Hili ni janga la dunia, lazima tufuate template inayoeleweka, nyie wenyewe hapo bila aibu mnaomba misaada mabeberu ilhali bado mnataka mfanye mambo yenu yasiyoendana na mantiki yoyote, data za nini unakaa ndani nazo, hii hata mabingwa wa kuficha data akina China na Urusi wote wanataarifu hali yao, nyie na umaskini wenu wa Kiafrika mnasuasua ya nini halafu mnakuja kushtukiza na kupita majirani zenu wote kwa idadi ya maambukizi.
Halafu nyie ndio nchi ambayo mpaka leo mnakusanyika kwenye vilabu vya pombe, majirani zenu wamewafungia mipaka maana nyie ni wakaidi na wabishi kuliko maelezo, mnapukutika hadi wabunge na bado mnaendelea kukaidi, namba za waathirka wenu zinapandisha kwa kishindo ilhali mnapima watu wachache sana na bado hamuoni kama issue.
Mngekua mnapima kwa kasi kama majirani zenu yaani ndio mngeelewa nini kinaendelea duniani.