DOKEZO Kero IFM Mwanza Campus, mamlaka husika tusaidie wanafunzi

DOKEZO Kero IFM Mwanza Campus, mamlaka husika tusaidie wanafunzi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Habari bila picha/video clip sawa na takataka tu. Dunia ya leo
 
Huwa nikipita maeneo ya rock city mall..naona vijana wamebeba vidaftari pale kwa nje kumbe huwa kuna chuo palee...kwa yale mazingira kusoma chuo tena cha elimu ya juu ni ngumu sana aiseee
 
Naandika hapa jamiiforums ili kupata msaada baada ya meneja wa campus daktari Ally Zawadi kushindwa kutusaidia.

BAADHI YA KERO:

1: UBOVU WA MAZINGIRA YA KUJIFUNZIA
Kwa muda sasa, kampasi hii imepoteza mwelekeo. Tupo wanafunzi zaidi ya 1000 hapa Mwanza na tunalipa ada isio pungua milioni moja kwa mwanafunzi, meaning kwa mwaka tunalipa zaidi ya bilion moja chuoni. Ina maana IFM wameshindwa kununua jenereta lake?

Siku ya Jana Jumatano ya tarehe 14.12.2022 Umeme ulikatika saa moja jioni tukiwa katikati ya mitihani na ikaahirishwa tukiwa tumeanza kufanya.

Leo Tena mchana umeme umekatika. Kwa kuwa madarasa baadhi hayana vioo kulingana na partition zake hivyo kuwa Giza hata mchana, tumerundikwa katika madarasa machache yenye mwanga hafifu huku joto likiwa Kali.

Kwa kuwa chuo kimepanga rock City Mall, tunapata shida kwani kwa idadi ywtu , maeneo ya kujisomea Ni machache mno.

Usalama wetu upo wapi? Afya zetu zipo na usalama gani? Ada zetu zinatumika wapi Kama hata kununua jenereta hamuwezi? Mnafundisha financial management ilhali mambo madogo mnashindwa ku manage.

2: CUSTOMER SERVICE YA HOVYO
Baadhi ya watumishi Wana customer service ya hovyo kabisa, hasa ofisi ya admission na examination office.
Wanafunzi wakiwa na shida ya kutatuliwa, madam L.N wa examination office huwajibu hovyo na kufoka! Pia ofisi ya admission Ina watu wasio jali wanafunzi na wenye lugha ngumu. Hapa kinara wao ni Mr T na Mr E.F. Nimetumia initials kwani mamlaka zinawajua waliopo ofisi hiIlzi

Kwa ujumla, Kuna shida na IFM MWANZA CAMPUS itazamwe na mamlaka zinazo husika ili wanafunzi tusiendelee kutaabika.

NAWASILISHA.
Mwanafunzi, Mwanza Campus.

Soma pia:

Kuifanya elimu iwe biashara ndio msingi wa kuparaganyika Kwa elimu Tanzania, kwanza Campus inaongozwa na Dr. Badala ya Professor hiko chuo ni Utopolo, mtakuwa mnasoma mapopoma tupu, wametanua wigo wa kuongeza mapato tuite "IFM Primary School Campus, Mwanza Branch'
 
Kuifanya elimu iwe biashara ndio msingi wa kuparaganyika Kwa elimu Tanzania, kwanza Campus inaongozwa na Dr. Badala ya Professor hiko chuo ni Utopolo, mtakuwa mnasoma mapopoma tupu, wametanua wigo wa kuongeza mapato tuite "IFM Primary School Campus, Mwanza Branch'
Duuh
 
Back
Top Bottom