeleo, shida ni nini?

Kenya imeiacha Tanzania parefu sana kimaendeleo, shida ni nini?

Wangaya

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2018
Posts
569
Reaction score
1,228
Wakuu twende mbele turudi nyuma, nchi ya Kenya imeitupa Tanzania mbali sana kimaendeleo. Nakiri sijawahi kufika Kenya, lakini nimekuwa mfuatiliaji sana wa mafanikio ya wenzetu kupitia kupitia Luninga na hasahasa Google Earth ambayo inaweza kukupeleka popote pale na kukuonesha mandhari mbalimbali duniani.

Nchi ya Kenya eneo lake kubwa ni Jangwa kama ionekavyo hapo chini ukifananisha na Tanzania. Pia eneo lake ni dogo ukilinganisha na Tanzania.

Sijaainisha ni maendeleo gani wametupita ila karibu nyanja zote utakazozifikiria wewe wao wapo mbele yetu.
Sisi Tz tunakwama wapi?
~ Je, ni historia ndio iliyoturudisha nyuma?
~ Je, ni mfumo wa Elimu?
~ Je, ni wanasiasa?

Shida ni nini hasa? Au sisi ni wavivu kufanya kazi? Nchi yetu imebarikiwa kila rasli mali, mito mingi, maziwa yametuzunguka, bahari, mbuga za wanyama, mlima Kilimanjaro, madini mbalimbali... Tufanye nini kuisaidia nchi yetu kusonga mbele?

Nimewiwa tu kuandika hivi nikiamini wapo wajuvi humu ndani na tunaweza kujadili pamoja.

Mungu ibariki Tanzania.

Screenshot_20221224-200047.jpg
 
..tatizo la Watanzanio sio kutokufanya kazi kwa bidii.

..we work as hard as Kenyans, if not harder.

..tofauti kati yetu, na haswa nikiangazia kilimo na ufugaji, ni kutokutumia maarifa na utaalamu wa kisasi.

..ukitaka kulitambua hilo angalia jinsi Wakenya wanavyolima na kufuga ulinganishe na Watanzania.

..Majirani na ndugu zetu wa Kenya wanatumia mbegu bora iwe kwenye kilimo au ufugaji, na mbinu zao ni za kisasa.
 
Wakuu twende mbele turudi nyuma, nchi ya Kenya imeitupa Tanzania mbali sana kimaendeleo. Nakiri sijawahi kufika Kenya, lakini nimekua mfuatiliaji sana wa mafanikio ya wenzetu kupitia kupitia Luninga na hasahasa Google Earth ambayo inaweza kukupeleka popote pale na kukuonesha mandhari mbalimbali duniani.
Nchi ya Kenya eneo lake kubwa ni Jangwa kama ionekavyo hapo chini ukifananisha na Tanzania. Pia eneo lake ni dogo ukilinganisha na Tanzania.
Sijaainisha ni maendeleo gani wametupita ila karibu nyanja zote utakazozifikiria wewe wao wapo mbele yetu.
Sisi Tz tunakwama wapi?
Je ni historia ndio iliyoturudisha nyuma?
Je ni mfumo wa Elimu?
Je ni wanasiasa?
Shida ni nini hasa? Au sisi ni wavivu kufanya kazi? Nchi yetu imebarikiwa kila rasli mali, mito mingi, maziwa yametuzunguka, bahari, mbuga za wanyama, mlima Kilimanjaro, madini mbalimbali....
Tufanye nini kuisaidia nchi yetu kusonga mbele?
Nimewiwa tu kuandika hivi nikiamini wapo wajuvi humu ndani na tunaweza kujadili pamoja.

Mungu ibariki Tanzania. View attachment 2456941
Wakenya ni wapambanaji wakubwa (Hustlers) wametapakaa kila pembe ya dunia kusaka fursa pia wanapeana sapoti wao kwa wao kwenda ughaibuni kusaka fursa na demokrasia yao ipo vizuri hasa sera ya kuruhusu Uraia pacha kwa raia wake.

Hii inawasaidia watu kwenda nje kutafuta ujuzi, Ajira na "in return" fedha wanazopata kama Diaspora zinachangia ukuaji wa uchumi

Pia Kenya wana mfumo mzuri wa Elimu na katiba yao pia ni nzuri.

Njoo bongo sasa Kupata pasipoti ya kusafiria tu hadi uzungushwe weeeehh!!! Utoe Rushwa weeeh! Uhojiwe maswali ya kijinga! Uambiwe mara leta barua ya uthibitisho uendako,mara barua ya Afisa mtendaji, Mara wakwambie majina yako kwenye vyeti hayafanani!!???? Process kibao!

Tz bado ina wajinga wengi sana na sera za kijinga na kipumbavu za Uchawa na kusifia ujinga wa viongozi wao.

Tanzania is doomed to remain poor!!!
 
Wakuu twende mbele turudi nyuma, nchi ya Kenya imeitupa Tanzania mbali sana kimaendeleo. Nakiri sijawahi kufika Kenya, lakini nimekua mfuatiliaji sana wa mafanikio ya wenzetu kupitia kupitia Luninga na hasahasa Google Earth ambayo inaweza kukupeleka popote pale na kukuonesha mandhari mbalimbali duniani.
Nchi ya Kenya eneo lake kubwa ni Jangwa kama ionekavyo hapo chini ukifananisha na Tanzania. Pia eneo lake ni dogo ukilinganisha na Tanzania.
Sijaainisha ni maendeleo gani wametupita ila karibu nyanja zote utakazozifikiria wewe wao wapo mbele yetu.
Sisi Tz tunakwama wapi?
Je ni historia ndio iliyoturudisha nyuma?
Je ni mfumo wa Elimu?
Je ni wanasiasa?
Shida ni nini hasa? Au sisi ni wavivu kufanya kazi? Nchi yetu imebarikiwa kila rasli mali, mito mingi, maziwa yametuzunguka, bahari, mbuga za wanyama, mlima Kilimanjaro, madini mbalimbali....
Tufanye nini kuisaidia nchi yetu kusonga mbele?
Nimewiwa tu kuandika hivi nikiamini wapo wajuvi humu ndani na tunaweza kujadili pamoja.

Mungu ibariki Tanzania. View attachment 2456941
Miji mikubwa minne ya Kenya Nairobi, Mombasa, Nakuru na Kisumu imeendelea sana tu kama miji ya Africa Kusini na hiyo ina beba kama robo ya kenya. Robo nyingine imeendelea kawaida tu kama kanda ya ziwa hivi au niseme kanda ya kaskazini huku Tanzania ila NUSU ya Nchi ya kenya ni masikini wa kutupwa, hawana hakika na mlo, hakuna shule, Hospitali , hakuna usalama nk wanaishi maisha ya taabu na wanakufa kwa njaa kila mwaka
Kwenye hiyo miji minne pia kuna Viwanda Vingi vya Wazungu ambavyo vinafanya pato la Nchi liwe kubwa. Nahisi utafiti wako umeangukia kwenye hiyo miji minne ambayo inabeba kama robo tu ya Kenya.

Wako mbele kiuchumi ila kwa pato la mtu mmoja mmoja hali si shwari!
 
Shida ilianzia kwa Kenyatta na Nyerere. Kenyatta alikuwa mkulima hivyo aliweka sera za kuwalinda wakulima. Nyerere alikuwa anajidai mkulima, sera alizoweka zikavuruga kabisa ukulima.

Nyerere alikuwa mnyonyaji mkubwa kuliko hata Kenyatta.
 
Wakuu twende mbele turudi nyuma, nchi ya Kenya imeitupa Tanzania mbali sana kimaendeleo. Nakiri sijawahi kufika Kenya, lakini nimekua mfuatiliaji sana wa mafanikio ya wenzetu kupitia kupitia Luninga na hasahasa Google Earth ambayo inaweza kukupeleka popote pale na kukuonesha mandhari mbalimbali duniani.
Nchi ya Kenya eneo lake kubwa ni Jangwa kama ionekavyo hapo chini ukifananisha na Tanzania. Pia eneo lake ni dogo ukilinganisha na Tanzania.
Sijaainisha ni maendeleo gani wametupita ila karibu nyanja zote utakazozifikiria wewe wao wapo mbele yetu.
Sisi Tz tunakwama wapi?
Je ni historia ndio iliyoturudisha nyuma?
Je ni mfumo wa Elimu?
Je ni wanasiasa?
Shida ni nini hasa? Au sisi ni wavivu kufanya kazi? Nchi yetu imebarikiwa kila rasli mali, mito mingi, maziwa yametuzunguka, bahari, mbuga za wanyama, mlima Kilimanjaro, madini mbalimbali....
Tufanye nini kuisaidia nchi yetu kusonga mbele?
Nimewiwa tu kuandika hivi nikiamini wapo wajuvi humu ndani na tunaweza kujadili pamoja.

Mungu ibariki Tanzania. View attachment 2456941
Vijana kama Hawa mchango wao kwa taifa ni mdogo sana.
 
Kagera War (1978-1979)

Waakanzia kutupiga gape hapo.
Kisa vita ya kidini (Mkatoliki Nyerere vs Muislamu Amin)

..Kenya walikuwa wametuacha kimaendeleo hata kabla ya vita vya Kagera.

..kumbuka Tanzania tulivyohangaika kuanzisha viwanda mara baada ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kuvunjika kwasababu tulikuwa tukitegemea bidhaa toka Kenya.
 
Mnabwabwa ujinga tupu.
Kama mtu wa kupiga soga kama hivi huwezi kuelewa Kenya walivyotuzidi.
Unaijua paypal? Kenya wanatuma na kupokea pesa kutoka paypal. Mtandaoni kuna fursa nyingi sana tunazikosa.
Kuna makampuni yanalipa kwa Paypal na Payoneer. Mfumo wa paypal ni rahisi unaingia kwenye simu moja kwa moja.
Wakati mwingine huwa natamani hata ningekuwa mkenya.
 
Kama mtu wa kupiga soga kama hivi huwezi kuelewa Kenya walivyotuzidi.
Unaijua paypal? Kenya wanatuma na kupokea pesa kutoka paypal. Mtandaoni kuna fursa nyingi sana tunazikosa.
Kuna makampuni yanalipa kwa Paypal na Payoneer. Mfumo wa paypal ni rahisi unaingia kwenye simu moja kwa moja.
Wakati mwingine huwa natamani hata ningekuwa mkenya.
Kwa hicho ndio kigezo ulichotumia?

Eleza kwa nini Tz tunawazidi kwenye Inclusive Economy hao Wakenya?
 
Wakuu twende mbele turudi nyuma, nchi ya Kenya imeitupa Tanzania mbali sana kimaendeleo. Nakiri sijawahi kufika Kenya, lakini nimekua mfuatiliaji sana wa mafanikio ya wenzetu kupitia kupitia Luninga na hasahasa Google Earth ambayo inaweza kukupeleka popote pale na kukuonesha mandhari mbalimbali duniani.
Nchi ya Kenya eneo lake kubwa ni Jangwa kama ionekavyo hapo chini ukifananisha na Tanzania. Pia eneo lake ni dogo ukilinganisha na Tanzania.
Sijaainisha ni maendeleo gani wametupita ila karibu nyanja zote utakazozifikiria wewe wao wapo mbele yetu.
Sisi Tz tunakwama wapi?
Je ni historia ndio iliyoturudisha nyuma?
Je ni mfumo wa Elimu?
Je ni wanasiasa?
Shida ni nini hasa? Au sisi ni wavivu kufanya kazi? Nchi yetu imebarikiwa kila rasli mali, mito mingi, maziwa yametuzunguka, bahari, mbuga za wanyama, mlima Kilimanjaro, madini mbalimbali....
Tufanye nini kuisaidia nchi yetu kusonga mbele?
Nimewiwa tu kuandika hivi nikiamini wapo wajuvi humu ndani na tunaweza kujadili pamoja.

Mungu ibariki Tanzania. View attachment 2456941
Mi ni mtz, ila Tz ni ya hovyo Sana!
 
Shida ilianza hapo kwenye "Palefu" badala ya "parefu". We unazani kwa mwendo wa kusema "Mologolo" badala ya "Morogoro" tutawakuta kimaendeleo?
[emoji16][emoji16] Shida sana! Nyie walimu wa Lugha mmechangia pakubwa sana kuirudisha nchi nyuma.
 
Back
Top Bottom