Kesi namba 456: Jamhuri dhidi ya JamiiForums - Oilcom na Uchakachuaji/Ukwepaji kodi bandarini Dar

Kesi namba 456: Jamhuri dhidi ya JamiiForums - Oilcom na Uchakachuaji/Ukwepaji kodi bandarini Dar

viva lissu, Mungu wa Ibrahimu, Isaka, na Yakobo atasimama nawe

kwa mtazamo wangu hii kesi ingefaa kuwa ya defamation lakini kwasababu imechanganyika na siasa basi imekuwa criminal case
 
Tuache mambo ya Vyama. Namshauri Mhe. Rais amteue Tundu Lissu kuwa Jaji wa Mhakama Kuu.
 
Na mweshimu Mh. Lissu sana kama Mbunge na Mwanasheria anayejua kujenga hoja na anayejua kutetea wataje wake.

Ninachotaka kusema hapa Mh. Lissu ni binadamu, si Mungu wa sheria. Hivyo ninaamini wapo wanasheria wengine wanaoweza kumbana kama watatumia mbinu zile anazozitumia yeye ila wakiwa wameziboresha. Kama ungetumia jicho la tatu kusoma post yangu ungegundua kuwa nilikuwa na wahimiza wanasheria wengine waboreshe mbinu zao za kiuanasheria na pia hata yeye (Mh. Lissu) astuke. Astuke asije akabweteka (kwa uungu wakisheria wa baadhi ya wenzake wanaompa) na baadaye akawaabisha TLS. Wanasheria wengine badala ya kubuni na kuboresha mbinu za kukabiliana na changamoto za kiuanasheria wawapo kazini, wanavizia kumsikiliza Mh. Lissu tu anavyofanya vitu vyake mahakamani ili nao watumie mbinu zake hizo (tena kibaya zaidi kwa kukopi na kupesti) katika shughuli zao.

Kwa utaratibu huu wanasheria hawa hawataweza kuwasaidia watanzania. Ndiyo maana nimeandika hicho kilichokuprovocke ili wabadilike! Ila ukweli unabaki pale kuwa kwa mbinu hizo mbili nilizozisema awali, kama Mh. Lissu hataboresha mbinu zake, anaweza kutolewa kwenye reli wakati anamfanyia mtu cross examination kama mtu huyo atazitumia mbinu nilizoeleza!

Tusimfanye Mh. Lissu Mungu wa sheria ila tumtumie kama role model tu wa kisheria na tujifunze kwake ila tusimkopi.
=====
Utakuwa umenielewa.

Mie sio mwanasheria ila nadhani unapokuwa unafanyiwa cross examination unatakiwa ujibu maswali kama unavyoulizwa, na hapo ndipo inapokuwa shida, ukienda kinyume tu na swali kwa nia ya kutaka kumtoa nje ya mstari wakili unarudishwa palepale na hakimu/judge. Anakurudisha uendelee kuulizwa maswali hata kama ni ya kuudhi.

Nakumbuka kwenye kesi ya magabacholi wakati wa Mtikila, wafuasi wake walikamatwa kwa kuzua tafrani baada ya mkutano wake Jangwani, huku wakiimba Mtikila Oyee na kuwatusi magabacholi.

Wakati wa kesi shahidi aliulizwa na Lamwai;

Lamwai: Hawa mliowakamata ni wafuasi wa Mtikila?
Shahidi: Ndio ni wafuasi wa Mtikila
Lamwai: Mlijuaje kuwa ni wafuasi wa Mtikila
Shahidi: Walikuwa wanaimba Mtikila, Mtikila, Mtikila huku wanatukana Magabacholi
Lamwai: Naomba uimbe, Mtikila, Mtikila...
Shahidi: Hapana siwezi kuimba
Hakimu: Tafadhali shahidi imba kama ulivyoelekezwa
Shahidi: Mtikila, Mtikila...
Lamwai: Je wewe ni mfuasi wa Mtikila?
Hiyo inaonesha jinsi ambavyo shahidi anapokuwa na wakati mgumu sana mahakamani hata kama ana uwezo na akili nyingi.
 
Serikali yetu inatumia nguvu kubwa kuandaa mashitaka bila kuandaa wanasheria wake na mashahidi. Kodi zetu zinatumika vibaya.
 
Kwan wanataka wamjue huyo Furhar ili iweje sasa?

Nilitegemea serikali ifutilie habari aliyoileta na kuwafungulia mashtaka hao Oilcom, wao wanatumia nguvu nyingi kumpata mleta taarifa!
 
Back
Top Bottom