Kesho ni kufa na kupona uwanja wa Mkapa, tuhamishie waganga wote wa jadi uwanja wa Taifa ili tusidhalilike

Kesho ni kufa na kupona uwanja wa Mkapa, tuhamishie waganga wote wa jadi uwanja wa Taifa ili tusidhalilike

Daa! Inasikitisha sana. Kwamba karne hii ya 21 bado mnategemea uchawi na ulozi kwenye soka?
 
Kesho kwetu ni fainali, naiona safari ya Morocco kama kila mtanzania mwenye uchungu na uzalendo na nchi hii ataomba dua na sala kwa ajili ya wachezaji wetu na nchi kwa ujumla.

Kiukweli umoja na mshikamano wa watanzania kesho ni muhimu sana kuliko wakati wowote ule, silaha zote kesho zihamishiwe uwanja wa mkapa tukaishangilie stars mwanzo mwisho.

Ndugu yangu Hemed Morroco na Juma Mgunda, nyie wote watu wa Pwani, kule Zanzibar ndiko Simba na Yanga waliko watu wao, watu wa nje ya uwanja wako huko, Zanzibar ndio kwenye wataalamu wa kweli, leteni watu kutoka Pemba, leteni watu kutoka kwetu kule Mwakidila, Mwahako, Mabokweni, Mkinga nk.

Guinea ameshangilia sana alipomfunga DRC akidhani amemaliza, kesho mapema tu tunamaliza shughuli.

Tafadhalini makocha, golini Manula, kulia Kapombe, kushoto Zimbwe, Nne Bacca, Tano Job, Sita kesho axcheze Mudathir, winga Kibu, winga Msuva, Nane Feitoto, Tisa Samatta, Kumi Mzize.

Naiona safari ya Morocco, Naiona Safari ya Morocco, Mungu ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Tanzania, Inshaaallah mapema tu niko uwanjani na wataalamu wangu wawili.
Sita apewe Ibrahim ame wa mashujaa asaidie kumkaba yule striker wao
 
Back
Top Bottom