Kero: RC DSM tuondolee kampuni zinazokamata magari ni kero na zinachochea rushwa rushwa

Kero: RC DSM tuondolee kampuni zinazokamata magari ni kero na zinachochea rushwa rushwa

ommytk

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2015
Posts
520
Reaction score
1,143
Kilio chetu kwa mkuu mkoa DSM sisi wananchi mkoa DSM kuna tabia sasa imerudi ilikuwepo zamani ikaondolewa wakati fulani sasa imerudi tena kwa kasi.

Kuna kampuni zimesajiliwa sijui na TARURA kukamata magari barabarani pale unaposimama na kupaki mahali au gari ikiwa imeharibika njiani.

Kwanza ni watu wameokotwa wapi sijui wamekaa na uchu wa pesa tu bila kujua hata Sheria wapo kusaka pesha tu ni vitisho kuna bomu mnatengeza. Kwanini mnapenda kuwapa shida wananchi wachukuie Serikali kwa mambo ambayo hayana umuhimu wowote?

Wale jamaa ni wala rushwa wakubwa aisee sijui hata Serikali inapata nini kwa hizo hela wanazochukua barabarani ni kichaka tu cha wizi.

Serikali izitoe zile kampuni ni wizi tu unaendelea
 
HIZI NI KAMPUNI ZA KIPIGAJI TU.,NA KERO KWA JAMII.

ONDOENI KAMPUNI ZA KIPIGAJI.

Aidha waonapo tukio wawe na kamera wapige picha, pia wawe na machine za risiti watoe risiti na aliyevunja sheria apewe wiki mbili za kulipa, badala ya sasa mapato yooote yanajaza mifuko yao, na kadada kaa kabubu.
 
Ningekuwa namiliki silaha nadhani ningekuwa na jinai tayari. Hawa jamaa hawana kabisa akili. Ni ni wajinga sana. Unakuta wanakukamata halafu wanakuambia eti twende ofisini tukaelewane ukifika ofisini wanakufungia gari halafu vinakuja vijamaa vinakuambia bila kutoa hela hutoki. Mi kuna siku nilikuwa nimeenda kuchukua hela kwa ajili ya mambo ya msiba nilikuwa nimefiwa, yaani mi nipo kwenye gari, mtu kashuka kidogo kuchukua hela wakaja wakafunga nikawabembelezq wapi. Hawa jamaa wanafaa kuuawa tu ni wajinga sana
 
Waliwai nikuta nimepaki kituo cha daladala niko na double hazard light zangu. Ety kwa nini umepaki kwenye kituo cha daladala. Nikauliza sheria gani nimevunja ebu sema. Unajua ni kosa kupark hapa. Tunaomba tuzungumze ili swala.

Mmoja anataka kufungua mlango waingie nikamuuliza hii gari ulinunua wewe. Unajua bei yake hadi ulete uchafu wako ndani. Sikia siendi popote mkitaka muite traffic aje nipiga faini. Huwezi andika gari namba tutafutane mjini.

Walinywea kmmk
 
Back
Top Bottom