Kero za kudate mume wa mtu

Kero za kudate mume wa mtu

Kuna mubaba alinipigia simu siku moja,kaanza mbali wer akawa ananiambia huo ujinga eti mke wake ana kiburi,mara sasahivi hashiki mimba
Mara mkewe kakatisha sebuleni,akabadilisha lugha,akaanza kuongea kingereza[emoji23]
Nikamuacha akatiririka wee,,mtu na heshima zake..halafu sasa mimi ni mama mdogo wake wa mwisho.

Lengo lake sasa,Eti toka unakua nakuona ni binti mwenye nidhamu,nadhani utanifaa...Chaaa

Nikamwambia muombee mkeo sana.
Nikamwambia mie nadate na mdogo wako,alishtuka akaanza kujikanyaga.
Wee DA Anne ulimkomeshajee, huyo mubabaa,
Nimechekaaa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]r
 
Hey
,Weekend kwangu ipo poa sana,Natumaini hata yako imetulia,kinyume na hapo jipe moyo siku hazifanani na pia hazigandi...
Leo shangazi nimeona niongee hili suala kidogo la kudate na mwanaume aliye kwenye ndoa,ninaongea kwa experience yangu na kwa experience ya kuangalia mahusiano ya wengine...Jamani,kina dada hii kitu mimi ilishanishinda sijui wenzangu mnawezaje kuwa happy na mahusiano ya namna hiyo,yaani ukute huu muda dada uko zako hotel happily na married man sijawahi enjoy,nishajaribu kudate nao mara kadhaa ila mara nyingi nimekuwa nikiangukia pua sifiki mbali yaani kuna vitu ambavyo nashindwa kuroll nao,mfano
1.UONGO,
Jamani hao viumbe ni waongo Shetani akasome,utasikia mwingine anasema hampendi kabisa huyo mwanamke kwanza alilazimishwa kumuoa,mwingine utasikia kwanza silali nae chumba kimoja mpe miezi sita utamuona huyoo anampeleka mkewe clinic
,ukisikia hizo mambo za design hivo sister,Don't buy it!

2.UNAFIKI
Hao jamaa achana nao,kuna wale wanafiki uko nao ila kila muda utasikia wife this,wife that,yaani anajifanya anampeeeeendaaaaa unabaki kushangaa kama unampenda mbona unamcheat?nikishasikia tu mume wa mtu kaanza wife sijui nini nini,hilo penzi linanishinda kabisaa,Inakata sana stimu

3.UMBEA
kuna wale wasengenya wake zao oooohooo usiombe ukutane nao anamuanika mkewe unabaki kushangaa,huyu kama mkewe aliyemtolea hadi mahali hivi mimi sasa si ndio atanipiga na picha hapo ni ndukiiii

NUKSI
Ukiwa nao hao mambo hayaendi kabisa kuna namna tu unakuwa unakwama,sijui maombi ya wake zao yanaweka kizuizi,au ni vile mi mwenyewe nakuwaga napata kauoga na ka guilty utasikia kale ka kamstari ka Ebr 13 :4 " ndoa na iheshimiwe na watu wote na malazi yawe safi"kanakuwa kananijiajia tu bila sababu za msingi

KUFICHWAFICHWA.
Yaani unakuwa kama heroine,huku bado upangiwe muda wa kumpigia simu,utasikia "Baby ndio nimefika home usinipigie,usiku mwema ,nakupenda sana🙄🙄🙄"Whaaaaat?

Anyway yako mengi,sijui wenzangu mnawezaje,ila kupanga ni kuchagua ,maana unaweza kudhani uko kwenye mahusiano unakataa watu wema kumbe uko single..wake up weekend njemaaa
Kuna mada niliona asbh

Ungekuwa wewe,ungemshauri nini huyu mtu?


Ameandika hivi;
""HabariNipo ktk fumbo sijui nini nifanya
Ni Mimi ni mtu wa imani,Kuna wakati nilipitia shida nikapiga goti nikamuomba Mungu aniinulie mtu wa kunisaidia
Baada ya mda akainuka mume wa mtu,Cha achabu vile vitu nilivyoomba yeye akavifanya Kwa asilimia kubwa.
Baadae nikawa najiuliza hivi aliyenijibu ni Mungu kweli ?

Nikawa siamini,nikawa nafanya juhudi niachane naye kwani kiimani ni dhambi,lkn Cha ajabu kila ninavyopambana kumuacha linatokea tatizo na anayelisolve ni huyo huyo.
Napambana Tena kumuondoa mara naota ndoto ikielezea huyo ni mtu mwemaaaa hautakiwi kumuondoa ktk maisha Yako.
Kiimani naona nakosea,lkn nifanyajee mwenzenu

Je niamini ni Mungu alimuinua,na wakati wa kumuondoa ukifika atamuondoa mwenyewe au nifanyajee Mana Kuna muda najiuliza kweli Mungu anaweza niletea married man kama msaada wangu?lkn nakumbuka nilioomba Kwa imani,nashindwa kumjudge Mungu,
Nimepitia MENGI MAGUMU,lkn aliyesimama na Mimi ni huyo peke yake
Amekuwa zaidi ya ndugu,
Japo sielew fumbo hili
Naomba watu wa imani mnisaidie fumbo hili mana Mimi nimeshindwa kulifumbua"
 

Attachments

  • Screenshot_20240921-212856.jpg
    Screenshot_20240921-212856.jpg
    437.1 KB · Views: 5
U see!umenipata ninachosema sasa...mcheps alikuwa fundi,akkakupagawisha alivyoweza,na mtoto akakuzalia see you now upo hapa UNASHUKURU unazeeka pamoja na mke wako
Ulitaka azeeke na mchepuko?
Utaota moto na uliyeokota nae kuni
Ndiyo maana amerudi kwa wife wake
 
Wee DA Anne ulimkomeshajee, huyo mubabaa,
Nimechekaaa [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]r
😂😂😂😂
Yaani mtu sijawahi kuwa na mazoea naye
Siku hiyo nikashangaa amenipigia..
Akauliza kwanza,upo Na nani hapo karibu?
Nikamwambiaa Niko mwenyewe..
Hee nikaona anatiririka wee
Matatizo yake yooootee.. toka anamtongoza huyo mkewe..mara anasema mkewe alimdanganya miaka
Amegundua eti ni mkubwa kuliko yeye
Aisee yaani nyie wanaume sio watu😂

Nikamwambia hakuna mtu ambaye hana matatizo.
 
Kuna mada niliona asbh

Ungekuwa wewe,ungemshauri nini huyu mtu?


Ameandika hivi;
""HabariNipo ktk fumbo sijui nini nifanya
Ni Mimi ni mtu wa imani,Kuna wakati nilipitia shida nikapiga goti nikamuomba Mungu aniinulie mtu wa kunisaidia
Baada ya mda akainuka mume wa mtu,Cha achabu vile vitu nilivyoomba yeye akavifanya Kwa asilimia kubwa.
Baadae nikawa najiuliza hivi aliyenijibu ni Mungu kweli ?

Nikawa siamini,nikawa nafanya juhudi niachane naye kwani kiimani ni dhambi,lkn Cha ajabu kila ninavyopambana kumuacha linatokea tatizo na anayelisolve ni huyo huyo.
Napambana Tena kumuondoa mara naota ndoto ikielezea huyo ni mtu mwemaaaa hautakiwi kumuondoa ktk maisha Yako.
Kiimani naona nakosea,lkn nifanyajee mwenzenu

Je niamini ni Mungu alimuinua,na wakati wa kumuondoa ukifika atamuondoa mwenyewe au nifanyajee Mana Kuna muda najiuliza kweli Mungu anaweza niletea married man kama msaada wangu?lkn nakumbuka nilioomba Kwa imani,nashindwa kumjudge Mungu,
Nimepitia MENGI MAGUMU,lkn aliyesimama na Mimi ni huyo peke yake
Amekuwa zaidi ya ndugu,
Japo sielew fumbo hili
Naomba watu wa imani mnisaidie fumbo hili mana Mimi nimeshindwa kulifumbua"
Ni huyo huyo Mume wa mtu ameletewa na Mungu, kwa maombi yake. Lol
 
Wanaume wote tuliooa tungeamua kutulia tu na wake zetu majumbani, wasimbe wote mjini mngetembea na madera yenye viraka matakoni dadeq😡
😂😂😂 madera yanaraukaga makwapani kushuka chini. Ikirauka aaah, unachomekea chini ya ziwa na hivi ni mashangazi, ndala kiasi chake dera inakaa sawa sawa maisha yanasonga 🤣
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Yaani mtu sijawahi kuwa na mazoea naye
Siku hiyo nikashangaa amenipigia..
Akauliza kwanza,upo Na nani hapo karibu?
Nikamwambiaa Niko mwenyewe..
Hee nikaona anatiririka wee
Matatizo yake yooootee.. toka anamtongoza huyo mkewe..mara anasema mkewe alimdanganya miaka
Amegundua eti ni mkubwa kuliko yeye
Aisee yaani nyie wanaume sio watu[emoji23]

Nikamwambia hakuna mtu ambaye hana matatizo.
Ninapochoka kwa waume za watu, kutoa siri za familia yao kwa mchepuko.
Najiuliza wanawezajee kufanya hivyo? Hawana hata uoga? Aibu je?
Aaaaah
 
Kuna mada niliona asbh

Ungekuwa wewe,ungemshauri nini huyu mtu?


Ameandika hivi;
""HabariNipo ktk fumbo sijui nini nifanya
Ni Mimi ni mtu wa imani,Kuna wakati nilipitia shida nikapiga goti nikamuomba Mungu aniinulie mtu wa kunisaidia
Baada ya mda akainuka mume wa mtu,Cha achabu vile vitu nilivyoomba yeye akavifanya Kwa asilimia kubwa.
Baadae nikawa najiuliza hivi aliyenijibu ni Mungu kweli ?

Nikawa siamini,nikawa nafanya juhudi niachane naye kwani kiimani ni dhambi,lkn Cha ajabu kila ninavyopambana kumuacha linatokea tatizo na anayelisolve ni huyo huyo.
Napambana Tena kumuondoa mara naota ndoto ikielezea huyo ni mtu mwemaaaa hautakiwi kumuondoa ktk maisha Yako.
Kiimani naona nakosea,lkn nifanyajee mwenzenu

Je niamini ni Mungu alimuinua,na wakati wa kumuondoa ukifika atamuondoa mwenyewe au nifanyajee Mana Kuna muda najiuliza kweli Mungu anaweza niletea married man kama msaada wangu?lkn nakumbuka nilioomba Kwa imani,nashindwa kumjudge Mungu,
Nimepitia MENGI MAGUMU,lkn aliyesimama na Mimi ni huyo peke yake
Amekuwa zaidi ya ndugu,
Japo sielew fumbo hili
Naomba watu wa imani mnisaidie fumbo hili mana Mimi nimeshindwa kulifumbua"
Mungu hawezi kukuinulia mume wa mtu awe msaada kwako hata siku moja,kutembea na mume wa mtu ni dhambi ya USALITI,usaliti unaleta maumivu kwa msalitiwa,usaliti unaondoa upendo,usaliti unaleta chuki,usaliti unaleta roho ya kisasi,usaliti unaondoa amani,usaliti unaondoa baraka ...huyo dada hakutakiwa kuanza kutembea na mume wa mtu akiwa katoka kwenye maombi,alivyotoa tu hiyo nafasi alimpa shetani nafasi akajigeuza kama malaika wa nuru,hapo anadhani ni Mungu hapana,agizo la Mungu ni ndoa iheshimiwe...kama kweli ni mtu wa imani na maombi alitakiwa kujua pia namna ya kutafakari majibu kwa njia ya roho na sio njia ya mwili...binafsi ningemshauri pombe toba na rehema na aachane na huyo mtu
 
Back
Top Bottom