Kero za askari wa usalama barabarani: Utaratibu wa kutoza adhabu barabarani uangaliwe upya

Kero za askari wa usalama barabarani: Utaratibu wa kutoza adhabu barabarani uangaliwe upya

Chendembe

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2019
Posts
444
Reaction score
488
Nitangulize kupongeza wote waliohusika kubadili utaratibu wa kutoza adhabu za vyombo vya usafiri barabarani badala ya ule wa awali ambapo mahakama pekee ndio ilikuwa inatoza.

Hakika, walikuwa na nia njema ya kuondoa usimamaji wa vyombo vya usafiri kusubiri hukumu ya mahakama.

Pamoja na nia hiyo nzuri, watekelezaji wa sheria hiyo wamekuwa wakitumia nafasi yao vibaya na kusababisha kero kubwaaa kwa wasafirishaji/wasafiri na kuikosesha serikali mapato. Tatizo kubwa ni kukosa busara, hekima ,utovu wa nidhamu, na huruka za kujipatia kipato kwa baadhi ya Askari wetu.

Nadhani wanajiwekea malengo ya kukusanya kipato Chao zaidi kuliko cha serikali kwa siku.

Nashawishika pia kuamini labda baadhi ya vituo vya polisi yanakuwa ni malengo ya kituo kizima kwa vile sijawahi sikia mkuuu wa kituo yeyote kuwai kuwawajibisha askakali wa usalama barabarani. Mbaya zaidi, hata kama ukienda kituoni kulalamika juu yao, unazinguliwa tu.

Sio siri, yanajulikana mengi katikati idara hii ya polisi wa usalama barabarani.

Ivi wakuu wa kituo/RPCs hawajuwi michango ya siku wanayotozwa wasafirishaji wa abiria mijini maarufu daladala?

Nini kinatokea Kama hutoi michango hiyo?

Kuna nini Kati ya Traffic na vi carry, malori ya mchanga na hata mabasi yaendayo mikoani?

Wenzetu hawa hawana kushauri, kuelimisha Wala onyooo. Mwendo wa kutishia kuandikia makosa mawili au matatu.

Pamoja na lengo zuri lililokakusudiwa katika kuanzisha utaratibu huu, nashauri serikali iondoe mamlaka ya kutoza faini za barabarani kwa askali wetu kwakuwa inadhalilisha wananchi na kupelekea kupoteza Imani kwa jeshi hili.

Serikali ibainishe makosa ya kutozwa faini kuzuwia Tabia ya askali waovu kutunga makosa wapendavyo.

Ukaguzi wa magari uwe sehemu maalumu kuzuwia Askari waovu kufuata magari mbali ya miji na kutekeleza uonevu wao ili wapate kipato kama wafanyavyo Traffic was Tunduru ambako Traffic wanatoka na gari la binafsi nje ya mji na kukamata pikipiki/magari na kutoza faini kulingana na sura ya Mwenye chombo.
 
Lakini pia madereva wengi hawataki kufuata sheria za usalama barabarani.

Kwanini mnaendesha magari kwa mwendokasi?

Mwendokasi ni kosa la kisheria.

Hivi mnapataga muda wa kujitafakali kuhusu maisha?

Hivi mnawapenda wategemezi wenu?

Hata kama ninyi wenyewe pengine mmefika pa kujikataa na kwamba chochote kikitokea hamna cha kupoteza , Je vipi kuhusu wategemezi wenu hamna huruma nao? Mliwazaa waje wateseke wakose mahitaji ya msingi?

Maisha ya siku hizi siyo ya kutegemea ndugu akulelee mwanao wakati wake analea kwa mbinde.

Tutafakali zaidi.
 
Hivi mfano gari yako ina vitu vya msingi kama zimamoto,

Mwendo wako wa kisheria kuna askari atakusumbua kweli?

Mimi kama nimejithidi ku comply halafu askari alete za kuleta kiukweli tutazinguana.
 
Msingi wa sheria za usalama barabarani ukiufuata ni kwa faida yako wewe na usipoufuata ni kwa hasara yako na wakwenu maana mchuma janga hula na wakwao.
 
Kuna mmama Hapo junction ya Massana mweusi tii ana roho mbaya jaman[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] yaan hatak maelezo wala chochote akikudaka anakuandikia na ikitokea una daiwa anaforce ulipe happhapo ili akuandikie nyingine
 
Ivi kuna magari yanayoendeshwa kwa kasi Tanzania kuliko ya viongozi? Kuna ajali zimerekodiwa kuhusu mwendo huo?
Ajali ni mpango wa Mungu.
Lakini pia madereva wengi hawataki kufuata sheria za usalama barabarani.

Kwanini mnaendesha magari kwa mwendokasi?

Mwendokasi ni kosa la kisheria.

Hivi mnapataga muda wa kujitafakali kuhusu maisha?

Hivi mnawapenda wategemezi wenu?

Hata kama ninyi wenyewe pengine mmefika pa kujikataa na kwamba chochote kikitokea hamna cha kupoteza , Je vipi kuhusu wategemezi wenu hamna huruma nao? Mliwazaa waje wateseke wakose mahitaji ya msingi?

Maisha ya siku hizi siyo ya kutegemea ndugu akulelee mwanao wakati wake analea kwa mbinde.

Tutafakali zaidi.
 
Lakini pia madereva wengi hawataki kufuata sheria za usalama barabarani.

Kwanini mnaendesha magari kwa mwendokasi?

Mwendokasi ni kosa la kisheria.

Hivi mnapataga muda wa kujitafakali kuhusu maisha?

Hivi mnawapenda wategemezi wenu?

Hata kama ninyi wenyewe pengine mmefika pa kujikataa na kwamba chochote kikitokea hamna cha kupoteza , Je vipi kuhusu wategemezi wenu hamna huruma nao? Mliwazaa waje wateseke wakose mahitaji ya msingi?

Maisha ya siku hizi siyo ya kutegemea ndugu akulelee mwanao wakati wake analea kwa mbinde.

Tutafakali zaidi.
Hiri ni Rimambosasa
 
Kila jambo lafaa kwa kiasi.

Hata kama unaendesha gari barabarani hakuna foleni jifunze kuwa muungwana endesha gari lako kwa mwendo wa usalama wa kisheria itakusaidia wewe na wadau wengine wa barabarani.

Kwanini unakuwa mlafi barabarani?

Ni sawa na kuwekewa chakula kingi bufee mbele yako lakini haina maana ushindane nacho ukimalize kukila hapana bali unapaswa kula kidogo kwa wastani wa kiasi cha kuridhisha huo Ndiyo ustaarabu.

Kuendesha gari kwa mwendokasi ni sawa na ulafi mtu ambae hajazoea kula vizuri nyumbani kwake anaenda kwenye sherehe na ulimbukeni wake.

Mwendokasi unaua.
 
Hivi mfano gari yako ina vitu vya msingi kama zimamoto,

Mwendo wako wa kisheria kuna askari atakusumbua kweli?

Mimi kama nimejithidi ku comply halafu askari alete za kuleta kiukweli tutazinguana.
Kuna gari ukiendesha hata kama ni jipya askari lazima akusumbue
Jaribu kuendesha kirikuu utakuja leta mrejesho
 
Hivi mfano gari yako ina vitu vya msingi kama zimamoto,

Mwendo wako wa kisheria kuna askari atakusumbua kweli?

Mimi kama nimejithidi ku comply halafu askari alete za kuleta kiukweli tutazinguana.
Mbaya kwa hawa watu, wanachukuwa namba ya gari na kwendanayo kuandikia kosa watakavyo.
Utakuta gari imepaki nyumbani, lakini deni linasoma.
Kuwe na utaratibu wa kupiga picha kosa na kuliandika kwenye mfumo.
Vinginevyo ni upuuzi tu.
 
Siku moja nipo safari na mutukaa yangu nikasimamishwa..! Wakati nataka maelezo ya kunisimamisha likapita gari la bwana mmoja mwenye asili ya mkoa wa Bukoba akiwa mafuta na Mark X yake nyeupe. Aliposimamishwa akaambiwa umezidisha mwendo, akauliza tu kosa ni hilo tu? Akaambiwa ndio! Akasema haya andika haraka..! Akapewa nyaraka yake ya malipo akaendelea na safari. Mimi nilibakia pale na muda ukaenda sana tukieleweshana.

Ninachotaka kusema ni kwmba baadhi ya madereva sisi, hasa wengi wetu hatupendi kutoa fine hata kama tunajua tuna makosa..! Ndio maana askari wanatumia mwaya huo kufanya yao.

Maendeleo ya nchi yanaanza na wewe! Ukiambiwa una makosa na ukiandikiwa fine uwe na moyo mkunjufu wa kulipa fine, hapo tutapunguza maelezo nakuitana chemba. Ambako mwisho wa siku kunazua kuchukiana na kurushiana maneno ya shombo!
 
Ungezungumzia hizi[emoji116]
20210606_142442.jpeg
 
Mchango wangu kwa mada hii ni kwamba hizi Freeways zetu bado sana, zipo mno chini ya kiwango kinachotakiwa,pamoja na sheria za usalama barabarani kuwepo utekelezaji wake unakua mgumu kutokana na miundo mbinu ya Hizi barabara.

Ukiangalia hii T1 yetu alama za usalama almost hakuna,njia ni nyembamba mno na why speed limit ni 50km/hr (hii ni speed ya barabara za mitaani sio high way)tujenge upya hizi freeway way na tuziwekeee techonolojia ili kuzilinda kama kuwa na fixed speed cameras,ondoa ule uchafu wa matuta ,futilia mbali vitochi(ni rushwa tupu)na pale Mikumi National park tupanue ile njia na tufweke nyasi na miti yote within 20m both side of the road ili kulinda usalama wa wanyama pori.
 
Makosa ya barabarani yalitumika kama token ya kukusanya mapato, kwenye utawala wa tano

Hata ukusanyaji wa madeni kwa faini zilizobet kuna mapato yanaenda kama bonus kwa askari aliyekamata deni hilo, ndo maana kuna baadhi ya sehemu askari trafiki anakamata magari hata yaliyopaki na kuamuru yalipe.

So its like a chain, askari wanaandika sana makosa ili watengeneze faida za kutosha wanapokamata magari yenye madeni na pesa ya bonus.

Mahakama ,zingekuwa huru, huu mchezo ungeisha.
 
Lakini pia madereva wengi hawataki kufuata sheria za usalama barabarani.
Na kuna mara nyingine Sheria za Barabani haziwataki Madereva, Kwa mfano unakuta Ishara na Alama nyingi zimefutika na Vibao havipo kabisa sasa hilo ni kosa la nani?
 
Nimeuza Noah yangu kwa sababu ya askari wa barabarani, akiona tu nakuja anajua nabeba abiria, lazima 5 initoke. Saa hz nina kistarlet old school hakuna anayenisumbua.

20210516_220421.jpg
 
Back
Top Bottom