Kesi ya Babu Seya na wanae - Ukweli ni upi haswa?

Kesi ya Babu Seya na wanae - Ukweli ni upi haswa?

Tatizo la wabongo tunapenda kuhukum mambo kwa kutumia hisia na ushabiki HIV ni nan mwenye uhakika kwa asilimia Mia kwmba babu seya na nguza walisingiziwa? Hii yote inatokana na umaarufu wao kabla ya tukio hilo lait wangekuwa watu wa kawaida wala msingetokwa na povu kias hiki watanzania tumekuwa na huruma sna has kwa mtu am aye amefanya kosa kwel hii huruma yetu imeingia mpk kwny mfumo wetu wa sheria tht y unamuona lulu uraian huruma imefanya mpk mafisad kuachiwa au kufungwa kwa miaka midogo gerezan achanen na reference ambazo hazina mashiko tupen data za kutosha zioneshe kwel hawa jamaa walisigiziwa
unaamini ktk lipi?km huamin upande wowote bac usitoke povu na wewe,waache wenye imani zao watoe hisia zao
 
Big up sana, kuna watu wanatoa hoja zao kwa kufata stori za vijiwe vya mtaani, ni hoja za kishabiki shabiki!
ni hisia zao hata km n za mitaani,na we toa hisia zako kwa kufuata story za chumbani,shida iko wapi hapo?heshimu hisia za watu!
 
Mdau ndio maana mambo ya sheria waachie wanasheria...mtu anaongea hapa lakini haelewi hata kesi ilianzia wapi na ikaishia wapi.
tuambie sasa ilianzia wapi na imeishia wap?huenda unafaham zaidi
 
Watu tunaropoka sana. Ukiambiwa ulete ushahidi kuwa babu seya alisingiziwa huna,unabaki kuokoteza maneno ya mitaani eti jk anahusika. Kina babu seya sio malaika mjue. Tunaongozwa na hisia tu. Kama kweli waliwabaka watoto.waozee huko huko ndani
acha kuropoka,leta ushahidi km wanahusika
 
Akili mbovu hata humu Jf wamo.....Maamuzi ya Mahakama zote siyo ushahidi tuu?.........mna matatizo gani nyie Someni mwenendo wa Kesi ndio mutajua mbivu na mbichi.............!!!!!!!!
 
Siku zote wasiojua ujificha nyuma ya wanaojua na siku zote wanasheria wetu hawa ambao ndo walikuwa wahusika wakuu wa kushindwa kusoma na kubaini mikataba ya kifisadi leo tumebeba gunia la mzigo wa mikataba feki alafu ndo haohao eti leo kwenye kesi hii wanajificha nyuma ya sheria,wazandiki wakubwa nyinyi.

Ya kesi ya babu seya yanafahamika mtaani kuliko hata huko kwenye masinagogi yenu(mahakamani), kama hamtaki ulizeni vizuri.
 
Mtu yeyote duniani ambaye anaona jambo lisilo la kawaida lazima ataongea kwa hisia isipokuwa Mchawi tu ambaye hawezi kuguswa na mateso ya mtu fulani. Mi binafsi naskitika sana kwa kile kilichomtokea Baba wa watu - Babu Seya. Inaniuma mno! Hivi kisheria mtu ambae akatafuta zana na kuvunjia mlango na akampa jambazi, je huyo anaachwa huru? Ndo maana wengi wanahisi kwamba hii kesi ni ya kisiasa zaidi kuliko facts zenyewe. Babu Seya mwenyewe alisema iwapo Mungu yupo, siku ya mwisho ndiye atakaetoa hukumu ya kweli ambayo yeye hatoipinga. Mi naungana nae na nipo nae katika shida na majonzi yanayompata.
 
Akili mbovu hata humu Jf wamo.....Maamuzi ya Mahakama zote siyo ushahidi tuu?.........mna matatizo gani nyie Someni mwenendo wa Kesi ndio mutajua mbivu na mbichi.............!!!!!!!!
punguza povu MJINI CHAI,sheria kweli zipo lkn zinafuatwa nchini humu?km kweli we ni great thnker utakubaliana nami kwamba ktk mambo mengne vitu km sheria na taratibu huwekwa pembeni na kutumia akili ya kibinadamu kufikia maamuzi muafaka,hii kesi hebu itazame kibinadamu zaidi na c kisheria zaidi.
 
There is no justice nowadays its about what you can prove in the court of law that's all matters..:help:
 
Wakuu, natambua kuwa bado Tanzania hatujawa na mfumo wa kimahakama wenye kufuata sheria na haki kwa asilimia mia moja. Ila ndiyo mfumo tuliokuwa nao kwa sasa basi inabidi tuukubali na kuuheshimu maamuzi yake bila kuanza kuingiza hisia zetu na kuweka pembeni ukweli.

Hakuna hata mmoja amabaye alikuwepo kama jury pale mahakani. Ni wao (jury) ndiyo walioona ushahidi ambao sisi hatukuwa na fursa nao na kutoa uhamuzi kutokana na mtazamo wao wakiamini ndiyo maamuzi sahihi ya kesi ile kutokana na ushahidi uliombele yao .

Ni hatari na tuache mambo ya kuukumu kwa hisia binafsi( personal emotions). Hivyo naombeni muwe mnaheshimu maamuzi ya kimahakama na muache mahakama ifanye kazi yake haya mambo ya speculations hayafai. Na huu ni mtazamo wangu tu unaweza ukaukunbali au kuupotezea . Ahsanteni
 
ushahd wangu ni ule wa mahakamani. Wewe kama una ushahd kuwa hawakubaka mpeleked marando ili asaidie kuwatoa jela wanateseka bure. Kama huna funga bakuli lako
sijasema nina ushahidi kwamba hawajahusika,ninachoshangaa ni wewe kuwaponda wanaoamua kuweka hisia zao hadharani!kila mtu ana utashi wake na uhuru wa kusema anachohisi,sasa km wewe unapingana nao basi lete ushahidi wako jukwaani sio kupinga mawazo ya wengine
 
Binafsi toka mwanzo wa kuifahamu kesi hii iliyojaa kila aina ya mbwembwe na umaarufu kwa sababu ya washtakiwa wenyewe siku zote na kwa mtazamo wangu na upande wa pili unisamehe ila imani yangu ni kwamba pale hakuna kesi zaidi ya siasa chafu na visasi vya kila aina,chuki na ubinafsi wa nafsi ndio vilivyofanya paka leo hii familia ya Nguza Viking ikiteseka bila sababu.Yashasemwa mengi sana kuwa kuna mlono wa mtu pale na hata ukiangalia mwenendo mzima wa kesi utakubaliana nami pasipo shaka kuwa pale kuna ujanja unaofanyika ingawa ni ngumu na siwezi kutibitisha moja kwa moja ila rai yangu na maombi yangu juu yao waweze kuwa huru tena na kama walifanya kweli basi uhuru wao hakika hautadumu huku uraiani...Mtazamo wangu binafsi.
umemalizia vizuri, asante kwa taarifa
 
Ipo siku yatawashukia wale wote waliofanya haya,MUNGU WEWE WAJUA,NA OKOA WAJA WAKO

Nyie mmekazana kulaumu viongozi tu na mmewasaha TAMWA walivyoishikia kidedea kesi hii utadhani aliyebakwa ni Bi Helen Kijo Bisimba au Anelelia Nkya! Walishupaa hao usipime! Kumbe ni mpango wa kuangamiza familia nzima! Wao ndio wanaharakati eti wa haki za binadamu! Mbona hawafanyi tena uanaharakati wa kuokoa familia waliosingizia? Kesi iliendeshwa kwa mashinikizo sana ya watu hao! Mi nawashangaeni mnapowasahau!
 
mdau natumia simu hapa afu hizo documents ni kubwa kidogo ila naweza kukuforwardia ni PM email address yako ili ushare na wadau
'hebu zishushe hapa mkuu wazione kiongozi.................where we dare to talk openly-JF'
 
hapana sikubaliani na wewe..labda uniambie ni page namba ngapi ya hiyo proceeding ambayo huyo mwalimu alitoa ushahidi huo au kwenye judgement hipi ambayo ilisema hiyo ndio ilikua sababu ya kumwacha huru huyo mwalimu. ebu thibitisha haya usemayo...na je unajua ground za review wanayoiomba sa hivi.. ??
ka unalolisema ni la kweli kwanini malando asingeongezea kama ground nyingine ya review

Kitu kilichoniumiza sana ni pale Mwl aliyetajwa kuwa alikuwa anawapeleka watoto kwa Babu Seya kisha wakati akitoa ushahidi wake Mwl aliiambia mahakama kwamba kamwe asihusishwe kwenye mambo ambayo hajawahi kufanya kwani yeye ni mlokole na hajawahi kuona wala kuwapeleka watoto kwa Babu Seya. Mahakama ikamuona hana hatia ikamwachia huru. Swali kama kulikuwa na Mwl aliyekuwa akiwapeleka watoto hao kwa Babu Seya ni Mwl yupi huyo kama huyu hakuwa na hatia japo mwanzo alionekana ndiye, tena aliiumbua mahakama kuwa hajawahi kusikia kitu kama hicho. Hospital watoto walipimwa ikaonekana hawajaingiliwa kwa vyovyote dokta akatimuliwa akaitwa mwingine kuandika PF3 kuwa waliingiliwa akafanya hivyo muziki usio na mchezaji ukaendelea.
 
Akili mbovu hata humu Jf wamo.....Maamuzi ya Mahakama zote siyo ushahidi tuu?.........mna matatizo gani nyie Someni mwenendo wa Kesi ndio mutajua mbivu na mbichi.............!!!!!!!!

Nani anaziamini mahakama za Tanzania? tumeona kesi nyingi tu zenye maamuzi ya kuelekezwa, shame on them!
 
Back
Top Bottom