Kesi ya Mbowe: Haki Haikuonekana Kutendeka

Kesi ya Mbowe: Haki Haikuonekana Kutendeka

How come mawakili wa utetezi hawakuomba huyo lijenje na meja urio waletwe mbele ya mahakama?

Hata kama wangeomba Jaji huyu angekuwa na yake.

Tayari maelezo yalikuwa nje ya muda na washitakiwa walikuwa wameteswa. Hata mtoto mdogo anajua hivyo.

Utetezi hawakuwa na haja ya kwenda the longer way.

Jaji kaamua kwa ushahidi wa Kingai, Mahita na Msemwa pekee. Siyo maajabu ya Mussa hayo?

Kwanini hakuzingatia kabisa ushawisi wa utetezi?
 
Mwambie kaselabantu au james mapalala tuone kama atakubaluana nàwe

Akisikia kuna kina Ben Azory Lijenje na wa watu kwenye viroba, kina Lissu na risasi mwilini, kina Mawazo na mapanga mwilini, Kwamba tuna magaidi humu nchini kisa kudai katiba mpya, Kwamba tuna mahakimu na majaji maalumu tokea wanakoita kitengo nk - kwa hakika atakubali kuwa Nyerere aliko ni kiongozi wa malaika.

Au nasema uongo ndugu yangu?
 
Niliambatanisha hiyo hukumu nikiamini utaipitia kuona mapungufu yake, kisheria, na hatimaye uipinge ipasavyo. Badala yake ulioyaandika ni hisia zaidi za kuthibitisha lawama dhidi yake Jaji

Sasa nakurejea:

Kama ilivyo katika kesi zote, ushahidi wa upande wa mashtaka na utetezi hukinzana. Ndipo inapokuja kazi ya mahakama ambapo ni kutumia yote yanayowezekana kupata ukweli ili kuhukumu kwa haki na kwa mujibu wa sheria.

Ushahidi wa upande wa mashtaka na wa utetezi kama ulivyo kwa Jaji uko hapa:

Hoja za Mawakili wa Serikali dhidi ya Adamoo

Kwa ajili ya hukumu, Jaji katumia ushahidi wa mashtaka (Kingai, Mahita na Msemwa) pekee kwamba huo ndiyo ulio kweli na kweli tupu.

Jaji kautupilia mbali ushahidi wote wa utetezi (Adamoo, Ling'wenya, na mke wa Adamoo). Bila shaka kwamba wote huo hauaminiki.

Vigezo alivyovitumia kukubali yote ya Kingai, Mahita na Msemwa havina uhalali wowote.

Vigezo alivyovitumia kuutupilia mbali ushahidi wote wa utetezi havina uhalali wowote.

"Detention register ya Moshi haikuwapo kuonyesha mizunguko ya Adamoo Moshi, japo kujiridhisha. Adamoo ana makovu mwilini ambayo yangeweza kukaguliwa hospitali, kujiridhisha"

Moses Lijenje alitumika kuwatishia beyond imagination kuwa alikuwa kesha tupwa kama shinikizo juu ya yaliyotokea Moshi.

Jaji hakuona umuhimu wa Moses Lijenje kuwapo mahakamani ili kujiridhisha na ukweli wa madai ya upande wa utetezi?!

Kazi yake Jaji ilikuwa nini basi pale mahakamani akiwa amekabiliwa na majumuisho ya ushahidi wa pande mbili zenye kukinzana 100%?

Ikumbukwe si jambo geni katika hukumu Jaji kuwa biased kwa sababu mbalimbali.

Ni sahihi basi kuona kuwa Jaji Siyani amekuwa biased kuelekea upande wa mashtaka kwa kuamua kutumia ushahidi wao pekee kwa ajili ya hukumu kwa sababu zake binafsi.

Kwani Jaji Siyani yeye ni malaika kuweza kujua ushahidi wa haki na wa uongo kuwa ni upi kwa kusikiliza tu bila kuchukua hatua zozote zaidi za kujiridhisha pasipo kuwa na shaka, kwa minajili ya kutenda haki?

Maswali yataendelea kumfuata Jaji Siyani hadi kaburini:

Kwanini ushahidi pekee aliotumia kuamulia kesi ni ule tu wa Kingai, Mahita na Msemwa kuwa ndiyo wa kweli pekee?

Kwanini si ule wa Adamoo, Ling'wenya au mkewe Adamoo?

Kwanini si ushahidi wote?

Kwa hakika Jaji Siyani ameidogosha hadhi ya mahakama mbele za mamilioni waliomshuhudia akifanya hivyo.
 
Sasa nakurejea nakurejea:

Kama ilivyo katika kesi zote, ushahidi wa upande wa mashtaka na utetezi hukinzana. Ndipo inapokuja kazi ya mahakama ambapo ni kutumia yote yanayowezekana kupata ukweli ili kuhukumu kwa haki na kwa mujibu wa sheria.

Ushahidi wa upande wa mashtaka na wa utetezi kama ulivyo kwa Jaji uko hapa:

Hoja za Mawakili wa Serikali dhidi ya Adamoo

Kwa ajili ya hukumu, Jaji katumia ushahidi wa mashtaka (Kingai, Mahita na Msemwa) pekee kwamba huo ndiyo ulio kweli na kweli tupu.

Jaji kautupilia mbali ushahidi wote wa utetezi (Adamoo, Ling'wenya, na mke wa Adamoo). Bila shaka kwamba wote huo hauaminiki.

Vigezo alivyovitumia kukubali yote ya Kingai, Mahita na Msemwa havina uhalali wowote.

Vigezo alivyovitumia kuutupilia mbali ushahidi wote wa utetezi havina uhalali wowote.

"Detention register ya Moshi haikuwapo kuonyesha mizunguko ya Adamoo Moshi, japo kujiridhisha. Adamoo ana makovu mwilini ambayo yangeweza kukaguliwa hospitali, kujiridhisha"

Moses Lijenje alitumika kuwatishia beyond imagination kuwa alikuwa kesha tupwa kama shinikizo juu ya yaliyotokea Moshi.

Jaji hakuona umuhimu wa Moses Lijenje kuwapo mahakamani ili kujiridhisha na ukweli wa madai ya upande wa utetezi?!

Kazi yake Jaji ilikuwa nini basi pale mahakamani akiwa amekabiliwa na majumuisho ya ushahidi wa pande mbili zenye kukinzana 100%?

Ikumbukwe si jambo geni katika hukumu Jaji kuwa biased kwa sababu mbalimbali.

Ni sahihi basi kuona kuwa Jaji Siyani amekuwa biased kuelekea upande wa mashtaka kwa kuamua kutumia ushahidi wao pekee kwa ajili ya hukumu kwa sababu zake binafsi.

Kwani Jaji Siyani yeye ni malaika kuweza kujua ushahidi wa haki na wa uongo kuwa ni upi kwa kusikiliza tu bila kuchukua hatua zozote zaidi za kujiridhisha pasipo kuwa na shaka, kwa minajili ya kutenda haki?

Maswaliyataendelea kumfuata Jaji Siyani hadi kaburini:

Kwanini ushahidi pekee aliotumia kuamulia kesi ni ule tu wa Kingai, Mahita na Msemwa kuwa ndiyo wa kweli pekee?

Kwanini si ule wa Adamoo, Ling'wenya au mkewe Adamoo?

Kwanini si ushahidi wote?

Kwa hakika Jaji Siyani ameidogosha hadhi ya mahakama mbele za mamilioni waliomshuhudia akifanya hivyo.
Hoja zako zina mashiko kasoro hitimisho lako lina walakini (harufu ya chuki). Ushauri wangu, mapungufu yaliyomo kwenye Hukumu hiyo, naamini Wakili Kibatala na Wenzake watayatumia kwenye kesi ya msingi
 
Hoja zako zina mashiko kasoro hitimisho lako lina walakini (harufu ya chuki). Ushauri wangu, mapungufu yaliyomo kwenye Hukumu hiyo, naamini Wakili Kibatala na Wenzake watayatumia kwenye kesi ya msingi

Chuki? Chuki ya Nini na itoke wapi? Nini sikukijua kabla, wakati au baada ya hukumu hii?

Chini ni bandiko langu:

Post #85 uzi huu:

Kulingana na ushahidi wa kesi ndogo ndani ya kesi kubwa uliotolewa, Je unadhani maelezo ya Adamoo aliyoandikisha polisi yatapokelewa kama ushahidi..?

2970174_IMG_20211020_132118_488.jpg
 
Chuki? Chuki ya Nini na itoke wapi? Nini sikukijua kabla, wakati au baada ya hukumu hii?
...
View attachment 1983458

Wenye fikira/mtazamo/mategemeo kuwa Katiba (au inavyodaiwa Katiba mpya) ni mwarobaini ya kila tatizo/kero nchini, ni wafinyu au wavivu wa fikra.

Katiba yoyote ile inaweka misingi ya mahusiano, lakini, kamwe haibadili tabia ya mtu. Ni kwa sababu hiyo ndio maana kuna Katiba ikitafsiriwa kwa vitendo (utekelezaji wake) kwa Sheria., Kanuni na Taratibu.
 
Wenye fikira/mtazamo/mategemeo kuwa Katiba (au inavyodaiwa Katiba mpya) ni mwarobaini ya kila tatizo/kero nchini, ni wafinyu au wavivu wa fikra.

Katiba yoyote ile inaweka misingi ya mahusiano, lakini, kamwe haibadili tabia ya mtu. Ni kwa sababu hiyo ndio maana kuna Katiba ikitafsiriwa kwa vitendo (utekelezaji wake) kwa Sheria., Kanuni na Taratibu.

Hayo ni mawazo yako mkuu kama ambavyo yeyote anaweza kuwa na yake.

Si sahihi ku "assert" mawazo yako juu ya wengine kana kwamba wewe ni malaika.

Ustaarabu huwa kila mtu aheshimu mawazo ya wengine, tusemezane, tushawishiane kwa hoja na mwisho wengi wape.

Au nasema uongo ndugu yangu?
 
Mi sielewi, ina maana huyo shaidi alitoa statement ya kuwatia hatiani, ndo maana upande wa utetezi wanahaha kuweka pingamizi ili hiyo statement isitumike kwenye case,, kwani hawezi kuikana statement wakati case ikiendelea?, Kesi inadai mbowe gaidi,, swali alifanya ugaidi gani na wapi?,
Kama statement inadai alipanga kufanya,, endapo mshitakiwa atakana statement, mahakama itamla imisha? [emoji848][emoji848]
Kilichotokea ni kwamba mmoja ya watu watatu waliotuhumiwa na Mbowe alikiri kosa. Upande wa utetezi wanadai kwamba alikiri baada ya kuteswa na kutishwa. Nafikiri walikosa ushahidi wa kutosha na hiyo inaweza kuwa sababu kwa mahakama kutupilia mbali madai yao
 
Hayo ni mawazo yako mkuu kama ambavyo yeyote anaweza kuwa na yake.

Si sahihi ku "assert" mawazo yako juu ya wengine kana kwamba wewe ni malaika.

Ustaarabu huwa kila mtu aheshimu mawazo ya wengine, tusemezane, tushawishiane kwa hoja na mwisho wengi wape.

Au nasema uongo ndugu yangu?
Uchambuzi wako wa hukumu ulikuwa na hoja nzito, lakini sioni uhusiano wa kesi dhidi ya Mbowe na Katiba ya JMT.

Hivyo basi, najiuliza kama kungekuwa na Katiba Mpya ingezuia Mbowe kutuhumiwa au yeye kutenda makosa anayotuhumiwa.

Je, wewe Mkuu brazaj, Katiba iliyopo inakuathiri kwa vipi?
 
Rufaa itakatwa lakini hiyo hakuondoi ukweli kuwa Jaji yuko upande wa prosecution. Jaji hatuko neutral.

Jaji kachukua ushabiki wa Kingai, Mahita na Msekwa at face value kuwa ni sahihi kama ulivyo.

Hakuzingatia lolote kutoka upande wa utetezi.
Hii kanuni 'Judges like Caesar's wife must be beyond suspicion' naona inakuwa kama inasahaulika na kwa sababu hiyo kunakuwa na mashaka kuhusu independence na impartiality ya mahakama.
 
Yaani uchomwe na bisibisi, uning'inizwe miguu juu, halafu maelezo yawe ya hiari, mateso yalikuwa ya nini? Hata mie si mwana sheria ila nauwezo wa kutafakari na kupima maelezo na hali na mazingira yaliyokuwepo, nahisi hukumu imeadhiriwa na majukumu mapya!
 
Uchambuzi wako wa hukumu ulikuwa na hoja nzito, lakini sioni uhusiano wa kesi dhidi ya Mbowe na Katiba ya JMT.

Hivyo basi, najiuliza kama kungekuwa na Katiba Mpya ingezuia Mbowe kutuhumiwa au yeye kutenda makosa anayotuhumiwa.

Je, wewe Mkuu brazaj, Katiba iliyopo inakuathiri kwa vipi?

A: Uhusiano wa Mbowe na Katiba mpya:

1. Tambua kuwa kesi hii ni mwendelezo ule ule wa kubambikiziana kesi ambapo mhanga hana kimbilio utumikao na mamlaka kama gumbo kwa wapinza kutokana na kuwa na katiba mbovu. Kama japo Mahakama au Bunge vingekuwa huru, ule uliojichimbia ambao kupitia polisi ndiyo waasisi wa yote haya ungezingatia sheria na haki wala Mbowe asingekuwa mhanga.

2. Anachotendewa Mbowe si haki na kwa mwingiliano wa mahakama uliopo tokea kwa ule mhimili mrefu zaidi, Mbowe hana namna ili kusubiria tu ambacho ule mhimili mrefu utakuwa umedhamiria kufanya.

3. Hata mtoto mdogo anajua figisu lote la kesi ya Mbowe ni jitihada za serikali kuzima madai halali ya watu kudai katiba mpya. Haupo ugaidi pale Sirro, Kingai, CCM, Samia nk wote wanajua hivyo. Kudai katiba mpya ni kudai mustakabala bora tu wa utangamano. Si sahihi kuwazuia watu kujadiliana hili.

4. Kumbuka Mbowe alikamatwa kwenye mkesha wa kongamano la katiba mpya Mwanza. Yeye pamoja na yeyote aliyekuwa kwenye harakati za kongamano hilo walkamatwa. Hoteli husika ilizingirwa, kongamano likazuiwa na hata aliyevaa sare za kongamano popote alikamatwa huko Mwanza siku hiyo na hata siku kadhaa baadaye.

5. Kwamba kesi ya Mbowe haina cha kufanya na madai ya katiba mpya hicho ni kisingizio tu kama ulivyo msingi mzima wa hukumu ya Jaji Siyani.

IMG_20211021_190628_385.jpg


Hayo hapo ni halisi.

7. Tulipo, Samia kama ilivyo kuwa jiwe anaitamani mno post 2025 presidency. Kwenye hilo ni wazi watafanya lolote. Bila Chadema anauhakika wa urais baada ya 2025. Inafahamika bila katiba mpya si tu kuwa Chadema haitashiriki, bali yale mambo yetu ya 2020 au ya kule Konde #2 - wizi wa chaguzi ni halali.

8. Ni faida kwa Samia na washirika wake, Mbowe kuwa na kesi kidhwalimu tu kwa ajili ya mavuno ya Samia 2025 wakijifunika ndani ya mwamvuli wa katiba iliyopo. Kumbuka wafuasi wa Samia wala si CCM bali zaidi bila shaka ni wale watu wasiojulikana.

Wanao mhimili uliojichimbia zaidi. Si mahakama wala bunge linaloweza kuwawajibisha au hata kuwakemea, kwa nini wajiweke rehani na katiba mpya?

Makosa anayotuhumiwa nayo Mbowe ni ya kubumba. Makosa anayotuhumiwa nayo Mbowe yana lengo la kumshikilia mahabusu, kumpotezea muda, kuidhoofisha Chadema na kuipunguza kasi ya kudai katiba mpya ilinkumhakikishia Samia kamseleleko ka 2025.

B: Kwanini katiba mpya ni muhimu kwetu sote:

Ama kwa hakika katiba iliyopo inaniathiri sana kama inavyo muathiri yeyote ukiwamo wewe. Mada hii imejadiliwa sana ikiwamo humu JF.

Anaathirika dereva wa lori sembuse nani asiathirike?

Katiba Mpya ni muhimu kwa Sekta Zote

Hata wewe weka shughuli zako hapa kama wewe si Kingai au mtu usiyejulikana. Vipi usiathirike na katiba hii?

Kwa urahisi wako nadhani nitakuwekea rejea halisi kwenye bandiko linalouwa kwenye hilo ukapate kujiridhisha zaidi mwenyewe kwa raha zako.

Marejeo yamewekwa post #186 ya uzi huu.
 
Hii kanuni 'Judges like Caesar's wife must be beyond suspicion' naona inakuwa kama inasahaulika na kwa sababu hiyo kunakuwa na mashaka kuhusu independence na impartiality ya mahakama.

Hiyo ina apply kwenye mahakama za haki. Kuliko na uhuru kamili wa mihimili. Ndiyo maana ya umuhimu wa katiba mpya. Siyo kwenye "kangaroo courts" za kwenye zile nchi pendwa za Trump.

Mwingiliano wa mihimili umetufikisha hapa:

2970174_IMG_20211020_132118_488.jpg


Kwenye hopelessness.

Nani wa kulaumiwa?
 
Yaani uchomwe na bisibisi, uning'inizwe miguu juu, halafu maelezo yawe ya hiari, mateso yalikuwa ya nini? Hata mie si mwana sheria ila nauwezo wa kutafakari na kupima maelezo na hali na mazingira yaliyokuwepo, nahisi hukumu imeadhiriwa na majukumu mapya!

Jaji na kina Kingai ni timu moja labda naye ni shahidi upande wa mashtaka
 
Mheshimiwa huu mwendelezo wa comment #183 kwenye uzi huu:

Kwanini katiba ni muhimu kwetu sote:

1.
Tuwatambue wanaohaha kutusambaratisha kama Taifa

Comment #13 inahusika:

IMG_20211023_152909_320.jpg



Zipo nyuzi zaidi zenye maudhui hayo:

1. Tuwatambue Wanaopotosha Ajenda kuhusu Katiba Mpya

2.Katiba Mpya: Heri Rais Samia akaruhusu mchakato, asisubiri mashinikizo

3.Katiba Mpya: Ukweli Usiosemeka

4.Wanufaika wa Katiba Iliyopo hawahitaji elimu

Nk nk.

Nadhani tumepiga kelele ya kutosha. Nadhani nini tunataka na kwanini tunataka hakuna asiyeelewa hadi sasa.

Bila shaka mengine ni kujitia hamnazo tu.
 
Back
Top Bottom