Kenya is not serious ona hii

Kenya is not serious ona hii

Hapo itakuwa shida kidogo. Kuna suala la lahaja, wao Kenya wana Kiswahili chao na sisi Tz kuna chetu. Kama pande zote tumekubaliana kuwa hiki ndicho Kiswahili sanifu hapo sawa. Ni kweli, sote tunafahamu historia ya usanifishaji wa Kiswahili kuwa Kiunguja ndicho kiikubalika na kuwa lahaja iliyotumika kusanifisha Kiswahili, lakini, ni kweli mpaka leo Kiunguja ndicho kinatumika ukanda wote wa Afrika ya mashariki kama rejea ya Kiswahili sanifu? Jibu ni hapana,kwani hata Tz bara bado tuna tofauti kubwa na Kiunguja, aidha, ni kawaida kwa wabara kuwabeza waunguja kwa matamshi ama miundo yao ya lugha ya Kiswahili, na wao pia wamekuwa wakifanya hivyo kwetu. Kwahiyo hali ipo hivi, wakati wewe una umeme, mkenya ana stima, wewe una ugali ,mkenya ana sima, wewe una mlinzi, mkenya ana bawabu n.k.

Pengine hoja yako itufungue masikio sasa, tuanze kufikiria kuwa na msamiati sanifu tutakaoutumia pande zote. Jambo la kuzingatia ni kuwa hii si kwa Kiswahili pekee, hata lugha kama Kiingereza hukutana na changamoto hizi, Kimarekani, Kiautsralia, Ki-british n.k havifanani hata. Na wao kila mmoja ana standard yake, hawajakubaliana kuwa na lahaja moja sanifu. Ukijifunza lugha zao inabidi ujue najifunza cha wapi.

Ni sawa kabisa kuwa tuna tofautiana kilahaja na Unguja. Lkn ukweli tukubali ukweli kwamba kunapokuwa na mabishano au mgongano wa neno au kifungu cha maneno kati ya Tanzania na kenya, au na nchi nyingine yoyote, rejea iwe kiswahili cha Tanzania.
Umetaja vizuri sana mfano wa nchi zinazo zungumza kiingereza. Lkn nao wana kanuni moja. Mgongano ukitokea, basi rejea yao haiwi mahala pengine popote, bali ni kiingereza cha Uingereza.
 
Wacha ujinga ,hii ni sawa na "colour" ya Uingereza na "color" ya Marekani ama "truck" ya Marekani na neno "lorry' linalotumiwa Uingereza ....hizo neno zote ni sawa na hakuna nchi moja wanaojiona wajuaji zaidi.
au tyre na tire.... ni the same.
 
Sasa unamfunza mtu mwenye hta kiswahili hakitilii maanani....mwenzako huyo ana lugha zenye yupo vizuri sana hta zaidi ya kiswahili..

Ni sawa na kumchukua msukuma wa usukumani au wale jamaa wa kagera na bukoba....halafu useme wanaongea kiswahili sanifu...[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]


Umesha anza kuwa msemaji wa watu humu ndani!!?
Nani kakwambia hakizingatii kiswahili??
 
Ni sawa kabisa kuwa tuna tofautiana kilahaja na Unguja. Lkn ukweli tukubali ukweli kwamba kunapokuwa na mabishano au mgongano wa neno au kifungu cha maneno kati ya Tanzania na kenya, au na nchi nyingine yoyote, rejea iwe kiswahili cha Tanzania.
Umetaja vizuri sana mfano wa nchi zinazo zungumza kiingereza. Lkn nao wana kanuni moja. Mgongano ukitokea, basi rejea yao haiwi mahala pengine popote, bali ni kiingereza cha Uingereza.


Hayo uansema wewe ndugu kadiri unavyojisikia wala huna ushahidi wowote. N anakuelewa sana,kwamba hivyo ni vile unajisikia, hisia zako zinakutuma hivyo. Linapokuja matumizi ya lugha, humpangii mtumiaji. Si unaona hata hapa kwetu, BAKITA, TUKI na siku hizi tuna TATAKI, wanajitahidi kuja na msamiati kwa maneno mageni hasa ya tekolojia lakini mzungumzaji gani umesikia anasema tarakilishi badala ya kompyuta, nani anasema vimbaka badala ya toothpick n.k.?

Mfano huo hapo juu ni wa ndani, nyinyi kwa nyinyi, sasa kama hata kitaifa kuna changamoto hizi , kimataifa je? Wewe ni nani umshurutishe nchi nyingine kuongea utakavyo? Hapa haijalishi lahaja yako ni bora au la, msingi wa lugha upo kwenye kuwasiliana, wenyewe wanawasilaina, wewe ni nani uwaambie hivyo ni vibaya?

Umetoa mfano wa Kiingereza cha Marekani na UK, usemacho si kweli, si kweli, si kweli, si kweli hata chembe.Hakuna hata mmoja kati ya nchi mbili hizi inayokubali Kiingereza cha mwenzake. UK inaona US ni takataka, wao ndiyo wenye Kiingereza, na US inakiona ki-UK ni ubabu, kimepitwa na wakati na ni lahaja ya kikoloni. Na kuna mazingira uchumi unasaidia kuifanya lugha yako kuwa juu, hivyo, kwa sasa UK amekaliwa kwani kwenye uchumi na teknolojia lahaja maarufu ni ya USA. unakutana na kompyuta, itakupa machaguo kama unataka UK ama USA, cha ajabu default ni USA, na ni kama inakulazimisha, mara kwa mara inakurudisha USA.

Kwa kifupi lahaja zote kati ya USA na UK hutumika. Kinachotakiwa mwandishi usiyumbeyumbe, unashauriwa ukichagua lahaja moja baki hapohapo kuepusha mkanganyiko.
 
Ahsante kwa Maelezo mujaarabu mkuu
Hapo itakuwa shida kidogo. Kuna suala la lahaja, wao Kenya wana Kiswahili chao na sisi Tz kuna chetu. Kama pande zote tumekubaliana kuwa hiki ndicho Kiswahili sanifu hapo sawa. Ni kweli, sote tunafahamu historia ya usanifishaji wa Kiswahili kuwa Kiunguja ndicho kiikubalika na kuwa lahaja iliyotumika kusanifisha Kiswahili, lakini, ni kweli mpaka leo Kiunguja ndicho kinatumika ukanda wote wa Afrika ya mashariki kama rejea ya Kiswahili sanifu? Jibu ni hapana,kwani hata Tz bara bado tuna tofauti kubwa na Kiunguja, aidha, ni kawaida kwa wabara kuwabeza waunguja kwa matamshi ama miundo yao ya lugha ya Kiswahili, na wao pia wamekuwa wakifanya hivyo kwetu. Kwahiyo hali ipo hivi, wakati wewe una umeme, mkenya ana stima, wewe una ugali ,mkenya ana sima, wewe una mlinzi, mkenya ana bawabu n.k.

Pengine hoja yako itufungue masikio sasa, tuanze kufikiria kuwa na msamiati sanifu tutakaoutumia pande zote. Jambo la kuzingatia ni kuwa hii si kwa Kiswahili pekee, hata lugha kama Kiingereza hukutana na changamoto hizi, Kimarekani, Kiautsralia, Ki-british n.k havifanani hata. Na wao kila mmoja ana standard yake, hawajakubaliana kuwa na lahaja moja sanifu. Ukijifunza lugha zao inabidi ujue najifunza cha wapi.
 
Kwani wahaya hawawezi kuongea?
Sasa unamfunza mtu mwenye hta kiswahili hakitilii maanani....mwenzako huyo ana lugha zenye yupo vizuri sana hta zaidi ya kiswahili..

Ni sawa na kumchukua msukuma wa usukumani au wale jamaa wa kagera na bukoba....halafu useme wanaongea kiswahili sanifu...[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
Back
Top Bottom